Kutoka Arusha: ITAC - Mkutano wa Kimataifa Kuhusu Uwazi na Uwajibikaji Nchi za Afrika. "Bila Uwazi, Hakuna Uwajibikaji" -Ludovick Utouh

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
itac-2021-conference.png




Wanabodi, niko hapa jijini Arusha, kuwaletea live, kinachoendelea, kwenye mkutano wa kimataifa wa ITAC

ITAC is a brainchild of WAJIBU designed for people to meet and discuss trends on transparency and accountability, sharing best practices, successes and challenges in order to promote an interdisciplinary learning in hastening the transformation process by promoting the culture of transparency and accountability in our societies.

The conference theme is “Transformation to a culture of total transparency and accountability”.

The conference is held from 18th – 19th November, 2021 at the Gran Melia Hotel in Arusha, Tanzania.

Kwa kuanzia, msikilize Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Wajibu, Ludovick Utouh akiuzungumzia mkutano huu.



Bila Kuwepo Uwazi Serikalini, Hakuna Uwajibikaji!- Ludovick Utouh, Aaandaa Kongamano la Kimataifa la Uwazi na Uwajibikaji Afrika.

Mkurungenzi Mtendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Wajibu, Ludovick Utouh, amesema bila ya kuwepo kwa uwazi katika utendaji wa serikali, uwajibikaji hautakuwepo, ili uwajibikaji uwepo, ni lazima kwanza utanguliwe na uwazi, baada ya kuwepo kwa uwazi kwa kila mtu kujua kila kinachofanyika, watendaji watajikuta wanalazimika kuwajibika maana kila kitu kitakuwa kiko wazi.

Utouh ameyasema hayo, jijini Dodoma, katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi, wakati akilitambulisha kongamano la kimataifa la kujadili umuhimu wa uwazi na uwajibikaji katika kusukuma mbele maendeleo, sio tuu ya nchi ya Tanzania, bali maendeleo ya bara lote zima la Afrika.

Bwana Utouh, amesema Kongamano hilo la siku mbili, linafanyikia jijini Arusha, litaanza kesho Alhamisi, tarehe 18 November, 2021 na kumalizika Ijumaa, tarehe 19, November, 2021 ambapo mada mbalimbali kuhusu umuhimu wa uwazi na uwajibikaji, zitawasilishwa na wataalamu wabobevu wa kimataifa kutoka Tanzania, Afrika na Kimataifa.

Bwana Utouh amesema, kongamano hilo lina umuhimu wa kipekee, kwasababu bila kuwa na uwazi katika utendaji kazi serikalini, utendaji unakuwa haupo, na kusisitiza, hoja za uhitaji wa serikali kutenda kazi kwa uwazi, ni takwa la kikatiba, na lipo kwenye katiba ya Tanzania ya mwaka 1977.

Mkutano huu unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 500 kutoka sehemu mbalimbali.

Mgeni rasmi alipaswa kuwa Makamo wa Rais, ila for now, ametuma mwakilishi

Mkutano umeanza, mwakilishi wa mgeni rasmi amewasili, nitaendelea kuwapatia kinachoendelea hapa.

Karibu.

Paskali
 
Pascal

Ukweli ni kuwa Changamoto za msingi kwa walio wengi ni ukosefu wa huduma muhimu za kijamii ikiwemo afya,elimu,maji,umeme, mazingira mazuri ya kupata kipato n.k

Kuwepo kwa uwazi & uwajibikaji bila kupatikana kwa huduma hizo muhimu kwa Wananchi is meaningless

All the same I wish you the best of luck!
 
Pascal

Niwatakie Kila la kheri!

Ila ukweli ni kuwa Changamoto za msingi kwa walio wengi ni ukosefu wa huduma muhimu za kijamii ikiwemo afya,elimu,maji,umeme, mazingira mazuri ya kupata kipato n.k

Kuwepo kwa uwazi & uwajibikaji bila kupatikana kwa huduma hizo muhimu kwa Wananchi is meaningless

All the same I wish you the best of luck!

Sasa hivi hamna uwazi, je hizo huduma ziko kama inavyotakiwa?
 
Mkutano unafunguliwa kwa kuhutubiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAJIBU, Bw. Yona Kilaghane

Ametoa makaribisho kwa kuwakaribisha wajumbe wote kwenye mkutano huu muhimu.

Nikiangalia kwa macho composition ya washiriki, Watanzania ambao lugha yao ni Kiswahili, wako 90%, na wageni, wakiwemo wazungu ni just 10%, ila kwavile huu ni mkutano wa kimataifa, lingua franca ya mkutano huu ni Kiingereza, hivyo Yona Kilaghane anashuka na kizungu, mtanisamehe, sisi tuliosoma St. Kayumba, Kiingereza chetu ni kile tuu cha kuombea maji, hivyo mtanisamehe kushindwa kutafasiri alichoongea Kilaghane.

P
 
Pascal

Ukweli ni kuwa Changamoto za msingi kwa walio wengi ni ukosefu wa huduma muhimu za kijamii ikiwemo afya,elimu,maji,umeme, mazingira mazuri ya kupata kipato n.k

Kuwepo kwa uwazi & uwajibikaji bila kupatikana kwa huduma hizo muhimu kwa Wananchi is meaningless

All the same I wish you the best of luck!
Mkuu Uzalendo Wa Kitanzania , kwanza nakubaliana na wewe kuhusu changamoto za msingi za mwananchi wa kawaida ni huduma muhimu za jamii, chakula, malazi, makazi, afya, elimu na usafiri, maji,umeme, mazingira mazuri ya kupata kipato n.k na sio uwazi na uwajibikaji.

Kitu usichokijua, ni bila uwazi wa kujua how much resources zimekuwa committed kwenye huduma hizo muhimu za jamii, huna uwezo wa kujua kama kuna uwajibikaji au laa na kwanini huduma hizo muhimu za jamii zimekosekana, mfano bila transparence ya kujua how much is allocated to kwenye utoaji huduma za maji, kwanini maji hayatoki, na huwezi kushinikiza uwajibikaji wa mtu yoyote kwasababu hujui chochote.

Mfano Baba amenipa nauli nikuletee wewe upande daladala na pesa ya kumlipa kibarua, kuvuna mihogo, ulete nyumbani tupike, bila transparence ya Baba, kukutuma wewe, na badala yake, baba akanituma mimi ndio nikulee nauli na pesa ya kumlipa kibarua.

Mimi nilipokuja kwako, nikakueleza baba kunituma, wewe uende shambani kwa miguu, uvune mihogo na kuibeba kwenye kiroba, utembee tena kwa miguu kuipeleka nyumbani. Kwa vile wewe hauna info kuwa nina nauli yako na pesa ya kibarua, utakwenda shamba kwa mguu, utamenyeka mwenyewe na utarudi home hoi bin taaban, huku mimi ile nauli yako na posho yako za kibarua, nimeichikichia, na kwenda kuitumbua na Fatuma kwa raha zetu.

Laiti baba angekuwa muwazi kwako kuwa nimemtuma Pasco akuletee nauli na pesa ya kibarua, wewe usingeteseka vile, nilipokutuma, ungelazimisha uwajibikaji kwa upande wangu.

Kuna miradi mindi inabuniwa na kupitishwa, na fedha za utekelezaji wa miradi hiyo, zinatolewa, ila kwa vile hakuna uwazi wa kutosha, fedha hizo zinaishia kutafunwa na kuiingizwa tumboni kwa wenye meno, huku wananchi wakiteseka, laini kungekuwa na uwazi tangu mwanzo, kungekuwa na uwajibikaji zaidi, maana mtoa fedha anasema wazi nimetoa fedha kiasi hiki, kwa ajili ya shughuli hii, mpokeaji nae anakiri amepokea, kinachopaswa kufanyika kisipofanyika, mpokeaji ataulizwa, na kwa vile kila mtu anajua, then, hawezi kithubutu kutafuna hata senti tano!.
P
 
Back
Top Bottom