Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,014
Wakuu,

Kutokana na wadau kadhaa kuja na mijadala anuai inayoonyesha kuwa wanayo mitaji yenye kuanzia kiasi cha TZS 100,000/= hadi TZS 999,999/=, tumeona ni vema tukawa na mjadala mmoja endelevu ambao utatoa mawazo mbalimbali ya jinsi ya kutoka kimaisha ukiwa na mtaji huo.

Aidha, tunashauri usome maoni mbalimbali ya wadau kuweza kupata kujua wengine wametokaje kwa viwango hivi na unaweza kufikiria namna unayoona inafaa kwako. Tumejitahidi kupangilia posts humu kukurahisishia usomaji kwa ufanisi wako.

Asante



Biashara za kuanzia 100,000 - 200,000

-----
----
----
----
----
----
----


Biashara za mtaji wa kuanzia 300,000-500,000


-----
----
----


Biashara za mtaji wa kuanzia 600,000-900,000


----
 
Du kwa mtaji huo?ningeweza kusema ufungue shoe shine lakin hauta tosha,basi fanya hiv nenda JF saccos iweke hiyo hela ugenerate three time upate angalao laki 6 labda utaweza fanya kitu.

Mitaji kama hii inahitaji biashara ya kupita mikononi, yaani ununue kwa producer na uuze kwa mlaji bila kukaa na bidhaa , ukishaanza kununua vitendea kazi vya biashara yako basi hutafika uendako.
 
Mitaji kama hii inahitaji biashara ya kupita mikononi, yaani ununue kwa producer na uuze kwa mlaji bila kukaa na bidhaa , ukishaanza kununua vitendea kazi vya biashara yako basi hutafika uendako.
Mkuu hiyo biashara ya mikononi ndio me naitaka,nimeisha anza na vocha,naona haiko vibaya sana,so nataka kuzifanya za aina mbalimbali nctegemee ya aina moja tu.
 
mkuu hakuna biashara duniani inayoanzishwa na mtaji kamili
anunue atakavyoweza vingine ataazima
Mkuu mimi kila nikiiangalia laki 2 aisee naona bora jamaa akomae na vibarua aiongezee kwanza, haka kamtaji kwa kujiajiri mwenyewe bado naona kama ni ndoto aisee!

Sababu tatizo ni kwamba hakuna biashara ambayo inapick up katika start up stage, sasa usishangae jamaa akaja akapoteza laki 2 badili ya kuiongeza hiyo laki 2, na am sure jamaa kajituma vya kutosha kupata hiyo laki 2 so bora aikeep na akomae na vibarua tu.
 
Sababu unauza vocha tayari ongezea kwenye biashara yako ya vocha yafuatayo:-
  • magazeti (haya hayaitaji mtaji unachukua kwa wakala ukiuza unakata (tshs 40 yako au zaidi sina uhakika) na yanayobaki unamrudishia wakala
  • sigara, biscuits, pipi, n.k. (huu mtaji wake ni mdogo)
  • juice (tena tengeneza zako mwenyewe) hapo profit margin itakuwa kubwa.., lakini utahitaji zile dumu portable ili uweke barafu ziwe za baridi pia unaweza kuuza na maji
  • Ongea na wafanyabiashara wenye maduka ili hata uweke pesa kidogo rehani (kama laki moja) ili wawe wanakupa bidhaa za kuuza kwa mali kauli, yaani ukishauza unawapa pesa zao na wewe unachukua faida usipouza unawarudishia
  • Karanga (kuna mtu aliniambia hii biashara Tshs 1 inazaa Tshs 1)
  • Sababu Arusha watalii wengi inategemea location yake sababu vilevile unaweza ukaongea na watu wenye ule urembo wa kitamaduni na vinyago ukaweka sample kwenye kijiwe chako ukiuza basi unapata commission yako usipouza basi hauna hasara.
Kumbuka kama umefanikisha kupata mkate wa kila siku kwa kuuza vocha ambazo faida ni ndogo kwa unit moja (basi inaonekana unauza volume kubwa sana) just imagine kama utatengeneza juice zako mwenyewe..., ukipata wateja hao hao wanaonunua vocha ukawaconvince wakanywa juice basi huenda faida ikawa zaidi 300%
 

Jitahidi kufuata ushauri aliotoa hapa maana ndivyo hata mie nafikiria. Si vema kuanzisha biashara nyingi ambayo inaweza kukuongezea gharama za uendeshaji, bora hii ya vocha uendelee nazo na papo hapo ongeza bidhaa nyingine kama livyoshauri mdau hapo juu hadi mtaji wako uongezeke.

Usifanye haraka kujenga ghorofa, bora weka msingi imara kwanza. Sipendi kuongelea mengi nisijechafua hayo aliyokushauri mdau.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…