Kikwete adai tatizo ni ujamaa!

Mhhhh! Nyerere kang'atuka 1985 miaka 26 iliyopita na waliomfuatia baadaye walijaribu kwa kasi sana kuachana na siasa za ujamaa na kutoiheshimu miiko ya Viongozi na maadili mbali mbali ya awamu ya Mwalimu na hata kulivunja Azimio la Arusha. Sasa baada ya miaka 26 ya kung'atuka kwa Mwalimu bado tunataka kuendelea kulaumu sera za Mwalimu za ujamaa na kujitegemea kwa madudu mbali mbali yaliyofanywa na Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete!? Mtamsingizia Mwalimu kila kitu kibaya hata vile ambavyo hastahili kabisa kulaumiwa.
Mkuu platform ya siasa za Tanzania ni ile ile, viongozi ndio wale wale waliokuwa pamoja na Nyerere.

Kinacho fanyika ni huyu kuingia chama iki huyu kuhama chama kile.

Hapa tunajifariji tu kushabikia vyama tofauti tofauti.

Nahisi labda watoto watakao zaliwa baada ya Urais wa kikwete ndio watakao ikomboa Tanzania.
 
Hawastahili wanachokipata kwasababu mfumo unaowapatia viongozi hao tayari una wa betray...Again,i firmly beleive serikali haijawajengea wananchi mazingira ya kujiendeleza.Huo ni wajibu wake namba moja.Seriiali inatakiwa iwe facilitators wa maendeleo ya wananchi,inapokuwa kinyume ndo haya.

Kama hawastahili wanachopata kwa nini wasi-take their country back? Kama hawastahili wanachopata kwa nini hao viongozi licha ya kuharibu, kila wanakokwenda pretty much wanapewa red carpet treatment?

Si umeona Tunisia walivyowatolea uvivu viongozi wao?
 
Kama hawastahili wanachopata kwa nini wasi-take their country back? Kama hawastahili wanachopata kwa nini hao viongozi licha ya kuharibu, kila wanakokwenda pretty much wanapewa red carpet treatment?

Si umeona Tunisia walivyowatolea uvivu viongozi wao?
NIDHAMU YA WOGA mkuu wangu, siasa ni mchezo mchafu sana unaweza hata mkataa mama yako mzazi ukiambiwa ni mchawi..
 
Kama hawastahili wanachopata kwa nini wasi-take their country back? Kama hawastahili wanachopata kwa nini hao viongozi licha ya kuharibu, kila wanakokwenda pretty much wanapewa red carpet treatment?

Si umeona Tunisia walivyowatolea uvivu viongozi wao?


Hata hivyo vyama mbadala vmeshindwa kabisa kuja na sera mbadala za kulikomboa taifa kutoka kwenye umaskini.

Hii ni evidence kwamba viongozi dhaifu ni zao la wananchi, taifa dhaifu, lenye siasa lakini halina ideology.

Maneno mengi utekelezaji sifuri.

NIDHAMU YA WOGA mkuu wangu, siasa ni mchezo mchafu sana unaweza hata mkataa mama yako mzazi ukiambiwa ni mchawi..

wananchi dhaifu ndio wanakuwa na nidhamu ya woga.
 
Kama hawastahili wanachopata kwa nini wasi-take their country back? Kama hawastahili wanachopata kwa nini hao viongozi licha ya kuharibu, kila wanakokwenda pretty much wanapewa red carpet treatment?

Si umeona Tunisia walivyowatolea uvivu viongozi wao?
Naelewa lakini hiyo ni a different way of fighting for a cause.Mfano wakati wa upiganiaji uhuru,nchi nyingine zilimwaga damu,nyingine hazikfanya hivyo.Kila nchi ilikuwa na njia zake za tofauti za kupambana na wakoloni.Inategemea na jamii na historia pamoja na culture zake.
Kwahiyo basi kama dola ndiyo tatizo,na kama bado litaendelea kuwa tatizo,then people will find the way to overcome when the right situations arrives.
Kupewa red carpet watapewa kwenye maeneo ambayo wana ushawishi,ndiyo siasa zilivyo.Hata Saddam kule Tikriti angekuwa hai leo hii wangemwekea red carpet.Kuwa na wafuasi na kuwekewa red carpet siyo shida,shida ni kama kuna ukweli wa hapo unapodai kuwa ni kila wanapokwenda wanapewa red carpet treatment,i certainly dont agree with you sir,Mkapa alikuwa akizomewa na JK nasikia huko Mbeya waliompopoa mawe.
Kuwa wana influence?yes,kwenye circles zao?even more.
 
