Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
...kunusurika katika ajali mbaya kama ile na kuweza kukumbuka wapi simu na 'nyaraka muhimu' kunaweza zua utata mwingi,

...'mwonekano' na inavyodaiwa, gari lilibiringika mara tano, japo Mallya mwenyewe anasema alisikia kishindo tu na vumbi!

...Mkuu wewe umeona nini, 'when a picture is worth a thousand words'?.


ni wakati gani Wangwe alibamiza ndani ya gari? wakati limeacha njia, wakati "linabingirika"? au karibu mwishoni kabisa? Kumbuka kuwa:

a. Kule gereji wanasema alipofika pale alikuwa amerudisha kiti chake nyuma na kupumzika na mzee aliyekuja kumsaidia anasema hivyo kwamba alikuwa amelala nyuma na mwili wake umebanwa na mlango wa nyuma (consistence) (mashahidi hawa wawili wanakubailiana). If that is the case, Wangwe hakujigonga mbele kwa sababu alikuwa amefungwa mkanda. Which means, kama alikufa katika ajali hiyo ushahidi uko kwenye mlango wa kushoto wa gari. Lakini kama ni uso ndio umeharibika, tunauliza ni kitu gani kitakuwa kimefanya hivyo kwa sababu kama amelala chali, umbali wa uso wake na paa la gari ni mkubwa zaidi kuliko akiwa amekaa ambapo utosi ndio unakuwa karibu. Kama gari lilibingirita the nature of injuries ingekuwa utosini zaidi kuliko usoni.
 
ni wakati gani Wangwe alibamiza ndani ya gari? wakati limeacha njia, wakati "linabingirika"? au karibu mwishoni kabisa? Kumbuka kuwa:

a. Kule gereji wanasema alipofika pale alikuwa amerudisha kiti chake nyuma na kupumzika na mzee aliyekuja kumsaidia anasema hivyo kwamba alikuwa amelala nyuma na mwili wake umebanwa na mlango wa nyuma (consistence) (mashahidi hawa wawili wanakubailiana). If that is the case, Wangwe hakujigonga mbele kwa sababu alikuwa amefungwa mkanda. Which means, kama alikufa katika ajali hiyo ushahidi uko kwenye mlango wa kushoto wa gari. Lakini kama ni uso ndio umeharibika, tunauliza ni kitu gani kitakuwa kimefanya hivyo kwa sababu kama amelala chali, umbali wa uso wake na paa la gari ni mkubwa zaidi kuliko akiwa amekaa ambapo utosi ndio unakuwa karibu. Kama gari lilibingirita the nature of injuries ingekuwa utosini zaidi kuliko usoni.

...pheeewww!...

nilidhani karibia watu wapige ukelele wa 'Eureka!',...maana ukijumlisha huo mswada Marehemu aloshindwa kuuwakilisha na hizo nyaraka muhimu alizoshikilia 'Mallya'...

...sawa, Tuendelee kuchambua picha.
 
Mwanakijiji,

Impact ya speed just over 80kph inategemea na
1.aina ya gari na security features zake
2.umbile la gari

kwa ajali hii na gari lenyewe nililivyo liona majeraha ya aina nyingi tu yaweza kuwa true........who knows uso wake uliangalia wapi.....because not necessarily uso uwe chali.......ndio majeraha fulani yatokee.........
I've been in three different fatal accident ambazo zote nilitoka salama.....just minor michubuko na kila mtu anashangaa niliwezaje kupona.........ninachoweza kusema ni seat belt na kwenye ajali nyingine both seat belts na airbags..........ofcourse na senses nilizokuwa nazo just before the accidents.........kwa kweli namshukuru Mungu

..........nina wasiwasi pia ile gari ni hizi re-conditioned from Japan.......ambapo magari ya aina hiyo yana kila aina ya historia..........

............check modal ya ile gari ni ya mwaka gani halafu waweza kupata security features zake wakati wa accidents from different angles......
 
Hiyo picha moja kwa moja inaonyesha kuwa Kijana Deus alikuwa Dereva No doubt..........kwa jinsi nilivyoliona lile gari most likely mtu aliyekuwa anaendesha anaweza kupona............well............tuendelee kutoa tafsiri zetu............

Mkuu Ogah,

Nakubaliana na theory yako. Pia sidhani kama lile gari liliviringika, ila kwa vyovyote lili crash upande wa kushoto. Inaweza kucrash kwenye kitu chochote hata kama udongo hasa kama mataili yalipasuka. Sijaliona vizuri eneo la ajali lakini huenda ni tambalale, hivyo sio rahisi sana gari dogo kuviringika. Ingelikuwa shangingi hapo sawa.

