Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Kuna mahali nimesoma kuwa Mallya aliwahi kupitia mafunzo ya kijeshi na alikuwa anamiliki kihalali bastola ambayo alikuwa anatembea nayo. Vile vile alishahudhuria mafunzo ya kijeshi katika nchi mbalimbali ikiwamo Libya na Misri.


Je maelezo hayo ni kweli au ndiyo ya kutuvuruga vichwa tena? Najua sasa hivi kuna kila aina ya porojo inaweza kuandikwa hapa.

Mafunzo ya kijeshi tuu...? Atakuwa Sloppy Assassin au ndio kazi yake ya kwanza...?
 
Ninachoona hapa ni kuwa hii independent autopsy itaonyesha chanzo cha kifo kama ni ajali au ni risasi. Ikionekana kuwa chanzo cha kifo siyo ajali, basi utatakiwa uchunguzi mzito wa kipolisi kubaini motive ya wauwajii, na kuwafikishe mbele ya sheria wale wote walioshiriki kwenye kupanga na/au kutekeleza mauaji yenyewe.


The dataz ni kwamba idara tayari imeuchukua mkondo wake kama kawa, hakuna kitakachotoka nje, yote yataishia huko huko ndani, hakuna matokeo yatakayotoka nje, kuanzia jana usiku walikuwa tayari wame-take over,

Kisa na mkasa, amani ya taifa, unaweza ku-fillin the blanks.........!
 
Hii picha ya Mallya ilipigwa baada ama kabla ya ajali?. Kama ilipigwa baada ya ajali mbona haonekani kama alihusika katika ajali mbaya namna ile?.

Hii mkuu alipigwa baada ya ajali angalia damu hizo kwenye sharti lake inaonyesha kama alijipaka.Au alizipata wakati wanamtoa Wangwe kwenye gari.
 
Hii picha ya Mallya ilipigwa baada ama kabla ya ajali?. Kama ilipigwa baada ya ajali mbona haonekani kama alihusika katika ajali mbaya namna ile?.

Sura inabeba uzito inaonyesha kama ni mutu anaetafuta huruma kwa kosa alilolifanya (Je pistol aliyobeba inaonyesha kutmika au haikutumika ,imekutwa na risasi ngapi na inabeba risasi ngapi)
 
Hapana chijana bado unayumba yumba katika ufahamu,Labda nijaribu tena kuweka sawa.
Ndani ya Chadema kuna mgogoro kati ya Wangwe na wengine au uongozi.
Sasa kwa picha ilivyo ikiwa Wangwe atauliwa moja kwa moja vidole na mawazo yataelekezwa kwa wenziwe aliokuwa na ugonvi nao.
Sasa hebu niambie kwa nini akina Zitto na wenziwe ilibidi wahifadhiwe na habari nyengine zinasema wameondoshwa na kupelekwa Musoma ? Nataka sababu ya hayo ili niendelee kukufafanulia.

Kina Zitto kuhifadhiwa inamaanisha watu wanadhani CHADEMA inahusika. Lakini haimanishi ni maadui wa CHADEMA ndio wamehusika. Usiruke mbali bila kuunganisha vipengele vikaleta mantiki.

CHADEMA, kama ilikuwa ni tishio kwa serikali ya CCM, basi ilitokana na wabunge wawili watatu hapa na pale. Ukitaka kuzima hilo tishio huui chama chao, unawazima wao wenyewe. CHADEMA hata ikisambaratika wale vinara wanaotikisa serikali ya CCM bado watakuwepo. Isitoshe, CCM haikuwahi kutetereshwa na CHADEMA kiasi cha kutaka kuwaua. Tikisiko kubwa kuliko yote iliyowahi kupata serikali ya CCM lilikuwa ni kazi ya wabunge wa CCM yenyewe. Huui upinzani wa wabunge wawili watatu kwa kuua mtu wa chama chao ili ionekane wameuana wenyewe ili chama chao kisambaratike. Nadharia yako bado haijaunganika ikaleta mantiki.

Una nadharia nyingine ?
 
Kabla sijaunganisha hii topic na inayo-exist naomba kuwafahamisha haya pembeni kwanza... After 1hr the topics will be merged.