Mkuu platform ya siasa za Tanzania ni ile ile, viongozi ndio wale wale waliokuwa pamoja na Nyerere.

Kinacho fanyika ni huyu kuingia chama iki huyu kuhama chama kile.

Hapa tunajifariji tu kushabikia vyama tofauti tofauti.

Nahisi labda watoto watakao zaliwa baada ya Urais wa kikwete ndio watakao ikomboa Tanzania.

Hapo kwenye nyekundu Nyerere hakuwa fisadi wala mroho wa utajiri wa haraka haraka na siku zote aliweka maslahi ya Watanzania mbele. Sasa kama hawa Viongozi tuliokuwa nao ndio wale wale waliokuwa na Nyerere mwenye maadili, mwenye kutetea maslahi ya Tanzania na Watanzania iweje tena hawa wawe tofauti na Mwalimu na hivyo kutoheshimu maadili ya uongozi, kuweka mbele maslahi ya matumbo yao na utajiri wa haraka haraka, kusaini mikataba chungu nzima (uchibbaji wa dhahabu, ununuzi wa Rada, magari ya jeshi na helicopters, ndege ya Rais, Dowans/Richmond, Kiwira Coal Mining, Net Group Solutions n.k.) ambayo haina maslahi kwa Watanzania (ambayo Nyerere kamwe asingekubali kuisaini)
 
Naye Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alisema si rahisi kuwarudisha mawaziri darasani ila wanachopaswa kufanya ni kubadili fikra, ili kwenda na wakati na kuachana na tabia za urasimu.

Rais Kikwete alisema ujamaa ndio umesababisha watumishi wengi wa serikali kuona ubepari kama uadui hivyo hata mtu anayetaka kuja kuwekeza anasumbuliwa hadi anaamua kuondoka.

“Kweli ujamaa ndio umetufanya tuone ubepari ni dhambi hivyo mwekezaji akija anaangaliwa kama vile mwizi, na hilo linafanya wawekezaji wengine kuamua kwenda kutafuta sehemu zingine za kuwekeza, sisi serikalini tumeligundua hilo na ndo maana tumeanza mkakati wa kuajiri vijana wengi zaidi wenye fikra mpya katika nafasi mbalimbali,” alisema Rais Kikwete.

“Bado kuna tatizo la watumishi kubadili fikra ili watekeleze maono yetu, hilo tunapambana nalo kweli kweli ili twende na dunia ya sasa, ila kuwarudisha darasani hapana,” alisema Rais Kikwete na kusababisha kicheko.

Tatizo si Ujamaa, Ujamaa ulikufa 28 yrs ago.....Tatizo ni kama walivyosema UVCCM kila mtu anatafuta 20% hawajali manufaa kwa nchi...

Sasa kama wewe ulivyowaleta Sinclair and co utategemeaje watumishi wafanye tofauti....ama kweli kama asemavyo Nyani Gabu "MIAFRIKA NDIYO ILIVYO
"
 
Hata hivyo vyama mbadala vmeshindwa kabisa kuja na sera mbadala za kulikomboa taifa kutoka kwenye umaskini.

Hii ni evidence kwamba viongozi dhaifu ni zao la wananchi, taifa dhaifu, lenye siasa lakini halina ideology.

Maneno mengi utekelezaji sifuri.



wananchi dhaifu ndio wanakuwa na nidhamu ya woga.
Kwa hiyo ni swala la kiimani..Unafikiri Rwanda na Uganda leo wamepata viongozi shupavu kwa sababu wananchi wake ni mashupavu?
 
Kwa hiyo ni swala la kiimani..Unafikiri Rwanda na Uganda leo wamepata viongozi shupavu kwa sababu wananchi wake ni mashupavu?

of course, huwezi kuwa la Taifa lenye wananchi shupavu halafu likachagua, na zaidi lilakubali kuongozwa na viongozi dhaifu.

Na M7 unaamini ni kiongozi shupavu, nae dhaifu tu anaongoza wananchi dhaifu waliomchagua.
 