Kuna mtu aliandika kwanini hakuchomoa funguo ili lizimike? Hata uwe superman na uweze kuchomoa funguo bado Newton's first law of motion (kama sijakosea) bado itakupeleka mbele tu mpaka kupatikane kitu cha kulizuia gari.

Bado naamini kama kila mtu kwenye lile gari angefunga mkanda, kuna uwezekano mkubwa wote wangetoka salama, sana sana majeraha tu. Ajali mbaya ni kugonga gari kwa mbele au nyuma. Kulia au kushoto kama una mkanda, unakuwa na nafasi kubwa ya kupona.
 
mtanzania, nakubaliana na wewe ndio maana mwanzoni ningependa kweli kuona picha ya eneo hasa baada ya habari kuwa gari liligonga miti. Hiyo miti ndiyo ingetuonesha na kama imevunjika kwa sababu gari likigonga mti na mti ni mkubwa kanuni ya newton italisimamisha gari hilo hapo, hii miti gani iliyogongwa na gari kuendelea mbele kwa mita 50 unless siyo miti mikubwa?
 
Nyie mnauliza nini ati
Inamaana nyie hamjawahi kuona basi linachinja watu zaidi 40, harafu mwingine anatoka anajipangusa vumbi anaondoka,mwingine hata vumbi hana anaondoka zake.cha ajabu ni kipi?

Mimi mwenyewe shuhuda niliwahi kuanguka na basi nikielekea shule BwiRU BOYS yani nilitoka ktk basi hilo nikiwa wa mwisho lakini nilitoka kama nilivyoingia msafiiii wala sikujikwaruza wala nini nilitoka nikapanda Tanganyika Bus nikaendelea hadi shule.sasa mnachoshangaa ni kipi?

ujasusi unatoka wapi? RIP Chacha kafa kwa ajali wataalamu wameshathibitisha.
 
Ni bora kuwa na wanasiasa mafisadi wakivinjari kuliko wanasiasa mufilisi mbele ya vyombo vya habari......

Hawa jamaa wote waliletwa TARIME na ndege aliyokodisha MBOWE. Walipoifika msibani wakaachwa nyuma na kundi la mashabiki wa MBOWE kumuingiza katika eneo la shughuli ya mazishi.

Hawa ndio waliokuwa wakiimba RAISI, RAISI,...MPAKA KIELEWEKE....wakiwa na mabango lukuki yakihoji kifo cha WANGWE lakini hakuna hata moja lilikuwa likihoji uhusika wa CHADEMA au MBOWE. Hawa waliendelea kupiga kelele hata RC MAchibya am baye ni dui number moja wa wakazi wa TARIME alipopanda jukwaani na kuwataka wanyamaze. Hata kufikia kusema watulie ili waweze kumsikia RAIS wao...meaning MBOWE. RC Machibya aliendelea kuongeza lakini hakuna aliyemsikiliza huku vijana wawili wakiendelea kupiga kelele bila ya kutulia. Ni pale tu Zitto alipokuwa akiongea ndipo walitulia kidogo. Cha ajabu ni kuwa RC Machibya aikuwa hafurahishwi na hali hiyo kiasi cha kumnyang'anya Zitto MIC kila vijana hao wakiwa wanatulia na hivyo kuanzisha kelele nyingine. Mkumbuke kuwa MACHIBYA anaendesha operation ya kuzuia kusafirishwa chakula kwenda TARIME kwa madai kuwa wanatorosha chakula kwenda Kenya.

Cha ajabu zaidi ni kuwa Binamu wa Marehemu anayejulikana kama Mzee KEBA ambaye walikuwa na ushindani mkubwa kisiasa na Marehemu CHACHA WANGWE yeye akiwa kada na kiongozi wa CCM, alipanda jukwaani na kuwaonyeshea alama ya dole tupu waliokuwa wakipiga kelele hapo na hata kuchukua BANGO lilikuwa likiuliza kama Ni RISASI ama AJALI na kuliinua juu akilizungusha kwa kila mtu kuliona.

Hata hivyo vijana hao haswa wale wawili hawakuwa tayari kunyamaza hadi Zitto alipochukua MIC tena na kuanza kutumia slogans za CHADEMA ambazo ziliitikiwa kwa nguvu na kuanza kunyamaza ndipo alipomkabidhi MIC Prof Wangwe ambaye alitoa taarifa ya kuahirishwa kwa mazishi na kuwepo kwa uchunguzi mwingine wa mwili wa marehemu.

Baada ya hapo ndipo askari wa polisi na vijana wa ulinzi wa CHADEMA wakawachukua viongozi wote zaidi ya hamsini waliokuwepo plae na kuwaoonda mahala hapo kwa haraka kupitia chumba kilichokuwa na mwili wa marehemu ambacho kina milango miwili mmoja wapo ukiwa ni geti la chuma la kuingilia hala unatokea kwnye uwa wa nyumba kabla ya kupita mlango mwengie unaotokea mbel ya nyumba na kutoka nje kupanda magari.

