Emekha Ikhe
Member
- Jul 14, 2021
- 52
- 84
Nimesoma HUKUMU ya Kesi ya THADEY KWEKA ambayo imetolewa jana kinyemela hata bila yeye mwenyewe kujitetea au kutetewa na Mawakili wake tangu kukamatwa kwake, Ninasikitika Kuona kwamba hata Mahakama kupitia Hakimu imejielekeza Vibaya Kutoa HUKUMU husika
Raia Wanategemea Mahakama itende Haki na sio kushirikiana na Vyombo Vya Ukamataji na Uchunguzi kuminya Haki za KIKATIBA za Mtuhumiwa kama ambavyo nitaeleza Juu ya Sakata la THADEY KWEKA kama nyaraka zinavyojifafanua, binafsi nitaandika kwa ufupi na straight to the point
Kitendo cha Ofisi ya DPP kufungua kesi dhidi ya Mtuhumiwa (Thadey Kweka) ya kuitaka Mahakama kutoa Amri dhidi ya KWEKA ili atoe Nywila(Password) yake ili Polisi na Ofisi ya DPP kufanya Uchunguzi, na kesi Kusikilizwa na Mahakama hata bila Mtuhumiwa kupewa wito ili kuwepo kwa utetezi au kutetewa na Wakili wake, Kunaibua maswali Mengi ya kisheria dhidi ya Vyombo Vya Uchunguzi pamoja na Mahakama yenyewe
Mosi, Kesi umesikilizwa Upande mmoja kwa hati ya dharura bila mtuhumiwa wala Wakili wake kujulishwa kwa wito wa Mahakama huku kesi iliyofunguliwa ikiwa Inter-Parte Application (Kwamba Mtuhumiwa alipaswa kupewa wito kwa utetezi) na sio Exparte Application (Kwamba kesi isikilizwe Upande mmoja kulingana na nyaraka zilizofailiwa
Ukisoma Wito wa Mahakama( Chamber summons) hauonyeshi kwamba kesi hii ilikuwa ya Kusikilizwa Upande mmoja (Exparte Application) hivyo, Thadei alipaswa kuwakilishwa na Wakili au kujiwakilisha katika utetezi wake ili Kutekeleza Haki ya Asili ya Kusikilizwa inayolindwa na Katiba ya Nchi kabla ya Mahakama Kuja na Uamuzi uliotolewa
Bahati Mbaya sana Hakimu aliyetoa Uamuzi anakili kwamba kesi hii ilikuwa kwa hati ya dharura ili isikilizwe Upande mmoja kinyume na nyaraka zilizowasilishwa Mahakamani na Hakimu anaamua kesi husika bila kutii Katiba ya Nchi na Sheria zake kama nitavyofafanua hapa;
Mahakama hazina Mamlaka ya ku-dis regard Haki za Msingi za Kikatiba mathalani haki ya Faragha (Right to privacy) bila Kutoa Haki ya Kusikilizwa kwa Mtuhumiwa (Principle of Natural Justice) kama ambavyo Hakimu alivyojielekeza vibaya katika Uamuzi wake unaopswa kukatiwa Rufaa haraka iwezekanavyo
Pia Kifungu cha 32 cha Sheria, Cyber Crime Act, licha ya kwamba Kifungu hiki kimeipa Mamlaka Mahakama Kutoa Amri husika, Sheria husika haijaipa Mamlaka Kufanya Maamuzi kwa KUVUNJA Sheria na Katiba ya Nchi, hususani kukinzana na matakwa ya Katiba juu ya Haki ya Kusikilizwa (Fair hearing) kabla ya uamuzi
Ifahamike kuwa, Polisi na DPP hawezi Kumkamata Mtuhumiwa kwa tuhuma hewa za jinai ( kupublish Taarifa za UONGO (False nformation) bila kuzitaja in specific kama Kifungu cha 32 cha Sheria ya Cyber crime Act kinavyotaka
Ni Bahati mbaya sana Hakimu huyu wa Mahakama(RMC) ametoa HUKUMU ya Amri ya Mtuhumiwa Kutoa nywila zake bila kujua ziitwazo Taarifa za UONGO ni zipi ambazo zilipelekea Mtuhumiwa kukamatwa kama Sheria inavyotaka
Ni takwa la Sheria zetu kwamba,Mahakama katika Kutoa HUKUMU au Uamuzi wake haswa katika kesi ya Jinai inapaswa kuongozwa kanuni ya kuthibitisha bila Shaka (Prove Beyond Reasonable drought), kwenye hili Mahakama imejielekeza Vibaya hivyo Uamuzi husika unapaswa kukatiwa Rufaa haraka
Hatuwezi tukawa na Mahakama ambazo Hakimu anaamua kesi ya Jinai bila kujua in specific( details za kosa (criminal offence), bila kumpa Haki Mtuhumiwa kujitetea au kutetewa na Wakili wake (Fair hearing) na Kutoa Maamuzi
Hii ruling inapaswa kukatiwa Rufaa haraka, Ni Muhimu Mahakama zetu kujiongoza vyema katika Kulinda Haki za Binadamu ambazo zinalundwa na Katiba ya Nchi yetu
Raia Wanategemea Mahakama itende Haki na sio kushirikiana na Vyombo Vya Ukamataji na Uchunguzi kuminya Haki za KIKATIBA za Mtuhumiwa kama ambavyo nitaeleza Juu ya Sakata la THADEY KWEKA kama nyaraka zinavyojifafanua, binafsi nitaandika kwa ufupi na straight to the point
Kitendo cha Ofisi ya DPP kufungua kesi dhidi ya Mtuhumiwa (Thadey Kweka) ya kuitaka Mahakama kutoa Amri dhidi ya KWEKA ili atoe Nywila(Password) yake ili Polisi na Ofisi ya DPP kufanya Uchunguzi, na kesi Kusikilizwa na Mahakama hata bila Mtuhumiwa kupewa wito ili kuwepo kwa utetezi au kutetewa na Wakili wake, Kunaibua maswali Mengi ya kisheria dhidi ya Vyombo Vya Uchunguzi pamoja na Mahakama yenyewe
Mosi, Kesi umesikilizwa Upande mmoja kwa hati ya dharura bila mtuhumiwa wala Wakili wake kujulishwa kwa wito wa Mahakama huku kesi iliyofunguliwa ikiwa Inter-Parte Application (Kwamba Mtuhumiwa alipaswa kupewa wito kwa utetezi) na sio Exparte Application (Kwamba kesi isikilizwe Upande mmoja kulingana na nyaraka zilizofailiwa
Ukisoma Wito wa Mahakama( Chamber summons) hauonyeshi kwamba kesi hii ilikuwa ya Kusikilizwa Upande mmoja (Exparte Application) hivyo, Thadei alipaswa kuwakilishwa na Wakili au kujiwakilisha katika utetezi wake ili Kutekeleza Haki ya Asili ya Kusikilizwa inayolindwa na Katiba ya Nchi kabla ya Mahakama Kuja na Uamuzi uliotolewa
Bahati Mbaya sana Hakimu aliyetoa Uamuzi anakili kwamba kesi hii ilikuwa kwa hati ya dharura ili isikilizwe Upande mmoja kinyume na nyaraka zilizowasilishwa Mahakamani na Hakimu anaamua kesi husika bila kutii Katiba ya Nchi na Sheria zake kama nitavyofafanua hapa;
Mahakama hazina Mamlaka ya ku-dis regard Haki za Msingi za Kikatiba mathalani haki ya Faragha (Right to privacy) bila Kutoa Haki ya Kusikilizwa kwa Mtuhumiwa (Principle of Natural Justice) kama ambavyo Hakimu alivyojielekeza vibaya katika Uamuzi wake unaopswa kukatiwa Rufaa haraka iwezekanavyo
Pia Kifungu cha 32 cha Sheria, Cyber Crime Act, licha ya kwamba Kifungu hiki kimeipa Mamlaka Mahakama Kutoa Amri husika, Sheria husika haijaipa Mamlaka Kufanya Maamuzi kwa KUVUNJA Sheria na Katiba ya Nchi, hususani kukinzana na matakwa ya Katiba juu ya Haki ya Kusikilizwa (Fair hearing) kabla ya uamuzi
Ifahamike kuwa, Polisi na DPP hawezi Kumkamata Mtuhumiwa kwa tuhuma hewa za jinai ( kupublish Taarifa za UONGO (False nformation) bila kuzitaja in specific kama Kifungu cha 32 cha Sheria ya Cyber crime Act kinavyotaka
Ni Bahati mbaya sana Hakimu huyu wa Mahakama(RMC) ametoa HUKUMU ya Amri ya Mtuhumiwa Kutoa nywila zake bila kujua ziitwazo Taarifa za UONGO ni zipi ambazo zilipelekea Mtuhumiwa kukamatwa kama Sheria inavyotaka
Ni takwa la Sheria zetu kwamba,Mahakama katika Kutoa HUKUMU au Uamuzi wake haswa katika kesi ya Jinai inapaswa kuongozwa kanuni ya kuthibitisha bila Shaka (Prove Beyond Reasonable drought), kwenye hili Mahakama imejielekeza Vibaya hivyo Uamuzi husika unapaswa kukatiwa Rufaa haraka
Hatuwezi tukawa na Mahakama ambazo Hakimu anaamua kesi ya Jinai bila kujua in specific( details za kosa (criminal offence), bila kumpa Haki Mtuhumiwa kujitetea au kutetewa na Wakili wake (Fair hearing) na Kutoa Maamuzi
Hii ruling inapaswa kukatiwa Rufaa haraka, Ni Muhimu Mahakama zetu kujiongoza vyema katika Kulinda Haki za Binadamu ambazo zinalundwa na Katiba ya Nchi yetu
Attachments
-
inbound6150996344563864447.jpg70.7 KB · Views: 10 -
inbound4300967958931106526.jpg189.6 KB · Views: 9 -
inbound6074964550284767534.jpg241 KB · Views: 9 -
inbound4658300855320504533.jpg159.3 KB · Views: 10 -
inbound9018582459540547332.jpg276 KB · Views: 7 -
inbound48069550307847023.jpg314.6 KB · Views: 5 -
inbound6518991479493533616.jpg313.8 KB · Views: 8 -
inbound4527793917683548279.jpg252 KB · Views: 13