Kama huyu kijana ndiye alikuwa anaendesha gari, hana leseni, na kwa mwendo kasi; kwanini ameshtakiwa kwa makosa ya kutokuwa na leseni na kuendesha gari kasi bila kushtakiwa kwa kosa la kusababisha kifo? Akili mukichwa. Tukubali tu ilikuwa ni ajali ya kawaida (kwamba mtu asiye ne leseni, anaenda kasi, anamuendesha Mbunge wa Bunge la Muungano - ni kawaida tu)?
Mkuu MWKJJ,mpaka hapo tulipo sasa hata akishitakiwa kwa kosa la kusababisha kifo siyo hoja kubwa sana kulingana na aina ya tukio.Akishtakiwa tu hivyo na akihukumiwa itakuwa shangwe kwa upande wa wataka mabaya kwani atakata rufaa na atashinda kesi.Niamini mimi.Hadi hapo bado ni traffic case. "KUNA DREVA MMOJA WA DALADALA ALIKUWA ANAFANYA SAFARI ZAKE KILA SIKU KUTOKA POINTI A KWENDA B HUKU GARI LAKE LIKIWA HALINA BREKI.ALITUMIA UZOEFU WA KUSIMAMA KWA KUWEKA GIA KUBWA,SIKU MOJA GARI LIKAMSHINDA AKALIPINDUA NA KUUA ABIRI WOTE.POLISI WAKAMKAMATA NA KUMSHITAKI KUSABABISHA VIFO.AKAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA.BAADAE AKAKATA RUFAA,KATIKA RUFAA AKAACHILIWA HURU KWANI JAJI ALISEMA MSHITAKIWA ALIKUWA ANAFANYA KAZI ZAKE KILA SIKU NA HAKUWAHI KUUA,NA HAIKUWA MARA YA KWANZA KUENDESHA GARI LIKIWA HALINA BREKI.HIVYO IKABIDI AHUKUMIWE AS TRAFFIC CASE KWA KUENDESHA GARI LIKIWA HALINA BREKI NA KUTWOZWA FAINI 20,000/=
Labda tuwekane sawa (kisheria) kuwa ili kesi iwe ya mauaji kuna elements zake za ili tendo hilo lijitokeze la mauaji. Yaani namaanisha kuwa kuna kitu kinaitwa "intetion".Kuendesha gari kwa kasi bado kisheria hai-intend kuua.Mallya kwenye utetezi atasema hivyo.Niamini mimi.Lakini kwa undani wa nje ya sheria utaona dhairi kuwa intetion ya Mallya ilikuwa ni kuua.Sasa hapo ndo kuna utata.Kimsingi hadi hapo mallya alipo atatoka tuu.Ila kama kweli polisi wetu ambao mimi mara zote nawaita wazee wa ku-bold na italic wako serious na issue hii basi waende hatua nyingi tu mbele ya suala hili ili tupate intetion za Mallya kisheria za kuua hili shitaka libadilike na asomewe mauaji.
NINGEKUWA MIMI POLISI,zooote hizi nisingesumbuka nazo sana ila ningeanza tu na upatikanaji wa siraha -pistol.
Jamani tufungue macho,kama kweli mallya alikutwa na pistol,wote tunajua process za kumiliki siraha TZ zikoje.Nimemsoma mallya kwenye picha na nimeona umri wake,hulka na silka yake bado natatizwa na umiliki wake halali wa siraha hasa pistol kama kweli alikuwa nayo.Yaani hapo ndo ningeunganisha dots na kupata pa kumshikia.
Kumpa Mallya ujasusi mimi bado inanipa wasiwasi.Tunamkuza mno.Hakuna jasusi hasiyekuwa makini kiasi hicho.Yaani jasusi anakana hadi kujua kuendesha gari??????Nope.Angekuwa jasusi palepale angekubali kuwa yeye ndo alikuwa dreva.Kwisha habari.Tusingefika kote huku.ILA UKIONA HIYO TREND UTAGUNDUA KUWA MALLYA ALIKUWA ANAPEWA MAELEKEZO NA MTU/WATU WENGINE.Yaani kuna watu walikuwa wanamshauri afanye nini hasa kukubali kuwa yeye ndo alikuwa dreva na mambo mengine kama hayo.so kuna vitu bado vimejificha vingi tuu.
-huyu mallya mimi namuona kama alikuwa ni nyoka tu ila kazi yake ya unyoka anaijua barabara,si wa kucheza nae akikupatia sehemu zake,hata hivyo kajawa na usanii hicho ndo kimemharibu zaidi na haridhiki.