Ni kweli kabisa kuwa huwezi ukafananisha WCC,Vatican na OIC kwa namna yoyote ile.Ishu ya kujiunga OIC ni vritical na in anyway lazima tujiulize consequeces za kujiunga na kubaki tulivyo as a nation.Kama wapo wasioafiki lazima ziwepo sababu ambazo ziko shared na kila mtanzania na kama wapo wanaoafiki lazima ziwepo sababu ambazo zinakuwa shared na kila raia.
Tusipapatikie kujiunga OIC kwa sababu za kidini na wala tusipinge OIC kwa sababu za kidini.Tuwe na sababu za kitaifa.Tutafika tu
mAENO YAKO YANANIKUMBUSHA kauli ndani ya kitabu kilichotolewa na na
Halmashauri Kuu ya Maaskofu ya Baraza la Kanisa la Pentekoste la Tanzania(PCT), mwaka 2000 kitabu kile kiliitaka serikali iitishe kura ya maoni kwanza, kabla ya kuamua kujiunga na (OIC), ili kupata ridhaa za Watanzania
Kitabu hicho, kilichopewa jina la
"Amani katika Tanzania italindwa kwa:kutenganisha Dini na Mamlaka ya nchi", kinaeleza kuwa kitendo cha serikali ya Tanzania kutaka kujiunga na OIC si jambo dogo. Nijambo linalowahusu Watanzania wote, Waislamu na wasiokuwa Waislam, na hata wale wasiokuwa na dini yo yote. Zaidi ya hayo kile kitabu kilidai kuwasuala la OIC halifai kujadiliwa kijuujuu tu, kwa kupitia katika vyombo vya habari, na
wala haifai kuachiliwa Bunge peke yake kuamua juu ya jambo zito kama hilo.
VILE VILE Halmashauri Kuu ya Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, kwa kupitia katika kitabu hicho, walisisitiza kuwa serikali iitishe kura ya maoni ili ipate kuelewa msimamo wa Watanzania wote, wa dini mbalimbali, juu ya jambo hilo...waliendelea kudai kuwa si kazi ya Bunge kutunga sheria za kidini, kwa kuwa OIC ni taasisi ya kidini, ni muhimu taasisi nyingine za kidini zilizopo hapa nchini nazo zishirikishwe kikamilifu katika uamuzi mzito kama huo.
In short Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, katika kitabu kile , walilitilia mashaka uhusiano huo kama utaanzishwa. Wawalidai edai kuwa lengo la misaada inayotolewa na taasisi hiyo ni kwa ajili ya kutaka kueneza imani ya dini hiyo katika nchi wanachama.....maneno ambayo hayana sana tofauti na wana JAMII FORUMS wanaoipinga OIC humu...wale maaskofu pia waliendelea kusema kuwa kama Tanzaniaitajiunga na taasisi hiyo basi itakuwa ni sawa na kuwasilimisha Watanzania bila ya nidhaa yao!
sounds familiar?
Huhitaji kuwa scientist wa BIG BANG ukaelewa kuwa kile kitabu kilitolewa na kanisa la Pentekoste, kama ni onyo kwa serikali isijiunge na OIC, baada ya kumsikia mgombea wa kiti cha urais wa Zanzibar mwaka 2000 Amani Karume katika madahalo ulioandaliwa na BBC, ambako alisema kuwa serikali imekwishafanya utafiti na imeona kuwa Tanzania ijiunge na taasisi hiyo, kwa kupitia serikali ya Muungano, na siyo kupitia serikali ya Zanzibar..yes that was back in 2000!!!
Binafsi sikuzote huwa nawapa heshima kubwa maaskofi kwa kuwa naamini kuwa wao walisoma theology kwenye shuleza seminary ambazo tunaambiwa kuwa wanaproduce wasomi waliobobea lakini kwa vyovyote vile, mtazamo huuu wa Maaskofu pamoja na wa wana JF wanaoipinga OIC kwa sababu tuu Maaskofu walisema na zaidi kwa sababu:
1)umekosa uadilifu
2)Ni mtazamo ulioelekezwa katika kuuangalia upande mmoja tu wa shilingi na kuupuuzia upande wa pili.
3)Ni mtazamo chongo! Ni sawa na mtu mwenye macho mawili lakini akaamua, kwa makusudi, kufumba jicho moja na kuangalia kwa jicho moja.
UHUSIANO WETU NA VATICAN
Kama serikali ya Tanzania haifai kujiunga na OIC, bila ya kuitisha kura ya maoni kama baadhi ya watu humu mnavyodai, eti kwa sababu OIC ni taasisi ya kidini; basi lazima tukubali kuwa kwa hoja hiyohiyo, serikali hiyo ya Tanzania itakuwa imefanya kosa kuanzisha uhusiano, tena wa kibalozi, na Vatikano, ambayo ni taasisi ya kidini, na siyo nchi yenye raia!
Furthermore, uhusisano huo wa serikali ya Tanzania na Vatikan, ingawa ni uhusiano baina ya nchi hii na Kanisa Katoliki duniani, lakini jambo la kustaajabisha hakuna yeyote anayehoji juu ya uhusiano huo, si serikali wala makanisa ya Kikristo!!!! au ndio tunaendeleza double standards kama kawaida yetu?
Mheshimiwa Aboud Jumbe, ambaye kwa rate ya members wasio ambao JF inawaatract kila kukicha ambaye aliwahi kuwa Makamu Rais wa Jamhuri ya Miuungano wa Tanzania, na pia, Makamu Mwenyekiti wa CCM, katika kitabu chake alichokiita,
"The Partner-ship" ambacho ninacho hapa amesema,
"Kwa mfano, kuwepo kwa ubalozi wa Vatican nchini Tanzania hakukupata kuhojiwa, pamoja na kuwa serikali hii inadai kuwa si ya kidini. Kanisa, CCM na serikali, vyote vimekaa kimya huku vikijua kutendeka kwa hilo lakini vitazibwa mdomo." (Uk.126).
Kama ningekuwa msemaji wa waislam wa Tanzania niaba yao, ningalikubaliana na matakwa hayo ya Maaskofu, kwamba iitishwe kura ya maoni, isipokuwa kwanza, kwa vile uhusiano wa Tanzania na Vatikan haujawahi kupigiwa kura hiyo ya maoni ili kuwauliza Watanzania kama wanautaka au la, tungelianza kuupigia kura hiyo uhusiano huo, ilitupate kuuhalalisha.
Vile vile kutokana na sensitivity ya kuala lenyewe kwa upande mwingine naafikiana kabisa na wazo la Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, kuwa jambo hilo lisijadiliwe katika vyombo vya habari, na pia lisiachiliwe Bunge kuamua peke yake. Nina sababu mbili kuu nazo ni:
1) kwa vile vyombo vingi vya habari Tanzaniai, aidha, vinamilikiwa na kusimamiwa na Wakristo basi kama vyombo hivyo vitalijadili jambo hilo, kuna kila aina ya uwezekano wa kuupendelea Ukristo kuliko Uislamu na kusababisha jambo hilo lionekane halifai. mfano ni IPP MEDIA ambao huhitaji kuwa na PHD ukajua kama siku zote wao wamekuwa biased against waislam
2) kama jambo hilo litapelekwa Bungeni, basi pia, kwa vile Wabunge wengi wa mabunge yote yaliyopita, katika nchi hii, wamekuwa ni Wakristo, bila ya shaka yo yote, watatumia jazba na ukereketwa wao kukwamisha mswada huo, kama walivyojaribu katika vika vya Bunge vilivyokwisha na mfano ni ile issue ya wao kupinga suala la wanafunzi wa kike katika mashule kuvaa sare zinazoendana na maadili ya dini zao!
Najua kuna watu watadai kuwa hii ni sumu lakini ukweli ni kuwa uwanja kama wa JF ndiko mahala pake kujadili hata yale tusiyopenda kuyajadili as long as tunajibizana kwa hoja. Na wakati watu wanakatazwa wasichanganye dini na siasa, kuna ushahidi kuthibitisha kuwa, Wakristo, kwa kupitia katika vitengo vyao vya kanisa, wamekuwa wakiandaa mikakati ya makusudi kuhamasishana wagombee nafasi za ubunge....again this is no brainer kwani kwa kuthibitisha hayo, P
adre wa Kikatoliki, Dkt. John C. Sivalon, katika kitabu chake alichokiita
"KANISA KATOLIKI NA SIASA YA TANZANIA BARA -1953 HADI 1985" ambacho ninacho hapa ameeleza kuwa ;
"Mwishowe, SSY ilitoa msisitizo juu ya jukumu la walei katika jamii. Haya yalitokea wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 1970.
Dkt. Sivalon akaendelea kusema,
"Ingawa hakuna utafiti uliofanywa kuonyesha uhusiano kati ya SSY na wabunge waliochaguliwa, mmoja kati ya watu waliohojiwa alidaikuwa: SSY na Baraza vimeleta msisimko huu ambao umewaamsha Wakatoliki kupigania viti katika uchaguzi wa Wabunge na mimi nikiwa mmoja wao."
Padre huyo anaendelea kusema,
"Baadaye huko Bungeni tulifanya utafiti usio rasmi na kugundua kwamba asilimia 75 ya waliochaguliwa walikuwa Wakristo, na kati ya hao asilimia 70 walikuwa Wakatoliki"
( mwenye hiki kitabu atazame Uk.49).
Kwa hali hiyo, kama vyombo vya habari vya Tanzania pamoja na Bunge la nchi hii vitaachiwa vijadili juu ya suala hili, kwamba Tanzania ijiunge na OIC au isijiunge, basi tujue kuwa Wakristo waliomo katika vyombo hivyo, watatumia wingi wao kupinga serikali isiwe na uhusiano na taasisi hiyo! haikatazwi suala kujadiliwa lakini be prepared for one sided bias toka kwao...
Lakini kama suala hilo wataachiwa Watanzania walipigie kura ya maoni, ni wazi kuwa wengi wataliunga mkono kwa sababu katika nchi ambayo Waislamu ni wengi kuliko Wakristo,(according to STATE DEPARTMENT) ingawa baadhi ya waandishi wa Kikristo wamekuwa wakijaribu sana kuipindua sura hiyo ili kuonesha kuwa Wakristo ndio wengi kuliko Waislamu!
vILE VILE TUSISAHAU KUWA Ndugu Mohamed Said, mwandishi wa kitabu,
"The Life and Times of Abdulwahid Sykes", ambacho nacho ninacho hapa akieleza juu ya suala hilo amesema,
"D.B. Barret anatoa takwimu zinazoonesha Waislamu ni wachache Tanzania. Idadi ya Waislamu imefanywa ionekane kuwa ni asilimia 26, Wakristo asilimia 45, dini za kienyeji asilimi 28. Takwimu za Tanzania National Demographic Survey, kwa 1973,zimewaweka Waislamu katika Tanzania juu kidogo ya Wakristo, ni asilimia 40,Wakristo asilimia 38.9 na dini za kienyeji asilimia 21.1. Lakini kwa mujibu (wa Kitabu) "Africa South of the Sahara", Waislamu katika Tanzania wanaongoza kwa wingi, ni asilimia 60. Idadi hii imebaki hivyo hivyo katika matoleo yake yote tokea 1982."
Kwa kuwa haikufanywa sensa ya makusudi ya kutaka kuelewa idadi ya Waislamu na Wakristo katika Tanzania, basi ni vyema tukafuata ushauri na Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, kuendesha kura ya maoni siyo kwa suala la kujiunga na OIC tu, bali pia na suala la uhusiano na Vatikano, kama hatukuja kushitukia OIC inakubalika na Vatikano inakataliwa, hapo ndipo tutakapoelewa wepi ni wengi Tanzania, ni Waislamu au Wakristo?
Na kwa nini tufikishane mpaka kwenye kuandaa kura ya maoni?
Kwa nini tuvutane?
Jambo liko wazi na kigezo tunacho! Ikiwa muasisi wa Taifa hilo, Hayati Mwalimu Nyerere,(ambaye ana watetezi wakubwa tuu humu JAMII FORUMS) ndiye aliyekuwa wa kwanza kuanzisha uhusiano wa kibalozi baina ya serikali yake na taasisi ya kidini ya kanisa Katoliki duniani, Vatikano, vipi sisi, tunaojifanya tunafuata nyayo za kiongozi huyo, na kudai kuwa tunayaenzi mema yake, tupinge serikali kujiunga na taasisi ya kidini ya OIC?
Au ni kwa sababu mtazamo chongo umetulevya mpaka tukaona uhusiano na taasisi ya Kikristo ni sawa lakini uhusiano na taasisi ya Kiilslamu ni dhambi?
Kwa nini hatufunui macho yote mawili tukaona sawasawa?
Ama swali la kutaka kuwasilimisha Watanzania bila ya ridhaa yao, hilo halipo na hata Kur'ani Tukufu inasema,
Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia)katika dini, uongofu umekwisha pambanuka na upotofu (Al-Baqarah). Surely Maaskofu waliobobea kwenye theolofy wanalijua hilo kwa hivyo si sawa kutumia jazba katika kuangalia mambo ya dini.
Aidha, pamoja na watu kuleta info na links za OIC its quite clear kuwa misaada inayotolewa na OIC si ya kidini na wala haina lengo la kuwaingiza watu katika uislamu.
Kama taasisi ya kidini inapotoa misaada huwa lengo lake ni kuwavuta watu waingie katika dini hiyo basi na misaada inayotolewa na Vatikano, kwa kupitia kanisa Katoliki nayo itakuwa inalenga kuwaingiza Watanzania katika Ukristo...mbona waislam hawalalamiki kuhusu CARITAS ?
Kanisa Katoliki limejenga shule, zahanati na hospitali na zinatumiwa na Watanzania wote bila ya kujali tofauti zao za kidini, jee kanisa hilo nalo nia yake ni kuwabatiza wanaopata huduma hizo?
Jamani OIC inatoa misaada ya kijamii tu. Inajenga mashule, mahospitali, barabara, madaraja na mfano wa hayo, kwa ajili ya faida ya jamii nzima na siyokuwa Waislamu tu. Misaada hiyo haitolewi kwa vikudni binafsi, inatolewa kwa nchi nzima, ndiyo maana taasisi hiyo ikataka nchi inayotaka ifaidike na misaada hiyo ijiunge na taasisi hiyo.
Uganda na Mozambique si nchi za Kiislamu, na wala hazina Waislamu wengi; lakini serikali za nchi hizo zimejiunga na OIC na zinafaidika na misaada inayotolewa na taasisi hiyo, bila ya kulazimishwa nchi hizo kufuata imani ya Kiislamu. Chuki za kuuchukia Uislamu zisiwe ndiyo sababu ya kutowatendea uadilifu Waislamu.
na kama picha hiyo hapo chini utaona waislam hawana khiyana na serikali kama ikiacha kuwaingilia mambo yao
Just my 2 cents