Hapo kwenye nyekundu Nyerere hakuwa fisadi wala mroho wa utajiri wa haraka haraka na siku zote aliweka maslahi ya Watanzania mbele. Sasa kama hawa Viongozi tuliokuwa nao ndio wale wale waliokuwa na Nyerere mwenye maadili, mwenye kutetea maslahi ya Tanzania na Watanzania iweje tena hawa wawe tofauti na Mwalimu na hivyo kutoheshimu maadili ya uongozi, kuweka mbele maslahi ya matumbo yao na utajiri wa hataka haraka, kusaini mikataba chungu nzima ambayo haina maslahi kwa Watanzania (ambayo Nyerere kamwe asingekubali kuisaini)
Ufisadi walikuwa nao sana tu, leo hii tunasikia majina yao, only because tuna uhuru kidogo na vyombo vya habari, lakini enzi hizo hatukuweza kuyasikia haya kwa sababu vyombo vyote vya habari vilimilikiwa na chama na serikali.
 
of course, huwezi kuwa la Taifa lenye wananchi shupavu halafu likachagua, na zaidi lilakubali kuongozwa na viongozi dhaifu.

Na M7 unaamini ni kiongozi shupavu, nae dhaifu anaongoza wananchi dhaifu.
nakumbuka Nixon, Johnson na Jimmy Carter wanasemekana kuwa ndio viongozi dhaifu waliowahi kutawala Amerika, ndio kusema Waamerika walikuwa wadhaifu wakati wakiwachagua viongozi hao au?
 
Ufisadi walikuwa nao sana tu, leo hii tunasikia majina yao, only because tuna uhuru kidogo na vyombo vya habari, lakini enzi hizo hatukuweza kuyasikia haya kwa sababu vyombo vyote vya habari vilimilikiwa na chama na serikali.

Ufisadi unaodai kuwepo huwezi kulinganisha na huu wa sasa.......Kama ulikuwepo ulikuwa chini sio mpaka IKULU......
 
nakumbuka Nixon, Johnson na Jimmy Carter wanasemekana kuwa ndio viongozi dhaifu waliowahi kutawala Amerika, ndio kusema Waamerika walikuwa wadhaifu wakati wakiwachagua viongozi hao au?

Udhaifu wa viongozi wa Marekani ni tofauti. Na kwanza kati ya hao uliowataja ni wangapi walichaguliwa kuongoza kwa mihula miwili?
 
nakumbuka Nixon, Johnson na Jimmy Carter wanasemekana kuwa ndio viongozi dhaifu waliowahi kutawala Amerika, ndio kusema Waamerika walikuwa wadhaifu wakati wakiwachagua viongozi hao au?


I am conversant with neither American history nor politics.
 
Ufisadi walikuwa nao sana tu, leo hii tunasikia majina yao, only because tuna uhuru kidogo na vyombo vya habari, lakini enzi hizo hatukuweza kuyasikia haya kwa sababu vyombo vyote vya habari vilimilikiwa na chama na serikali.

Kama upi Mkuu!? Hebu ufafanue ufisadi uliofanywa wakati wa awamu ya Mwalimu na kuwaneemesha wale waliokuwa madarakani na hatimaye kuwa mabilionea. Tulikuwa tunasota nao mtindo mmoja katika mashule yetu ya bongo kuanzia msingi hadi vyuoni na walikuwa wanaishi maisha ya kawaida kabisa, lakini leo hii wamejikusanyia utajiri wa hali ya juu kupitia ufisadi na hata shule zetu hawakanyagi tena. Pamoja na kuwa hakukuwa na uhuru wa vyombo vya habari lakini tulikuwa tunawaona kwamba maisha yao hayakuwa na tofauti kubwa sana na Watanzania wengi kama ilivyo sasa ambapo wengi wa mafisadi hao ni mabilionea kwa kupitia njia za haramu.
 
Udhaifu wa viongozi wa Marekani ni tofauti. Na kwanza kati ya hao uliowataja ni wangapi walichaguliwa kuongoza kwa mihula miwili?
Mkuu wangu udhaifu hauna muhula mmoja wala miwili, Johnson alikuwa makamu wa rais na kuwa rais.. Nina kama hawa jamaa zetu ndio mashupavu wasingemwezesha Nixon na Johnson kutawala..

Kweli kabisa siwezi kufananisha Marekani na Tanzania kwa sababu wenzetu wanafuata vigezo vya mgombea kabla hajagombea kuwa sababu ya kumpa uongozi wakati sisi tunachagua sura...

