Kikwete adai tatizo ni ujamaa!

mindset za wananchi zimejazwa ghilba za chuki na majungu na wanasiasa; watu hawafanyi kazi na kama wanafanya hawafanyi kwa bidii na ufanisi.
Waliopewa dhamana wanajiona waungu watu (serikalini, taasisi za umma na binafsi na katika vyama vya siasa. Umaskini utaondokaje?


Watu watafanyaje kazi kwa ufanisi kama hawalipwi vizuri?Serikali yenyewe ndiyo inafanya watu wake wawe wavivu na wazembe.Mtu anafikiria kwanini aenyeke ofisini kwa mshahara kiduchu huku wengine ni mabilionea bila kutoka jasho.Chanzo cha yote haya ni Serikali kushindwa kupambana na rushwa na ufisadi.Na ndiyo point ya August kama nimemuelewa vizuri kuwa tatizo siyo ujamaa wala ubepari bali ni uongozi dhaifu.
 
Mbona tayari mie dokta, na totoz wa kizungu nawa operate vizuri tu na hajafa hata mmoja. Sasa tuhuma zako hazina msingi maana nakubalika kama dokta.

ok, achana na hayo, ninachokiona ni kwamba watu wanayatazama mambo kama yalivyo bila kujali mazingira shilikishi, watu hawaangalii mazingira ya kipindi cha mwalimu, watu wanasahau kama uchumi uliyumba, watu wanasahau kwamba tulipigana vita pamoja n akuzisaidia nchi kama msumbiji kupata uhuru, pamoja na kukosa watalamu kwani ndo tulikua tunaanza kujenga nchi uku wananchi almost wote walikua hawajui maana ya utaifa, hivyo sera ya ujamaa kwa kuanzia kuweka misingi ya utaifa Nyerere alikua sahihi kabisa.

Hivi mnazani Kikwete angeipokea nchi kutoka kwa wakoloni saizi tungekua wapi??? tukisema ''tulipata viongozi waadilifu lakini bado tulikua
masikini'' ni kauli sahihi lakini inaficha mambo mengi, ambayo yangeambatanishwa yangejenga taswira sahihi zaidi.

Hakuna tatizo lisilokuwa na uhusiano na mazingira usika, lazima tuelewa mazingira yetu sisi kama watanzania then tatafute solution ya matatizo yetu kwa njia na mifumo inayoendana na mazingira yetu, na siyo tu kuanza kutaja mifumo ya wenzetu bila kujali mazingira yetu.
 
Watu watafanyaje kazi kwa ufanisi kama hawalipwi vizuri?Serikali yenyewe ndiyo inafanya watu wake wawe wavivu na wazembe.Mtu anafikiria kwanini aenyeke ofisini kwa mshahara kiduchu huku wengine ni mabilionea bila kutoka jasho.Chanzo cha yote haya ni Serikali kushindwa kupambana na rushwa na ufisadi.Na ndiyo point ya August kama nimemuelewa vizuri kuwa tatizo siyo ujamaa wala ubepari bali ni uongozi dhaifu.

unataka kusema TRA hawalipwi vizuri? EWURA? ATC?

Uongozi dhaifu unatokana na kuwa na taifa lenye watu dhaifu. Kama wananchi dhaifu unadhani viongozi madhubuti wanatoka sayari Jupiter au Gambia? Lazima watoke kwenye jamii hiyo hiyo.
 
Mkandara
Naona hujapata jiswi na chengu siku nyingi.
Wewe unakubali kabisa mfumo wa kikoministi/ujamaa ndo umewanufaisha viongozi harafu ukifika kwa Tz unapaa vihunzi.Kifupi mfumo ndo huo huo ndo maana utaona viongozi wa kikoministi/ujamaa ndio hao hao wanaomiliki na watoto wao na kudhibiti wengine.

Ukijichanganya mitaani na ukafanya kazi ndo utagundua ukoministi/ujamaa ni tatizo kuu kwa vizee vya Tanzania, mie nimefanya kazi bongo kama fundi mchundo lakini lilikuwa tatizo kubwa sana kwa vizee vya VETA.