  1. Daktari aliyekuwa amekodiwa kutoka Kenya amekataliwa na serikali kwakuwa sheria za nchi haziruhusu na hivyo familia ikaambiwa imtafute daktari mwingine mzalendo ili awasaidie katika suala la uchunguzi.
    • Familia ikaomba daktari kutoka Muhimbili lakini aliyetolewa na serikali ni yule yule aliyefanya uchunguzi kule Dodoma hivyo familia ikamkataa moja kwa moja kuwa huyu alishafanya uchunguzi wa awali na hawauamini na sasa wakatakiwa kutafuta daktari mwingine mzalendo binafsi. Mpaka sasa (wakati naandika) hakukuwa na jibu la daktari gani atatumika.
  2. TBC wamehamisha kambi kutoka Dodoma (ambapo walitakiwa kuonesha Bunge 'Live' ) na crew nzima imehamia Musoma - Tarime. Sijui nini wanamaanisha kwa kufanya hivi na priority iko wapi kwa serikali yetu.
Zaidi tutaendelea kuhabarishana
 
The dataz ni kwamba idara tayari imeuchukua mkondo wake kama kawa, hakuna kitakachotoka nje, yote yataishia huko huko ndani, hakuna matokeo yatakayotoka nje, kuanzia jana usiku walikuwa tayari wame-take over,

Kisa na mkasa, amani ya taifa, unaweza ku-fillin the blanks.........!
Duniani hakuna siri,wandugu wake wa karibu lazima watataka kuwajulisha WaTanzania.Hivyo idara itaficha nini wakati wahusika na dakitari anatoka kenya si hasha wengine wanamngojea hukohuko Kenya ili awape taarifa .
 
Kizaazaa Tarime (Tanzania Daima)




na Joseph Senga, Tarime



MAZISHI ya aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, yameingia dosari baada ya kuahirishwa kutokana na shinikizo la wananchi kutaka uchunguzi mwingine ufanyike kubaini chanzo cha kifo chake.

Familia ya Wangwe ilikubali matakwa ya waombolezaji waliotaka kufanyika upya kwa uchunguzi huo kwa madai ya kutokuwa na imani na uchunguzi wa awali.

Hali hiyo ilimlazimu kaka wa marehemu Profesa Samwel Wangwe, kutoa taarifa rasmi ya familia kukubali kuahirisha mazishi hayo hadi leo.

Wangwe ambaye alikuwa akisikika kwa shida kutokana na kelele za vurugu za waombelezaji hao, alisema wameamua kuahirisha ili kupisha uchunguzi wa kifamilia ufanyike leo.

"Naomba tusikilizane, kwa niaba ya familia, mazishi yameahirishwa leo mpaka hapo uchunguzi wa mwili wa marehemu kipenzi chenu utakapofanyika kesho (leo), ili kuondoa haya manung'uniko yaliyopo," alisema.

Alisema wamefikia uamuzi huo ili kuepuka baadaye kuja kufukua mwili wa marehemu kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Alisema sheria za nchi hii zinatoa ruhusu kwa familia kufanya uchunguzi kwa mara ya pili kama haijaridhishwa na matokeo, na uchunguzi huo utafanyika chini ya mtaalamu wa kujitegemea pamoja na shuhuda wa serikali.

‘Uchunguzi huu ni kwa ajili ya kujiridhisha lakini pia atakuwepo shuhuda wa serikali, na baada ya hapo ndipo tutafanya taratibu za mazishi," alisema Wangwe.

Naye Waziri wa Kilimo na Chakula Stephen Wasira, alisema serikali haina kipingamizi juu ya uchunguzi wa kifo cha Wangwe.

Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema tangu awali aliweka wazi kuwa kuna haja ya kufanyika uchunguzi huru juu ya kifo cha Wangwe.

Alisema kifo hicho kimezua maswali mengi miongoni mwa jamii, hivyo njia pekee ni kufanyika kwa uchunguzi utakaoweza kuwaridhisha wana familia na Watanzania kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA, John Mnyika, alisema CHADEMA inaungana na familia ya marehemu kutaka kufanyika kwa uchunguzi kwa mara ya pili.

Alisema utata wa kifo cha Wangwe umewafanya CHADEMA kumwandikia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Said Mwema, kutaka kufanyika kwa uchunguzi.

Pamoja na kaka wa marehemu huyo kuueleza umma uliohudhuria mazishi hayo, bado alikuwa na wakati mgumu, kwani wananchi hawakutaka kumsikiliza zaidi ya kupaza sauti kutaka uchunguzi huo ufanyike upya na matokeo yatangazwe hadharani kabla ya mazishi.

Wakati hatua hiyo inafikiwa, maandalizi ya mazishi hayo, ikiwa ni pamoja na kaburi na mfuniko wa zege uliokuwa utumike kufunika kaburi hilo, vilikuwa tayari, na kusubiri kumalizika kwa ibada.

Hata hivyo hasira za waombolezaji hao, zilibadilika na kuwa furaha pale alipowasili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.

Mbowe aliwasili nyumbani kwa marehemu, majira ya saa 7:30 mchana, akitokea Dar es Salaam kupitia Musoma kwa ndege ya kukodi.

Kana kwamba wananchi hao walikuwa wamemsubiri afike ili waanze kueleza dukuduku lao, walimpokea kwa shangwe na nderemo huku wengine wakisema ndiye shujaa pekee aliyebaki.

"Umebaki wewe tu Mbowe, kamanda wetu, wametuondolea mbunge wetu, tunataka watuambie, nani kamuua, vinginevyo watuue na sisi," walisikika baadhi ya vijana.

Aidha, katika kile kilichoonekana kumlinda Mbowe, vijana hao walimsindikiza hadi katika meza kuu ambako alijumuika na viongozi wengine.

Baada ya Mbowe kuketi katika meza kuu, na hatimaye mwongozaji wa shughuli za mazishi alipoanza kutaka kueleza ratiba ya mazishi, vijana hao waliisogelea meza kuu huku wakiangua vilio na miluzi, wakitaka waelezwe mbunge wao yuko wapi na mambo mengine.

Sakata hilo halikuishia hapo, vijana hao walizidi kuongezeka sehemu ilipokuwa meza kuu, wengine wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakiwa na hamaki ya kutomsikiliza kiongozi yeyote, hata wale waliowafahamu kutoka kijijini hapo.

Hali ilipozidi kuwa mbaya, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), aliamua kupanda juu ya meza na kuanza kuwaomba vijana hao watulie ili shughuli ianze.

Kusimama huko kwa Zitto kulionekana kuwa suluhisho la kadhia hiyo, kwani walimshangilia na kunyamaza.

Zitto alitoa ombi kwa vijana hao kumsikiliza msemaji wa familia, Profesa Wange kuhusu utaratibu wa mazishi.

Hata hivyo Profesa Wangwe hakufika mbali, kelele zilianza tena kwa kumtaka asizungumze chochote mpaka hapo watakapojua chanzo cha kifo cha kipenzi chao, Chacha Wangwe.

Baada ya kaka huyo wa marehemu kushindwa kuendelea na utaratibu huo, ilikuja ajenda ya pili, nayo ni kufanyika kwa uchunguzi.

Ajenda hiyo ilitolewa ufafanuzi na Zitto Kabwe kuwa familia imeridhia kufanyika kwa uchunguzi tena wa kifo cha marehemu Chacha Wangwe na ndipo kelele za mayowe ya kukubaliana naye zilipolipuka.

"Uchunguzi wa kina utafanyika, wananchi msiwe na hofu hata kidogo, utahusisha pande zote zinazohusika, na endepo itabainika kuwa kifo chake kilikuwa na mkono wa mtu, tutahakikisha haki inatendeka na taarifa zitatolewa kwa uwazi," alifafanua Zitto.

Ufafanuzi huo wa Zitto, uliwafanya waombolezaji hao kutulia na kumwezesha Wangwe kuendelea na hotuba yake.

Kwa mara nyingine, Wangwe alisema familia imekubali ombi la kufanyika upya kwa uchunguzi huo leo, na taarifa yake kutangazwa hadharani kabla ya mazishi.

Baada ya maelezo ya Profesa Wangwe, ambayo hata hivyo hayakusikika vizuri kutokana na kelele za watu, ndipo Zitto Kabwe alipolazimika kurudia tena kupanda mezani, kujaribu kuwatuliza.

Hali ilizidi kuwa tete, kwani watu walipoanza kutawanyika kukazuka vurugu za kurushiana mawe.

