Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

Wakuu heshima mbele, kama tulivyoahidi kuwa tutahitimisha dataz za nec,

1. Kulikuwa na wazungumzaji wengi siku hiyo, kutoka makundi mawili yaisyokubaliana na kupendana kabisaa kama ilivyojionyesha kwenye mjadala huu wa siku ya mwisho, ingawa kati ya wote waliooongea, ni watatu ndio hoja zao ni worhty kuziweka hapa, nao ni muungwana, sendeka, na selukamba.

2. Sendeka, alianza kwa kumshambulia muungwana kwa nguvu sana kuwa anawalinda mafisadi, ndio maana wanakuwa na kichwa cha kuweza kwenda kwenye majimbo yao ya uchaguzi na kutengeneza sherehe zao kubwa za mapokezi na kulidhihaki taifa na hotuba zao chafu.

3. muuungwana alismama kujibu tena kwa hasira sana kuwa maneno ya sendeka hayana ukweli kwa sababu, kama sio yeye muungwana, el bado nagekuwa na madaraka mpaka leo, ".....ninasema kuwa siku nne kabla ya kwenda Dodoma kwenye kikao cha ile ripoti, edward alikuja kwangu na kuniomba kuwa nimpe nafasi ili ajieleze kuhusiana na ripoti, lakini nikamkatalia kata kata na kumtaka aende mbele ya wananchi kule bungeni akajieleze na kujitetea kwa sababu mimi siwezi kumsaidia....", " .....lakini kwa mshangao mkubwa akaniletea barua ya kujiuzulu, badala ya kujitetea bungeni......"

4. Ikaja zamu ya selukamba, aliyemshambulia sana sendeka kuwa ni kibaraka wa mama kilango, na kusema kuwa choko choko zote za kina sendeka na wenziwe zinaanzia kwa mama kilango, alismea kuwa "........kuna watu ambao hawaonekani kuelewa kuwa uchaguzi wa urais uliiisha zamani bado wanataka urais mpaka leo, hivi hawajui kuwa Tanzania tuna rais tayari?...."

selukamba aliwashangaza wajumbe wote kwa kauli nzito aliyoitoa kuwa anaomba kulindwa maana mama kilango (ambaye hakuhudhuria kiako siku hiyo), amemtishia sana kuwa anaweza kumpiga au kumfanyia ubaya.

5. sendeka alirudi tena na kumjibu selukamba kuwa ni kibaraka wa mafisadi na hasa el na akamuonya muungwana na njama kubwa wanaozizfanya za kutaka el awe rais mwaka 2010, "....tunajua kuwa mnajitayarisha kugombea urais mwaka 2010 sio siri sasa kama sio unafiki ni nini mwambieni tu rais yupo hapa?....", ilibidi muuungwana aingilie kati maana sasa wajumbe walikuwa karibu washkane mashati, alianza kwa kujaribu kumsafisha el lakini wajumbe wakaguna sana kwa mshangao, ndipo alipoanza kunawa mikono kama nilivyozileta jana.

6. Ishu ya Mkamba kuondolewa ukatibu ilisemwa wazi pamoja na juhudi zote za baadhi ya mafisadi kuitoa kwenye agenda na ilikubaliwa kuwa itapelekwa kwenye kikao cha karibuni cha cc kwa uamuzi wa mwisho. Na pia wanachama wote watakaobainika kuwa ni mafisadi watafukuzwa chama.

7. Mbunge wetu shujaa Mwakyembe bado hajarudi Dodoma, mpaka sasa hivi ninapoandika, akiendelea na uchunguzi wa madikatari bingwa DAr, naye Spika amewapa masaa 72 wale wote kuanzia polisi mpaka uwt waliokuwa wakichunguza ile soo ya bunge, kumpa matokeo mara moja. Sasa the showdown ya makundi haya mawili kati ya mafisadi na wengine inahamia bungeni, ambako the dataz ni kwamba kati ya siku mbili zajazo kutakuwa na mashambuliano ya kukata na shoka, kwenye mjadala wa bajeti.