Wakati wote huo hakuna waliokuwa wametoa silaha za aina yoyote na hata kutupa mawe. Kama ni kushambuliwa magari basi ilikuwa ni magari a serikali ambayo yalikuwa yakigongwa gongwa kwa mkono kama wafanyavyo wapiga debe wa daladala....

Ni kweli hapo nje kulikuwa na mtafaruku ambao ulisababishwa na panick iliyokuwepo miongoni mwa waheshimiwa wengi waliokuwepo hapo na kupelekea kukimbili katika magari yao na hata wegine kuingia katika magari yasiyo yao.

Ni wazi kuwa RC, RPC na watendaji wengine wa serikali walikuwa wamepanick na hata wakati mwengine kuonekana kuwa wanapenda kuonesha hali ya vurugu ipo.

Ni kweli pia katika hali kama ile ilikuwa ni busara kuwaondoa WAHEMSHIMIWA wale kwa haraka kwani eneo lile halikuwa na nafasi yoyote ya kuwalinda. Kilichofanya wao kupita katika kichumba ambacho ndipo mwili wa marehemu ulikuwepo ni kujaa kwa watu katika sehemu ya kuingilia katika eneo hilo ma tu baada ya MBOWE kungia na kundi la mashabiki ambao walijaa eneo lote la kuingilia kuelekea jukwaani na wengine wakijaribu kutoa mikono kwa waheshimiwa walikuwepo hapo haswa MBOWE na SLAA.

Zitto ndio alikuwa kiongozi wa mwisho kutoka eneo hilo na kuelekea nje ambak askari walimlazimisha kuingia katika gari la MHESHIMIWA MKONO akiwa na MESHIMIWA SARUNGI na mlinzi wake mmoja aliyepewa na IGP. Huyu alipewa baada ya yeye kukataa ulinzi wa FFU watatu ambao DC na KAIMU RPC wa MUSOMA walitaka aongozane nao MARA alipofika MUSOMA mjini........

Ukweli maizngira ya uwezekano wa vurugu kubwa na hatari yalikuwepo lakini si kweli kuwa siku ile kuna waliokuwa wakitishia maisha ya MBOWE. Na kama kuondolewa pale na askari hilo lilifanyika kwa wote walikuwa wamekaa kweny viti vya waheshimiwa wakiwemo wabunge zaidi ya 20, viongozi wa vyma zaidi ya 5, Viongozi wa CCM kadha ambao walikuja na mavazi yao ya chama kitu kilichopelekea hata MWenyekiti wa Moa aliyekuwa amekaa katika eneo la viongzi kutolewa na vijana wa CHADEMA na kuhamishiwa sehemu nyingine aliyopaswa kuwepo.

Wakina MREMA wao walichokuwa wakikifanya tangia wakati huo ni kuchochea sumu tu wakisaidiana na baadhi ya wanafamilia na kina MAMA KABAKA, Mzee GACHUMA na wengineo huko. Sumu yao pamoja na reporting ya kina GEORGE MARATO na mwenzake wa CHANEL TEN amao dio chanzo cha habari za kupotosha katika vyomb vingi vya habari ndio vilipelekea hali mbaya zaidi siku iliyofuata kwani hata baadhi ya watoto wake walianza kuamini kuwa marehemu aliuawa na risasi.

Mbaya zaidi ni kuwa hata wakati uchunguzi wa mwili ukiendelea TARIME MJINI kuna mtu alituma msg kijijini kuwa imethibitika kuwa kulikuwa na risasi mbili katika mwili wa marehemu....kitu ambacho kilifanya hata viongozi wengine wa CHADEMA kuamua kurudi TARIME mjini na wengine kuondoka hapo mara baada ya uchunguzi wa pili kwisha.

Kwa kweli sikuona ajabu kwa MREMAna MBATIA kufanya walichokifanya lakini ya Prof LIPUMBA yamenifanya kujiuliza zaidi kama nijiunge na siasa za vyama hivi ama laa. Iweje msomi kama yeye kutumia propaganda hovyo kama za kumhusisha MALLYA na UGAIDI eti kwa kuwa alikutwa na kikaratasi kikiwa na maandishi ya kiarabu ama aliwahi kwenda LIBYA. Hii haina tofauti na taswira iliyojengwa duniani kuhusu waislamu. Yaani hapa anahalalisha sumu hiyo dhidi ya uislamu na waislamu. Na yeye bado anajitambulisha yeye kama muislamu.

Na anaposema kuwa kichwa kilikuwa kimepondeka inabidi ajihadhari na hilo maana ukweli ni kuwa postmortem zote zinapaswa kufanywa na kurekodiwa na video. Nina uhakika wa hilo kwa uchunguzi wa TARIME maana alikuwepo mtaalamu wa ID wa polisi akirekodi zoezi zima.

Hawa kina MREMA na MBATIA waace waendelee kkupalia moto hii chuki inayopandikizwa hapa wakidhani itakwisha kwa WACHAGA Mbowe na Mallya tu.....Hii inakwenda zaidi ya hapo. Hata hivyo sidhangai sana kwao kuvaa siasa hovyohovyo kama hizi kwani upeo wao unajulikana...Lakini la LIPUMBA linatisha....

Kwa mimi niliyekuwepo TARIME kuanzia mwili ulipoingia hadi siku ya kuzikwa nashukuru wengi wenu hapa jinsi mnavyochemsha kwani mnaniwezesha kujielimisha mambo mengi ikiwemo hili suala la kujenga imani kwa misingi ya hisia zilizokosa chembe ya ujuvi......

Tanzanianjema
 
Ndugu zangu kama wengine walivyotangulia kuomba mapema, kama kuna mtu anamjua vizuri Deus Mallya atupashe hapa.Hii itasaidia kulinganisha na kuona kama kweli inawezekana alimfanyia hujuma mbunge. Mimi ninamfhamu Deus Mallya...ambaye nikiambiwa ndiye aliyekuwa kwenye ajali...tuhuma dhidi yake hazitanishangaza. Jamani anayemjua huyo Deus aseme
 
Kama kuna picha ya Deus Malya mtuhumiwa naomba iwekwe hapa
 
mtanzania, nakubaliana na wewe ndio maana mwanzoni ningependa kweli kuona picha ya eneo hasa baada ya habari kuwa gari liligonga miti. Hiyo miti ndiyo ingetuonesha na kama imevunjika kwa sababu gari likigonga mti na mti ni mkubwa kanuni ya newton italisimamisha gari hilo hapo, hii miti gani iliyogongwa na gari kuendelea mbele kwa mita 50 unless siyo miti mikubwa?

Mwanakijiji,

Hii ya kugonga mti kwa mbele sahau,labda kichaka, hilo gari halikugonga kitu kigumu kwa mbele. Angalia picha iliyotumwa sasa hivi, inaonyesha kioo cha mbele kimebaki.

Kama iligonga mti basi ni upande wa kushoto. Lingegonga mti kwa mbele hata huyo kijana asingelitoka salama kama alivyotoka.

Pia nimeona hii picha mpya, eneo ni tambalale.

Swali ambalo halina uhusiano sana na ajali hii, hivi kwanini Watanzania huwa hatupendi kufunga mikanda? Mimi baada ya kuona hizi ajali zinavyotokea na namna ya kujiokoa, hata kwenye basi lazima nifunge mkanda, labda kama basi halina mikanda.

Kitu kingine ambacho naona ni tatizo kwa Watanzania, wakiona basi linapata ajali, wanakimbilia kutaka kuruka nje. Jamani tuanze kujifunza njia za kujikoa hata kama hazifanyi kazi wakati wote.
 
Date::8/4/2008
Babake mzazi wa Mallya azidi kuchanganya mambo





Francis Matey Mallya, baba mzazi wa Deus Mallya akiwa katika ofisi za Mwananchi, mjini Moshi kumtetea mwanae jana.
Na Daniel Mjema, Moshi

BABA mzazi wa kijana aliyekuwa na Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe (Chadema) kwenye gari lililosababisha kifo chake, amezidi kuchanganya mambo baada ya kueleza kwamba, mwanaye hakuwahi kusoma sekondari Nairobi, nchini Kenya, kama mwanaye huyo alivyodai.


Akizungumza katika ofisi za gazeti hili mjini hapa jana, Francis Matey Mallya, ambaye ni baba mzazi wa Deus Mallya, alisema mwanaye hakuwahi kabisa kujiunga na shule yoyote ya sekondari ndani au nje ya nchi kwa vile hakuwa na uwezo wa kumsomesha masomo hayo.


Kijana huyo (27), ambaye ameshitakiwa kwa tuhuma za kuendesha gari bila leseni na kwa mwendo kasi uliosababisha kifo cha Wangwe, wiki iliyopita, alikaririwa na gazeti hili akidai kwamba, ana fani ya usanifu aliyoipata Nairobi katika Chuo cha Mtakatifu Hubert baada ya kumaliza sekondari kidato cha nne.


Hata hivyo, katika maelezo yake aliyoyatoa jana, Francis alisema anakumbuka kwamba, mwanaye alizaliwa mwaka 1983 katika Kijiji cha Kichare na kubatizwa kisha kusoma shule ya msingi Umbwe hadi darasa la saba.


"Kwa sababu mimi sikuwa na uwezo wa kumpeleka sekondari aliendelea kujisomea akawa ananunua vitabu vya kujisomea, lakini baadae akaondoka kwenda Dar es Salaam alikojifunza kozi ya kompyuta," alisema Francis.


Francis alisema mwanaye alipita tu Nairobi alipokuwa akirejea kutoka nchini Libya, ambako hadi sasa hafahamu hasa shughuli iliyompeleka huko (Libya).


Mzee huyo, alisema aliporejea kutoka Libya, alishukia Nairobi ambako alikutana na rafiki yake waliorejea wote jijini Dar es Salaam.


Alisema anachofahamu ni kwamba kulikuwa na mtu ambaye hamfahamu, ambaye alikuwa akiwasiliana na mwanae kwa ajili ya kwenda Libya na alipokwenda hakufikisha wiki alirejea nchini.


Francis alisema mwanae aliweza kumudu vyema mafunzo ya kompyuta baada ya kupata mtu wa kumfundisha na baada ya kumudu mafunzo hayo alijishughulisha na kazi ya kutengeneza fulana, ambayo anaendelea kuifanya hadi sasa.


Alishutumu mwelekeo unaoanza kujitokeza wa kutaka kuhalalisha kuhusika kwa mwanae na kifo cha Wangwe.


"Kumuita mtoto wangu ni jasusi bila kumpa nafasi ya kumsikiliza wala vyombo vya dola havijathibitisha hilo ni kumhukumu, jambo ambalo ni kinyume cha katiba…wanamhukumu vipi kwa hisia?," alihoji Francis.


Alidai kauli ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ya kumuita mwanae ni jasusi, ina lengo la kuushawishi umma uamini mwanae anahusika na kifo cha Wangwe.


Francis ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Kichare katika kijiji cha Umbwe Sinde alisisitiza kilichotokea ni ajali kama ajali nyingine na suala hilo sasa liachiwe mahakama ambayo itachambua ushahidi na kujua lipi la kweli na lipi halina ukweli.


"Kwa muelekeo huu ninaouona, naomba taasisi zinazotoa msaada wa kisheria zisaidie kulinda haki ya mwanangu, ambaye tangu akamatwe hatuna mawasiliano naye na ndugu wamezuiwa kuonana naye," alidai.


Akielezea tabia ya mwanae, alisema anamfahamu vyema na kwamba hajawahi kushika bunduki wala kisu achilia mbali kutembea na wahuni, bali alikuwa akifuata maadili mema ya Kanisa Katoliki.


Alisema anamfahamu mwanae kama mtu anayejishughulisha na kazi ya kuchapisha maandishi na picha kwenye fulana na kazi hiyo ndio ambayo amekuwa akiifanya kwa ajili ya shule, makanisa na vyama vya siasa.


Alifafanua kuwa mara tu baada ya ajali, mwanae alimpigia simu akimuarifu kuwa alikuwa akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam akiwa na mbunge mmoja, lakini kwa bahati mbaya gari imepata ajali na mbunge amefariki dunia.


"Aliniambia kuwa gari imepinduka mara sita na kujikuta nje ya gari akiwa hana simu yake ya mkononi huku akiwa na majeraha miguuni na kichwani na mbunge alifariki dunia papo hapo," alidai Francis.


Aliendelea kusema kuwa: "Alinitaka nisiwe na wasiwasi sana kwani hajaumia sana ila masikitiko yake ni kwamba mbunge amefariki…nilimuuliza nani alikuwa anaendesha gari akasema ni mbunge mwenyewe."


Kwa mujibu wa Francis, hata wakati anakwenda kwake Dodoma mwanae alimpigia simu na kumjulisha kuwa anakwenda huko kikazi kwa wiki moja na baadae atarejea Dar es Salaam kabla ya kwenda tena Dodoma kwa kazi ya fulana.


Katika hatua nyingine, Ramadhan Semtawa anaripoti kutoka Dodoma kuwa Deus Mallya anayedaiwa kuwa dereva wa marehemu Wangwe, amezidi kugonganisha vichwa vya watu baada ya Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Juma Kilimba, kusema hamjui wala hana urafiki na kijana huyo.


Kauli hiyo ya Kilimba inapingana na ile aliyotoa Mallya kwamba anafahamiana vema na mbunge huyo kwani walikuwa wote katika safari yao ya kwenda Libya mwaka jana.


Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili nje ya viwanja vya Bunge mjini hapa jana, Kilimba alisema licha ya kutomfahamu pia alishangaa na hadi sasa hajui kijana huyo aliingiaje katika msafara wao wa kwenda Libya hapo mwaka jana.


Kilimba alifafanua kwamba, alisikia Mallya kwamba anamfahamu yeye (Kilimba), alishangaa na kuongeza kwamba: "Siyo urafiki tu, simjui na sijawahi kuwa na ukaribu naye."


