Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Invisible na wengine,

Mie naona ni vizuri TBC1? kuonesha Live,Hata CNN huwa wanakatisha habari na shughuli zote kama kukiwa na Breaking News.This is Breaking New and they are right to show the events.mambo mengine hatujui ila kuonesha ni haki na wamefanya Vyema.Wewe ungejuaje haya yote kama siyo TBC!?

Msilifanye suala hili kuwa la kisiasa,nilishasema toka jana..Ole wenu CHADEMA,kwa vyovyote vile bado mnalo...hata kama,kuna kosa lillishafanyika na lazima watu walinywe sasa nomatter who did but it will be like it is.Poleni coz mmeshikwa pabaya

Kama ni chadema iweje serikali ya CCM inawekea ngumu uchunguzi with independent pathologist. Wewe ndiyo unaleta siasa hapa. Ndungu zake wanataka kufahamu ukweli wa mambo. Kitu ambacho ni halali yao, sasa kama serikali haitaki kuwapa independnt person then inatia mashaka kuwa kuna kitu serikali inakijua na wanataka kutuficha.
 
Nadhani sheria inayotumika niyakawaida kabisa. kwamba kila Daktari hata mtanzania kabla ya kuruhusiwa kufanya kazi nchini lazima aweamesajiliwa, nadhani pia mawakili nao wanahili la kusajiliwa kabla ya kuruhusiwa kufanya kazi sehemu flani. so huyo Daktari kama hajasajiliwa nchini haiwezekani kufanya kazi nchini. Nadhani mnakumbuka walipogoma madaktari Muhimbili waliwafutia baadhi usajili hivyo kuwafanya kushinda kufanya kazi nchini. Sioni ubaya wa hii sheria hata kidogo, la sivyo kila mtu anaweza kujifanya Dr. na hio itakuwa kushoto zaidi.

Shida ni kuleta daktari huyo huyo for a verification job. hauwezi ukafanya uchunguzi mwenyewe na kujikagua tena mwenyewe haileti maana yoyote
 
Huyu Deus Francis Mallya baada ya kusoma michango mbali mbali ya wana JF nimejifunza kitu, kwamba kule kujifanya ndiye Invisible alikuwa na lake jambo kwa timu nzima ya MwanaHalisi bila shaka mmoja baada ya mwingine angefanyiwa kitu kama hicho alichofanyiwa Mh Wangwe.

Jambo la pili ambalo napo nimepata wazo fulani jinsi walivyofanikisha kuhitimisha maisha ya Wangwe ni kwamba inawezekana huyu Mallya alimbembeleza sana kusafiri kwenda Dar ili kuhakikisha anafanikisha hilo, kwani 1. Mafundi waliofanya matengenezo walimuona Mallya akiendesha gari ndani akiwemo Wangwe.
2. Inaelekea baada ya kutoka huko gereji na safari ikaanza mbele kulikuwa na mtu mwingine huyo ambaye alitoweka baada ya ajali.
3. Inaelekea pia Wangwe aliuawa akiwa garini kabla ya ajali.
4. Inaelekea gari lilifanyiwa usanii fulani likapata "ajali" likapinduka peke yake bila wao kuwamo ndani ya gari. Nasema hivi kwa sababu kwa jinsi gari lilivyo haiwezekani mtu ukatoka bila hata michubuko.
 
Hivi postmortem ya kwanza iliofanyika dodoma imesema nini? na ile bastola ya malya mbona ina utata,mtu una basola unakubali kuibiwa kila kitu hupigi hata risasi moja hewani?


na vibaka hawakuionma hiyo bastola wala simu!!
Inawezekana hakuwa na ufahamu wakati anaibiwa ndo mana hakuweza kuitumia. Swali la msingi hapa ni je inaonyesha imetumika siku hiyo ( idadi ya risasi au maganda ya risasi karibu) kama ndiyo basi aliitumia nani na kwa lengo gani.

Ila Deus Mallya kweli ukatoe sadaka ya shukrani. Ajali kama ile umenusurika hivyo? bil aahata kuteguka mkono. Mungu wako anakupenda sana
 
kabla Sijaunganisha Hii Topic Na Inayo-exist Naomba Kuwafahamisha Haya Pembeni Kwanza... After 1hr The Topics Will Be Merged.

  1. daktari Aliyekuwa Amekodiwa Kutoka Kenya Amekataliwa Na Serikali Kwakuwa Sheria Za Nchi Haziruhusu na Hivyo Familia Ikaambiwa Imtafute Daktari Mwingine Mzalendo Ili Awasaidie Katika Suala La Uchunguzi.
  2. tbc Wamehamisha Kambi Kutoka Dodoma (ambapo Walitakiwa Kuonesha Bunge 'live' ) Na Crew Nzima Imehamia Musoma - Tarime. Sijui Nini Wanamaanisha Kwa Kufanya Hivi Na Priority Iko Wapi Kwa Serikali Yetu.
Zaidi Tutaendelea Kuhabarishana

basi Na Apelekwe Kenya Ili Uchunguzi Ufanyike Kule.............au Sheria Hairuhusu....
 
basi Na Apelekwe Kenya Ili Uchunguzi Ufanyike Kule.............au Sheria Hairuhusu....