Hali hiyo iliwafanya baadhi ya watu kutafuta njia ili kunusuru maisha yao huku wangine waliotoka salama wakishukuru kwa kunusurika katika vurugu hizo.

Waombolezaji hao, walianza kurushiana mawe wenyewe kwa wenyewe, hali iliyohatarisha maisha ya baadhi yao.

Baadhi ya watu waliozungumza na Tanzania Daima, walisema kuna uwezekano mkubwa wa watu wachache kujitokeza katika mazishi hayo leo, kwa kuhofia vurugu.

Hadi watu walipotawanyika katika eneo hilo, chakula na vinywaji vilikuwa tayari, lakini hakuna mtu aliyevitumia.

Baadhi ya viongozi, hususan wale wanaotoka Mkoa wa Mara, hawakwenda mbali, akiwamo Wasira, walirejea katika eneo la tukio na kufanyiwa mahojiano na vyombo vya habari, ambapo waliezea kusikitishwa kwao na tukio hilo.
 
Wangwe burial delayed: Family demands new autopsy

THISDAY REPORTERS
Dar es Salaam and Tarime

THE family of opposition Member of Parliament Chacha Wangwe postponed yesterday's scheduled burial of the politician in Mara Region and ordered a second autopsy to be conducted on his body to conclusively ascertain the cause of death.

This follows suspicions that probable gunshot wounds to the head of the late Tarime legislator on a CHADEMA ticket were overlooked in the first postmortem supervised by the government in Dodoma.

Sources confirmed that an independent pathologist from neighbouring Kenya is today expected to perform the new autopsy on Wangwe's body in Mara Region.

''There are strong suspicions that the official government autopsy conducted in Dodoma earlier this week somehow overlooked possible gunshot wounds to the deceased's head,'' said a source close to the family.

There were scenes of chaos in the late MP's hometown of Tarime yesterday as angry mourners demanded answers on what exactly led to the death of their beloved lawmaker.

Riot police had to be called in to calm hundreds of mourners and rescue the CHADEMA national chairman, Freeman Mbowe, from the angry crowd.

The deceased's brother, Prof. Samuel Wangwe, confirmed to reporters in Tarime yesterday that the family had ordered another autopsy to be performed on the body, to be conducted in Mara Region.

He said the new medical examination will follow normal hospital procedures, with a government representative present.

Although Prof. Wangwe did not specify reasons for conducting the second postmortem, sources close to the bereaved family said there were unconfirmed reports that the first one conducted in Dodoma by a pathologist from the Muhimbili National Hospital had produced questionable results.

''It appears the first autopsy missed serious head injuries on Wangwe's body, which could have possibly been caused by bullets piercing through the head. That's why a second autopsy is to be conducted, to either verify these reports or erase all fears of foul play once and for all,'' the sources said.

In Tarime, police had to be deployed to calm down hundreds of mourners who became restless after apparently being told they could not pay their last respects to the late MP's body.

A delegation of around 20 MPs who had arrived in Tarime to attend the scheduled burial of their former colleague, had to be flown back to Dodoma after the announcement of the funeral delay.

In Dodoma, police continued to interrogate Deus Mallya, the survivor of Monday night's road crash that killed Wangwe.

Apparently there have been conflicting statements from Mallya, who claimed Wangwe was driving the vehicle when it crashed, although the late MP's sons say that Mallya was the man behind the wheel when the two of them left Dodoma to start the ill-fated journey to Dar es Salaam.

Police sources say Mallya was a person of interest and is believed to possibly have more answers on what actually transpired before, during and after the crash.

According to other unconfirmed reports, eyewitnesses to the crash are also claiming there could have been a third person in the car, who disappeared immediately afterwards.

CHADEMA has already formally demanded a proper police investigation into the cause and circumstances of the crash, to include a thorough background check on Mallya to establish who he really is and what his connection with Wangwe was.

In a letter to Inspector General of Police Saidi Mwema, CHADEMA acting secretary general John Mnyika said the investigation should be conducted swiftly and its findings made public as soon as possible.

He suggested that the investigation should centre on Mallya as a prime suspect, and that it was important to find out who exactly was driving the car (Wangwe or Mallya) at the time of the accident.

''We want Deus Mallya to help the police in their investigations, and to be interrogated thoroughly on this matter, since his statements so far have been very suspicious indeed,'' said the CHADEMA letter to the IGP.