Hivyo maana yangu haswa ni kwamba mfumo mzima wa kiutawala unaomwezesha mtu Popular bila kigezo ila umaarufu wa mitaani kuwa rais ndio tatizo letu zaidi ya wananchi kuwa wadhaifu..Kisha basi hata wale wenye uwezo wa kiutawala hawafiki tk mchakato wa kitaifa kwa sababu mfumo wetu wa kiutawala ni wa kichama zaidi ya mgombea...

Pengine naweza kusema hapa ndipo Ujamaa unapoingia na ulaumiwe, kwani bado kabisa tunatumia mfumo wa chama kimoja kupata viongozi wetu.. Salim A salim alienguliwa kwa rangi yake, Kigoda alienguliwa tu kwa kusema mzee wa kaya ana mdudu! Mwandosya hapendeki kwa sababu ni Mnyakyusa na kadhalika, hivyo mchakato unaanza ndani ya vyama na tunacholetewa mezani ni chakula ambacho tayari kimeisha pikwa. U only have one choice to choose from - JK, Mbowe, Lipumba, Mrema ambao wote ni maarufu ndani ya chama na sii ktk utendaji kazi wao..Kifupi wananchi hawana choice a viongozi bali wanapitisha moja kati ya majina waliyoletewa..
 
Kama upi Mkuu!? Hebu ufafanue ufisadi uliofanywa wakati wa awamu ya Mwalimu na kuwaneemesha wale waliokuwa madarakani na hatimaye kuwa mabilionea. Tulikuwa tunasota nao mtindo mmoja katika mashule yetu ya bongo kuanzia msingi hadi vyuoni na walikuwa wanaishi maisha ya kawaida kabisa, lakini leo hii wamejikusanyia utajiri wa hali ya juu kupitia ufisadi na hata shule zetu hawakanyagi tena. Pamoja na kuwa hakukuwa na uhuru wa vyombo vya habari lakini tulikuwa tunawaona kwamba maisha yao hayakuwa na tofauti kubwa sana na Watanzania wengi kama ilivyo sasa ambapo wengi wa mafisadi hao ni mabilionea kwa kupitia njia za haramu.
Mkuu yaani ujui kabisa kama kulikuwa na wati ambao wakifirisi hapa wanahamishwa pale?

Kusoma na watoto wa viongozi si vigezo kuwa baba zao hawakuwa mafisadi, tatizo tu ni kuwa viongozi walikuwa wanaabudiwa sana, na maisha ya wakati huo wa ujamaa, ukionekana upo tofauti na wengine, cha moto utakiona...! Yaani walijuwa kula na vipofu.
 
Mkuu yaani ujui kabisa kama kulikuwa na wati ambao wakifirisi hapa wanahamishwa pale?

Kusoma na watoto wa viongozi si vigezo kuwa baba zao hawakuwa mafisadi, tatizo tu ni kuwa viongozi walikuwa wanaabudiwa sana, na maisha ya wakati huo wa ujamaa, ukionekana upo tofauti na wengine, cha moto utakiona...! Yaani walijuwa kula na vipofu.

Kufilisi na ufisadi Mkuu ni vitu viwili tofauti. Narudia tena wakati wa Mwalimu hatukuwahi kabisa kusikia madudu kama haya ya kifisadi. Kwa hiyo kutaka kuyahusisha haya madudu mbali mbali ya ufisadi na Mwalimu Nyerere ni kumtomtenda haki Mwalimu kabisa. Alikuwa na mapungufu yake na ndio kuna watu waliovurunda katika mashirika mbali mbali ya umma lakini kuvurunda huko huwezi kulinganisha na wizi uliopo sasa kama ule uliofanywa na Mkapa wa kuiba Kiwira, kama ule ulifanywa wa kulazimisha kununua rada (Watanzania hata majani tutakula lakini lazima rada inunuliwe) kumbe walikuwa tayari wameshachora mchoro wao wa mabilioni, kutudangaya kwamba kampuni ya Houston, Texas inakuja kufua umeme kumbe ni wizi mtupu na sasa wanatakiwa kulipwa $94 million, kuingia kwa RITES mikono mitupu na sasa wanastahili kulipwa $87 million eti kwa kuvunja mkataba!

Sijui Nyerere alikukosea nini Mkuu hata kutaka kumuhusisha na mabaya yote nchi mwetu hata baada ya kung'atuka madarakani miaka 26 iliyopita.
 
Back
Top Bottom