I like this. Kutoka pale nyumbani kwao mpaka Kenya ni umbali mfupi sana. Ila sijui kama Kenya watataka marehemu awe na viza.
 
Ndio hivyo Mkuu.Nasikia alikuwa amelewa Moshi Club then akaanza kubwata ovyo yakamkuta.Kalazwa Hospitali wakampelekea a bottle of wine wakamwambia next time it will be your neck.
We have never heard of him since then.probably he was eliminated.

...astaghafirullah!

yalimkuta mitaa ya nyumbani kwake pale karibu na Ikulu, nakumbukia huyu babu alikuwa mtu wa mtungi sana, siku hiyo ali 'tresspass' kwenye yale maeneo yanayoandikwa 'USIPITE HAPA', mbaya zaidi alikaidi amri ya kusimama na kujitambulisha, (mambo ya mtungi, na ego ya udakitari bingwa), kilichofuatia ndio hicho,...anyway, alikufa kifo cha kawaida, umri pamoja na athari za pombe muda mrefu.

R.I.P (babu) Prof Shaba, daima utakumbukwa!
 
Mie nataka kuulilza,

inaonekaana watu wanaju ammbo mengi zaidi kuhus msiba huu,
Je mnahisi au mnajua ni nani alihusika na kumpiga risaisi Wangwe kama mnavyosema?Kuna kitu nafikiri mie na ambao hatujui wapo wanojua.watuelezee

Gembe,
Watu wengi hawajui nani kamuua au chanzo cha kifo. Ukisikia mtu anasema ni chama au mtu fulani kamuua huyo jamaa anachemka. Kama navyosikia Tv ta Mhando inadai kuwa ni ugomvi wa CHADEMA na Wangwe, hizo ni PUMBA. Ukisikia mtu anasema kuwa KAPIGWA RISASI, jua huyo anachemka. Ukweli hadi sasa ni kuwa KAFA kwa ajali ya gari. Ila mwili wake majeraha yana unautata. Sasa ili kuondoa UTATA huo, inabidi kufanya uchunguzi kujua kulikoni. Uchunguzi huu uwe huru inabidi ufanyike. Kama amekufa kwa ajali ya gari, kwa nini SERIKALI ya CCM/JK inakataa au kuleta vipingamizi?
Mwisho mie nasema nduguze wapeleke MWILI KENYA. Huko ufanyiwe uchunguzi. WADANGANYIKA wote ambao wamechoka kudanganywa washughulikie hadi mwili uende Kenya na kufanyiwa uchunguzi na kesho urudi kwa mazishi. Serikali ikitaka kupeleka muwakilishi wake basi na ifanye hivyo. Pia ikibidi, si waupeleke MWILI UFANYIWE X-RAY? Kama kuna tundu kichwani litaonekana tu kuwa TUNDU. Na kama sikosei siku hizi kuna mashine kali zaidi.
 
What ican Tell..

Watu wa ulinzi na Usalama wanapitia mawasiliano ya simu ya Deus na Chacha na watu wengine kwa takribani miezi sita nyuma kujua nini Chanzo.tuwe wavumilivu.ila Ole Wenu CHADEMA....
 
Familia iamue kwenda kumzika Kenya kusudi huyo dokta akamfanyie uchunguzi , tuone maajabu mengine kama kuna sheria ya inayozuia kumzika raia wa Tanzania nje.

Mura,

hakuna Mtu wa Shemeji zangu aliyewahi kuzikwa nje ya kemakorere...hiyo ni ngumu ,hiyo ni laana..suala limeshakuwa la kisiasa
 
Mie nataka kuulilza,

inaonekaana watu wanaju ammbo mengi zaidi kuhus msiba huu,
Je mnahisi au mnajua ni nani alihusika na kumpiga risaisi Wangwe kama mnavyosema?Kuna kitu nafikiri mie na ambao hatujui wapo wanojua.watuelezee

Swali zuri mkuu lakini nadhani umetupeleka mbele sana. Inabidi kwanza tuwe na uhakika kwamba kweli alipigwa risasi. Kama unavyosema, kuna watu wanataka kugeuza hisia zao kuwa facts. Ni jambo rahisi tu, serikali iruhusu huo uchunguzi ufanywe ili ukweli ujulikane, kama alipigwa risasi, ndipo waanze kumtafuta mpigaji risasi
 
Hakuna ubishi kuwa kifo hiki kina mkono wa mtu. Kama ni cha kisiasa, the prime suspect ni kwenye chama chake ambacho alikuwa na mtafaruku nacho! Lakini wahenga walisema kufa kufaana, huenda waovu wengine wametumia hali hii kujipenyeza na kuleta dhahama hii.

Huyu pathologist huru angetusaidia kujua sababu ya kifo chake, kama ni ajali ya gari, risasi au panga hakuna ajuaye kwa sasa! lakini kwanini serikali ikatae uchunguzi huru? Inaogopa nini? Mbona kuna Madaktari wengi kutoka nje hufanya kazi TZ? Hata hospitali ya Sinza Palestina tulipata kutibiwa na Wapelstina... Au tatizo ni Usajili wa huyo Daktari kwamba hajasajiliwa Bongo? Kuna kitu hapa, lakini tutajua tu!
 
Huyu Deus Francis Mallya baada ya kusoma michango mbali mbali ya wana JF nimejifunza kitu, kwamba kule kujifanya ndiye Invisible alikuwa na lake jambo kwa timu nzima ya MwanaHalisi bila shaka mmoja baada ya mwingine angefanyiwa kitu kama hicho alichofanyiwa Mh Wangwe.

Jambo la pili ambalo napo nimepata wazo fulani jinsi walivyofanikisha kuhitimisha maisha ya Wangwe ni kwamba inawezekana huyu Mallya alimbembeleza sana kusafiri kwenda Dar ili kuhakikisha anafanikisha hilo, kwani 1. Mafundi waliofanya matengenezo walimuona Mallya akiendesha gari ndani akiwemo Wangwe.
2. Inaelekea baada ya kutoka huko gereji na safari ikaanza mbele kulikuwa na mtu mwingine huyo ambaye alitoweka baada ya ajali.
3. Inaelekea pia Wangwe aliuawa akiwa garini kabla ya ajali.
4. Inaelekea gari lilifanyiwa usanii fulani likapata "ajali" likapinduka peke yake bila wao kuwamo ndani ya gari. Nasema hivi kwa sababu kwa jinsi gari lilivyo haiwezekani mtu ukatoka bila hata michubuko.

Hivi Jmushi yuko wapi????
 
Kuna watu wengine hawafi kimyaa ... kabla ya kuzikwa kila kitu kitakuwa hadharani tunaamini ... Mungu msaidie mja wako huyo katika kazi anayoifanya kudhihirisha uma kwamba alidhulumiwa uhai wake ... wadhalilike wahusika wote na wajulikane na uma wote wa Tanzania
 
Kama ni chadema iweje serikali ya CCM inawekea ngumu uchunguzi with independent pathologist. Wewe ndiyo unaleta siasa hapa. Ndungu zake wanataka kufahamu ukweli wa mambo. Kitu ambacho ni halali yao, sasa kama serikali haitaki kuwapa independnt person then inatia mashaka kuwa kuna kitu serikali inakijua na wanataka kutuficha.
Sheria za Nchi haziruhusu Daktari yeyote ambauye hajasajiliwa Nchini kufanya Uchunguzi,inabidi waombe kibali kwanza cha Daktari huyo
 
Ingawa mimi siyo mtaalamu wa sheria, nakuhakikishia kuwa hakuna sheria ya namna hiyo, vinginevyo Rotary Club na Lions Club wasigekuwa wanaleta madakatri wao wa macho na kuruhusiwa kufanya kazi zao kwa muda bila kubugudhiwa na serikali. Daktari wa kufanya autopsy hana tofauti kabisa kiutendaji na dakari wa macho.

Kichuguu,

Una uhakika na unachosema? Princess Diana alivyokufa, waingereza hawakugusa mwili wake kule mpaka aliporudishwa UK pamoja na kutaka kushiriki kwenye initial investigation.

Pakistan alivyokufa Bhutto hakuna daktari wa nje aliyeruhusiwa kwenda kuchunguza mwili wake.

Tumesisitiza sana umuhimu wa kufuata sheria hapa, tukiwa agents wa kutaka zivunjwe tena
tunakosea sana. Sheria mbovu hazivunjwi wakati wa majanga, wakati kama huu ndio wakati wa kujua sheria fulani ni mbovu ili baadaye ifanyiwe marekebisho na sio kuivunja.

Kutibu mgonjwa na kuchunguza chanzo cha kifo ni vitu tofauti.

Dunia hii haina shortcuts, lazima tuheshimu sheria zilipo na kama ni mbovu, dawa sio kuzivunja bali kuzifanyia marekebisho au kuziondoa.

Kwenye hili labda jawabu ni kutumia mtanzania na hao wengine kuwa mashahidi kwenye huo uchunguzi kama sheria inaruhusu.
 
What ican Tell..

Watu wa ulinzi na Usalama wanapitia mawasiliano ya simu ya Deus na Chacha na watu wengine kwa takribani miezi sita nyuma kujua nini Chanzo.tuwe wavumilivu.ila Ole Wenu CHADEMA....

Kwa nini unazungumza vitu vya kijinga kiasi hiki , ni nani anayestopisha huu uchunguzi kama sio CCM na serikali yake?
 
Kwa mujibu wa Invisible ni kuwa...
Daktari amepatikana na sasa ndio Mwili unachukuliwa na kupelekwa Hospitali.Jina La Daktari na Hospitali anayopelekwa anafuatilia..Mwili ndio unachukuliwa dakika hii.

Naomba kuwasilisha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom