Wanabodi,
Natanguliza samahani mbele ya haya nitakayo yasema kwa sababu sina hakika kama yamekwisha zungumziwa.
Moja ni kuhusiana na Prof Wangwe ambaye inaonyesha kabadilisha msimamo wake kuhusiana na kesi hii, limewatatiza wengi lakini wameshindwa kufahamu kwamba hata Vyombo vya Usalama kama Polisi wanaweza kubadilisha msimamo kulingana na ushahidi unavyo zidi kupatikana. Mkisiwa wa kwanza akawa huru, na mtu mwingine kabisa nje akavutwa ndani kama mhusika maadam file halijafungwa. Na hata kama limefungwa linaweza kufunguliwa upya na madai mapya kabisa yakatokea!. Hii haina maana Polisi ni wajinga kufikia uamuzi wa kwanza.
Nikirudi ktk sakata hili la wangwe nimesoma mahala wanabodi wakihoji hoja ya wangwe ambayo ilikuwa iwakilishwe bungeni.. Ukweli ni kwamba ninavyofahamu mimi mbunge yoyote anayetaka kuwakilisha hoja huipeleka kwa Spika ili apatiwe ruksa na hupitiwa kuangalia nafasi yake, uzito wake na kadhalika. Kisha mbunge hujulishwa kwamba hoja yake itasimama. kama mnakumbuka vizuri Dr. Slaa alipeleka hoja ya BoT bungeni ikakataliwa au kwa namna fulani alishtuka yeye kwamba haiwezi kukubaliwa. Zito pia (kama sikosei ama mbunge fulani) kuna sehemu kama nakumbuka vizuri alihoji kuhusiana na swala moja ambalo halikuwa ktk hoja yake ya awali (inayotambuliwa na spika) kiasi kwamba ilitolewa nje hali uzito wake ulikuwa mkubwa... sasa basi kama Wangwe alikuwa na hoja ambayo alitaka kuiwakilisha bungeni kuna uwezekano mkubwa kuwa spika ameisha ipata, lakini hapo hapo kwa kutumia njama CCM wanaweza kabisa kuibadilisha na kuweka hoja tofauti kwa sababu sio lazima Chadema wafahamu hoja ya Wangwe ambayo ilikuwa inawakilisha jimbo lake kama mbunge wa Tarime..Nasema hivi kwa sababu wapo wabunge wa CCM ambao huingiza hoja kuuliza viongozi wa wizara fulani bila viongozi hao kuwa na taarifa za hoja hiyo nje ya bunge.
Hakuna kiongozi wa CCM aliyejua kwamba mama Kilango angeuliza swali kuhusiana na Mafisadi wa EPA kabla ya bunge kuanza ila kuna uwezekano watu wa karibu naye iwe ndani ya CCM, ama marafiki wanaweza kuwa nataarifa hiyo kutokana na ukaribu wao kwa mtoa hoja...
Hofu yangu kubwa isije kuwa CCM wakaunda FITNA na kusema kwamba hoja ya Wangwe inahusiana na Mbowe wakati swala na matatizo ya ndani ya chama cha Chadema huwasilishwa kwa wanachama wa chama hicho wazee, ama viongozi wa chama na sio bungeni..
Kwa hiyo tuwe macho tuelewe kwamba hapa CCM wanaweza kusuka FITNA na dalili zimeshaanza kujitokeza kiasi kwamba mimi hapa najiuliza ilikuwaje CCM wawe na nakala za malalamiko ya Wangwe kuhusiana na viongozi wa Chadema hali marehemu alisema anapeleka kesi hiyo kwa wanachama na hata ikibidi kufika Mahakamani atakwenda kupata haki yake.. hapo hapo tunaelewa wazio kwamba laptop yake ilipotea ama kuibiwa!...
I mean guys kweli hapo kijijini kibaka aibe laptop na kuacha simu za mkono..Of all the thing -laptop ndio ya kwanza kuondoka na huyu Mallya mbali na msukosuko wa ajali aliweza kufahamu kwamba laptop imechukuliwa na vibaka..
Muda gani alikuwa nao kutazama vitu vilivyoibiwa na ashindwe hata kuwafukuza wezi kwa sababu hakuwa na jeraha, alitoka mzima hana hata vumbi!..
Guys something is very wrong!...Ndivyo hata FBI huunda kesi zao jamani tusifikirie tu kwamba hii ni ajali na Mungu ndiye aliyepanga....Basi kama ni kweli Mungu ndiye aliyepanga (mawazo yalifungana na Utumwa wa akili) inakuwaje Mungu huyo huyo amhukumu moto wa Jahanam muuaji hali ni yeye aliyepanga kifo hicho sio muuaji?..
Guys Mungu katupa uwezo wa kuchagua kati ya mema na mabaya.. ni uchaguzi wetu sisi wenyewe ktk kila matendo yetu.. na yeye hujalia mema au mabaya kutokana na maombi yetu wenyewe kufanikisha azma zetu..Shetani ambaye ni nafsi za ubaya wa binadamu hutuangamiza sisi wenyewe hakuna mkono wa Mungu ktk mema ama mabaya na ndio maana tutahukumiwa kwa kila tuliyoyafanya(if you believe in judgement day..).Hii ni imani yangu mimi binafsi..