Hivi idara ya usalama wa taifa wa Tanzania inahusika na kila kitu hadi uuzaji wa nyanya na vitunguu magengeni?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,242
113,627
Siyo mjuzi sana wa habari za idara ya usalama wa taifa, Tanzania.

Lakini katika pitapita zangu humu JF, nimekutana na mada kadhaa zilizonishangaza kidogo.

Mtu akienda dukani akikuta bidhaa ambayo haipendi, lawama anabebeshwa usalama wa taifa.

Msanii Diamond umaarufu wake ukianza kupungua, lawama zinaenda kwa usalama wa taifa!

Timu za mpira za Tanzania zisipofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa, lawama kwa usalama wa taifa!

Ni mimi tu ambaye sielewi dhima nzima ya usalama wa taifa au inakuwaje?

Kwa mfano, usalama wa taifa wanahusikaje na uwepo wa bidhaa za Kenya kwenye maduka ya Tanzania?

Kwa akili zangu hizi za panzi, waamuzi wa mafanikio ya bidhaa ni wateja/ wanunuzi.

Kama wateja/ wanunuzi wanaona bidhaa fulani ni bora kuliko bidhaa ingine, basi wataendelea kuiunga mkono kwa kuinunua.

Na ubora wa bidhaa sidhani kama unahusiana chochote na idara ya usalama wa taifa.

Ubora wa bidhaa unatokana na ubunifu wa mzalishaji. Mzalishaji anapotengeneza bidhaa iliyo bora halafu akaitangaza kwa umma, umma huo ndo utaamua mafanikio ya hiyo bidhaa.

Sasa kama makampuni ya Tanzania hayatengenezi bidhaa zilizo bora kutokana na kushindwa kuwa wabunifu, lawama kwa usalama wa taifa zinahusikaje?

Hmm…..yawezekana ni mimi tu na hizi akili zangu za panzi ndo maana labda sielewi.

Wajuvi na wajuzi wa mambo nijuzeni, tafadhali.
 
Usalama wa taifa katika uchumi.

Watu wako inapaswa wawe salama kiuchumi. Ukiona kuna bidhaa inatoka nje ni bora kuliko ya kwenu mnatakiwa mfanye namna mjifunze mbinu na technology yao ili wananchi went wawazidi wale wa nje

Usalama ktk mpira.

Kama viongozi wa mpira wanapanga kikosi cha taifa kibwegebwege na kuna watanzania wazuri ndani na nje ya nchi
 
Siyo mjuzi sana wa habari za idara ya usalama wa taifa, Tanzania.

Lakini katika pitapita zangu humu JF, nimekutana na mada kadhaa zilizonishangaza kidogo.

Mtu akienda dukani akikuta bidhaa ambayo haipendi, lawama anabebeshwa usalama wa taifa.

Msanii Diamond umaarufu wake ukianza kupungua, lawama zinaenda kwa usalama wa taifa!

Timu za mpira za Tanzania zisipofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa, lawama kwa usalama wa taifa!

Ni mimi tu ambaye sielewi dhima nzima ya usalama wa taifa au inakuwaje?

Kwa mfano, usalama wa taifa wanahusikaje na uwepo wa bidhaa za Kenya kwenye maduka ya Tanzania?

Kwa akili zangu hizi za panzi, waamuzi wa mafanikio ya bidhaa ni wateja/ wanunuzi.

Kama wateja/ wanunuzi wanaona bidhaa fulani ni bora kuliko bidhaa ingine, basi wataendelea kuiunga mkono kwa kuinunua.

Na ubora wa bidhaa sidhani kama unahusiana chochote na idara ya usalama wa taifa.

Ubora wa bidhaa unatokana na ubunifu wa mzalishaji. Mzalishaji anapotengeneza bidhaa iliyo bora halafu akaitangaza kwa umma, umma huo ndo utaamua mafanikio ya hiyo bidhaa.

Sasa kama makampuni ya Tanzania hayatengenezi bidhaa zilizo bora kutokana na kushindwa kuwa wabunifu, lawama kwa usalama wa taifa zinahusikaje?

Hmm…..yawezekana ni mimi tu na hizi akili zangu za panzi ndo maana labda sielewi.

Wajuvi na wajuzi wa mambo nijuzeni, tafadhali.
Mi najiuliza tuu hadi huu ubadhilifu unafanyika ngazi ya halimashauri wao ofisi ya DSO huwa ipo busy na majukumu gani?
 
Hata humu JF wamo wanachungulia tunayoyaandika.

Kama jina linavyojieleza,wao ndo chanzo kikuu cha hali halisi ya nchi. Binafsi nahisi ni kwa sababu wao wana uwezo mkubwa wa kufikia kila aina ya taarifa inayohitajika na kufikishia taasisi husika.
Umeongelea bidhaa mfano za Kenya.
TRA ina kazi ya kudhibiti magendo. Waonapo bidhaa za Kenya madukani,hakika wana wajibu wa kujua zimeingiaje. Kwa maana ushuru umelipwa? Maana zikiingia kiholela,mapato ya serikali hamna. Na ikiwa hivo,hata siraha na ujangili na mambo mengine ya ovyo yatapita njia hio.

Na ubora wa bidhaa sidhani kama unahusiana chochote na idara ya usalama wa taifa: TBS ni kitengo cha taifa chenye jukumu la kusimamia ubora wa bidhaa watumiazo raia. Mfano nchi furani imeingiza kinywaji ambacho kinaweza kuwa na madhara kikitumiwa. Si alietengeneza anataka tu hela? Madhala yake kumbuka yataighalimu serikali. Kwa hiyo usalama wa taifa wanahusika kila kona uijuayo. Ni siri zao sisi hazituhusu,lakini utakuta kwenye kila tuhuma, na wenyewe wapo.
 
Wao Ni kila kitu nchini na lazima wapewe lawama...la viroba vya maiti inasemakana waliliweza, ila mafisadi, Mpaka tenda itangazwe upya...
 
Kuna mmoja humu kaulalamikia usalama wa taifa kwa uwepo wa sabuni ya jamaa. Duh! Kama ni hivyo basi usalama wa taifa labda utakuwa unahusika na bidhaa kama nyanya na vitunguu huko masokoni. Hata mimi pia sijui mukhtadha wa usalama wa taifa shughuli zao zinaanzia na kuishia wapi zaidi ya stori za vijiweni kuwa usalama wa taifa wapo kila idara
 
Siyo mjuzi sana wa habari za idara ya usalama wa taifa, Tanzania.

Lakini katika pitapita zangu humu JF, nimekutana na mada kadhaa zilizonishangaza kidogo.

Mtu akienda dukani akikuta bidhaa ambayo haipendi, lawama anabebeshwa usalama wa taifa.

Msanii Diamond umaarufu wake ukianza kupungua, lawama zinaenda kwa usalama wa taifa!

Timu za mpira za Tanzania zisipofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa, lawama kwa usalama wa taifa!

Ni mimi tu ambaye sielewi dhima nzima ya usalama wa taifa au inakuwaje?

Kwa mfano, usalama wa taifa wanahusikaje na uwepo wa bidhaa za Kenya kwenye maduka ya Tanzania?

Kwa akili zangu hizi za panzi, waamuzi wa mafanikio ya bidhaa ni wateja/ wanunuzi.

Kama wateja/ wanunuzi wanaona bidhaa fulani ni bora kuliko bidhaa ingine, basi wataendelea kuiunga mkono kwa kuinunua.

Na ubora wa bidhaa sidhani kama unahusiana chochote na idara ya usalama wa taifa.

Ubora wa bidhaa unatokana na ubunifu wa mzalishaji. Mzalishaji anapotengeneza bidhaa iliyo bora halafu akaitangaza kwa umma, umma huo ndo utaamua mafanikio ya hiyo bidhaa.

Sasa kama makampuni ya Tanzania hayatengenezi bidhaa zilizo bora kutokana na kushindwa kuwa wabunifu, lawama kwa usalama wa taifa zinahusikaje?

Hmm…..yawezekana ni mimi tu na hizi akili zangu za panzi ndo maana labda sielewi.

Wajuvi na wajuzi wa mambo nijuzeni, tafadhali.
Mimi hiko hakinishangazi.....kinachonishangaza ni Kadhia ya Wizi na Ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na uhujumu Uchumi wa Taifa unaofanywa na baadhi ya Viongozi huku tukiaminishwa kuwa hawa jamaa wako kila kona kila ofisi?
Dhima yao hasa ni nini?

Usalama wa Taifa si pamoja na Uchumi wa Taifa?

Naamini Taifa lenye uchumi dhaifu si taifa salama hata kidogo.
 
Kuna mmoja humu kaulalamikia usalama wa taifa kwa uwepo wa sabuni ya jamaa. Duh! Kama ni hivyo basi usalama wa taifa labda utakuwa unahusika na bidhaa kama nyanya na vitunguu huko masokoni. Hata mimi pia sijui mukhtadha wa usalama wa taifa shughuli zao zinaanzia na kuishia wapi zaidi ya stori za vijiweni kuwa usalama wa taifa wapo kila idara
Umesahau tu......ulikuwa ukisikika tu unalalamika vyuma vimekaza unatiwa ndani. Sembuse Sabuni??
 
"Kwa mfano, usalama wa taifa wanahusikaje na uwepo wa bidhaa za Kenya kwenye maduka ya Tanzania?

Kwa akili zangu hizi za panzi, waamuzi wa mafanikio ya bidhaa ni wateja/ wanunuzi."

Kweli kwa akili zako. Ila ziko chini sana. Ungeuliza ufafanuliwe.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Kuna mmoja humu kaulalamikia usalama wa taifa kwa uwepo wa sabuni ya jamaa. Duh! Kama ni hivyo basi usalama wa taifa labda utakuwa unahusika na bidhaa kama nyanya na vitunguu huko masokoni. Hata mimi pia sijui mukhtadha wa usalama wa taifa shughuli zao zinaanzia na kuishia wapi zaidi ya stori za vijiweni kuwa usalama wa taifa wapo kila idara
Hata sasa hivi mvua hizi zinazonyesha lawama ziende kwa usalama wa taifa!
 
Back
Top Bottom