Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,945
- 4,506
Maswali mazito ambayo Polisi wanatakiwa kuyafanyia kazi haya hapa;-
Ili polisi wajivue lawamani inabidi wafanye uchunguzi kwa kufuata maswali hayo.
1."Kwa nini Deus Mallya alianza urafiki na marehemu hivi karibuni ndani ya wiki tatu au
nne na urafiki huo ukawa karibu kwa haraka namna hiyo?
2."Kwa nini Deus Mallya ndiye alikuwa anashinikiza hiyo safari ya usiku wakati watoto wa Chacha na mke wake walikuwa wanamshauri asisafiri siku hiyo usiku?
3.Ilikuwaje Deus ana shida na safari hiyo kuliko watu wengine wakiwemo marehemu mwenyewe na watoto wake na mke wake?
4."Kwa nini hapo awali Deus hakutaka ajulikane kwamba yeye ndiye alikuwa anaendesha
gari hilo.
5."Kwa nini Deus hajaeleza kuhusu huyo mtu wa tatu aliyeonekana kuwa pamoja
na waliopata ajali?
6."Kama huyo mtu wa tatu alitoweka baadaye kuonekana na waliofika katika eneo
la ajali alikuwa anakimbia nini?
7.Kwa nini Laptop ya Deus ambayo alikuwa anafanyia kazi zake nyingi ilitoweka baada ya ajali wakati simu na fedha zilikutwa katika eneo la ajali?
8."Je ni kawaida wananchi wa kawaida kuona kwamba ni muhimu kuchukua Laptop kuliko kuchukua simu na fedha?
9.Kwa nini Deus alidai kwamba waliondoka Dodoma saa 9 mchana wakati familia yake inajua kwamba waliondoka baada ya saa 12 jioni?
10.Kwa nini Deus hakutaka ifahamike kwamba waliondoka usiku?
Ili polisi wajivue lawamani inabidi wafanye uchunguzi kwa kufuata maswali hayo.