Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

Jana, raisi wa Jamhuri ya ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benk 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti zatu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini anaweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Mkuu bila kuitaja urusi uzi haukamiliki🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Nimeshangaa zaidi Rais ameshindwa hata kumtaja huyo mwizi, tutajie mwizi wa pesa zetu tumjue, sioni sababu ya kumficha hata kama ni masuala ya kiusalama.

Siku hizi kuna interpol, wape information wafanye kazi yao, kuliko kutuambia tu kuna mtu amekopa benki tano akakimbia, naona ni bora angekaa kimya kabisa.
Ameamua kututia machungu roho yake isuuzike,
 
Ukienda kukopa bank kama Nmb unachunguzwa mpaka chupi hata kama umekopa songesha wanajua na unaulizwa maswali kibao, sasa uyo mwenzetu ilikuwaje? Na mkuu wa Nchi kaongea na imeisha iyo hutoona chochote kinafanyika kwa wausika, ila kwa mengine eitha upinzani au machinga jamaa wanalibeba na wanakwambia kauli ya Raisi ni sheria
 
Huyu mtu analaumiwa kwa lipi hasa, kakopa siyo kaiba, nasema tena kakopa, tena kakopa mchana kweupe na jua linawaka. Sasa kama halipi madeni yake si mali alizoweka rehani ziuzwe ??? Na kama analipa madeni yake kelele za nini? Kama sheria inakataza kukopa zaidi ya benki moja, basi hapo kuna tatizo. Lakini sheria kama iko kimyaa tusipoteze muda humu kujadili vitu vilivyofanywa kisheria.

Tuhangaike na wale wa billions za ndege ya mizigo ambao wako mkononi mwa Rais. Namtafuta anifundishe kukopa benki zaidi ya kumi na mimi nifaidi looh
 
Hivyo Kipilimba angeweza kupewa nafasi ya kufundisha vijana wapya na pale UDSM wakawa na Department ya masuala haya ya security and risk management
Maneno yako yanaonyesha as if Kipilimba is the only dude kwenye system ambae anajua risk management, ndio hadi unataka awe mwalimu pale UDSM.
Kitu ambacho ni kibaya kwenye system.
 
Nakubaliana andiko

Ila tunaweza kuwalaumu TISS wakati sheria imewabana na wanashindwa kuitisha PRESS kusema walimshauri fulani fulani akutekeleza au kueleza kumefanikiwa hili na lile.

Nilimsoma sana mzee Mkuchika alivyokuwa anatoa ufafanuzi...
 
Huyu mtu analaumiwa kwa lipi hasa, kakopa siyo kaiba, nasema tena kakopa, tena kakopa mchana kweupe na jua linawaka. Sasa kama halipi madeni yake si mali alizoweka rehani ziuzwe ??? Na kama analipa madeni yake kelele za nini? Kama sheria inakataza kukopa zaidi ya benki moja, basi hapo kuna tatizo. Lakini sheria kama iko kimyaa tusipoteze muda humu kujadili vitu vilivyofanywa kisheria.

Tuhangaike na wale wa billions za ndege ya mizigo ambao wako mkononi mwa Rais. Namtafuta anifundishe kukopa benki zaidi ya kumi na mimi nifaidi looh
Kama amekopa tu kawaida kwenye benki tano tofauti na kutokomea mbona raisi nae ashangaa.

Hiyo yamaanisha kwamba benki zimefanya checks baada ya kutoa fedha na kisha kugundua kuwa mkopaji hakuwa si mtu wa kawaida.
 
Nakubaliana andiko

Ila tunaweza kuwalaumu TISS wakati sheria imewabana na wanashindwa kuitisha PRESS kusema walimshauri fulani fulani akutekeleza au kueleza kumefanikiwa hili na lile.

Nilimsoma sana mzee Mkuchika alivyokuwa anatoa ufafanuzi...
TISS hushughulikia mambo kama haya nyuma ya pazia kisha kumpa kazi ya PR IGP aongee na vyombo vya habari.

TISS haipaswi kabisa kujulikana kazi zake hufanywa siri lakini vema sana.

Hii ipo kote duniani mazee hushughulika nyuma ya pazia kisha kuwaacha polisi wakimalizia pamoja na mahakama.
 
Kuilaumu TISS ni kupoteza muda. Mtu hawezi kopa mabilioni gavana asijue. Na isitoshe ukikopa benki yoyote ile lazima benki zingine watajua ukienda kukopa kwao kwasababu kabla ya kukupa hela lazima waangalie kama una deni kwingine. Hizo dhamana za kukopa mabilioni zilithibitishwa na nani? Idara ya uhamiaji iliwezaje kumpa vibali vya kuishi hadi kuweza kukopa? Kimsingi hapo kuna wazito wengi sana wamedaka mpunga tangu ile siku huyo mtu anaingia nchini. Akamatwe ili tuwajue walioko nyuma ya huo mpango wake. Lakini je hatutangaziwa msiba wake kabla ya yeye kukamatwa? TUSUBIRI HAPAHAPA JF.
 
Kuilaumu TISS ni kupoteza muda. Mtu hawezi kopa mabilioni gavana asijue. Na isitoshe ukikopa benki yoyote ile lazima benki zingine watajua ukienda kukopa kwao kwasababu kabla ya kukupa hela lazima waangalie kama una deni kwingine. Hizo dhamana za kukopa mabilioni zilithibitishwa na nani? Idara ya uhamiaji iliwezaje kumpa vibali vya kuishi hadi kuweza kukopa? Kimsingi hapo kuna wazito wengi sana wamedaka mpunga tangu ile siku huyo mtu anaingia nchini. Akamatwe ili tuwajue walioko nyuma ya huo mpango wake. Lakini je hatutangaziwa msiba wake kabla ya yeye kukamatwa? TUSUBIRI HAPAHAPA JF.
Si kwamba TISS yalaumiwa bali yakumbushwa kuwa dunia sasa imebadilika.
 
TISS hushughulikia mambo kama haya nyuma ya pazia kisha kumpa kazi ya PR IGP aongee na vyombo vya habari.

TISS haipaswi kabisa kujulikana kazi zake hufanywa siri lakini vema sana.

Hii ipo kote duniani mazee hushughulika nyuma ya pazia kisha kuwaacha polisi wakimalizia pamoja na mahakama.
Mkuu hapo tunawatuhumu vipi kama TISS haikufanya kazi?

Hili suala linategemea na utashi wa head of the state kama akiwa lege lege ndiyo mambo kama haya, unakumbuka tulivyokuwa na head of the state makini singa singa mzee wa IPTL alikamatiwa AIRPORT alikuwa anataka kutoroka.

Fikiria report ya CAG watu wamepiga pesa dhahiri shahiri, anawambia ajitathmini kama wana tosha, Tupo serious kweli?
 
Jana, raisi wa Jamhuri ya ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benk 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti zatu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini anaweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Tiss wajishughulishe na mikopo? Hili mbona ni kosa la benki? Benki inakopeshaje mtu ambaye haimjui? Dhamana anazoweka kwanini hawazihakiki? Huu ni mchongo wa benki na TISS unawaonea bure. Hujui hata inavyofanya kazi pengine.
 
Back
Top Bottom