Haya ndio niliyosema hapo juu kidogo, kuwa wazee wa kazi tayari wameshashika mkondo, na it is over, sasa tuendelee tu na uchunguzi wetu:-
1. Daktari aliyekuwa amekodiwa kutoka Kenya amekataliwa na serikali kwakuwa sheria za nchi haziruhusu na hivyo familia ikaambiwa imtafute daktari mwingine mzalendo ili awasaidie katika suala la uchunguzi.
2. Familia ikaomba daktari kutoka Muhimbili lakini aliyetolewa na serikali ni yule yule aliyefanya uchunguzi kule Dodoma hivyo familia ikamkataa moja kwa moja kuwa huyu alishafanya uchunguzi wa awali na hawauamini na sasa wakatakiwa kutafuta daktari mwingine mzalendo binafsi. Mpaka sasa (wakati naandika) hakukuwa na jibu la daktari gani atatumika.
3. TBC wamehamisha kambi kutoka Dodoma (ambapo walitakiwa kuonesha Bunge 'Live' ) na crew nzima imehamia Musoma - Tarime. Sijui nini wanamaanisha kwa kufanya hivi na priority iko wapi kwa serikali yetu.
Zaidi tutaendelea kuhabarishana