Sina uhakika kama kasema hayo kwa kuwa source hakuleta conclusive events kuhalalisha mada yake,anyway kasema hakusema, SI SAHIHI kwa Mwanachama au kiongozi yoyote wa CCM kusema tatizo ni UJAMAA. Please kama haya maneno yametoka mdomo mwa mwanaccm No ni HATARI tena kupita HATARI.
ITIKADI YA CHAMA CHA MAPINDUZI ni "UJAMAA NA KUJITEGEMEA"mimi binafsi kama Dotcom Generation sina tatizo na ITIKADI hii au mlengo ambao mwasisi wa Taifa na BABA WA TAIFA aliuanzisha kwa kuzingatia HISTORIA YA YETU WAAFRICA na UTAMADUNI WETU wa kuishi pamoja kama JAMII.
Yeye Mwalimu kama kinara wa ITIKADI hiyo alitumia elimu yake kuunda mfumo wa kuishi wa aina yake [Unique] na aliona waafrika hapo kale waliishi kama jamii moja na mpaka sasa tuna maisha ya kijamaa kuanzia hadhi ya familia [Extended Family] mpaka hadhi kitaifa [Makabila].Leo hii Mhaya anaoa Mkurya, Mpare anao Mhangaza, Mchaga anaoa Mgogo, Mngoni anaolewa na Mmasai,kutoka hapo tunataifa la WATANZANIA ambao lugha ya mama ni KISWAHILI.
DOT COM GENERATION: Ni kizazi cha Mchanganyiko wa makabila], ndio ujamaa wenyewe, ndio mazao ya mfumo huo ambao mwalimu aliusimamia kwa kuzingatia historia. Kwa kuona hilo pia Mwalimu akaongeza KUJITEGEMEA. Kujitegemea huku Mwalimu alitizama Mtanzania ataishi ndani ya jamii yake kama mwanajamaa lakini ataendesha maisha yake kwa kujitegemea huku akipata ushirikiano wa wana jamii yake.
Sikuzaliwa wakati Mwalimu anaanzisha mwelekeo wa Taifa hili, lakini nilimwelewa kupitia elimu ya Historia na sauti ya kulekodiwa [Recorded Speech] ambazo zimejaa ukweli wa maisha kwa kuzingatia ukweli sahihi wa UTU NA HESHIMA YA MWANADAMU.
Nina imani Mwalimu JK Nyerere si kuwa akuwa mdadisi wa mfumo wa KIBEPARI [CAPITALIST] kwa maana ya kuutumikia lakini katika namna inayozingatia mazingira ya kiafrika na sio kwa kukopi kama ulivyo toka ulaya na kuutumikisha kwenye mazingira ya Kiafrika yenye utamaduni na Jadi tofauti na Ulaya. Nafikiri mpaka kifo alichokua anatafuta ni jinsi gani awaelimishe watanzania waweze kuishi katika mfumo wa kujitegemea [Find your own bread una tofauti gani na Ubepari hapa katika njia ya Kiafrika].
Mwalimu JK Nyerere alizingati historia na utamaduni wa Kiafrika, Leo hii viongozi wengi wa Chama na Serikali wanaishi na Mama ama Baba zao majumbani mwao wakiwalea yote hiyo ni kwa sababu ndio jamii ya Kitanzania inavyotakiwa kuishi [Extended Family].[Kwa kukopi Ubepari wanaoukumbatia si wangewapeleka wazazi wao nyumba za kulea wakongwe kama mfumo wa Kibepari unavyojiendesha?]
Hatuitaji kukopi na kutumikisha mfumo wa kibepari [Copy and Paste] tunaitaji kubuni aina ya mfumo huo lakini unaozingatia HAKI na USAWA na mazingira yetu halisi kama Watanzania na Waafika,kama ni mechi ya mpira tunasema Fair Play Game. Kwa kuwa CCM ndio UJAMAA ndio ITIKADI YAKE basi inaangalia HAKI NA UTU WA MWANADAMU vivyo hivyo Serikali inayoundwa na chama hicho,na kuakikisha mlengo huo haupotezi maana bali unazingaia NYAKATI NA ZAMA.Hata leo hii ndoa ya mtoto wa Kifalme Prince Williams ni ya kifalme sawa kihadhi kabisa na ya Baba yake ama Babu yake lakini katika taswira na vionjo vya kisasa kwa kuangalia nyakati na zama za kizazi chake. [Theme ya kizazi chake]. Kama leo hii Morning BBC wanaendelea na Ku-document Royal wedding waingereza na jeuri yao ya kujali chao wamechanganya vionjo vya muziki kwa kudocument vionjo vya wimbo " I WANNA BE A MILLIONARE SO F................BAD NEXT QUEENE and OPRAL", NA Kionjo cha "ITS NOT ABOUT THE MONEY.
CCM KIMEKOSEKANA NINI KWA CHAMA CHA MAPINDUZI NA SERIKALI YAKE? Kuendeleza ITIKADI YAKE YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA KWA KUZINGATIA NYAKATI NA ZAMA MPYA.
Napata shida kuona wafuasi wa Mwalimu alioafundisha awafuati maelekezo yake na wameitupa ITIKADI ya CHAMA CHA MAPINDUZI. Leo hii Dot Com Generation, wanavyomwelewa na kukubali maelekezo yake, wazee hawa [TYPEWRITER GENERATION] wanajisikiaje kuona watoto na wajukuu zao wakiimba ''Kama sio juhudi zako Nyerere na nanii....................angesoma wapi? Kumbe Dotcom Generation wanajua ni bidii binafsi za mawazo ya Mwalimu kujenga Taifa lenye jukumu la kujenga UJAMAA kwa kutambua JAMII inajukumu la Kulea,Kusomesha, Kujali na kutambua jamii yatakiwa kuishi kwa kujaliana na kuheshimu binadamu mwingine hata kama kuna tofauti ya vipato.
Leo hii omba omba mitaani,serikali ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA kumilki ombaomba mpaka wa umri wa miaka minne [4] ni HATARI ZAIDI YA HATARI. Kwani kwa ITIKADI YA UJAMAA ,omba omba ni jukumu la Serikali [Basi tungekopi kwa mabepari tungesema state property] vyote hivyo hatupo.
Mwalimu ansasema unapokua unataka Uraisi ni kutaka Matatizo sio Neema,"Ikulu kuna nini?Ikulu ni Mzigo wa Matatizo,Unapita Mabarabarani huko Wananchi wako wanashida, shida za wananchi hao ni mzigo wako wewe".
Kwa mantiki hiyo kama KWELI Viongozi wa CCM ndani ya mioyo yao dhamila yao si kuendeleza TAIFA LA UJAMAA lenye mfumo wenye kuzingatia mazingira halisi ya Mtanzania wa leo na nyakati alizopita na zinazokuja, basi KWELI NITAANZA KUAMINI JAPO, NILIKUA SIAMINI KIFO CHA CCM [RISE AND FALL PRINCIPLE ILISHAANZA KUFANYA KAZI ZAMANI NA INAKARIBIA MWISHO NAFIKIRI]