Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
...kuna jambo linanitatiza ...ni kwa nini ccm walianza kusambaza waraka wa chacha ..siku ile kabla ajali haijatokea????....walipanga kutumia tukio la ajali kama mtaji wa kuimaliza chadema??...na walijuaje kaama ajali itatokea???
 
...wakuu kwa nini ccm walianza kusambaza waraka wa wangwe dhidi ya chadema siku ile kabla ya ajali ...mikoani...,walipanga kutumia kisiasa...na walijuaje kama wangwe angefariki ..ili huo waraka upate nguvu kisiasa??
 
kwa nini ccm walisambaza kwa kasi waraka wa siri wa wangwe...[ref mwananchi]..ile siku kabla ya ajali....walijuaje kuwa wangwe angepata ajali ..ili huo waraka uwe na nguvu kisiasa!!!...........inawezekana hii plot imefanywa na .....ili wautumie kuimaliza chadema...hasa kutokana na mgogoro uliokuwepo?????...........
 
Source ni Mwanachi kama unavyoona hapo chini na Mwandishi ni Fredrick Katulanda
**************************************************************
Date::8/4/2008
Rafiki ya Chacha Wangwe afichua vituko vya CCM Taarime
Frederick Katulanda

MIONGONI mwa watu wanaomfahamu kwa undani aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Zakayo Wangwe, ni Diwani wa Kata ya Kemambo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Agustino Neto Sasi................


.

nimeamua kuwawekea picha ya diwani huyo aliyeeleza mambo hayo Bw. Sasi, ambaye ndiye ninaimani kuwa aliongea na mwandishi huyo.
 

Attachments

  • P1010243.JPG
    P1010243.JPG
    459.4 KB · Views: 86
Kuna taarifa za kuaminika kuwa Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu Mwenyekiti wa kamati ya wabunge aliyeenda Tarime Akiongoza timu ya wabunge atatoa ripoti ya kilichojiri huko .

Tusubiri tuone kuwa Bunge litaungana na upande upi kati ya ule wa Lyatonga Mrema ,Lipumba na Mbatia,pamoja na waandishi wa habari ama litaungana na Zitto,pamoja na Jukwaa la Wahariri.

Jambo hilo linategemewa kufanyika kuanzia majira ya saa nne na nusu asubuhi hii ,hivyo tufuatilie .
 
hawa viongozi wetu wa upinzani hawana intelligence system yao. wanunganisha habari za magazeti wanaconclude. they may mislead us if we are not careful enough
 
...kuna jambo linanitatiza ...ni kwa nini ccm walianza kusambaza waraka wa chacha ..siku ile kabla ajali haijatokea????....walipanga kutumia tukio la ajali kama mtaji wa kuimaliza chadema??...na walijuaje kaama ajali itatokea???

KWELI hili linashangaza lakini nadhani kuwa, 1. pengine ni kweli walikuwa wakishirikiana naye, 2. pengine mchezo unaotajwa kuwa ajali ilipangwa unaweza kuwa sahihi kwa maana kuwa walaka huo ulitoka kwa makamba kwenda kwa viongozi wake wasaidizi ili kungojea kifo waanze sambaza.
Shabaha ya kusambaza nafikiri inaweza kuwa hii:

1.Kutumia tamko hilo kwa vile linaeleza wazi uchafu wa Mh. Mbowe kwa kina (kama ni kweli waraka huu ni wa Wangwe).
2.Kupatikana kwa waraka huo ilikuwa siraha tosha kwa kuisambaratisha Chadema,
3. Kwa vile walianza kuusambaza siku moja kabla ya kifo chake inanitia shaka huenda wakawa wamepanga ajali hiyo ili wazushe mbowe kahusika na ndivyo ilivyotoke sasa chadema imelazwa ICU kutokana na msiba huo wa Wangwe.

ukiuangalia kwa makini waraka huo unaweza kuamini kuwa Wangwe alimshika pabaya Mbowe na hivyo unaweza kuingia katika Propaganda za CCM kuwa huenda Mbowe kahusika. Yote ni utata mkubwa.
 
Ni kweli kuwa Sas aliweza kuhukumiwa vifungo hivyo, na pia kuna jambo hamlijui huyu mzee Sas ni mwanajeshi mstaafu kutoka JWTZ.

Ntaweka simu yake kwa wale mtakaotaka kumhoji zaidi ana story za kuhuzunisha sana sana ,kwani hata nyumbani kwake walitaka kumtoa kwa kile kinachoitwa wanakijiji wamemkataa n.k.

Nchi hii ina mambo mengi sana ya ajabu ajabu.
 
Shelukindo ataanza kunena hivi punde kuhusiana na kilichojiri humo Tarime na kilichowasibu mpaka wakarudi na rambirambi zao.
 
Baadhi ya hawa wa kwetu saa nyingine wanaona fahari kujitambulisha kwamba wako IKULU!
 
Ana fani ya usanifu aliyoipata Nairobi katika Chuo cha Mtakatifu Hubert baada ya kumaliza sekondari kidato cha nne.

Mafunzo ya kompyuta baada ya kupata mtu wa kumfundisha na baada ya kumudu mafunzo hayo alijishughulisha na kazi ya kutengeneza fulana, ambayo anaendelea kuifanya hadi sasa.

Anayejishughulisha na kazi ya kuchapisha maandishi na picha kwenye fulana na kazi hiyo ndio ambayo amekuwa akiifanya kwa ajili ya shule, makanisa na vyama vya siasa.

Hapa kuna walakini
 
Vita vya panzi furaha ya kunguru. Hivi CHADEMA mlikuwa mnafikiri mtagombana na CCM watakaa kimya wakiwaombea mpatane? Hiyo ni naivity ya hali ya juu sana hasa kwenye siasa.

Mbona Kolimba aliposema CCM haina dira, mlikuwa wa kwanza kurukia kwenye huo ugomvi na kufanya naye vikao vya siri?

Mchawi hapo ni huo ugomvi wenu. CCM wametumia tu hiyo nafasi mkiwa mnagombana ili kuingiza sumu yao. Mtasema CCM walipata wapi waraka wa Wangwe, mnafikiri Wangwe alikuwa mjinga apigane peke yake? Kama ambavyo CHADEMA ina magazeti ya propaganda kama Tanzania Daima, kwa vyovyote na yeye alitafuta watu wa kumsaidia kwenye vyombo vya habari ambavyo vingi vyao vinatumika kuenenza propaganda za CCM.

Ushauri hapo ni don't wash your dirty linen in public, maana huko nje kumejaa mafisi yanayozengea info kama hizo ili kukudhalilisha.
 
Anatoa maelezo chini ya kanuni ya 50 ya bunge, anasema kuwa kanuni zinaelekeza masuala ya kufanyika pindi inapotokea kuwa mbunge amefariki, na anasema kuwa yeye aliteuliwa na Mheshimiwa spika kuwa mwenyekiti wa ujumbe aakiwa na Wanyancha, mkono, john chetyo,sarungu,hamad ,mnyaa,slaa,juma kilimba ,zitto,kabaka,masunga joyce,jaeth masaburi.suzan lyimo ,james nsekela ,vedastus manyinyi .

waliondoka saa mbili na nusu asubuhi na kuwasili saa tano kamili asubuhi,na kupokelewa na mkuu wa mkoa akiwa pamoja na viongozi wengine wa kisiasa.

waliondoka na masafara wa magari ya serikali, na ujumbe ulipofika ulibaini kuwa mambo sio shwari kwani vijana wengi walikuwa wanarandaranda na mabaongo na kuonyesha kuwa palikuwa na mtafaruku, na walipodadisi kwa viongozi wa serikali waliambiwa kuwa mazishi hayatafanyika siku hiyo kutokana na ndugu kuwa na wasiwasi juu ya msiba husika , na baada ya hapo walijadiliana na ndugu hao wakiwa na mkuu wa mkioa wa mara na kwa kuwa ujumbe wa spika ulikuwa ni kwa ajili ya kusoma risala na kukabidhi mchango wa rambirambi .

wakataka wasome risala na ujumbe uweze kuondoka ,ila ilipofika saa nane na dakika 30 mtafaruku ulianza na wananchi walisema kuwa wako tayari kiumchagua mwingienwakamuue tena , na katika hali waliyoiona hawakuwa na njia nyingine ila ni kwa ujumbe kuondoka na kuelekea musoma na kurejea dodoma .

kabla ya kuwasilisha maelezo hayo ,walipata taarifa za uhakika kutoka kwa viongozi wa mkoa wa mara kuwa uchunguzi ulifanyika na ndugu kukubaliana na uchunguzi huo,na tayari alishazikwa.

Kwa kuwa mazishi yalishafanyika, wanaandaa utaratibu wa kuwasilisha mchango wa rambirambi ya bunge kwa familia ,anashukuru bunge kwa kuwapa heshima ya kuliwakilisha ,na jukumu lilikuwa zito na nyeti na lenye utata mkubwa.

mwisho anaushukuru kwa dhati uongozi wa mkoa wa mara kwa ushirikiano mkubwa na pia anawashukuru wabunge wenzake kwa uadilifu na pia ushirikiano kwa kipindi chote ,pia anampongeza spiaka kwa kuwezesha TBC kuweza kushiriki shughuli za mazishi na pia kwa wao kuweza kuonyesha mazishi hayo live.

amemaliza.

swali;mbona hakuna cha mapanga, sime,mishale, marungu .n.k?

yeye anasema kuwa waliona mabango na vijana wakiimba kwa uchungu,

hasemi kuwa walisindikizwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ,

sasa jadilini wenyewe,
 
Mzee Shelukindo ni mchaguaji mzuri wa maneno, mchambuzi mahiri wa pumba na mchele na mzoefu. Hawezi kuongea kama Mrema, Lipumba, Mbatia ambao kwao kila jukwaa ni sehemu ya kujipatia umaarufu wa KISIASA.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom