Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,237
- 44,470
Wanaulaumu Ujamaa kwa kushindwa kwa Ubepari; wanataka tuamini kabisa kuwa Ujamaa ndio tatizo la Tanzania. Lakini tukiwauliza nchi kama Uganda, Kenya, Zaire zilifuata mfumo gani - ubepari - tunashangaa mbona hawana sana tofauti na sisi? Wao walifikiri Ubepari ni "soko huru" au "Soko huria" na kwa muda mrefu hiyo ndiyo imekuwa nadharia yao.
Ukimuuliza JK ataanza "uchumi wa soko" a.k.a Ubepari na kutuelezea mambo ya "uwekezaji" na all the bs! Ubepari ni nadharia ya maisha siyo nadharia ya kiuchumi tu kama tulivyofndishwa katika classical economy au political economy na kama tunavyohubiriwa na mapebari wa CCM.
Tunaambiwa kuwa Ubepari ndio utatatua matatizo yetu yote kuwa tukiukumbatia bila kuuhojia au kuusahihisha (wakati wao walioutunga wameshaubadilisha kiasi kwamba unaonekana ni ndugu moja na Ujamaa na hawaachani) basi Tanzania itakuwa pepo.
Inasikitisha kuwa hakuna wananadharia ndani ya CCM - theorists - ambao wangeweza kutumia chembe zilizoko kwenye ubongo wao kuuchambua na kuuweka sawa mfumo ambao wanataka tuufuate. Kwa sababu tukianza kuuliza maswali yanayohusu Ubepari wa Tanzania mtashangaa kuwa watawala wetu walioshindwa wana fikra za Ubepari wa miaka ya 1970 wakati huo ukipambanishwa na Ukomonisti wa Kisovieti.
Leo hii Ubepari wa Kimagharibi unapambanishwa na Ukomonisti wa Kichina na mara moja tunatambua kuwa huitaji Demokrasia ya vyama vingi kuweza kuwa na mabadilishano ya kisiasa, huitaji uchumi usiomilikiwa na serikali au wananchi moja kwa moja ili kuweza kuleta maendeleo na kuwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja yanaweza pia kupatikana katika kuleta maendeleo ya jumuiya nzima.
Utaona kuwa fikra za Nyerere za Ujamaa zinakaribiana zaidi na za China ya leo kuliko fikra za Kikwete za Ubepari zisivyokaribiana na Marekani ya leo.
Ukimuuliza JK ataanza "uchumi wa soko" a.k.a Ubepari na kutuelezea mambo ya "uwekezaji" na all the bs! Ubepari ni nadharia ya maisha siyo nadharia ya kiuchumi tu kama tulivyofndishwa katika classical economy au political economy na kama tunavyohubiriwa na mapebari wa CCM.
Tunaambiwa kuwa Ubepari ndio utatatua matatizo yetu yote kuwa tukiukumbatia bila kuuhojia au kuusahihisha (wakati wao walioutunga wameshaubadilisha kiasi kwamba unaonekana ni ndugu moja na Ujamaa na hawaachani) basi Tanzania itakuwa pepo.
Inasikitisha kuwa hakuna wananadharia ndani ya CCM - theorists - ambao wangeweza kutumia chembe zilizoko kwenye ubongo wao kuuchambua na kuuweka sawa mfumo ambao wanataka tuufuate. Kwa sababu tukianza kuuliza maswali yanayohusu Ubepari wa Tanzania mtashangaa kuwa watawala wetu walioshindwa wana fikra za Ubepari wa miaka ya 1970 wakati huo ukipambanishwa na Ukomonisti wa Kisovieti.
Leo hii Ubepari wa Kimagharibi unapambanishwa na Ukomonisti wa Kichina na mara moja tunatambua kuwa huitaji Demokrasia ya vyama vingi kuweza kuwa na mabadilishano ya kisiasa, huitaji uchumi usiomilikiwa na serikali au wananchi moja kwa moja ili kuweza kuleta maendeleo na kuwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja yanaweza pia kupatikana katika kuleta maendeleo ya jumuiya nzima.
Utaona kuwa fikra za Nyerere za Ujamaa zinakaribiana zaidi na za China ya leo kuliko fikra za Kikwete za Ubepari zisivyokaribiana na Marekani ya leo.