Kwa haya wakuu naomba kusema ndio mwisho wa dataz kutoka kikao cha nec kilichoisha hivi karibuni, heshima mbele kwa wote waliochangia hii mada, na wale waliopitisha angalau macho yao tu, nia na madhumuni yetu ni moja tu nayo ni kuelimishana na kuhbarishana habari muhimu za taifa letu na kumuachia mwananchi aaamue mwenyewe cha kufanya, au kutokufanya. Ni muhimu kupeana za ndani kabla hazijafika kwenye media na kuwa spinned na kina Chiligati, maana sasa hata waki-spin tunawangalia kwa macho mawili maana we know the truth.

Ahsante Wakuu! tuendelee kukata ishus maana taifa liko njia panda!
 
Heshima Mkuu...shukurani kwa hizo dataz...tunstegemea mengi zaidi..
 
Wakuu heshima mbele, kama tulivyoahidi kuwa tutahitimisha dataz za nec,

1. Kulikuwa na wazungumzaji wengi siku hiyo, kutoka makundi mawili yaisyokubaliana na kupendana kabisaa kama ilivyojionyesha kwenye mjadala huu wa siku ya mwisho, ingawa kati ya wote waliooongea, ni watatu ndio hoja zao ni worhty kuziweka hapa, nao ni muungwana, sendeka, na selukamba.

2. Sendeka, alianza kwa kumshambulia muungwana kwa nguvu sana kuwa anawalinda mafisadi, ndio maana wanakuwa na kichwa cha kuweza kwenda kwenye majimbo yao ya uchaguzi na kutengeneza sherehe zao kubwa za mapokezi na kulidhihaki taifa na hotuba zao chafu.

3. muuungwana alismama kujibu tena kwa hasira sana kuwa maneno ya sendeka hayana ukweli kwa sababu, kama sio yeye muungwana, el bado nagekuwa na madaraka mpaka leo, ".....ninasema kuwa siku nne kabla ya kwenda Dodoma kwenye kikao cha ile ripoti, edward alikuja kwangu na kuniomba kuwa nimpe nafasi ili ajieleze kuhusiana na ripoti, lakini nikamkatalia kata kata na kumtaka aende mbele ya wananchi kule bungeni akajieleze na kujitetea kwa sababu mimi siwezi kumsaidia....", " .....lakini kwa mshangao mkubwa akaniletea barua ya kujiuzulu, badala ya kujitetea bungeni......"

4. Ikaja zamu ya selukamba, aliyemshambulia sana sendeka kuwa ni kibaraka wa mama kilango, na kusema kuwa choko choko zote za kina sendeka na wenziwe zinaanzia kwa mama kilango, alismea kuwa "........kuna watu ambao hawaonekani kuelewa kuwa uchaguzi wa urais uliiisha zamani bado wanataka urais mpaka leo, hivi hawajui kuwa Tanzania tuna rais tayari?...."

selukamba aliwashangaza wajumbe wote kwa kauli nzito aliyoitoa kuwa anaomba kulindwa maana mama kilango (ambaye hakuhudhuria kiako siku hiyo), amemtishia sana kuwa anaweza kumpiga au kumfanyia ubaya.

5. sendeka alirudi tena na kumjibu selukamba kuwa ni kibaraka wa mafisadi na hasa el na akamuonya muungwana na njama kubwa wanaozizfanya za kutaka el awe rais mwaka 2010, "....tunajua kuwa mnajitayarisha kugombea urais mwaka 2010 sio siri sasa kama sio unafiki ni nini mwambieni tu rais yupo hapa?....", ilibidi muuungwana aingilie kati maana sasa wajumbe walikuwa karibu washkane mashati, alianza kwa kujaribu kumsafisha el lakini wajumbe wakaguna sana kwa mshangao, ndipo alipoanza kunawa mikono kama nilivyozileta jana.

6. Ishu ya Mkamba kuondolewa ukatibu ilisemwa wazi pamoja na juhudi zote za baadhi ya mafisadi kuitoa kwenye agenda na ilikubaliwa kuwa itapelekwa kwenye kikao cha karibuni cha cc kwa uamuzi wa mwisho. Na pia wanachama wote watakaobainika kuwa ni mafisadi watafukuzwa chama.

7. Mbunge wetu shujaa Mwakyembe bado hajarudi Dodoma, mpaka sasa hivi ninapoandika, akiendelea na uchunguzi wa madikatari bingwa DAr, naye Spika amewapa masaa 72 wale wote kuanzia polisi mpaka uwt waliokuwa wakichunguza ile soo ya bunge, kumpa matokeo mara moja. Sasa the showdown ya makundi haya mawili kati ya mafisadi na wengine inahamia bungeni, ambako the dataz ni kwamba kati ya siku mbili zajazo kutakuwa na mashambuliano ya kukata na shoka, kwenye mjadala wa bajeti.

Kwa haya wakuu naomba kusema ndio mwisho wa dataz kutoka kikao cha nec kilichoisha hivi karibuni, heshima mbele kwa wote waliochangia hii mada, na wale waliopitisha angalau macho yao tu, nia na madhumuni yetu ni moja tu nayo ni kuelimishana na kuhbarishana habari muhimu za taifa letu na kumuachia mwananchi aaamue mwenyewe cha kufanya, au kutokufanya. Ni muhimu kupeana za ndani kabla hazijafika kwenye media na kuwa spinned na kina Chiligati, maana sasa hata waki-spin tunawangalia kwa macho mawili maana we know the truth.

Ahsante Wakuu! tuendelee kukata ishus maana taifa liko njia panda!

Kwa hiyo data za Lunyungu kuhusu Lowassa wewe huna!
 
Kwa hiyo data za Lunyungu kuhusu Lowassa wewe huna!

Lunyungu amesahau kuwa hapa JF We dare.........

Field Marshall ES said:
Wakuu heshima mbele, kama tulivyoahidi kuwa tutahitimisha dataz za nec,

1. Kulikuwa na wazungumzaji wengi siku hiyo, kutoka makundi mawili yaisyokubaliana na kupendana kabisaa kama ilivyojionyesha kwenye mjadala huu wa siku ya mwisho, ingawa kati ya wote waliooongea, ni watatu ndio hoja zao ni worhty kuziweka hapa, nao ni muungwana, sendeka, na selukamba.

Sidhani kuna umuhimu tena wa EL...tusimpe kichwa
 
Kikwete alisema haya wakati akijibu kutoka kwa Lowassa...

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza zaidi kuwa yaliibuka mabishano makali kutokana na mjadala wa hoja ya Richmond,baada ya Lowassa kusimama na kujitetea kuwa alishatoa ushauri mara mbili mkataba huo uvunjwe lakini alikataliwa.

Baada ya mabishano makali, inadaiwa kuwa Rais Kikwete alilazimika kusimama na kutoa ufafanuzi na kueleza kuwa Lowassa alikuwa na nafasi ya kutoa maelezo na kutojiuzulu nafasi yake, lakini mwenye aliona kujiuzulu ndio uamuzi wa busara.
HATA HIVYO...Aliyasema haya alipokuwa akimjibu Ole Sendeka...

3. muuungwana alismama kujibu tena kwa hasira sana kuwa maneno ya sendeka hayana ukweli kwa sababu, kama sio yeye muungwana, el bado nagekuwa na madaraka mpaka leo, ".....ninasema kuwa siku nne kabla ya kwenda Dodoma kwenye kikao cha ile ripoti, edward alikuja kwangu na kuniomba kuwa nimpe nafasi ili ajieleze kuhusiana na ripoti, lakini nikamkatalia kata kata na kumtaka aende mbele ya wananchi kule bungeni akajieleze na kujitetea kwa sababu mimi siwezi kumsaidia....", " .....lakini kwa mshangao mkubwa akaniletea barua ya kujiuzulu, badala ya kujitetea bungeni......"
Talking about USANII ama lack of LEADERSHIP?
 
