Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 18,030
- 25,015
thanks, but it does not make any sense to me.Kichuguu,
Una uhakika na unachosema? Princess Diana alivyokufa, waingereza hawakugusa mwili wake kule mpaka aliporudishwa UK pamoja na kutaka kushiriki kwenye initial investigation.
Pakistan alivyokufa Bhutto hakuna daktari wa nje aliyeruhusiwa kwenda kuchunguza mwili wake.
Tumesisitiza sana umuhimu wa kufuata sheria hapa, tukiwa agents wa kutaka zivunjwe tena
tunakosea sana. Sheria mbovu hazivunjwi wakati wa majanga, wakati kama huu ndio wakati wa kujua sheria fulani ni mbovu ili baadaye ifanyiwe marekebisho na sio kuivunja.
Kutibu mgonjwa na kuchunguza chanzo cha kifo ni vitu tofauti.
Dunia hii haina shortcuts, lazima tuheshimu sheria zilipo na kama ni mbovu, dawa sio kuzivunja bali kuzifanyia marekebisho au kuziondoa.
Kwenye hili labda jawabu ni kutumia mtanzania na hao wengine kuwa mashahidi kwenye huo uchunguzi kama sheria inaruhusu.
Nchi nyingi za ulaya na marekani zina sheria kuwa madakatri wote wanofanya kazi za kidaktari kuwa wamesajiriwa katika nchi husika. Sidhani kama Tanzannia tuna sheria ya namna hiyo, vinginevyo Lions Club and Rotary Club wasingeleta madaktari wao wa macho kutoka nje.