Ulaya magharibi hakuna ukoministi/ujamaa wala sidhani kama kuna chama chochote kinachofuata ukoministi/ujamaa kule kuna u-coservative , u-liberali nk.
Mkuu haiendi hivyo hata kidogo,ifike mahala unisome nachoandika badala ya kurudia kitu kile kile..Matajiri wote nchi za Kimomunist sii viongozi wao bali Matajiri hata nchi za Kibepari ni koo zile zile za Kiutawala toka kwa Malkia,Mubarak hadi kwa Kenyatta na kina Kamuzu Banda...Lakini maajabu ni kwamba tunawakuta maskini viongozi ktk Ukomunist koo za kina Nyerere, Nasser, Haile Mariam, Samora na wengineo hivyo usitake kujumuisha kila kitu ili kuleta maana ya ujumla.

Nimesema ni kweli utawala wa Kikomunist ulikuwa na mabaya yake ingawa ,malengo yalikuwa mazuri na wataalam wote wa kiuchumi wanakubaliana kwamba Ujamaa ktk mazingira na tabia za binadamu hauwezi kufanya kazi kama kama vile ZBiblia na Kuran zinavyopinga Utajiri kwa kutumikisha wengine. na ifahamike kwamba Ubepari sii mfumo unaokubali utumwa au kuwatumia watu kama ngazi.
Ujamaa unaozungumziwa hapa sio ule unaopinga watu binafsi kumiliki njia kuu za uchumi au kuhodhi mali bali ni Fikra zinazopinga Ukoloni mamboleo kuwa ni sehemu ya Ubepari na ndio utaratibu unavyotakiwa.

Msome vizuri JK na upate kuelewa kwamba watumishi wa Umma wanakuwa na chuki au wivu wanapokuja WAWEKEZAJI wakifikiria kwamba ni wezi, hivyo tuhuma nzima za JK hazihusiani na Ujamaa unaotaka maisha bora kwa kila mwananchi kupitia itikadi na sera zinazoiwezesha serikali kufikia malengo hayo. Na JK hakueleza wazi kama fikra za kibepari anazozipongeza ni zipi dhidi ya Ubepari ambao unatumika leo hii kwa sababu kumtuhumu mtu mwizi ina maana WIZI upo na kuna watu wa naina fulani ndio wanatuhumiwa kwa wezi..
je JK kafanya utafiti kufahamu kwa uhakika kwamba hao wawekezaji sio wezi isipokuwa ni wananchi ndio wenye mawazo na fikra za Kijamaa? je ni Ujamaa unaposhuku rasilimali za nchi kuibiwa na wageni wawekezaji ikiwa hakuna policies zozote zinazolinda mali za wananchi hao..Je ni fikra zipi za Kibepari zinazokubali wawekezaji pasipo safety measures kuwa moja ya taratibu za kudhibiti uhalifu?..

Leo hii mkuu wangu ndani ya Ubepari huwezi kuondoka na Dollar elfu kumi (10,000) Marekani, UK au Canada pasipo kupata kibali lakini unaweza kuondoka/au kuingiza mamillioni Tanzania na tusione tatizo la moneylaundry lkwa sababu utajiri ni wako wewe mwananchi has nothing attached to rule and regulations hata kama hazikulipiwa kodi au zimepatikana kinyume cha sheria...

Mkuu wangu ni wivu na Ujamaa kuulizia kwa nini Barricks wanatupa ruzuku ya asilimia 3 wakati Sinclair akichukua 1.9 ya ruzuku hiyo zetu kwa matangazo na kuinadi migodi yetu..Ni Ujamaa kupinga Ufisadi wa kina Lowassa, JK, Chenge, Mkapa na wengineo kwa sababu wote tuna fikra finyu za chuki watu wengine wanapoendelea.

Na ajabu ya Mungu ni kwamba hawa viongozi ndio wanawatuhumu wananchi na watumishi wa serikali kuwa Waajamaa hali wao viongozi ndio wamekuwa ndani ya Ujamaa na kuutumikia miaka yao yote ya ajira iweje wao wasiwe Wajamaa ila kizazi hiki ambacho kimezaliwa wakati wa Mwinyi maanake ndio wengi utawakuta ktk sekta za uwekezaji, kodi na kuhamasisha wawekezaji..