Zile style za Kingunge za KUKANUSHA KUWA SIKUKANUSHA!
Hawezi kuwatumikia mabwana wawili...Eti kujidai kuwa anapiga vita ufisadi na ndio maana Lowassa akajiuzulu huku akimwambia Lowassa kuwa yeye ni mtu mzuri ambaye hakutaka ajiuzulu bali yeye lowassa mwenyewe ndiye alitaka!
Usanii mwingine bana...Sasa kama alikuwa keshajua ni fisadi alitaka akajieleze bungeni badala ya kumkamata mara baada ya kujiuzulu?
Hivi watanzania wameweka Zecomedy madarakani?
 
Mkuu Fundi hatuwezi kukwepa kujadili yanayojiri kwenye tifa letu kwa kuogopa aibu, yaliyotokea na tunayo yajadili ndio hasa uwezo wetu wa-Tanzania kiakili ulipo, kwa sababu look watu waliosoma Harvad kina Obama sasa wako wapi na hawa wenzetu waliosoma Harvad kina Chenge na Mungai walipo?

Hatuwezi ku-denial uwezo wetu wa kufikiri na kuona mambo kitaifa, mkuu Fundi haya tunayoayajadili yana-reflect us as a nation, kuyakwepa kwa sababu ni aibu ni kujaribu kuyafukia sio solution yatakuja kurudi tu mbele ya safari!

Mimi sikatai kujadilikama unavyodhani, bali ninachopinga ni huku kushabikia na kuendekeza hizi imani potovu. Tunamhukumu Chenge kuwa Mlozi kwa kuingia ukumbini akiongozana na Afisa wa Bunge! Kuugua ghafla kwa Mheshimiwa kumetufanya wote tuamini kuwa ni lazima pana mkono wa mtu, hususan wa Chenge! Wakati huo huo huko kwa Obama, huyo graduate wa Harvard, ameanguka na kufa mwandishi mahiri na hakuna aliyekimbilia ulozi. Unauliza hawa wenzetu waliosoma Harvard wako wapi? Unategemea nini katika mazingira kama haya? Mazingira yaliyojaa imani za kishirikana unategemea kweli maendeleo? Huyo Chenge na Mungai wahukumiwe kwa madhaifu yao ( ambayo bila shaka ni mengi) lakini si kwa upuuzi huu! Viongozi wetu wanajulikana kwa kutoheshimu afya zao, leo tunashangaa wanapopata matatizo. Tunaingia gharama kubwa (mheshimiwa lazima ataenda ulaya kuangaliwa afya yake kama vile alivyoenda Pombe) kwa imani hizi zisizo na msingi. Imani ambazo zinachangiwa sana na usiri uliyodidima. Hivi palikuwa na shida gani ya kuonyesha hiyo video ili watu wajionee kama Chenge alibeba kibuyu au alikuwa kweli anaelekezwa sehemu ya kukaa?

Mimi siko kwenye denial. Najua jamii yangu ndivyo inavyoamini. Lakini kujua huku hakuniondolei hisia za aibu. Ni kama vile ambavyo ningependa majadiliano zaidi kwenye yale ambayo naona ni substantive lakini najua wengi wetu interest zao ni kwingine. Hii ni www, hatuwezi wote kuwa na interest zinazofanana.
 
.....................Tunaingia gharama kubwa (mheshimiwa lazima ataenda ulaya kuangaliwa afya yake kama vile alivyoenda Pombe) kwa imani hizi zisizo na msingi. ...............

........Fundi, jambo usilolijua ni sawa na usiku wa kiza Mkuu!!.........Tumuombee tu Mh Mwakyembe arudi salama bungeni na aendelee na ujenzi wa Taifa.............the MAFIA kingdom iliyopo kule nyumbani is so powerful
 
Nchi inayumba sana. ama kweli tuko kwenye auto pilot hadi 2010
 
Nchi inayumba sana. ama kweli tuko kwenye auto pilot hadi 2010

Ag,

Mimi naomba nitofautiane na wengi, nadhani taifa letu linapitia kipindi kizuri sana kwenye uhai wake... kwa hakika hiki ndio kipindi cha kimapinduzi kweli... yaani ya kifikra, kiitikadi na kidemokrasia... hii ili itokee lazima equilbrium ile disturb kidogo... na hili ndilo lililotokea..

Si muda mrefu tulikua tunakasirikia CCM kutoambiana ukweli, sasa hivi demokrasia ndani ya CCM inakuwa sana... na kwa kweli kama watu wako imara kuamua hata katibu mkuu aondolewe... hii ni demokrasia ya hali ya juu...

Mimi nadhani CCM inajiweka mahali pazuri kuliko tunavyodhani wengi wetu.

Na kwa kweli wana mwenyekiti mpenda demokrasia.... kama Mh. Ben Mkapa angekuwa anaruhusu mijadala wazi kwenye uenyekiti wake haya tunayoyaona leo tusingeyaona... sasa tusubiri next CC meeting kitu kitakachojiri

Mwisho: Come 2010 mutaona jinsi wafanya biashara wengi... watakavyoamua kutogombea... tusubirini pia mtakavyoona Dar es Salaam kutavyoanza kuwa na wabunge wa kweli... wala sio bora wabunge kama ilivyo sasa!
 
ANDREA!mwana wa chenge! nimekukosea nini mimi taifa lako? nimekusomesha hadi ndani na nje, nikakupa kiti cha enzi uweze kuwahukumu wenye haki na wakosefu, ukaamua kujilimbikizia mali za yatima na wajane! nimekukosea nini mimi taifa lako?

nikakupa wadhifa mkubwa kuwatetea hawa maskini wangu, ukaamua kuchukua chakula chao ukajilisha mwenyewe na kingine ukawatupia mbwa, nimekokosea nini mimi taifa lako?

ukaamua kuasi na kuuma mkono wako wa kulia! ukaamua kuungana na beel-zebul, ukaniasi mimi niliyekulisha ukanawiri.

tazama sasa nimekuacha! beel zebul ameamua kukuumbua, tazama sasa nimekuacha, nimekuacha uabike!

beel-zebul=shetani mkuu
Asante Mwikimbi
 
Kasheshe;
Wasiwasi wangu ni kinachotokea nyuma ya pazia yaani kundi A na kundi B ndani sisiem. Inaonyesha kuna mpasuko mkubwa/ombwe katika uongozi wa nchi yetu. Hivi kama tuko katika auto pilot, je mafisadi wakimdhibiti rubani itakuwaje? Pia ndugu yangu zingatia kwamba demokrasia ya kuua nchi sio demokarasia ifaayo kwani kadri mkuu FM alivyodokeza inaonekana sio demokrasia bali domokrasia ndani ya chama tawala.
 
Mkuu nashukuru kwa nyeti hizi.Sasa tunaanza kuyaona maisha katika mwanga ulio bora.Kama imefikia watu kupasuliana mchana kweupe!!!!,baaasi demokrasia ya kweli iko mlangoni inatroti.
Ukiona watu wanafikia kuchoka kiasi hicho ujue kuwa neema inakaribia.
 
Jamaa according to the dataz ni uwt, kumbe na yeye kuna deal nyingi ndogo ndogo ambazo amewahi kukatiwa mpango hata kabla hajawa ag, na pia kwenye hili deal inasemekana kuwa amekatiwa, kwa sababu kisheria yeye ndiye aliyetakiwa kuwa mstari wa mbele sasa hivi kudai sheria imevunjwa, lakini ndio kwanza najivuta vuta,

Sasa subiri tuone majibu ya Pinda, maana nasikia huko ndani kunawaka moto, waliokula wote wanahaha, kinachosikitisha hapa ni how sisi as a nation tuliweza kuwa na Waziri Mkuu mjinga mjinga kama Lowassa? The man is so arrogant nasikia ilifikia mahali alikuwa ani-run serikali kama Kingdom yake vile, yaaani nasikia viongozi wetu watu wazima na akili zao wenye wake nyumbani na watoto walikuwa wakimsujudia huyu fisadi, how? na WHY?

Wakuu kwa kweli inasikitisha sana kusikia ambayo hayajasemwa hadharani kuhusiana na huyu mkuu, yaani ndani ya bunge mkuu alikuwa akibadili wabunge kina mama kama nguo, ambao wote walilia sana ile siku, halafu eti anasema kuwa hakutegemea kuwa hawa wabunge wajinga wajinga wangeweza kumuondoa? Unajua wakuu ninaomba mzitafute dataz za huyu mkuu yaaani ni aibu hata kuitwa m-Tanzania!
Mzee wewe Nuksi....Nimekukubali.Kumbe unajua hata siri ya vile VILIO siku ile...!!!!!!!
Duh Mwanawani unatisha.
 
Kasheshe;
Wasiwasi wangu ni kinachotokea nyuma ya pazia yaani kundi A na kundi B ndani sisiem. Inaonyesha kuna mpasuko mkubwa/ombwe katika uongozi wa nchi yetu. Hivi kama tuko katika auto pilot, je mafisadi wakimdhibiti rubani itakuwaje? Pia ndugu yangu zingatia kwamba demokrasia ya kuua nchi sio demokarasia ifaayo kwani kadri mkuu FM alivyodokeza inaonekana sio demokrasia bali domokrasia ndani ya chama tawala.

Ag,

Kweli kuna mpasuko... lakini ungeweza kudumu tu kama, haya yangekuwa yanafanyika kwa siri na wananchi hawafahamu... kwa sasa yule aliyeko upande wa Wananchi ndiye mshindi!!! iko wazi kwamba sasa hivi waheshimiwa wa EPA/RICHMOND wakijaribu tu hata kwenda chama kingine ndio hivyo tena... career ya politics inakuwa mwisho wake...

Nakuhakikishia tuko kwenye kipindi kizuri sana... na namshukuru mwenyekiti wa CCM kwa kuwa na moyo wa demokrasia... kiasi hicho... CCM inavyoelekea itakuwa imara kuliko... miaka mingine yote... maana kabla ya hapo ilizana watu waoga na wenye kusema zidumu fikira za mwenyekiti wa CCM... sasa hivi ni tofauti... makada wapinzani wako wengi.
 
Aboh! Hollow Brain?how does it look like?kwi kwi a question is a question!u're an idiot kabisa!
For the sake of Mjadala uliopo mbele yetu.
Nawaomba wote,si Peasant na wengine on one side na hollo on the other.
ACHENI majibizano ambayo haya add value kwenye mada husika.
NAWAOMBA BINAFSI.FUTURE YETU NA YA WATOTO WETU INADEPEND KWENYE HAYA YANAYOTOKEA KWETU WAKATI HUU SISI AS A NATION.
NAWAOMBA SANA TUVUMILIANE KWA MASLAHI YA TAIFA HILI
 
Mimi kila nikiangalia hii njii yetu na mustakabari wa baadae nazidi changanyikiwa kabisa! Hivi huyu huyu alirudi kule bariadi na wakampokea kwa nderemo? ama kweli sisi ni wadanganyika! ndio maana wanatuibia halafu eanatufunga sisi wenye mali wao wezi wapo nje wanavuta hewa safi.