It is understood that results of the second autopsy on Wangwe's body could be made public as early as today.
 
Kwa wale wataalamu wa ajali naombeni mtusaidie kutafusili hizi picha ajari.
Huku ni mbele ya gari
5.JPG
Huku ubavuni ni upande wa kushoto
View attachment 1902
Na huku ni mbele
View attachment 1903
Watalaamu wa photography za ajari mtaweza kutusaidia kuelewa kwa kina.
 
Yaani hili la kifo cha Wangwe whether ni mgogoro ndani ya chama chake ama ni janja ya mafisadi kuisambaratisha Chadema kwa vile ni tishio kwao, ama janja ya CCM kama chama kutaka kukidhoofu Chadema kwa vile kime wakamata pabaya,

Kifo hiki kina nifanya nikubaliane na ule usemi kwamba SIASA NI MCHEZO MCHAFU!
 
Chadema:No foul play

By Samuel Kamndaya, Dodoma, and Beatus Kagashe, Dar

The opposition Chadema yesterday ruled out foul play in the death of Mr Chacha Wangwe, and called for peaceful mourning of the MP who died on Monday night in a car crash.

The party�s headquarters said the death of Mr Wangwe, who was recently suspended as party�s vice-chairman, should not be linked to his leadership row with Chadema chairman Freeman Mbowe.

Chadema�s acting deputy secretary-general and director of youth affairs, Mr John Mnyika, told reporters that Mr Mbowe was cutting short his trip to South Africa to join other Tanzanians in mourning �our departed hero�.

Mr Mnyika said Chadema believed the death of the Tarime MP had nothing to do with his recent suspension as vice-chairman or claims of a power struggle in the party.

The remarks were in response to rumours surrounding the accident which took place at the height of tensions within Chadema.

Following his suspension last month by the party�s politburo, the Tarime MP declared his intention to oppose Mr Mbowe when internal elections were called.

His death shocked and galvanised the country with President Jakaya Kikwete yesterday leading MPs, top government officials and other members of the public in paying their last respects at parliament grounds in Dodoma.

President Kikwete did not speak in Dodoma, but sent a message in which he condoled MPs, Tarime constituents and Chadema.

�Through you, I would like to pass my sincere condolences to all members of the parliament for the loss of their colleague at a time when they are fulfilling their obligations in national representation,� said the President in the note to the Speaker, Mr Samuel Sitta.

Mr Sitta was overcome with emotion earlier in the morning and openly shed tears as he adjourned business for the day to mourn Mr Wangwe, whom he described as a �lively character.�

�The responsibilities are once again upon my shoulders to announce to you the tragic news. Honourable Chacha Wangwe, our comrade, the Tarime MP, passed away yesterday (Monday) at around 8.55pm in a car accident,� said Mr Sitta while wiping away tears.

It was the fifth that had had announced the death of an MP in Parliament since the 2005 elections following the demise of former Cabinet minister Juma Akukweti, deputy minister Salome Mbatia and MPs Amina Chifupa and Benedict Losurutia.

In accordance to new parliamentary standing orders, Mr Wangwe�s body was taken through the debating parliament chamber in poignant remembrance of the deceased�s hearty and sometimes fiery contributions in debates.

The body was to spend the night at his residence in Dodoma before being flown today to Dar es Salaam from where it will be transported again to Tarime for burial tomorrow in his home village of Kemakorere.

Many other MPs, including Mr Kabwe Zitto and Mr Iddi Azzan, were seen wiping tears as Mr Sitta postponed parliamentary proceedings and called an emergency meeting of the parliamentary leadership committee to work on burial procedures.

Dressed in black, MPs gathered in groups outside the parliament building discussing in disbelief the untimely death of Mr Wangwe.

�We will miss his courage. He was a man who never gave up on what he believed was right. It will be a hard task to fill the gap that he has left behind,� said Ms Susan Lyimo (Special Seats-Chadema).

Other MPs said they would miss Mr Wangwe�s easy-going nature. �He was from the Opposition camp, but he was good at socializing with people across the political divide,� said Capt John Komba (Mbinga West-CCM).

Some were overheard wondering why the National Assembly usually lost a lawmaker during its budget sessions. Ms Chifupa died during last year�s budget session.