Sisi hatutaki ku face reality, tunatafuta mchawi kila siku hali UZEMBE mkubwa umetokana na mfumo mzima wa kuiga ku nya kwa Tembo na sasa msamba unapasuka tunajiuliza kama ni uzembe wetu, fikra za Kijamaa na kadhalika hali Ubepari unakwenda na uwezo wenu, yaani tunajipima suti kulingana na mwili wetu ingawaje mshono ni ule ule..Sisi maskini hatuwezi ku apply policies za nchi za nje wala hatuwezi kuendelea kuomba na kupewa masharti hali dunia ya leo ni ya Utandawazi na soko huria.

Tunatakiwa kuwa part of the mzunguko wa kibiashara na sii watumwa ndani ya mfumo huu na ndio maana tume fail na kilichobakia ni kulana sisi wenhyewe..Tanzania imegeuka kuwa uwanja wa mwenye nguvu ndiye atakula nyama, na hii haitokani na Ujamaa bali tumekosa mambo muhimu sana ktk maendeleo ya nchi - UONGOZI BORA...
 
Watu watafanyaje kazi kwa ufanisi kama hawalipwi vizuri?Serikali yenyewe ndiyo inafanya watu wake wawe wavivu na wazembe.Mtu anafikiria kwanini aenyeke ofisini kwa mshahara kiduchu huku wengine ni mabilionea bila kutoka jasho.Chanzo cha yote haya ni Serikali kushindwa kupambana na rushwa na ufisadi.Na ndiyo point ya August kama nimemuelewa vizuri kuwa tatizo siyo ujamaa wala ubepari bali ni uongozi dhaifu.
Hata wewe ukiwa kiongozi huwezi kutembea na pingu....TUKURURU ni kina nani?..na wamefanya nini hasa? I personally know a bunch of them!
 
Ukiritimba ndiyo tatizo na si ujamaa.Kwani si wabadili to procedures ili kuondoa ukiritimba?Mlolongo wa process na mipaper work isiyo na kichwa wala miguu ndiyo inayoondoa ile efficiency ambayo inajenga mazingira ya rushwa...Kila kitu bongo ni rushwa,everything,hakuna pahala pasipo na rushwa bongo.Ni mfumo wa rushwa ndiyo tatizo na si ujamaa.
Ujamaa labda ni kikwazo kwa wananchi na si viongozi,kwasababu wao wanagawana mali za umma kwa kudai ubinafsishaji.Nyumba za serikali kwa vigezo hivyo hivyo.Migodi nk.Sikutegemea maneno hayo haya yangezungumzwa na mkuu.Yanaonyesha kutofahamu kabisa matatizo ya wananchi na taifa kwa ujumla.Huwezi ukawa unafahamu matatizo ya nchi na wananchi halafu ukaongea maneno kama hayo.

Ahsante sana Mkuu kwa maneno yaliyojaa hekima na busara ya hali ya juu.
 
unataka kusema TRA hawalipwi vizuri? EWURA? ATC?

Uongozi dhaifu unatokana na kuwa na taifa lenye watu dhaifu. Kama wananchi dhaifu unadhani viongozi madhubuti wanatoka sayari Jupiter au Gambia? Lazima watoke kwenye jamii hiyo hiyo.

Ok TRA wanalipwa vizuri.Walimu je?Madaktari je?Unafikiri wanajisikiaje watu muhimu kama hawa wanaposikia kuwa mishahara yao inalingana na wapiga deki wa TRA??
Wala usiwalaumu watanzania kuwa ni dhaifu kwavile wanachagua viongozi dhaifu.Wengi wanachokikosa ni elimu ya kuwazibua masikio yao ili wazijue haki zao na umuhimu wa kura zao na kwamba umasikini wao unasababishwa na viongozi dhaifu.Mnafanya demokrasia ya magharibi wakati wapiga kura hawako well informed,unategemea nini?Na huu ndiyo mtaji mkubwa wa viongozi wetu
 
unataka kusema TRA hawalipwi vizuri? EWURA? ATC?