Mdanganyika amka sasa huu ni ndio wakati wa kweli ambao unanifanya nimkumbuka baba wa Taifa hili, kwani tunayoshuhudia sasa tayari alishayatabili katika hotuba zake mbalimbali.
 
Kwa hiyo data za Lunyungu kuhusu Lowassa wewe huna!

Wewe si upo Dodoma mbona huna dataz hata moja? Mijitu mingine bwana mbona hueleweki na majina yako 100 humu, huku unasema one thing halafu unageuka na kusema another ndio maana mkuu sipendi kuwatse my ku-debate na watu kama wewe,

Wazee msiokuwa na dataz hakuna mashindano hapa, wewe kama ulikuwa nazo za lowassa kilichokushinda kuziweka hapa ni nini hasa? Ningekuelewa kuwa wewe unanilipa mimi kuleta dataz na unanipa hizo dataz, then ni kweli una the rights kuniuliza kwa nini sikuleta za lowassa, mkuuu kula dataz hapa au waachie wenye vichwa wazichambue!

Na ninawaahidi kuwa tutaendelea kuleta dataz hapa JF kama kawa, halafu pole sana mkuu nasikia majuzi ulimpigia simu mama ukala mawe haijawahi kutokea pole sana!
 
Wewe si upo Dodoma mbona huna dataz hata moja? Mijitu mingine bwana mbona hueleweki na majina yako 100 humu, huku unasema one thing halafu unageuka na kusema another ndio maana mkuu sipendi kuwatse my ku-debate na watu kama wewe,

Wazee msiokuwa na dataz hakuna mashindano hapa, wewe kama ulikuwa nazo za lowassa kilichokushinda kuziweka hapa ni nini hasa? Ningekuelewa kuwa wewe unanilipa mimi kuleta dataz na unanipa hizo dataz, then ni kweli una the rights kuniuliza kwa nini sikuleta za lowassa, mkuuu kula dataz hapa au waachie wenye vichwa wazichambue!

Na ninawaahidi kuwa tutaendelea kuleta dataz hapa JF kama kawa, halafu pole sana mkuu nasikia majuzi ulimpigia simu mama ukala mawe haijawahi kutokea pole sana!



Yeah,kiroho mbaya; Manake mkuu unajua huku duniani watu wenye roho mbaya wasingekuwepo hii dunia ingeweza kuwa na matatizo sana?

Huyo mkuu aliekua anauliza kama wewe ulikua na dataz za EL ama la,mbona asinge-comfirm huko huko yeye?
 
Mimi siko kwenye denial. Najua jamii yangu ndivyo inavyoamini. Lakini kujua huku hakuniondolei hisia za aibu. Ni kama vile ambavyo ningependa majadiliano zaidi kwenye yale ambayo naona ni substantive lakini najua wengi wetu interest zao ni kwingine. Hii ni www, hatuwezi wote kuwa na interest zinazofanana.

Mkuu mambo ya siasa siku zote ni historia, tumeuona Amina Chifupa(RIP), akitishiwa kwa kutaka uenyekiti wa vijana, the next thing we know amekufa kwa sababu isiyoeleeweka, sasa leo ulitegemea nini viongozi wetu wawe wajinga kuupanda tena mkenge wa Chenge?

Mkuu ukweli ni kwamba viongozi wetu ni sisi wenyewe, juzi tumesikia mtoto anakula kichwa cha mtu, ndivyo tulivyo amesema mkulu wangu Nyani, mimi siamini uchawi lakini gari langu nalifunga na funguo, maana sina noma kwenda Bagamoyo, maana nasikia huko kwenye uongozi wa juu ni lazima ifahamike kua na wewe huwa unaenda kwa hiyo kabla ya kwenda ni kutangaza kuwa unaenda, na kuzunguka tu pale Bagamoyo mjini na kurudi inatosha,

Viongozi wetu na sisi wananchi wote ni washirkina period!
 
Back
Top Bottom