Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

[/B]
You're such a dumb with childish questions, no wonder you call yourself hollo, you must have a HOLLOW BRAIN.
Aboh! Hollow Brain?how does it look like?kwi kwi a question is a question!u're an idiot kabisa!
 
Field Marshall ES, bora ukapumzike ili utuletee habari nyingine kesho, sasa hivi huo ni kama mgodi wa madini, kalale mkuu. Usiku wema

Ahsante mkuu wangu kwa concern, maana ni kweli niko hoi sana, lakini kabla sijaenda kulala, unajua nimefukua data ndogo tu sasa hivi,

kuwa kumbe Lowassa na Mwakyembe, walisoma shule moja yaani Mirambo, Lowassa akiwa Form Six, na Mwakyembe form Five, wote walikuwa maa-artists, lakini Mwakyembe alikuwa ni the best artist kwa shule nzima, walipomaliza Lowassa alienda kusomea Arts, Mwakyembe alienda kusomea Journalism, baadaye ndio Mwakyembe aka-change the course na kusoma Sheria, na Lowassa aka-change na kwenda kusoma Administration,

Wabunge walipokutana kutafuta nani awe mwenyekiti wa ile kamati, kwa kauli moja wakasema yule yule aliyekuwa bingwa wa arts Mirambo, na anayemjua vizuri sana Lowassa, yaani Mbunge Shujaa Mwakyembe, tunaendelea kumuombea kuwa awe salama na kutokutwa na mabaya, kwa sababu we need him now more than anytime before kwa taifa letu,

Mungu Amlinde na Hizo Hewa Chafu, ili aweze kurudi bungeni ili kutuokoa wananchi na hawa mafisadi, kwa nguvu ya Mungu mafisadi wote watalegea na Mwakyembe atarudi bungeni na kuwatwanga zaidi na mashetani yao!

Sasa naenda kulala, kesho wakuu!
 
El na Chenge mavi ya ualo na blanket la mgonjwa wa kuhalisha wakati wa masika.
 
Huyo hawezi... tumchague muafrika wa kike! kwi kwi kwi

slow down slow down...you are in the right direction. Mama uchawi hawezi! -achaguliwe na nani na kwa nini-hayupo tayari kufatwa fatwa-anafanya kipenda roho. Watch ur step mchonganishi/mnafiki nambari wani wewe!
 
Ushirikina walichanganya Bunge

Martin Malera said:
Dodoma


HALI si shwari mjini Dodoma, wabunge sasa wanaonekana kuogopa kuusogelea ukumbi wa Bunge, baada ya kupatikana taarifa za mmoja wa wabunge kuingia ndani ya ukumbi huo na kufanya vitendo vya kishirikina.

Wabunge kadhaa waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili juzi na jana, walieleza wasiwasi wao kuhusu suala hilo na kudai kuwa iwapo hatua za haraka kudhibiti vitendo vya aina hiyo hazitachukuliwa, uwezekano wa kuwapo mahudhurio hafifu ya wabunge katika vikao vinavyofuata ni mkubwa.

“Hili tukio limetutia hofu, tunadhani kuna kila sababu ya kukamilisha uchunguzi wa tukio hili mapema. Spika ameeleza kuwa tukio hili linachunguzwa, tunaomba lichunguzwe kweli, tena kwa haraka, ili kutuondolea hofu tuliyonayo sasa,” alisema mmoja wa wabunge kutoka Mkoa wa Mwanza.

Mbunge mwingine ambaye pia hakutaka kutaja jina lake liandikwe gazetini, alilieleza gazeti hili kuwa Spika anapaswa kutoa taarifa ya tukio hili bungeni na kulitolea ufafanuzi badala ya kuendelea kulizungumza kwenye vyombo vya habari.

“Hizi taarifa zipo, wabunge wengi wanazijua, lakini Spika analizungumzia kwenye vyombo vya habari. Mimi nadhani suala hili linagusa maisha yetu, ni bora akalieleza Bunge nini kilitokea,” alisema mbunge huyo.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta, jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa, ofisi yake imekabidhi picha za video zilizomnasa mbunge huyo akiwa ameambatana na Ofisa Mwandamizi wa Bunge kwa siri, waliokuwa wakiweka vitu vinavyoaminika kuwa vya kishirikina au aina fulani ya sumu kwenye kila kiti cha mbunge.

Sitta alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa kutoa ufafanuzi juu ya tukio hilo ambalo hivi sasa limewachanganya baadhi ya wabunge kiasi cha kuhofia kuingia na kukalia viti vyao ndani ya ukumbi wa Bunge kabla ya uchunguzi kubaini kitu kilichowekwa.

Kwa mujibu wa Sitta, picha za mkanda huo zilizonaswa na kamera za usalama zilizomo ndani ya jengo hilo la kisasa, zimefifia kiasi cha kushindwa kubaini kwa haraka watu wanaoonekana ndani ya mkanda huo.