Uongozi dhaifu unatokana na kuwa na taifa lenye watu dhaifu. Kama wananchi dhaifu unadhani viongozi madhubuti wanatoka sayari Jupiter au Gambia? Lazima watoke kwenye jamii hiyo hiyo.

Nimependa jinsi uonavyo mambo na jinsi unavyoyaelezea. Haurembi rembi.
 
Kama hayo maneno ni kweli, basi hata mimi naunga mkono kauli hiyo. Siasa ya Ujamaa ni Zimwi linalo wasumbua viongozi wengi walioko madarakati.

Kiasi viongozi wengi wamekuwa waoga kiasi cha kukimbia vivuli vyao.


Mhhhh! Nyerere kang'atuka 1985 miaka 26 iliyopita na waliomfuatia baadaye walijaribu kwa kasi sana kuachana na siasa za ujamaa na kutoiheshimu miiko ya Viongozi na maadili mbali mbali ya awamu ya Mwalimu na hata kulivunja Azimio la Arusha. Sasa baada ya miaka 26 ya kung'atuka kwa Mwalimu bado tunataka kuendelea kulaumu sera za Mwalimu za ujamaa na kujitegemea kwa madudu mbali mbali yaliyofanywa na Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete!? Mtamsingizia Mwalimu kila kitu kibaya hata vile ambavyo hastahili kabisa kulaumiwa.
 
Ok TRA wanalipwa vizuri.Walimu je?Madaktari je?Unafikiri wanajisikiaje watu muhimu kama hawa wanaposikia kuwa mishahara yao inalingana na wapiga deki wa TRA??
Wala usiwalaumu watanzania kuwa ni dhaifu kwavile wanachagua viongozi dhaifu.Wengi wanachokikosa ni elimu ya kuwazibua masikio yao ili wazijue haki zao na umuhimu wa kura zao na kwamba umasikini wao unasababishwa na viongozi dhaifu.Mnafanya demokrasia ya magharibi wakati wapiga kura hawako well informed,unategemea nini?Na huu ndiyo mtaji mkubwa wa viongozi wetu

Kama watanzania sio wadhaifu watachaguaje viongozi dhaifu? unataka kuniambia viongozi dhaifu wanatoka mbinguni?

Viongozi ni miongoni mwananchi. Kama wananchi ni dhaifu lazima viongozi watakaopatikana ni dhaifu.
 
Mi nadhani hawa jamaa hawajui nini maana ya ubepari ndio maana kuna confusion within as a result we get the staggering economy.

Hiwe ujamaa hiwe ubepari uchumi hauwezi kukua kama watu hawana hela, the only way most people could get money is through employment. Na ajira ni zao la viwanda au uzalishaji wowote kibiashara. Sasa kama unataka watu waajiri watu halafu unaweka vikwazo kadamnasi kwenye kufungua biashara mpya ni tatizo.

Pili kuna baadhi wanaweza kuwa na mawazo mazuri na business plans lakini wanakosa investment. The option is to go through the banks na hizo interest za benki za Tanzania ni utani mmbaya. Hili ni tatizo kubwa kwa watu mafukara wenye kutaka kujaribu business ventures sasa sijui hizo ajira zitatoka wapi hiwapo viwanda vyenyewe vya serikali vinakufa na amna mipango mingine.

Tunategemea madini sijui mashamba kupata pato la taifa, if you ask me this is just pathetic put an environment where starting a business shouldnt be so difficult and maintaing the bussiness. Maana ushuru kwa kweli nao ni hatari, sasa hili linafanya watu waanze na bei za ajabu. Si ajabu its cheaper to import for most retailers than being encouraged to manufacture on their own.

Im telling you these guys Mkullo and Ndullu should be fired, lets just say they are useless.
 
Kama watanzania sio wadhaifu watachaguaje viongozi dhaifu? unataka kuniambia viongozi dhaifu wanatoka mbinguni?

Viongozi ni miongoni mwananchi. Kama wananchi ni dhaifu lazima viongozi watakaopatikana ni dhaifu.

wewe unaamini katika watanzania wote karibu 40M,hakuna kiongozi mzuri hata mmoja?tatizo siyo udhaifu wa wananchi,tatizo udhaifu wa viongozi kuwaandalia wananchi mazingira mazuri ya kuwawajibisha wanapoboronga
 
mimi kikwete akiongea kitu kwa mara ya kwanza hua sishituki maana najua kuna remix inafuata sasa nyie pigeni kelele lakini kesho kesho kutwa hatayakana haya maneno,
nani hasiyejua kwamba kikwete aliwambia mbayuwayu kwamba kima cha chini wanachotaka hakilipiki hata baada ya miaka minane, lakini jana kakikubali, wakati wa kampeni alisema hata kura za mbayuwayu kilichofuta.......
..kwa kweli inachanganya mwenyekiti wa chama kinachofuata itikadi ya UJAMAA na KuJITEGEMEA anapotoa kauli kama hizi.

..hivi inawezekana tukawa na chama tawala cha kijamaa lakini serikali yake ikawa ya kibepari?
 
Wananchi hao hao unaosema tusiwalaumu ndo wanaichagua serikali na kuchagua wawakilishi wao. Wanastahili wanachopata.
Hawastahili wanachokipata kwasababu mfumo unaowapatia viongozi hao tayari una wa betray hence viongozi ambao pia wanawa betray wananchi kwasababu wanajuwa iwe iweje madaraka ni yao,ni kama wameyahodhi,wana uhakika na utawala wao,hawaogopi kufanya chochote na wako juu ya sheria,usidhani mwananchi wa kawaida ana sauti kihivyo ndani na nje ya siasa za bongo...Again,i firmly believe serikali haijawajengea wananchi mazingira ya kujiendeleza.Huo ni wajibu wake namba moja.Serikali inatakiwa iwe facilitators wa maendeleo ya wananchi,inapokuwa kinyume na hapo ndo mambo kama haya...Umasikini uliokithiri.
 
Kama watanzania sio wadhaifu watachaguaje viongozi dhaifu? unataka kuniambia viongozi dhaifu wanatoka mbinguni?

Viongozi ni miongoni mwananchi. Kama wananchi ni dhaifu lazima viongozi watakaopatikana ni dhaifu.
Wananchi dhaifu sii sababu ya kuwa na Watawala dhaifu, bali hawa wananchi ni mazao ya utawala dhaifu... hivyo matunda yake lazima yawe yamenyauka kama ulivyo uchumi wetu....Waswahili wanasema mtoto umleavyo ndivyo akuwavyo, hii haina maana mzazi utamlea mtoto kutokana na juhudi zake bali wewe mzazi ndiye kiongozi unayejua na ku vision unataka mtoto wako apate malezi gani.

Amini maneno yangu, kesho ukiwaleta viongozi wa Ulaya wakaishika TZ kwa miaka mitano tuu utaona tofauti kubwa na watu hawahawa unaowaona wazembe watanyooka.. kwa sababu mikakati ya sheria na policies zao zitalenga na zitaondoa uzembe, kwaniwenzetu wana invest vitu kulingana na kile ulichonacho..na sii maisha ya Mzaire anayelala na kuishi Manzese kwa Mguga Mbwa lakini akiendesha Vogue.

Mimi nadhani tuna tatizo kubwa la kuelewa, viongozi wetu hawana vision, hawana malengo isipokuwa Kutawala kama vile tunavyopenda kuzaa na kuoa wake wengi pasipo kujua majukumu ya mzazi au mume.. Ni hulka ambayo utaitafsiri tu ikiwa mtu kafika stage ya Uongozi au Uzazi na kibaya zaidi hatuna mifano bora isipokuwa ile ya kutawaliwa.
 
mkuu sio kweli kwamba wananchi walimchagua kikwete, kikwete kachaguliwa na tume ya uchaguzi na katiba mbovu tuliyonayo,wakati wa uchaguzi serilika inakusanya wafanyakazi wake waaminifu kwayo kwenda kusimamia uchaguzi unategemea nani ashinde? kama sio rais wa wakati huo
Kama watanzania sio wadhaifu watachaguaje viongozi dhaifu? unataka kuniambia viongozi dhaifu wanatoka mbinguni?

Viongozi ni miongoni mwananchi. Kama wananchi ni dhaifu lazima viongozi watakaopatikana ni dhaifu.
 
Back
Top Bottom