Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

Mleta mada kama nawe unaweza kukopa na kusepa fanya tu.
Kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake.
Woga wako ndio umasikini wako.
Hapana tuache tamaa (greed) wizi na kupenda njia za mkato.

Tufanye kazi kwa bidii tulipe kodi na tujenge nchi kwa ajili ya vizazi vyetu vya baadae.

Mimi nimesoma, na hadi hapa nilipo nimefika kihalali kabisa na hata mkopo huwa napata kihalali kabisa kutoka katika benki zetu hakuna shida.

Nipo hapa Kibaigwa ndo makazi yangu na nafaidi matunda ya kazi zangu.
 
Hapana tuache tamaa (greed) wizi na kupenda njia za mkato.

Tufanye kazi kwa bidii tulipe kodi na tujenge nchi kwa ajili ya vizazi vyetu vya baadae.

Mimi nimesoma, na hadi hapa nilipo nimefika kihalali kabisa na hata mkopo huwa napata kihalali kabisa kutoka katika benki zetu hakuna shida.

Nipo hapa Kibaigwa ndo makazi yangu na nafaidi matunda ya kazi zangu.
Hapa JF hayo mambo yako ya kuacha tamaa watu hawatakuelewa nenda kanisani/msikitini huko utapata kusikika na kueleweka.
Watu hapa wanatafuta pesa kwa namna yeyote hata iwe kwa uchawi nk.
Kila mtu ana akili na mawazo yake.
Kama wewe umeridhika na maisha yako hapo Kibaigwa hongera sana endelea hivyo hivyo.
 
Nimeshangaa zaidi Rais ameshindwa hata kumtaja huyo mwizi, tutajie mwizi wa pesa zetu tumjue, sioni sababu ya kumficha hata kama ni masuala ya kiusalama.

Siku hizi kuna interpol, wape information wafanye kazi yao, kuliko kutuambia tu kuna mtu amekopa benki tano akakimbia, naona ni bora angekaa kimya kabisa.
 
Hapa JF hayo mambo yako ya kuacha tamaa watu hawatakuelewa nenda kanisani/msikitini huko utapata kusikika na kueleweka.
Watu hapa wanatafuta pesa kwa namna yeyote hata iwe kwa uchawi nk.
Kila mtu ana akili na mawazo yake.
Kama wewe umeridhika na maisha yako hapo Kinaitwa hongera sana endelea hivyo hivyo.
Hapana,mimi sijaridhika na maisha kwani bado natoa mchango wangu hapa JF na huko duniani ambako ndiko ujira wangu waingia kilaini kwa kazi zangu.

Kama serikali yajifungua nipo tayari kusaidia kimkakati na kitaalam kufanikisha uwezo wa idara zake kujiimarisha na kujiweka sawa kuendana na changamoto za kiteknolojia na kitaalam zaidi.

Wapo watu kama mzee Kipilimba ni wataalam wa "risk management" khasa kwenye vyombo vya fedha na masuala mazima ya usalama wa kisayansi lakini badala yake wamewekwa kando hivyo kukosa msaada wao wa kitaalam.

Natamani sana jamaa akamatwe na ajulikane na pia kuna mtu kasema kuna "Syndicate".

Hii Syndicate ni muhimu ikajulikana na waandishi wa habari za uchunguzi wapewe nafasi wafanye kazi zao.

Watu hawa (wezi) wakiwa wanafahamika inakuwa ni jambo la uzuri kwa nchi kwani kunaleta "awareness", if you know what I mean na yaleta chagizo kwa voymbo vya usalama, polisi na uhamjai kufanya kazi zao ipasavyo.

Lakini kusema ati mimi nimeridhika hapana, sijaridhika kabisa mkuu mpaka kieleweke.
 
Wapo watu kama mzee Kipilimba ni wataalam wa "risk management" khasa kwenye vyombo vya fedha na masuala mazima ya usalama wa kisayansi lakini badala yake wamewekwa kando hivyo kukosa msaada wao wa kitaalam.
Kwa maana hiyo hakuna watu wengine waliopikwa kwenye risk management wa kuziba nafasi ya kipilimba.
Angetangulia mbele za HAKI tusingesema kawekwa pembeni.
 
Haiwezekani mtu huyo kutokufahamika, abadani! H. A. I. W. E. Z. E. K. A. N. IIIII!!

Utaratibu wa kupata mikopo benki ipoje mpaka kutokumfahamu mtu huyo sshvi!!!?

Imefahamika vipi kua hayupo nchini!!!? ( Au ndio )

Hili halikubaliki
 
Kwa maana hiyo hakuna watu wengine waliopikwa kwenye risk management wa kuziba nafasi ya kipilimba.
Angetangulia mbele za HAKI tusingesema kawekwa pembeni.
Huu ni utaalam maalum hivyo huitaji mkakati wa serikali kuhakikisha ina watu hawa.

Hivyo Kipilimba angeweza kupewa nafasi ya kufundisha vijana wapya na pale UDSM wakawa na Department ya masuala haya ya security and risk management.

Huko ughaibuni sasa hivi wana shahada za ujasusi yaani Security & Intelligence na zingine.

Yategemea na mtazamo wa serikali kuhusu masuala haya.

Wenzetu China wakituma vijana wake kwenda Ulaya kusoma wapo ndani yake wana shughuli zingine kusomea masuala kama haya.
 
Tafadhali Mods msifute uzi huu kwani wahusu zaidi usalama taifa kwa ujumla.

hirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Raisi aliyopo ndo tatizo wala sio bank unakuta ni jamaaa amekuja hapo na smart breefcase kutoka Nigeria akaondoka na 50b sio mchezo
 
Tafadhali Mods msifute uzi huu kwani wahusu zaidi usalama taifa kwa ujumla.

Jana, raisi wa Jamhuri ya ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benk 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.
Akili inaniambia huyo aliyefanya hivyo ni miongoni mwao
 
Raisi aliyopo ndo tatizo wala sio bank unakuta ni jamaaa amekuja hapo na smart breefcase kutoka Nigeria akaondoka na 50b sio mchezo
Na labda aingine nchi zingine kuhifadhi fedha hizo kwani huko Ulaya sasa hivi wamejipanga kukataa fedha chafu kuingizwa katika banking systems zao.

Sasa hivi wameweka masharti kadha wa kadha yanozuia kuweka fedha kama hizo kuzuia utakatishaji fedha na kuchukua fedha za wizi.

Labda kule visiwani Jersey na kwingine.
 
Wewe kama unafikiri kukopa benki ni rahisi neenda ukakope uone ugumu wake.
huyo mkopaji lazima alikuwa anashirikiana na wafanyakazi wa hizo benki. Benki ni taasisi binafsi kwa asilimia kubwa na wao ndiyo wanatakiwa kuwachunguza wateja wao. Hiyo mikopo haikuwa na securities zo zote au amepewa tu kienyeji (labda kwa kuwa mzungu au muhindi).
 
Tafadhali Mods msifute uzi huu kwani wahusu zaidi usalama taifa kwa ujumla.

Jana, raisi wa Jamhuri ya ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benk 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti zatu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini anaweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Hawajalala, ni mchongo,

Branch managers wote Wana mfumo uliounganishwa jikoni.

Haiwezekani ipite 5 banks wasijue.
 
Hiyo ni syndicate ya hali ya juu inajulikana vizuri na ma boss wa Bot......ila sisi raia wa kawaida tunaanza kujadili masuala tusio ya jua, kufanya justification ya wizi tu.
Nafkiri hii ndo ingekuwa comment ya mwisho na uzi ufungwe 👍🏾
 
Wewe kama unafikiri kukopa benki ni rahisi neenda ukakope uone ugumu wake.
Taasisi zetu za fedha bado ziko nyuma saana. Pia, nchi bado iko nyuma kuhusu individual financial records ikiwa ni pamoja fedha alinazo mtu, mali zisizohamishika alizonazo mtu, madeni aliyonayo, na credit rating ya mtu. Nchi zilizo na records nzuri ukiingiza namba ya uraia unaona haya yote. Mkopo unatolewa baada ya kuona uwezo wa kukopa na kurudisha upo. Kwa mfano hili la mikopo 5 au 6 lingeweza kuonekana na kutoa shaka haraka.

Naona TISS wanalaumiwa, lakini hapa TISS wangefanya nini? Hata huko Ulaya kosa kama FBI au NIS hawawezi kulizuia, ila likifanyika wanaweza kupeleleza na kuona jinsi ya kuwapata. Upelelezi kama huu hauychukui siku moja au mbili. Upelelezi hukukuwa muda kwa sababu tahadhari huchukuliwa na wahalifu na wakati mwingine husaidiwa na mitandao mikubwa ndani na nje ya nchi.
 
Back
Top Bottom