Kutokana na hali hiyo, Sitta alisema ofisi yake imeamua kuukabidhi mkanda wa picha hizo kwa maofisa usalama wa taifa na kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, kwa ajili ya kuzifanyia uchunguzi zaidi.

Siku moja kabla ya kuanza kwa mkutano wa 12 wa Bunge la Bajeti mjini Dodoma, mbunge mmoja akiandamana na Ofisa Mwandamizi wa Bunge (jina limehifadhiwa kwa sasa), wanadaiwa kuingia ndani ya Bunge na kupita kwenye kila kiti cha mbunge, huku wakinyunyizia vitu vinavyoaminika kuwa sumu au aina fulani ya dawa za kishirikina, kwa sababu ambazo hadi sasa hazijaeleweka.

Baadhi ya wabunge na vyanzo vyetu vya habari, vilisema kuwa mbunge anayedaiwa kuhusika katika tukio hilo la aina yake ni mmoja kati ya mawaziri waliojiuzulu nyadhifa zao kutokana na tuhuma mbalimbali za ufisadi. Jina la mbunge huyo kwa sasa pia linahifadhiwa.

Hata hivyo mawaziri waliojiuzulu hivi karibuni kutokana na tuhuma za ufisadi ni pamoja na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha (wote walikuwa Nishati na Madini) na Andrew Chenge (Miundombinu).

Akizungumzia tukio la kuugua ghafla kwa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, Sitta alisema taarifa ya daktari aliyemtibu Dk. Mwakyembe imeonyesha kuwa halina uhusiano na aina hiyo ya dawa inayodaiwa kuwekwa ndani ya viti vya wabunge.

Alisema Dk. Mwakyembe, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati iliyochunguza mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, aliugua ghafla bungeni kutokana na sababu za kawaida na si vinginevyo.

Wakati Spika akitoa ufafanuzi wa tukio hilo, baadhi ya wabunge wamekuwa katika mjadala huku wakiwa na hofu ya kuendelea kukalia viti vyao bungeni, kwa hofu ya kudhurika kwa sumu au dawa hiyo inayodaiwa kuwa ya kishirikina.

Hata hivyo wapo baadhi ya wabunge wanaopuuza tukio hilo, kwa madai kuwa hakuna suala la ushirikina linaloweza kumdhuru mtu katika karne hii.

Wakati huo huo, Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana ilikuwa na semina iliyokuwa na lengo la kujadili hali ya uchumi, hususan mfumuko wa bei na jinsi ya kurekebisha hali hiyo.

Katibu Mwenezi na Itikadi wa CCM, Kapteni John Chiligati, alisema semina hiyo ambayo itaendelea leo, ilikuwa na ajenda kubwa juu ya hali ya uchumi, ambapo Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Beno Ndullu, alitoa mada ndefu juu ya hali ya uchumi nchini.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vya habari ndani ya semina hiyo, vilidai kuwa NEC pia ilijadili suala la ufisadi na hatua zinazochukuliwa kwa mafisadi, ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa sababu ya kudidimiza hali ya uchumi nchini.

Hata hivyo, Chiligati aliahidi kutoa taarifa kamili leo baada ya kumalizika kwa semina hiyo inayoendeshwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete
.
Source Tanzania Daima!
 
Of course, naomba kuwasisitiza wana JF kufikiria mbali zaidi. Hakuna uchawi, kuna kitu inatumiwa na inaua taratibu na mwisho mlengwa anakuwa ndio hivyo tena.

...Beware!

Imeshatajwa huko juu, sijui waungwana wanadoubt nini tena
 
mkuu asante sana kwa news

la kuvunda halina ubani. mwaka huu mambo yote lazima yawe namba nane kama ilivyo namba ya mwaka huu

Mkuu,


NAOMBA URUDI HAPA JAMVINI UOMBE MSAMAHA MEMBERS WOTE NA U-WITHDRAW STATEMENT YAKO YA KUSEMA KWAMBA ZITTO NDIYE ALIYENASWA NA CAMERA NDANI YA UKUMBI WA BUNGE.

Mkuu,Kwanini uliamua kumzushia huyu mkuu pasipo na sababu za msingi au kwa sababu zako binafsi?

Mbaya zaidi baadhi ya members hapa tulikuonya na bado ukasizitiza kwamba ni ZITTO.

Mkuu wangu,Kwa hizo tuhuma zako za moja kwa moja ulizomshushia Zitto ndizo zinazoweza kuwapa sababu Jeshi la polisi na maofisa usalama kama walivyofanya siku za Nyuma kutubandika majina ya ajabu ajabu,mara Magaidi,tunachafua majina ya watu etc.

Mkuu tunomba uje hapa kuliweka hili Sawa ili kuendelea kulinda heshima ya kijiwe hiki na members wa humu ndani.
 
Hivi wakuuu, Mheshimiwa akiulizwa sasa pale ulikuwa unafanya nini atajibu nini jamani? Mambo mengine ya aibu sana. Yaani wameona yale wanayoyafanya mbali huko hayatoshi sasa kaamua kuja nayo Live sio tena nje ya muda wa bunge. Da Kazi kweli kweli. Ila ninahisi labda ni mikakati waliyoifanya London wiki kadhaa zilizopita.
 
Bunge la wabunge wanaoogopa ushirikina? Wao wenyewe kabla ya kuingia bungeni, wengi wao walitembea uchi makaburini.

Halafu tunashangaa nchi yetu iko nyuma, kama tunaongozwa na hawa wajinga, unafikiri tutegemee nini?
 
Mkuu,


NAOMBA URUDI HAPA JAMVINI UOMBE MSAMAHA MEMBERS WOTE NA U-WITHDRAW STATEMENT YAKO YA KUSEMA KWAMBA ZITTO NDIYE ALIYENASWA NA CAMERA NDANI YA UKUMBI WA BUNGE.

Mkuu,Kwanini uliamua kumzushia huyu mkuu pasipo na sababu za msingi au kwa sababu zako binafsi?

Mbaya zaidi baadhi ya members hapa tulikuonya na bado ukasizitiza kwamba ni ZITTO.

Mkuu wangu,Kwa hizo tuhuma zako za moja kwa moja ulizomshushia Zitto ndizo zinazoweza kuwapa sababu Jeshi la polisi na maofisa usalama kama walivyofanya siku za Nyuma kutubandika majina ya ajabu ajabu,mara Magaidi,tunachafua majina ya watu etc.

Mkuu tunomba uje hapa kuliweka hili Sawa ili kuendelea kulinda heshima ya kijiwe hiki na members wa humu ndani.

ama kweli akili ni nywele kila mtu ana zake.

wapi nilisema aliefumwa na camera ni zitto hebu leta ushahidi huo na ukishindwa fanya uniombe radhi kwa kunizulia.

kaa usome vizuri na udadavue nini kiekusudiwa kabla ya kukurupuka angalia na utagundua umakini mkubwauliotumika ktk maandishi
 
Wanamtafuta Rev Kishoka maana yeye ni tofauti na wachungaji wengine

wachungaji wa Tanzania wanapokea michango kutoka kwa Mafisadi kila kukicha wakati wanajua hizo ni pesa za wizi ambazo zinasababisha vifo vya wananchi

Labda Rev kishoka wameona upo tofauti na akina askofu mkuu wa Jimbo la Arusha wanaosaidia kutandika Zuria hili Mwizi EL apite jamani

Nakubaliana na wewe Mkuu,

Haikuwahi kuniingia akilini eti askofu ataenda kumpokea fisadi eti ni shujaa. Ipo siku waumini tutaamka na kumwambia atuombe msamaha. Mambo taratibu. Kwa sasa tumeanza kwanza na hawa mafisadi wakubwa then tutakuja kwao. Kwa sasa natafuta Data za Maaskofu wote ambao hawajawahi kukemea ufisadi basi na wao ni mafisadi
 
Wanamtafuta Rev Kishoka maana yeye ni tofauti na wachungaji wengine

wachungaji wa Tanzania wanapokea michango kutoka kwa Mafisadi kila kukicha wakati wanajua hizo ni pesa za wizi ambazo zinasababisha vifo vya wananchi

Labda Rev kishoka wameona upo tofauti na akina askofu mkuu wa Jimbo la Arusha wanaosaidia kutandika Zuria hili Mwizi EL apite jamani

Inaelekea wameamua kuokoka na kumrudia bwana, wasaidie mchungaji,musiwakatae kondoo walioamua kweli kumgeukia bwana lakini angalia wasikufisadi na wewe
 
ama kweli akili ni nywele kila mtu ana zake.

wapi nilisema aliefumwa na camera ni zitto hebu leta ushahidi huo na ukishindwa fanya uniombe radhi kwa kunizulia.

kaa usome vizuri na udadavue nini kiekusudiwa kabla ya kukurupuka angalia na utagundua umakini mkubwauliotumika ktk maandishi



Mkuu,soma hiyo thread unayojifanya umeisahau.Kwa mara nyingine tena unaendelea kuwadhalilisha members hapa kwa kuwafanya ni watoto na hawaelewi au hawakumbuki ulichoandika.

Mkuu,usiwe kama huyo Mbunge aliyeenda kufanya vimbwanga huku akijua kuna security cameras.Na wewe hapa unanidai nilete ushahidi huku ukijua nikiitaka hiyo thread at any time nitaileta kwani haijaandikwa kwa Chaki au mkaa ndio ifutwe kwa maji.


Mkuu,tafadhali fanya uungwana tu kabla sijaamua kukupa heshima ya "MKURUPUKAJI NAMBARI WANI JF"
 
Back
Top Bottom