Hata hivyo, Kilimba aliongeza kwamba baada ya kusikia taarifa hizo alikumbuka kwamba wakati wakiwa uwanja wa ndege wa Zurich, Uswisi, katika safari hiyo kuelekea Libya mwaka jana, kijana huyo aliwahi kusahau hati yake ya kusafiria kwenye ndege.


Alisema kwa kuwa walikuwa katika msafara mmoja, yeye (Kilimba), alishauri asaidiwe baada ya kuzuka tafrani ndipo kiongozi aliyeshughulikia safari hiyo akamsadidia kijana huyo na wala si yeye.


"Niliposikia huyo kijana ana nifahamu mimi, kwanza sikuwa na fikra kabisa kwamba kuna kijana kama huyo aliwahi kuwa rafiki yangu au namfahamu, nikakumbuka kumbe ahaa, ni yule ambaye aliwahi kusahau pasi ya safari yake ndani ya ndege tukiwa Zurich,"alisema Kilimba na akaongeza:


''Mimi nilikuwa Bussines Class yeye alikuwa Economy, sikuwa nikimfahamu, nilishangaa hata mimi pale Zurich kumuona yuko katika msafara, nilihoji na hadi sasa sijajua, aliingiaje katika msafara ule, ndiyo maana nakwambia simfahamu kabisa zaidi ya kuonana pale.''


Aliongeza kwamba, watu aliokuwa nao na aliowafahamu ni pamoja na Makongoro Nyerere ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mara, Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mamuya, Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Issa Simba, Shehe Seleman Kilemile na Hebron Mwakagenda, ambaye ni kutoka Leadership Forum.


Mallya alifunguliwa kesi namba TR 103/08, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani hapa, kwa makosa ya kuvunja sheria za usalama barabarani, ambayo ni kuendesha gari kwa mwendo kasi na kusababisha kifo cha Wangwe na kuendesha gari bila leseni.


Tuma maoni kwa Mhariri
 
Date::8/4/2008
CCM yasambaza waraka wa Wangwe kuhusu mtafaruku wa Chadema
Frederick Katulanda, Mwanza

WAKATI kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Zakayo Wangwe, aliyefariki kwa ajali gari Julai 28 mwaka huu kinazidi kuleta utata, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamekuwa wakisambaza waraka wake wenye kurasa sita ukielezea jaribio la Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe kutaka kumvua wadhifa wake na uanachama.


Waraka huo umekuwa ukisambazwa kwa viongozi mbalimbali wa CCM ili kuwapatia ufahamu viongozi wake kujua kwa kina mgogoro huo wa Chadema ambao umekuwa ukihusishwa kama ndiyo chanzo cha sababu ya kifo cha mbunge huyo.


Waraka huo unaodaiwa kuwa umeandikwa na marehemu Wangwe mwenyewe, ingawa muda ambao alikuwa anakusudia kuutoa hadharani kwa wananchi na wanachama wa chama hicho kama sehemu ya kufafanua tuhuma ambazo anadaiwa kuhusika nazo na hata kuvuliwa wadhifa wake, hauainishwi.


Katika nakala ya waraka huo ukurasa wa nne, unaonyesha kwamba kwa mara ya kwanza ulitumwa kutoka Dodoma Julai 27 mwaka huu majira ya saa 9:42 alasiri toka namba (026) 2322965 ambayo imeonyesha Kusajili kwa jina la ‘KATIBU MKUU CCM DOD' tarehe ambayo ni siku moja kabla ya kifo cha Wangwe kilichotokea akienda Dar es Salaam.


Kwa maana hiyo waraka huo ulianza kusambazwa mikoani kwa viongozi wa CCM siku moja kabla ya kifo cha Wangwe.


Uchunguzi wa Mwananchi unaonyesha kwamba baada waraka huo kufika Dar es Salaam, ulianza kusambazwa kutoka Dar es Salaam kwa namba za faksi 2667457 iliyotanguliwa na kodi namba ya mkoa (022) ikimaanisha kutumwa kutoka Dar es Salaam Julai 31 mwaka huu majira ya saa 11:50 asubuhi mwenye kumiliki namba hiyo akitambuliwa kama SIGMA ICT.


Gazeti hili pia limebaini kuwa waraka huo umetumwa kwa baadhi ya viongozi wa CCM mikoani, wakiwemo makatibu wa mikoa na wilaya pamoja na wengine ukiwa ni mahususi kwa ajili ya kuwaonyesha kwa kina mgogoro wa Chadema ulivyo.


Katika tamko hilo imeelezwa kuwa sababu zote zilizotolewa na kumvua wadhifa marehemu ni za uzushi na kwamba hata kikao kilichoketi kumjadili kilikuwa na jumla ya wajumbe 31 ambao nusu yake walikuwa wajumbe wasio na uhalali wa kupiga kura, lakini kati yao 24 walipiga kura kinyume cha Katiba ya Chadema.


Marehemu Wangwe ameeleza katika waraka huo kwamba, chama hicho kikiwa chini wa uongozi wa Mbowe na wafuasi wake kati ya Sh 374milioni zilizopatikana kama ruzuku kati ya Januari Mosi na Juni 30, mwaka huu Sh 350milioni zilitumika makao makuu ya chama na Sh25m tu ndizo zilizokwenda wilayani kuimarisha chama na kueleza mgao huo umekuwa ukitukuza chama makao makuu na kukidhalilisha chama nchi nzima.


''Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa 2005, Mbowe alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama dola za Kimarekani181,949.00 sawa na Sh 218,338,546 na mpaka sasa chama kimemlipa Sh175milioni. Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha wilayani na makao makuu, niliamua kumshauri Mbowe asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku, kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa

usimamizi wa pesa za ruzuku kwa vyama vya siasa kutoka serikali.


''Mbowe alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibitishie pesa hizo anazodai alikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya Chadema kupitia hundi ipi na lini?'' ilieleza sehemu ya waraka huo.


Waraka huo pia umegusia suala lingine la uteuzi wa wabunge wa Viti Maalum kwa kueleza kuwa Mbowe na wafuasi wake walighushi orodha ya majina badala ya kupeleka yaliyopendekezwa na Kamati Kuu kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).


''Siyo siri, naamini hata Mbowe atakubaliana nami kuwa hili si moja ya siri anazodai nimevujisha,'' ilieleza sehemu ya waraka huo unaodaiwa kuwa wa marehemu Wange na kwamba chama hicho kimekuwa kikiendeshwa kwa ubabe na misingi ya kikabila jambo ambalo alieleza litasababisha kukosa wananchama.


Katika hitimisho la waraka huo umeeleza kuwa: ''Nilijikuta katika mvutano mkubwa kila nilipogusa eneo lolote kati ya hayo (yaliyoelezwa juu) nakiri kuwa kwa kiwango kikubwa sikuwa na uwezo wa kubadili mambo hayo yaliyokuwa yakiratibiwa kwa ukaribu na Mbowe na wafuasi wake kwani sikupewa ushirikiano wa aina yoyote na chama pale Makao Makuu. Ni vigumu kuamini, lakini ni kweli, kuwa sikuwa na ofisi Makao Makuu, sikupewa vitendea kazi kama magari, vipaza sauti na au vyombo vya habari, sikuwahi kupata taarifa yoyote ya kiutendaji kutoka makao makuu.''


Hii ni mara ya kwanza kwa CCM kujitokeza wazi kusambaza waraka wa Chadema, ikiacha maswali kama ilipewa waraka huo na Wangwe au ndiyo ilikuwa ikishirikiana naye katika kuendesha harakati zake ndani ya chama hicho cha upinzani.


Tuma maoni kwa Mhariri







Hizi siasa za kupandiliana migongongo hua sijui mwaasisi wake ni nani,?
 
Pichwa kubwa inaonyesha picha yote.

(1) Moja gari imebondeka upande wa kushoto juu
(2) Gari ilivingirika (angalia missing Side Mirror)
(3) Kiti kimelala kidogo hivyo kichwa kipo karibu na mahali fremu ya mlango inapopita.

Ukiangalia picha hiyo unapata picha hii:

Mallya alikuwa akiendesha kwa kasi huku Wangwe akiwa amelala. Tairi ilipasuka na vumbi kutimka (kwa wale ambao wamewahi kupata burst wanaelewa hili). Mallya alipanic na labda alifunga breki hivyo kusababisha gari kubingirita.

Marehemu Wangwe alikuwa amefunga mkanda lakini kutokana na motion kuwa kiupandeupande (sideway rolling) alipanda juu (slide up the seat) kutokana na seat kuwa katika obtuse angle rather than close to 90 degree. Kumbuka alikuwa hajajishika kokote tofauti na Mallya aliyekuwa ameshika Steering Wheel.

Rolling motion na compression ya roof ilivunja kioo cha pembeni. Hii ilisababisha kichwa kujipiga juu na kwenye ardhi gari ilipokuwa inabingirita.

Inaelekea kulikuwa na mawe au visiki vyenye ncha kali kwani hata bonnet lina scratches na tundu.

Other points:

- Gari hiyo ina body filler inayoonyesha imewahi kunyooshwa huko nyuma.
- Kama alislide na kufika nyuma alikutana na ncha kali iliyosababishwa na kona ya nyuma kujipinda kuelekea ndani.
 
confused,kweli mtu akifariki hata kama alikuwa adui yako utasema siyo ,dont understand the late wangwe ndiyo yule aliyekuwa anapigwa vijembe anataka kuisambaratisha chadema kama NCCR ilivyosambaratishwa then watu haohao leo mko positive naye kwamba alikuwa mpiganaji wa upinzani?
 
Duh, hili gari lilikuwa liwake (lichomwe moto?). Huyo mwanakijiji aliyewahi katibua mambo................mmm!!!
 

Attachments

  • 6.jpg
    6.jpg
    277.8 KB · Views: 75
Duh, Ama kweli sasa hivi ndio nzazidi kuchanganyikiwa kabisaaaa!
Hivi hawa CCM ni kundi la wendawazimu ama kitu gani?.. kusambaza huo waraka inaonyesha wazi kwamba wao walikuwa na uhusiano mkubwa na Chaha Wangwe kiasi kwamba marehemu awape hizo nyaraka. Au kuna uwezekano mkubwa wao kuwa mashahidi wa shutuma hizi zote...Wamezipata vipi hizi nyaraka ambazo ni za Marehemu aliyekusudia kuwapa wananchama wa Chadema.. Zimefika vipi mikononi mwa CCM wakati wa mashaka kama huu?

Jamani twendeni mbele turudi nyuma, haya yote mnayoyazungumza ni Theory zenu ama zetu sisi iwe kilichotokea ni Ajali ama sio Ajali.. Sote tunakisia na kujaribu kuchora ushahidi ambao hatuna mikononi wala hakuna mmoja wetu aliyetembelea sehemu ya ajali..
Picha alizoweka J.J Mnyika sikumbiuki ukurasa wa ngapi zinaonyesha wazi matairi hayakupasuka isipokuwa moja la nyuma ambalo hata ktk picha hiyo hapo juu linaonyesha kutokuwa na Upepo wa kutosha..Hakuna flat tyre hata moja kwa hiyo sababu ya ajali (kulitoa barabarani) haiwezi kuwa ni matairi. Je, ni kitu gani sote hatujui hivyo tuachie wachunguzi wa ajali kama wapo!..

Nitazidi kusema kwamba kuna kila walakini ktk ajali hii iwe vyovyote mtakavyoiweka.. Kama huyu Kijana ndiye alikuwa dereva mnajuaje kama anajua hata kuendesha ikiwa hana hata liseni na yeye mwenyewe alikwisha toa ushahidi kwamba hakuwa dereva!.. Huyo Wangwe alikaa kiti gani?..Cha nyuma ama mbele na nani anajua hakufunga mkanda! Haya report ya polisi Wangwe alikaa kiti cha mbele upande wa abiria. Je ilikuwaje damu zilionekana chini kiti cha nyuma sio kiti cha mbele..Marehemu alikutwa kiti gani? hadi sasa hakuna kati yetu anayefahamu kwa uhakika!

Mimi nafikiri ni vema tukisubiri report kamili inayowaweka wahusika wote ktk viti wamefunga mikanda ama hawakufunga kutokana na habari za watu waliomtoa marehemu ktk gari hilo, ili tupate kujenga hoja zetu. Haya maswala ya kwamba inawezekana mtu akapona ama sijui nini ni maswala ambayo hayana msingi kabisa kwani wapo watu waliokwisha pona ktk ajali na hawakufunga mikanda, wapo waliokufa kwa sababu ya mkanda na wapo waliokufa kwa kila njia maana hizi zote ni ajali tu.. Kikubwa ni sababu ya ajali hiyo bna ndicho kinachotolewa hukumu.! Nitasisitiza kwamba Ajali ni Ajali kama inavyoitwa isipokuwa panapokuwepo utata ni sababu ya ajali hiyo...Hii ndio pekee inayoweza kumhukumu mtu iwe Mallya ama Marehemu. Utata ktk kifo cha Wangwe ni sababu ya ajali hiyo!
 
Vitu vingine bwana
kwa hiyo Mallya alitia kasensa kake kwenye gari na ilipofika sehemu aka i remote gari maana anajua computer? ama huo ujuzi wake wa computer aliset robot gari ilipopata ajari tu robot likamroboti Mallya likamtoa nje.
 
confused,kweli mtu akifariki hata kama alikuwa adui yako utasema siyo ,dont understand the late wangwe ndiyo yule aliyekuwa anapigwa vijembe anataka kuisambaratisha chadema kama NCCR ilivyosambaratishwa then watu haohao leo mko positive naye kwamba alikuwa mpiganaji wa upinzani?


Maajabu kweli kweli mimi binafsi nime loose sense ubruptly.Baada yakuona hayo yanatokea ndani ya wiki tatu ktk mtandao huu huu nayakifanywa nawasomi wa juu kabisa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom