Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Mzee MKJJ hii issue unajiumiza kichwa tu na pengine hata hao scotland yard ni upotevu tu wa pesa tu za walipa kodi.

Tuwaite scotland yard kwani kodi zetu haziwatoshi hawa mashushushu?

Kinachohitajika ni ukweli hapa...Pamoja na ushirikiano...Ukweli ni kuwa kama wana uwezo wa ku mtrain kijana hivyo basi wana uwezo wa kuwa na wachunguzi wazuri tu.

Kwa kuanzia..Ningependa kujuwa muda kamili wa marehemu kufa..Hilo ni swali la kwanza kwenye uchunguzi kama huu...Mara nyingi wanaangalia chakula alichokula na kufanya comparisions ili kuweza kutambuwa kama muda aliokufa ni saa ngapi.....Kujuwa muda wa mwisho aliokula kungeweza kuestimate kuwa alikufa muda gani kwa ku calculate food digestion time....Hapo ingesaidia sana kwani kama ni kweli ajali ilipangwa..Basi tutajuwa kuwa muda walioutaja kuwa ndio alikufa si kweli.

Hapo ndio tungeweza kujuwa pa kuanzia..Ili kujuwa kama alifia pale kwenye hiyo ajali ama la.
Pia possibilities za kuwa poisoned...Posibility ya huyo kijana kuwa trained kwenye issues kama hizo pia imalizwe na upimaji wa traffic issues...Mfano..je kulikuwa na jitihada za kupiga breki?
Je kama Tairi hizo zilipasuka...Distance a kutokea barabarani hadi hapo gari lilipotuwa ni reasonable?
Je umbali huo unaweza kukubaliana na hoja ya kupinduka huko mara sita?
Na pia MKJJ...Kunahitaji vipi Scotland Yard kwa kijana kusema nani alimtuma na ni shughuli gani walikuwa nazo yeye na marehemu?

Kweli kunahitaji wapelelezi wa nje kwa wao kutueleza kuwa kijana alikwenda huko Libya na vongozi wetu kama nani?

Kama haya maswali rahisi yangejibiwa kwanza...Then tungefikiria hao SY.

Pia kulinganisha na taarifa zote ili pale penye ambiguties pawe ndio pa kuanzia.

Pia bastola ni ya nani...Ilitumika?

Mara ya mwisho kutumika ni lini nk.

Kitendo pia cha kijana kumpigia baba yake simu mara baada ya ajali sambamba na viongozi wengine kinshangaza sana ukichukulia kwamba alitakiwa awe shocked na ajali hiyo badal ya kuwa kama vile hata hakuna kilichotokea zaidi ya tumatone twa damu na funguo za gari pia cellphone.

Kama huyu alikuwa na mafunzo yote hayo badala ya kuitumia bastola yake kwa kumzuia jambazi asichukuwe laptop na pesa..Yeye akabahatika kuachiwa simu yake.

Yani majambazi waache bastola na simu yake...Duh!
 
...
another note: Hili gari liligongwa kwa nyuma upande wa kushoto? kwa sababu ukiangalia hizo picha utaona damage ni mbele upande wa kushoto na nyuma karibu na tanki... ilitakiwa moto uanze?

Mwkjj...kama iligongwa kwa nyuma, hiyo ni bumping technique, "tactical vehicle intervention". Kwa maana hiyo kuna gari ya pili ilihusika (?!), ukirudi kwenye BIG picha unaona scratch marks nyeupe ubavu wa kushoto gari ya Mheshimiwa

Swali; ...huenda 'gari nyeupe' ilihusika?
 
Mkjj hii kitu can be solved so fast ukiangalia hiyo list uliyoweka kuna clues nyingi za kuisolve hii kitu in minutes....!!! Je vyombo vya uchunguzi viko willing kusolve hiki kitu?
 
jmushi.. nani atawahoji Polisi ili waseme ukweli nani aliwapigia simu mwanzo, walifika pale saa ngapi, walikuta mwili vipi, walikusanya ushahidi vipi n.k n.k ???

Jibu lako ni Polisi hao hao wajihoji wenyewe halafu watuambie ukweli, siyo?
 
MKJJ Sirikali itakubali?
Kama walikataa kuhusu FBI na Ballali nani atakubali scotland Yard?
Kama huyo kijana ni operative wa serikali...Je unategemea wataruhusu ahojiwe na hao wapelelezi wa nje?
Labda tuelimishane hapo kuwa utaratibu ni upi.
Kwasababu hata kwenye upelelezi kama huo cha muhimu ni ushirikiano...Kama hawataki kusema walimpeleka Egypt kufanya nini unategemea watakubali ahojiwe na vombo vya nje?

Labda wabanwe...Lakini kama ni inside job...Basi hapa tunazidi kuwapa clues za kuufutilia ushahidi mbali zaidi.

Niliwaambia kabisa kuwa hata wakati wa EPA walisema wanataka wananchi waende wakotowe ushahidi...Ni sawa na ile listi ya madawa...Sasa listi ya madawa unaweza kuta waliyoipeleka ndio wanauwawa na waliotowa siri za serikali ndio pia wanauwawa.

Yani hapo tatizo la Deus Mallya ku appear both sides in chadema and ccm ni very symbolic to Wangwe's charateristic...Characteristic ambayo inaelekea imemponza!

Je...Kijana naye alitakiwa afe ajalini? Maana kuna theory ya kuhusu gari kulipuka...Inawezekana bastola ilikuwa ya kupiga risasi na kulipuwa gari...Inawezekana pia kulikuwa na gari jingine na labda walichelewa kwenda kumalizia shughuli kabla wananchi hawajafika..Kwenye shuguli kama hizo kila operative anakuwa na kipande chake cha shuguli...Na labda kuna mmoja alichemsha..Maana hata kwenye picha inaonyesha kuwa nyumba ziko karibu sana na eneo la ajali na hivyo bahati yao mbaya ni hiyo...The exact location....Mallya naye labda kaponea!?
Maana kama ni kweli ni dili la kumuuwa Wangwe...Then kumuacha SHAHID MKUU KAMA MALLYA NI KOSA LAO AMBALO SIDHANI KAMA WALIDHAMIRIA.

Sasa tuone watafanya nini...Kwani kwakuwa na yeye anajuwa siri za pande zote na HAJAFA...Hilo ni sawa kabisa na kusema Wangwe naye HAJAFA...Kama siri ya marehemu na Mallya naye ni LAZIMA ANAYO...Halafu wanasema NI JASUSI...Ila labda na yeye ana kihirizi chake na ameponea kufa.....Kwasabau kwa situation ilivyo..SIDHANI KAMA NA YEYE ALITAKIWA AWE HAI...Lingebakia jina tu kuwa mkibosho/mchagga alimwua Wangwe!

Kama Kesi ya marehemu haita solve tatizo zima la ufisadi...Then tunaweza kujikuta tukipoteza direction.

Mtizamo wangu mwingine ni kuwa...Kama Ballali ni karata ya chadema dhidi ya ccm...Basi naona ccm na wao wana karata yao.

Inabidi tuanze kujiuliza kama wote wamekufa ama la...Maana hata sura ya marehemu Wangwe mwenyewe ilikuwa haitambuliki..Labda ndugu wa karibu ndio waweze kuutambuwa mwili...Lakini kama ndugu wamekubali yaishe kwa kuridhika kuwa ni ajali...Then ni sawa tu na ndugu za Ballali waliporidhika kuwa na yeye kafa kwenye hospitali ilisoyojilkana.

Thats my take for now...Ila bado tunaangalia situation inavyo evolve.

NB:Kama hawawezi kutowa ushirikiano kwa wakuu wa dola...Watatowa vipi ushirikiano kwa wakuu wa dola wa nje?
watoe ushirikiano kwa nani kama mabosi wenyewe kimya?
Hadi aguswe mtu wa karibu ama waone kifo kinawasogelea ama labda wabanwe kisiasa ndio watakurupuka..Zaidi ya hapo itabakia kuwa SIRI KUU...Kwani hakuna anayejali vilio vya wananchi..Tulikuwa hapa wakati wa Ballali saga..Na sasa nimechoshwa!
Kama kifo kilichotokea hapa USA tulishindwa kukivalia njuga itakuwa vippi cha huko bongo?

Mbona maswali kama watu wa mwisho kuongea nao hayajajibiwa?
Ama ile assumption kuwa kama ni vodacom imekuwa kweli?
 
attachment.php

Ni bahati mbaya sina muda wa kutengeneza animation ya hiyo ajali, lakini iko obvious kulikuwa na burst na rolling.

Hakuna rangi nyeupe, rangi nyeupe unayoiona ni filler upande wa ndani baada ya kubanduka.

Siangalii collision theory kwa sababu:

Mallya kusema wamegongwa ilikuwa rahisi sana, na hata tukisema tukubali Consipiracy theory sio rahisi kukubali kugongwa ukiwa ndani, kwani rolling yake ni unpredictable at High Speed. Na gari isingeweza kujiendesha at high speed.

Pattern ya gari ya kugongwa haiko hivyo.

Tunaendesha upande wa kushoto hivyo ni rahisi kugonga upande wa kulia nyuma kuliko kushoto. Kwani anayegonga itabidi akate kushoto kuipata ile angle.

Hakuna rangi iliyobaki ya gari nyingine.

Hiyo unayoiona hapo ni roll and flip pattern ambayo ni natural kwenye burst with applied brake. Model hiyo ya Corolla haina ABS.

This is what happens when everything is politicized.

Sequence: Wangwe agombana na Chadema, bahati mbaya Wangwe apata ajali, CCM Propagandaist use this to cause rift, the propaganda backfires when Chadema uses counter propaganda and the family ends confused.

Sudden deaths are usual hard to believe.
 
chacha1om4.jpg


Hapa inaonyesha impact imetokea nyuma na wala sio mbele. Uhhh Makubwa haya.

Wana JF,
Chacha Wangwe amefariki kwa ajali na wala si vinginevyo.

Dereva wa gari alikuwa Mallya, na gari ilikuwa inakwenda mwendo wa kasi, ikamshinda nguvu huyu kijana na kuanza kutoka nje ya barabara. Mallya akaona isiwe shida akaachia kila kitu na kuruka. Gari likaviringika na kujipiga kwenye miti ama mawe upande wa nyuma. Wangwe alikaa kiti cha mbele na hakufunga mkanda hivyo alijibamiza kichwa kwenye nguzo ya gari ama mti na ndipo umati ulipomfika.
 
Hiyo unayoiona hapo ni roll and flip pattern ambayo ni natural kwenye burst with applied brake. Model hiyo ya Corolla haina ABS.


Point nzito sana, lakini tatizo ni kwamba taili la nyuma sio kubwa kiasi cha kuipindisha body hapo karibu na mlango wa nyuma, halafu kwa gari dogo lilikouwa na watu watatu wenye nguvu, ni lazima lilikuwa limekaribia max ya uzito wake, kwa hiyo lisingeserereka kwa umbali mrefu sana iwapo tuna-assume kuwa liliserereka kutokana na kuwa kwenye High Speed,

Hapa ni vyema tukapata ukweli wa condition ya hili gari kabla ya ajali, kwa sababu kama ilikuwa ni ajali tu ya kawaida, inatakiwa iwe ilikuwa ni nzee mno kiasi kwamba haikutakiwa kuwepo kwenye bara bara, kwa sababu sio rahisi kwa gari kuserereka na kuishia kuwa kama hii gari ilivyo sasa, ti is just impossible mkuu!

Halafu pia kuna maswali zaidi ya kuhusu Mallya, ni nani hasa huyu kijana? Anafanya nini for a living? Aliwezaje kumsogelea mpak kumfikia mbunge wa taifa, ambaye pia ni makamu wa mwenyekiti wa chama kikubwa cha siasa kama Chadema? Mpaka kufikia kupata trust ya Wangwe na familia yake kwa muda mfupi sana how did it happened?

Halafu pia tujue kama aliwahi kumuendesha mara ngapi toka wajuane? Nini tabia za binafsi za marehemu kwa sababu unaweza kukuta pia kuna ishus hapo, maana hii ya kuelewana na huyu kijana haijakaa sawa, kwamba exactly kulikuwa na nini kati yao? Unajua this is a national tragedy, sasa haiwezi kuchukuliwa kimzaha mzaha, siamini kuwa vyama vinahusika lakini ninaamini kuwa kuna mtu individually anayehusika.

Lakini ninaheshimu sana maoni yako mkuu Insurgent.
 
Insurgent,
Mkuu bado sijazipata picha za Mnyika na kama yupo hapa kijiweni namuomba sana aziweke tena maanake zilikuwa zinaonyesha gari hilo kwa pande zote.. Mkuu kama kuna tairi lililopasuka ni hilo la nyuma na kwa hali inayoonekna haliwezi kupindua gari kwa sababu bado lina Upepo..
Sasa basi pamoja na yote haya tuliyokwisha yapika, lets say Mallya ndiye alikuwa dereva Marehemu alikuwa kiti gani cha mbele upande wa abiria ama nyuma?.. na zaidi ya hapo tuondoe ile statement ya Mallya kwamba Marehemu ndiye alikuwa akiendesha, tutazame upya maelezo yake ambayo nimesema mara 100 kidogo kuwa iwewje yeye awe msafi?... nitaandika upya maelezo yake kwa waandishi wa habari akiwa hospital.

Speaking to reporters who paid him a visit at the hospital, Malya said Wangwe told him to move to the back seat to rest. cannot forget what took place at the scene (of the accident). I don't believe that I have escaped death and I am still alive,`` he said.
``I was seated in the front seat and was dozing off before the accident, but he advised me to move over to the back seat because it was not safe where I was seated,`` he said.
Je kweli alikuwa seat ya mbele?... hapana!
Malya said they stopped over on the way to buy recharge vouchers before they proceeded with their journey. We were at Pandambili when I heard a great bang and saw a cloud of dust. It is then that I realised that the car`s tyre had burst.
Tairi gani lililopasuka hadi kusababisha ajali, hilo la nyuma kwa jinsi navyofahamu haliwezi kabisa kupindua gari..
The vehicle was engulfed in dust. Wangwe moved from where he was seated to the place where I was with his head touching my legs.
Swali langu is this possible kweli jamani, kulingana na gari tunavyoliona yaani kichwa kiweze kugusa miguu yake kiti cha nyuma? unless alikuwa na maana yeye ndiye miguu yake ilipanda juu kutokana na kubwanwa..again hata hivyo kiti kimelala pande usio wa dereva..
Je kuna mtu mwingine aliyekuwa akiendesha ambaye aliingia ndani ya gari na Mallya hakumwona akiendesha hivyo kufikiria kuwa Marehemu ndiye alikuwa bado akiendesha? kama ni uongo iweje kila alichosema hapa kinaonyesha wote ni UONGO!..
He said by the time he wanted to see more on what had taken place, he realized that Wangwe's head had sustained a fracture and a lot of blood was coming out.
``My body was soaked in blood, but that blood was not mine but Wangwe`s,`` he said.
-
Jamani hivi kweli he was soaked in blood au picha zinatudanganya!..
Hapa ndipo maswali mengi yalipoanzia na upishi wa theory za conspiracy toka pande zote..Haya wataalam twambieni hilo Corolla ni aina gani na la mwaka gani!
 
Jasusi maana yake ni Spy kuna watu wamechanganya na neno Gaidi ambalo lina maana ya Terrorist!..
Je kuna uwezekano wa huyu kijana kuwa jasusi? UPO! sioni kitu gani watu wanampigia kelele Lipumba hali kiongozi huyu au HAWA wana uwezo wa kupata habari zenye uhakika kuliko sisi..

Yebo Yebo kuna mbunge kamruka kasema hamjui ati walikutana kwenye ndege tu.. Hivi kweli ni rahisi kwa mtu kudandia safari za viongozi bila wao kufahamu unahusika vipi wala kuhoji..Hivi kweli ni rahisi kwa kiongozi kukusaidia Immigration unapokwama ktk nchi ya ugenini bila kukufahamu?..Halafu basi hata hao immigration Officer wapikwe na kukubali kumwachia aendelee na safari?.. jamani acheni kutupaka mafuta hapa!..Kisha basi jinsi alivyoendelea na safari ndio hapo nilipokoma mwenyewe..

Insurgent,
Huyo baba yake huyu kijana hajui kitu zaidi ya kuwa na mwanae wakati akisoma shule ya msingi.. nina hakika hapo alipo hajui hata shule gani ya sekondari mwanaye alisoma!...Kifupi huyu baba yake hamfahamu mwanaye zaidi ya kumzaa!
Kweli kabisa tunahitaji vijana kama hawa wanaoweza kujisomesha wenyewe lakini sio kuanzia sekondary mkuu, hapa kijana huyu kwa umri pengine alikuwa na miaka 15 hizo fedha za kujisomesha atazipata wapi?..Je sii kusababisha Uhuni ama wizi mkuu kuwafanya vijana wadogo kama hawa watafute elimu zao wenyewe?.. ndio haya haya vijana kama hawa hugeuzwa kuwa assassin umeyaona Kongo, Uganda, Sierra Lione yaani nchi zote maskini sioku hizi vijana wadogo wenye njaa ndio hugeuzwa kuwa wauaji wakubwa!..They have nothing to loose!..
 
MIONGONI mwa watu wanaomfahamu kwa undani aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Zakayo Wangwe, ni Diwani wa Kata ya Kemambo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Agustino Neto Sasi.


Si tu kwamba anamfahamu kutokana na kuwa karibu naye kwa muda mrefu, bali pia kufuatia msimamo wa marehemu Wangwe katika kupigania haki za wananchi.


Sasi alimwambia mwandishi wa habari hii hivi karibuni kwamba, wakati huo yeye (Sasi) aliwa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kewanja na mwanachama wa Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM), alivutiwa sana na sera za Wangwe na hatimaye kuungana naye katika kuwatetea wananchi wa kijiji chake kudai fidia kwa mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu East Africa (East Africa Gold Mine).


Alifahamisha kwamba, wakati huo Wangwe alikuwa Mwenyetiki wa Chadema Wilaya ya Tarime na mwekezaji huyo alikuwa ameanza kujenga mgodi huo.


Sasi alidokeza kuwa katika harakati za kuwatetea wananchi waliokuwa kwenye eneo la mgodi huo, alikuwa akiwambia kwamba wanapaswa kuingia ubia na mwekezaji huyo na si kulipwa fidia kama walikukuwa wameahidiwa hivyo kuibua machafuko.


Alisema kutokana na hoja hizo za Wangwe, wananchi waliandamana na kuuvamia mgodi huo, hivyo kama Mwenyekiti wa Kijiji (Sasi) alikamatwa kwa madai ya kushirikiana na Wangwe kuwahamasiaha wakazi hao kuvamia mgodi huo.


''Wangwe alikuwa kiongozi wa chama cha upinzani na mimi nilikuwa mwenyekiti wa kijiji wa CCM, lakini kwa kuwa niliona anadai haki za wanyonge tulikuwa tukiongozana kwenye kampeni zake za kuwahamasisha wananchi kudai haki zao, hivyo tulikamatwa pamoja na watu wengine zaidi ya 15, lakini baada ya kufanyika uchambuzi tulibakizwa mimi na Wange tulifunguliwa kesi,'' alisema Sasi.


Alisema baada ya kukamatwa aliambiwa kuwa ailikuwa akishirikiana na kiongozi wa upinzani kukihujumu CCM akiwa kama kiongozi chama hicho.


''Tulishitakiwa na kufikishwa mahakamani pamoja na Wangwe, mimi nilikuwa mshitakiwa wa kwanza na John Mang'enye ambaye wakati huo alikuwa Diwani wa CCM pia alikamatwa na kuwa mshitakiwa wa pili na wa tatu alikuwa marehemu Christopher Iluga,'' alisema na kuongeza:


"Tulipofikishwa mahakamani na kushitakiwa wengine waliachiwa tukabaki mimi na marehemu Wangwe, mimi nikahukumiwa kwenda jela miaka miwili kwa kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha. Wakati naendelea kutumikia kifungo nilifuatwa jela na kufikisha mahakamani tena nikiunganishwa na Wangwe katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha na kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na marehemu alikuwa na kesi nyingine ambapo alifungwa mwaka mmoja jela.


''Baada ya kuhukumiwa miaka 30 jela, marehemu aliniambia kuwa nenda jela utarudi kwa sababu umefungwa kwa uonevu kutokana kutetea haki za wananchi.''


Kutokana na mazingira hayo, waliamua kunihamisha kutoka Gereza la Tarime na kunipeleka Butimba, nilikotumikia kifungo mpaka nilipotolewa na Mwanasheria wa Chadema Tindu Lisu.


"Lisu alinikatia rufaa na kushinda na kutolewa gerezani baada ya kubainika mahakamani kwamba nilifungwa kwa uonevu. Lisu alisimamia rufani yangu baada ya kumkatia rufaa marehemu Wangwe na kushinda.


Alisema baada ya kutoka grezani alibaini kwamba alichukuliwa hatua hiyo kwa shinikizo la CCM kutokana na yeye kushirkiana na Wangwe ambaye ni wa chama cha upinzani kudai haki za wananchi.


"Baada ya kutoka gerezani nilibaini kuwa CCM ndiyo iliyokubaliana kwamba nifungwe kwa sababu ya kushirikiana na Wangwe kudai haki za wananchi, hivyo niliamua kuihama CCM na kujiunga na Chadema.


Hata hivyo aliyenivutia zaidi kujiunga na chama hicho ni marehemu Wangwe ambaye alikuwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya wanyonge, alisema na kuyongeza:


"Nalimfahamu Wangwe kutokana na msimo wake thabiti katika kudai haki za wanyonge na kutokana na mimi kuwa mkereketwa wa haki, nilijenga urafiki mkubwa naye."


Alifahamisha kwamba baada ya kujiunga Chadema aliendelea na harakati zake za kutetea haki za wananchi mpaka akachaguliwa kuwa diwani Kata ya Kemambo kwa tiketi ya chama hicho.


"Baada ya kujiunga na Chadema, mwaka 2005 niliamua kugombea udiwani wa kata ya Kemambo nikashinda na Septemba 2006 nilienda Nigeria kuwaikilisha nchi yetu katika mkutano wa Afrika wa Migodi na Mafuta ( Pan African Mining and Oil Conference) ambako nilikaa siku saba na niliporudi tulianzisha (pamoja na Wangwe)hoja kwamba wananchi hao wajengewe nyumba na mgodi ikiwa ni sehemu ya fidia ya kuchukuliwa maeneo yao."

Source: Mwananchi


Na hili wanaforum mnasemaje? Inaonekana mengi yatazidi kufunuliwa.
 
deny_all,
Mkuu hii habari nzito sana tena inashtua sana lakini kabla sijaendelea zaidi naomba chanzo cha habari hii maanake umesema Sasi alimwambia mwandishi wa habari hii - Je, ina maana mwandishi hapa JF au chombo gani cha habari?..
Ningependa sana kupata uhakika wa habari hii..
 
Source ni Mwanachi kama unavyoona hapo chini na Mwandishi ni Fredrick Katulanda
**************************************************************
Date::8/4/2008
Rafiki ya Chacha Wangwe afichua vituko vya CCM Taarime
Frederick Katulanda

MIONGONI mwa watu wanaomfahamu kwa undani aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Zakayo Wangwe, ni Diwani wa Kata ya Kemambo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Agustino Neto Sasi................


.
 
Hii gari haijagongwa kwa nyuma hata kidogo.
Nimeona ajali nyingi sana hapa USA wakati wa ajali gari zinachakaa vibaya sana upande wa nyuma lakini si kwa kugongwa nyuma, ila ni kwa kugonga mbele kwanza na kisha kugeuka haraka sana na kugonga nyuma.Mara nyingi gari hugeuka haraka kiasi hicho kwa vile speed and mpact hufanya gari lielee angani kwa sekunde mbili au tatu hivi.

Gari limepondwa upande wa mbele kushoto na upande wa nyuma kushoto kwa hiyo ni lazima dharuba zilitokea pande hizo. Siwezi kusema kuhusu upande wa kulia kwa sababu sina picha inayoonyesha upande huo umeharibika kiasi gani.

Kwa kutumia upande unao onekana naweza kusema mambo kibao kukataa Theory ya kugongwa kwa nyuma, japo siwezi kukataa kabisa kuhusika ama kuwepo kwa gari la pili katika ajali hii.

Si lazima kwamba gari hii ilipasuka tairi kwanza ndipo mambo mengine yalifuata.
Yawezekana Dereva alisinzia na kuacha njia huku akiwa kwenye speed kali au gari lilimshinda kuongoza katika speed hiyo na hivyo kumfanya dereva abakie msindikizaji zaidi kuliko kwamba ni mwongozaji.

Kwa namna yeyote gari la Marehemu Wangwe liligonga kwa kubabatiza kitu kilicho simama upande wa kushoto wa barabara zaidi gema, ukuta au miti mikubwa.
Nasema kitu kilicho simama kwa sababu kingekuwa ni kitu kilicho kuwa kwenye mwenda,upande upande wa kushoto ungechakaa kwa kuchanjwachanjwa mistari katika mabati na mistari hiyo ingeonyesha kuanza upande wa mbele na kuishia upande wa nyuma, ingetengeneza kitu kama <. Au mabati ya gari yangeraruriliwa na kukunjwa kelekea nyuma.

Inaonekana kwa mara ya kwanza gari iligonga upande wa mbele huku ikiwa imelalia zaidi upande wa kushoto kwa kuzingatia kingo za barabara zilivyo. Kwa vile ilikuwa katika mwendo mkali nguvu ile ya kugonga iliisukuma gari kulekea barabara na hivyo kusababisha upande wa nyuma kwenda kugonga mahali upande wa mbele ulipogonga ikizingatiwa kwamba gari lilipaa hewani kwa sekunde kadhaa. Mara baada ya gari kugonga kwa mara ya pili ni lazima lilijaribu kurudi barabarani. Kwa vile siku zote barabara huinuliwa zaidi kuliko kingo zake, jitihada hizo za kurudi barabarani huenda zilifanya gari ipinduke upande wa kushoto ukianza na pengine kuvingirika na kurudi na kukaa sawa kwa matairi yake kama vile hakuna kilichotokea.

Gari ikiwa katika mwendo wa 65MHR au 120KMhr hekaheka ikitokea inaweza hata ikapaa na kukaa juu ya panda ya mti ulio karibu na barabara.

Mabati yanaonyesha kubonyea kutoka upande wa kushoto wa gari kuelekea upande wa ndani ya gari zaidi kuliko kuelekea nyuma ya gari au mbele ya gari.
Kwa hiyo gari haikugongwa kwa nyuma wala kwa mbele bali ilipata dharuba upande wa kushoto.
Milango yote miwili inaonekana bado imejikita vizuri kwa sababu lock zake za kuzuia isifunguke wakati wa ajali zilifanya kazi yake vizuri.

ukiangalia Frame ya kiyoo cha nyuma una ona wazi kwamba ile dharuba kutoka upande wa kushoto ilijaribu kugawana maumivu na upande wa kulia wa frame lakini upande wa kulia ukagoma kwa vile ulikuwa imara hivyo kupelekea kiyoo kuapasuka na frame yenyewe kukunjika katika jitihada za kuhamishia Force upande wa juu. Kitendo hicho cha frame ya kiyoo cha nyuma kukunjika ghafla kulekea juu kilifanya upende wa kusho wa paa la gari kuelekea karibu kabisa na alipokuwa Marehemu wangwe na pengine hii ndiyo asili ya kuumia kwake kichwani. Hasa ukizingatia kwamba wakati gari linageuka kuelekea barabarani tena Marehemu ni lazima aliendelea kuobey Newton Law na hivyo kufanya azidi kwenda kushoto wakati gari linakwenda kulia au kuzidi kwenda mbele wakati gari linakwenda kulia baada ya dhoruba kutokea.

Dhoruba ya gari kugonga kwa nyuma ilikuw kali sana kiasi cha bamba lote la nyuma na taa kung'ooka kabisa nakubakia pale pale ilipogonga. Ukiangalia upande wa kulia unaona taa bado zipo na shape ya Corolla bado inaonekana.

Je ni kweli gari iligongwa kwa nyuma??
 
Jamani hebu naombeni mnisaidie maana kamili ya neno JASUSI, manake nakumbuka hata polisi walishawahi kudiriki kusema Jambo Forum ni ya kijasusi...!

Sasa nini maana kamili ya JASUSi? na Je Jasusi ni mtu au kitendo?
Mhafidhina,'
Jasusi ni mtu. Si kitendo. Ujasusi ni kitendo. Jasusi katika nchi kubwa kama vile Marekani anaitwa CIA operative. Kule Moscow anaitwa KGB. Hawa ni watumishi wa serikali. Kazi yao ni undercover. Yaani anaweza mtu kujitokeza kuwa ni mfanyibiashara kumbe ni jasusi wa kutupa. Mengine jazia mwenyewe.
 
deny_all,
Mkuu hii habari nzito sana tena inashtua sana lakini kabla sijaendelea zaidi naomba chanzo cha habari hii maanake umesema Sasi alimwambia mwandishi wa habari hii - Je, ina maana mwandishi hapa JF au chombo gani cha habari?..
Ningependa sana kupata uhakika wa habari hii..


Amesema mwananchi sentensi ya mwisho kabisa:INAHUZUNISHA!!!
 
MIONGONI mwa watu wanaomfahamu kwa undani aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Zakayo Wangwe, ni Diwani wa Kata ya Kemambo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Agustino Neto Sasi.


Si tu kwamba anamfahamu kutokana na kuwa karibu naye kwa muda mrefu, bali pia kufuatia msimamo wa marehemu Wangwe katika kupigania haki za wananchi.


Sasi alimwambia mwandishi wa habari hii hivi karibuni kwamba, wakati huo yeye (Sasi) aliwa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kewanja na mwanachama wa Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM), alivutiwa sana na sera za Wangwe na hatimaye kuungana naye katika kuwatetea wananchi wa kijiji chake kudai fidia kwa mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu East Africa (East Africa Gold Mine).


Alifahamisha kwamba, wakati huo Wangwe alikuwa Mwenyetiki wa Chadema Wilaya ya Tarime na mwekezaji huyo alikuwa ameanza kujenga mgodi huo.


Sasi alidokeza kuwa katika harakati za kuwatetea wananchi waliokuwa kwenye eneo la mgodi huo, alikuwa akiwambia kwamba wanapaswa kuingia ubia na mwekezaji huyo na si kulipwa fidia kama walikukuwa wameahidiwa hivyo kuibua machafuko.


Alisema kutokana na hoja hizo za Wangwe, wananchi waliandamana na kuuvamia mgodi huo, hivyo kama Mwenyekiti wa Kijiji (Sasi) alikamatwa kwa madai ya kushirikiana na Wangwe kuwahamasiaha wakazi hao kuvamia mgodi huo.


''Wangwe alikuwa kiongozi wa chama cha upinzani na mimi nilikuwa mwenyekiti wa kijiji wa CCM, lakini kwa kuwa niliona anadai haki za wanyonge tulikuwa tukiongozana kwenye kampeni zake za kuwahamasisha wananchi kudai haki zao, hivyo tulikamatwa pamoja na watu wengine zaidi ya 15, lakini baada ya kufanyika uchambuzi tulibakizwa mimi na Wange tulifunguliwa kesi,'' alisema Sasi.


Alisema baada ya kukamatwa aliambiwa kuwa ailikuwa akishirikiana na kiongozi wa upinzani kukihujumu CCM akiwa kama kiongozi chama hicho.


''Tulishitakiwa na kufikishwa mahakamani pamoja na Wangwe, mimi nilikuwa mshitakiwa wa kwanza na John Mang'enye ambaye wakati huo alikuwa Diwani wa CCM pia alikamatwa na kuwa mshitakiwa wa pili na wa tatu alikuwa marehemu Christopher Iluga,'' alisema na kuongeza:


"Tulipofikishwa mahakamani na kushitakiwa wengine waliachiwa tukabaki mimi na marehemu Wangwe, mimi nikahukumiwa kwenda jela miaka miwili kwa kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha. Wakati naendelea kutumikia kifungo nilifuatwa jela na kufikisha mahakamani tena nikiunganishwa na Wangwe katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha na kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na marehemu alikuwa na kesi nyingine ambapo alifungwa mwaka mmoja jela.


''Baada ya kuhukumiwa miaka 30 jela, marehemu aliniambia kuwa nenda jela utarudi kwa sababu umefungwa kwa uonevu kutokana kutetea haki za wananchi.''


Kutokana na mazingira hayo, waliamua kunihamisha kutoka Gereza la Tarime na kunipeleka Butimba, nilikotumikia kifungo mpaka nilipotolewa na Mwanasheria wa Chadema Tindu Lisu.


"Lisu alinikatia rufaa na kushinda na kutolewa gerezani baada ya kubainika mahakamani kwamba nilifungwa kwa uonevu. Lisu alisimamia rufani yangu baada ya kumkatia rufaa marehemu Wangwe na kushinda.


Alisema baada ya kutoka grezani alibaini kwamba alichukuliwa hatua hiyo kwa shinikizo la CCM kutokana na yeye kushirkiana na Wangwe ambaye ni wa chama cha upinzani kudai haki za wananchi.


"Baada ya kutoka gerezani nilibaini kuwa CCM ndiyo iliyokubaliana kwamba nifungwe kwa sababu ya kushirikiana na Wangwe kudai haki za wananchi, hivyo niliamua kuihama CCM na kujiunga na Chadema.


Hata hivyo aliyenivutia zaidi kujiunga na chama hicho ni marehemu Wangwe ambaye alikuwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya wanyonge, alisema na kuyongeza:


"Nalimfahamu Wangwe kutokana na msimo wake thabiti katika kudai haki za wanyonge na kutokana na mimi kuwa mkereketwa wa haki, nilijenga urafiki mkubwa naye."


Alifahamisha kwamba baada ya kujiunga Chadema aliendelea na harakati zake za kutetea haki za wananchi mpaka akachaguliwa kuwa diwani Kata ya Kemambo kwa tiketi ya chama hicho.


"Baada ya kujiunga na Chadema, mwaka 2005 niliamua kugombea udiwani wa kata ya Kemambo nikashinda na Septemba 2006 nilienda Nigeria kuwaikilisha nchi yetu katika mkutano wa Afrika wa Migodi na Mafuta ( Pan African Mining and Oil Conference) ambako nilikaa siku saba na niliporudi tulianzisha (pamoja na Wangwe)hoja kwamba wananchi hao wajengewe nyumba na mgodi ikiwa ni sehemu ya fidia ya kuchukuliwa maeneo yao."

Source: Mwananchi


Na hili wanaforum mnasemaje? Inaonekana mengi yatazidi kufunuliwa.


Mkuu kuna la kusema hapa zaidi ya mshtuko tena mkubwa, acha nifute machozi kwanza
 
Mgagagigikoko,
Mkuu huyu baba yake kijana inaonyesha hamjui kwa sababu statement yake inaonyesha alimsomesha hadi darasa la saba toka hapo Mallya alihamia Dar, mzee hajui kitu zaidi ya kwamba alijisomesha.. Sasa wewe nambie kijana wa miaka 15 aliweza vipi kujisomesha hadi form four na zaidi ya hapo mzee anasema alijifunza Komputa unajua tena bongo hata ukienda kujifunza programs za window (word, excel na kadhalika basi upo kwenye utaalam wa komputa...
Huyu kijana mkuu anatisha!.. binafsi sina hamu naye naogopa CV yake!
 
deny_all,

Kwanza karibu sana kwenye kijiwe cha JF.


Mimi ni mtu mzima kiasi kuwa machozi yangu huwa hayatoki kurahisi kabisa. Ila stori hiyo hapo juu imeniumiza sana na kujikuta machozi yananilengalenga machoni.

Utadhani kuwa sisi tuliumbiwa mabaya tu, na inapokuwaa mazuri yanakuja basi yanakumbwa na misukosuko mingi sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom