sasa
GT unanichanganya
kama serikali hii ya CCM haikufanyii mema ndani ya BAKWATA je ni serikali hiyohiyo itakufanyia mema nje yani ktk OIC.
Hapa ndipo utatambua kuna walalamishi tu kwa vile ni wakulalama siku zote.
Sijasema mimi ni BAKWATA na kama utasoma post zangu za nyuma kuhusu misimamo yangu on mambo ya dini utaona napinga sana dini kuingizwa kwenye serikali
Hapa nishawahi kuanzisha thread ambayo ililenga kuondoa unafiki uliowajaa watu humu kujidai ohhh serikali haona dini lakini raia wake wanayo haki ya kuwa na dini
sasa swali kwa nini TUNAKUBALI NYIMBO YA TAIFA iliyojaa kuwabagua wasio na dini?
surely unapokuwa na nyimbo ya taifa inayosema MUNGU IBARIKI TANZANIA ...maana yake ni nini haswa kama si maombi?
Je watu wako tayari kujadili hayo? HAKUNA
on a flip side sikuzote huwa nasema udini uliiingizwa na Nyerere enzi za utawala wake na ni kweli hata serikali ilikubali kuwa waislam walikuwa wanakandamizwa na hilo halina mjadala ...na ni kweli walikuwa wanakandamizwa na CCM hilo nalo halina mjadala
Kama mnakubali kuwa CCM imerudisha nyuma nchi whats so difficult kukubali kuwa CCM hiyo hiyo ya akina MALECELA na kundi lake ilikuwa inawakandamiza waislam?
Kila kukicha tunambiwa na viongozi pamoja na watawala wetu kuwa Tanzania ni yetu sote, Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya haki na usawa kwa wote, Tanzania ni nchi inayothamini haki za binadamu, Tanzania ni nchi ambvayo haina dini, Tanzania ni nchi ambayo katiba yake ndiyo sheria mama n.k.
Lakini jambo la kushangaza ni kule kuwaona wale wanaotukumbusha kila siku juu ya sifa hizi za Tanzania wakienda kinyume na maneno yao wenyewe pale wanapotakiwa kutekeleza jambo. Na hapo ndipo decree ya kuwa wao ni wanafiki inapokuwa wazi na bayana kabisa. Wanakuwa ni wanafiki kwa vile kusema uongo, hawatimizi ahadi na kuchezea dhamana tuliyowapa hasa ile ya kulinda katiba ya nchi.
Lakini usipotosheke kuna kundi la akina MALECELA lilifanikiwa kupanda megu mbaya ya Chuki ambayo inapandikizwa ili iwatenge Watanzania katika misingi ya dini zao.Its no brainer, huu mjadala wa OIC unaonyesha kuwa kuna watu wanaujadili si kwa lingine zaidi ya yale mawazo ya kizamani eti leo hii mtu mwenye elimu, madaraka, mali, hadhi n.k. anatarajiwa awe Mkristo. Na kinyume chake ni Muislamu. Kiasi kwamba hashangai mtu kuiona hali hii bali mtu atashangaa sana anapoona kinyume chake.
Hali hii imeasisiwa, imelelewa, imekuwa na kukomaa na Nyerere na kundi lake na mifano ipo kusupport hoja hiyo hapo juu itakayoonyesha kuwa kuwa kuna watanzania wanataka kuwafanya wenzao kama vile wale jamaa kule Yugoslavia ya zamani walivyowafanya wenzao wa Bosnia.
Kwanza kabisa: ni kwamba Tanzania imefika mahali kwamba watu wengine wamejichukulia madaraka yanayowawezesha kuwapa Watanzania wenzi wao wa dini nyingine tafsiri ya dini yao na namna ya kuifuata. Waislam walipoanza kuquestion mamabo ya OIC walijibiwa na maneno ya kuchonga kama Mujahidina, msimamo mkali, siasa kali na mengine ambayo yaliibuka kwa msingi huu wenye lengo la kuwagawa na kuwakandamiza Waislamu wa Tanzania, watawala wa CCM hilo wanalijua fika
Nakumbuka hali hii in 1990's ilitufikisha mahali kuwa mwalimu wa shule ya serikali anaingia hofu na kutumia nguvu nyingi sana kupinga mwanafunzi Muislamu Mtanzania kuvaa vazi la dini yake....mpaka Rais akaliingilia
Pia nakumbuka back in 90's tulifika mahali maafisa wa Manispaa kubwa kama ya Dar es Salaam chini ya uongozi wa Tume ya Jiji walijipa mamlaka ya kutoa aina ya hijab anayopaswa kuvaa binti Muislamu shuleni! Mind you hapa siongelei NIQAB au lile vazi la ninja bali nazungumzia Hijab
Nakumbuka issue ilifikia mahala iliandikwa barua na Tume ya Jiji kwa Maafisa Elimu wa Kanda mwaka 1999 mabinti wanatakiwa wavae mashati maupe ya mikono mifupi! Je, uamuzi huu ulionyesha ujinga (kutojua) kwa watu wa Tume? Jibu ni hapana kwani walikuwa na nafasi ya kutosha kutaka ushauri kwa viongozi wa dini na hawakuona haja....
Kwanini basi walifanya hivyo? Jibu lake ni ule U MILOSOVICH niliosema mwanzo. Umilisovich huu humfanya mtu aone kuwa yeye anayo mamlaka ya kuamua ni sehemu gani ya Uislamu ifuatwe na sehemu gani isifuatwe. Wala hana wasiwasi kuwa anaweza akatokea Muislamu yeyote kumhoji. Na ikiwa atatokea basi ule mtandao wao utamtafutia moja ya yale majina niliyoyataja hapo juu na dola itashughulika naye....the same applies na marehemu kada mkubwa wa CCM DR OMAR ALI JUMA kuwapiga mkwara wale Ansar Sunna kuswali Iddi pale Jangwani kisa? BAKWATA hawakutangaza kuonekana kwa mwezi!!
PILI Rais MKAPA enzi hizo alitembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salam sehemu ya Mlimani. Katika ziara yake Rais alijionea mwenyewe UMILOSOVICH uliopo Mlimani.Hali ilijitokeza pale mmoja wa wanafunzi alipouliza swali kuhusu matumizi ya nguvu ya polisi yaliyopelekea kuuliwa Waislamu Mwembechai 1998.
Kilichojitokeza ni kuwa 'WAMILOSOVICH 'sikuhizi nawaita waliomeza BLUE PILL hao ndani ya ukumbi wa Nkrumah hawakuweza kusubiri muulizaji amalize swali lake bali walianza kuzomea hadi Rais alipoingilia kati na kuwatuliza hao. The same attitude si kazi sana kuona katika posters walipost humu kwenye issue ya OIC maana majibu yao hayakulenga kutaka watu wajadiliane bali ni kukandia all the way wakiongozwa na MCHUNGAJI KISHOKA. Anyway back to ziara ya BEN pale Mlimani....baada ya swali Rais alijibu kuwa suala la Mwembechai lipo mahakamani.
Japo siyo kweli kuwa wale polisi walioua Waislamu pale Mwembechai wameshakamatwa na kufunguliwa mashitaka na japo ni kweli kuwa wasomi wa Chuo Kikuu wanaufahamu ukweli huu, jibu la BEN lilishangiliwa sana!!
Kisha BEN akaombwa amfukuze kazi mara moja aliyekuwa Katibu wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu kwa kile walichokiita kutowajibika kwa Katibu huyo. Waziri ambaye ni Mkristo katika Wizara hizo, kama ilivyokwishajengeka yeye hana tatizo. Kinachofanya yote haya kutokea ni UMILOSOVICH uliopo miongoni mwa Watanzania hakuna cha zaidi.
TATU, hali katika mashule ya sekondari na vyuo vingine nchini ni hiyo hiyo. Ni aghalabu mwanachuo/mwanafunzi Muislamu kupigiwa kura ya kuwa kiongozi katika ngazi ya shule au chuo. Matangazo yote yanayohusiana na mambo ya Waislamu hayadumu katika mbao za matangazo vyuoni. Kila linapowekwa 'WAMILOSOCHICH' hulibandua. Haya mtu yeyote anaweza kuyathibitisha. Nenda Mlimani, nenda Chang'ombe T.T.C., nenda IFM n.k...kama kna members wa MSAUD humu ndani ya JF watakuelezeni zaidi
Hivi unahabari kuwa miezi 14 baada ya mauaji ya Mwembechai leo agenda kubwa ilikuwa ni kumsaka na kumkamata Ponda (dead or live)! Kwa hiyo its quite obvious kuwa lengo hapa lilikuwa ni kuwalinda wauaji; kufukia ukweli wa jambo na kumfanya Ponda ndio (issue) suala la kushughulikiwa...na serikali inshort ilikuwa so blinded na udini kiasi cha kwamba hata priority kwa vyombo vya usalama haukuwa kuwakamata wauaji wa Mwembechai na kuwafikisha mahakamani.
Wala hawafikirii kumkamata PADRI LWAMBANO ambaye alikuwa ni mzushi na mchochezi wa mauaji ya Mwembechai aliyeishinikiza serikali hadi ikapelekea kuua watu Mwembechai.
Ni kwa mtaji huu huu wale watu wanaghushi hati na kukabidhiwa nyumba za WAKFU zilizotolewa na waislam hulindwa na polisi na kuhatarisha usalama wao. Sasa leo hii hebu niambie hata kama kuna hoja za kujadili kuhusu OIC huwezi kuenda nazo mbele bila kuangalia hawa wanaodai kuwa wamekuwa wakionewa wanamawazo gani.Na hii issue ilikuwa polarized zaidi na akina Pengo kumpa directives rais afanyenini huku waislam wakiendelea kujenga hiyo siege mentality ya kuwa wanaonewa
Hujiulizi mbona wizara za serikali hazina bajeti ya kununua kadi za Ramadhani na Iddi lakini inazo za miti krismasi?