Home Affairs minister Lawrence Masha was yesterday scheduled to present his ministry�s budget estimates before business was adjourned. Mr Wangwe�s contribution to the debate on the ministry�s budget was being eagerly awaited.

He had always been vocal over repeated inter-clan clashes in Tarime Dictrict and his fellow MPs had expected that he would put the Home Affairs Ministry to task over its failure to contain insecurity in the area.

He had also prepared a private motion on the same clashes and cattle rustling according to deputy speaker Ms Anna Makinda who said she had on Friday helped the MP in procedures to file the motion.

According to Susan Lyimo, Mr Wangwe�s fellow opposition MPs will go on with the motion that he has left behind. Twenty MPs led by Bumbuli MP William Shelukindo will represent their colleagues at the burial.

Meanwhile Chadema asked all its branches countrywide to fly their flags half mast for a week as a sign of respect for Mr Wangwe who worked tirelessly to build the party in Mara region.

Mr Mbowe, who is expected to arrive today, will lead a team of party officials to the burial tomorrow, according to Mr Mnyika.
 
mkuu kuna kitu hapa kinafichika ndani.....mmh sheria za nchi kweli haziruhusu???Na kwa nini wanataka kupandikiza daktari.Maswali mengi sana yatatoka hapa bila majibu.
 
Haya ndio niliyosema hapo juu kidogo, kuwa wazee wa kazi tayari wameshashika mkondo, na it is over, sasa tuendelee tu na uchunguzi wetu:-


1. Daktari aliyekuwa amekodiwa kutoka Kenya amekataliwa na serikali kwakuwa sheria za nchi haziruhusu na hivyo familia ikaambiwa imtafute daktari mwingine mzalendo ili awasaidie katika suala la uchunguzi.

2. Familia ikaomba daktari kutoka Muhimbili lakini aliyetolewa na serikali ni yule yule aliyefanya uchunguzi kule Dodoma hivyo familia ikamkataa moja kwa moja kuwa huyu alishafanya uchunguzi wa awali na hawauamini na sasa wakatakiwa kutafuta daktari mwingine mzalendo binafsi. Mpaka sasa (wakati naandika) hakukuwa na jibu la daktari gani atatumika.

3. TBC wamehamisha kambi kutoka Dodoma (ambapo walitakiwa kuonesha Bunge 'Live' ) na crew nzima imehamia Musoma - Tarime. Sijui nini wanamaanisha kwa kufanya hivi na priority iko wapi kwa serikali yetu.
Zaidi tutaendelea kuhabarishana
 
Nimekata tamaa kabisa kama kweli serikali yetu inaendeshwa kwa haki. Mbona jana Wassira (anayewakilisha serikali katika msiba ule) alisema kuwa serikali itatoa daktari wake kama shahidi wakati familia itaruhiswa kutoa daktari wake?

Kwa nini yule daktari wa Kenya hakurusiwa? Ni sheria gani ambayo haimruhusu ilhali sasa hivi tuna ushirikiano wa afrika ya mashariki?


Mbona viongozi wakiugua wanakwenda kutibiwa na madaktari wa nje? hivi hawajui kuwa autopsy ni sehemu ya tiba pia?
 
Kwa mtindo huu kila Dr atakayeombwa kufanya uchunguzi hatakuwa huru kabisa.
 
Asante invisible kwa shocking news
Kwani huyo Mkenya angefanya bila usimamizi wa Daktari wa TZ?Mbona hofu inawapata serikali?
 
mkuu kuna kitu hapa kinafichika ndani.....mmh sheria za nchi kweli haziruhusu???Na kwa nini wanataka kupandikiza daktari.Maswali mengi sana yatatoka hapa bila majibu.
Mwenyewe nimeongea na walio huko ambao hata hivyo wamesema wamekata tamaa kwani wanachojua kutakuwa na mzunguko na kuna uwezekano mkubwa uchunguzi huo usifanyike!

Kilichonishangaza ni TBC kuamua kuhamisha van na crew nzima kutoka Dodoma hivyo kuicha StarTv pekee ndo ioneshe bunge live.

Halafu, kwanini wapewe daktari yuleyule aliyefanya uchunguzi wa awali kule Dodoma?

Haya mambo magumu kusema kweli
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom