Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Nziku,

Nimekwisha lijibu isipokuwa sema hukuridhika na majibu yangu..
Nitarudia kwa ufasaha zaidi....
Mwanakijiji aliuliza kuna ubaya gani tukiwa na Balozi OIC, jambo ambalo nilisema halina mantiki hata kidogo kwa sababu ni lazima kwanza upendekeze hoja hii ya kuwa na balozi ukieleza mazuri ya kuwa na Balozi!...

Hujajibu swali.

Swali lilikuwa kuna ubaya gani kujiunga na IOC ?

Umeshasema hilo la kwamba tutapata faida za "misaada ya Dafur."

Tunataka kusikia ubaya.

Kumbuka, ubaya.
 
Halka,
nadhani Ngekewa kakujibu vizuri sana na imenipunguzia kazi kubwa... Ila kitu kimoja tu ningependa kuongezea hapa.
Hivi kwa nini msijiulize imekuwaje UN, Umoja wa MATAIFA duniani wameweza kuvitambua vyombo vya kidini hali umoja huo hauna dini kama tulivyo Tanzania?....

Mkandara,
Nadhani kama ulisoma maswali yangu mafupi unajua kuwa sikujibiwa, na hakuna aliejibu mpaka sasa. Labda ni ya kijinga sana?

Mimi naona kuhalalisha OIC kwa kigezo cha Vatican, ni upotofu, kama mtoto anaelilia na mimi nataka mbona yule kapewa?
Ukweli ni kuwa kujiunga na ushirikiano huu ni bora uangaliwe kwa macho yote mawili, na sio jicho moja Vatican na jingine OIC,
Wakristu wasitetee Vatican, au waislam wasitetee oic tu, kama vipofu.
Wala mimi sioni haja ya ku risk uhusiano mzuri kati yangu na watanzania wenzangu, kukumbatia either vatican au oic.
Kama zina utata na kupingana na katiba zitolewe mara moja!!
 
Mkandara,
Nadhani kama ulisoma maswali yangu mafupi unajua kuwa sikujibiwa, na hakuna aliejibu mpaka sasa. Labda ni ya kijinga sana?

Mimi naona kuhalalisha OIC kwa kigezo cha Vatican, ni upotofu, kama mtoto anaelilia na mimi nataka mbona yule kapewa?
Ukweli ni kuwa kujiunga na ushirikiano huu ni bora uangaliwe kwa macho yote mawili, na sio jicho moja Vatican na jingine OIC,
Wakristu wasitetee Vatican, au waislam wasitetee oic tu, kama vipofu.
Wala mimi sioni haja ya ku risk uhusiano mzuri kati yangu na watanzania wenzangu, kukumbatia either vatican au oic.
Kama zina utata na kupingana na katiba zitolewe mara moja!!


Mawazo yako mazuri sana Haika.

Ila after all said,to be done.................. Utakua ''kondoo mpotevu''
Sikuzote wale wenye misimamo passive kwenye pande zote huwa wamepotea.
Ila nadhani kwa upande furani utakua umemuelewa vizuri sana MKANDARA which is good,unajua ukiwa bias unajenga nguzo ya UFISADI sasa bora ya kuwa mwangarifu........
 
Mawazo yako mazuri sana Haika.

Ila after all said,to be done.................. Utakua ''kondoo mpotevu''
Sikuzote wale wenye misimamo passive kwenye pande zote huwa wamepotea.
Ila nadhani kwa upande furani utakua umemuelewa vizuri sana MKANDARA which is good,unajua ukiwa bias unajenga nguzo ya UFISADI sasa bora ya kuwa mwangarifu........

nimeelewa mambo aliotaka yeye, maswali yangu masikini hajajibu.
 
Sasa kama alivyopendekeza mwanzoni Rev . Kishoka kuhusiana na Waislaam kuwa na chombo chao kama Wakristu hilo lingekuwa na usawa zaidi lakini serikali ndio imeshatufunga kamba za shingo siku nyingi.. Kelele za Waislaam mnaziona kama kelele za mlalahoi - Kikwete husema kelele hizo hazimzuii kulala. ..


Mkandara,

KUmekuwa na hili suala la kusema EAMWS ilifungwa na Nyerere. Inasemekana Bakwata ni chombo cha Serikali.

Swali langu ni hili, ikiw andani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunadai kuwa Waislamu hawana uhuru wa kuunda vyombo vyao, kuwawakilisha kwa kuwa EAMWS ilifungwa na Nyerere 1968, je kwenda OIC kutasaidia nini ikiwa ndani ya nchi hakuna mshikamano na kuna woga wa mzuka wa Nyerere?

Mimi ningefikiri na kufanya hivi kama ningekuwa ni Muislamu.

Kwanza ni kuleta msukumo wa kuundwa upya wa chombo cha kuwawakilisha Waislamu. na hili ningelianza kwa kutumia mkao wa madhehebu, kwanza, kila dhehebu liwe na chombo kikuu, iwe ismailia, Sunni, Shia, Ahmadiya au wenginewe.

Kisha vyombo vikuu hivi vya madhehebu, ndivyo viongoze wafuasi wao kiroho, vimiliki mali za misikiti na dhehebu.

Baada ya hapo, ndipo kuundwe baraza kuu la kuunganisha madhehebu haya kwa kutokana na viongozi wa vyombo vikuu vya madhehebu. Chombo hiki kikuu, ndicho kiwe mstari wa mbele kama vile TEC au CCT zilivyo na ndipo chombo hiki iwe ni Bakwata au EAMWS mpya kishike hatamu za kujiunga katika jamii na jumuiya nyingine za Kiislamu duniani, huku madhehebu yakiwa huru kujiwakilisha.

Ikiwa Ummah wa Sunni wataungana na jamaa wao wa Saudi na kujiwakilisha, hilo liwe ruksa, ikiwa wa Shia watasema sisi vijana wetu tunawapelea Iran kujifunza kwenye seminari, hilo liwe ruksa.

Kubwa zaidi ni kwa jumuiya hizi kuwa huru na kuondokana na kuitegemea Serikali ya Jamhuri katika maamuzi ya kila siku.

Inaelekea mgongano ndani ya Bakwata ni mkubwa kukiwa na pande mbili, wale ambao ni makuwadi wa Serikali na wale ambao ni huru wenye kutaka EAMWS irudi.

Sasa jambo la kujiuliza ni lini jamii hii itakaa chini na kuondokana na tatizo la uongozi ndani ya jamii na Baraza la uongozi?

Tanzania kama nchi kujiunga OIC, bado hakutakuwa suluhisho kumkomboa Muislamu ikiwa dhana ni kuwa kukimbilia nje ya nchi kupata misaada ndiyo suluhisho wakati kazi ya kwanza ya kumkomboa Muislamu inapaswa ianze ndaniya nchi kwa kuiunda upya Bakwata nakuifanya iwe huru na iwe na nguvu kuisukuma serikali kama vile inavyoonekana kuwa KKKT, CCT na TEC wanafanya.

Jukumu la kuiunda upya Bakwata na kuwaunganisha Waislamu wa Tanzania ni la Waislamu wa Tanzania na si OIC au Serikali ya Tanzania.
 
Nashukuru sana wanajf kwa mjadala wenu,mimi binafsi sioni manufaa ya kujiunga na jumuia hii.Kuna watu wengi wameweka mbele suala la misaada na mikopo isiyokuwa na riba kama sababu yao ya msingi kujiunga na jumuia hii.Kama kweli hii jumuia ni nzuri mbona imeshindwa kumaliza mzozo wa somalia,comoro,mauritania na darfur.Je hizi nchi sio wanachama OIC?
Nafikiri watz tunahitaji mjadala wa kina na utafiti kabla ya kujiunga na jumuia kama hizi.Mimi binafsi hizi hisia za kusonononeka kwa baadhi ya jamii zetu ni kutokana na kukosa sera na nia ya dhati ya kuimarisha uchumi ili uweze kufungua fursa nyingi za watu wetu kujipatia kipato kwa njia halali.Utashi wa kisiasa unakosekana wa kutafuta njia za dhati za kutatua tatizo la ufukara linalosababisha kuleta manung'uniko ndani ya jamii yetu.Nina uhakika kabisa kuwa hata bada ya kupata OIC na Mahakama ya kadhi bado umasikini unaowazonga watz utaendelea kuwepo kama njia za kutafuta thabiti ya kumilki uchumi hazitafanyika.
Namshukuru sana Rev Kishoka kwa kuandika waraka wake nafikiri watz wote tungekuwa na watu wenye kutmia fikra kutatua matatizo yetu nchi ingesonga mbele.Kwa sasa hivi viongozi wengi wa kiafrika wanapenda sana kufikiri kupitia matumbo yao.Hali hii imezalisha kada ya viongozi wanaopenda sana kutawala wakati uwezo huo hawana.
 
Nsaji Mpoki,

..Waislamu wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu sana. tatizo ni kwamba serikali haikufanya juhudi zozote zile ya kukaa nao, kuwazungumza na kuwaelewesha, kuhusu hali halisi.

..tumefika mahali ndugu zetu wamepata "Waalimu"[ponda,ba-salehe,...] ambao sidhani kama wanawaeleza ukweli kuhusu matatizo yao, ambayo kwa hakika kabisa ni yetu sote, na njia za kuyatatua.

..matatizo yetu wa-Tanzania hayatamalizwa kwa kutegemea misaada toka nje. hakuna nchi au jamii iliyopata kuendelea na kuuacha utegemezi kwa njia hiyo.

..hata ukiangalia hao Wakatoliki na madhehebu mengine ya Kikristo hali zao ni mbaya tu.hiyo ni pamoja na kuwepo kwa ubalozi wa Vatican na mashirika yake ya misaada kama Caritas etc etc.

..Kama Wakristo Tanzania wangekuwa wameendelea sana basi nchi hii isingekuwa ikitambuliwa kuwa kati ya nchi masikini wa kutupwa duniani. zaidi wangekuwa na ziada ya kuwapatia ndugu zao, majirani zao, Waislamu.

..binafsi nafikiri tujiunge tu na OIC. ninaamini watatoa misaada ya hapa na pale. lakini tukumbuke kwamba hata huko kwenye kuomba misaada tuna washindani kibao kama Uganda,Msumbiji,...halafu tatizo letu sisi Watanzania hata hiyo misaada hatuna utamaduni wa kuitumia vizuri.

..at the end of the day, naamini Watanzania tutagundua kwamba Vatican,Caritas,OIC,IMF,WB,Kuwait Fund,Saudi Fund, siyo muarubaini wa kuponya matatizo yetu. baada ya hapo nina hakika tutaanza kuwawajibisha viongozi wetu, na zaidi tutajielekeza ktk kutumia vizuri rasilimali zetu na vipawa vyetu kujiletea maendeleo.
 
Naombeni namba ya Mufti, Gorogosi, au Khalifa Khamisi.. I think we need to talk...
 
Naombeni namba ya Mufti, Gorogosi, au Khalifa Khamisi.. I think we need to talk...

Whaat!!?? kumbe hii mada inahusu ile jumuiya ya waislamu....mwenzenu nilikuwa nadhani inahusu International Olympic Committee (IOC)....mwanzilishi kachanganya herufi....ile ya waislamu nadhani ni OIC....
 
Nyani McCain said:
Whaat!!?? kumbe hii mada inahusu ile jumuiya ya waislamu....mwenzenu nilikuwa nadhani inahusu International Olympic Committee (IOC)....mwanzilishi kachanganya herufi....ile ya waislamu nadhani ni OIC....

Nyani,

..yaani unafikiri page 40+ watu wanabishana kujiunga IOC?!!!

..you made my day!!!
 
Nyani,

..yaani unafikiri page 40+ watu wanabishana kujiunga IOC?!!!

..you made my day!!!

si ndo maana niliipuuzia mwanzoni...maana nilikuwa najiuliza inakuwaje tulipeleka timu Beijing kama hatuko wanachama wa IOC....

lakini angalia heading ya mada...inasema IOC na sio OIC.......
 
"Sasa tumefanya utafiti wa kutosha na kugundua kuwa OIC ina faida kwetu na haina madhara, hivyo tunafanya mchakato wa kujiunga, lakini ni vema ikaeleweka wazi kuwa, Zanzibar wasingeweza kupata ridhaa ya kujiunga nayo kwa sababu si nchi katika uso wa kimataifa". - Membe (akizungumza kuhitimisha mjadala wa Wizara yake Bungeni).

Bahati mbaya hakupata nafasi ya kuulizwa maswali; labda ni wakati muafaka sasa:

Huo "Utafiti wa kutosha"

a. Ulifanywa lini ?
b. Kwa maagizoo ya nani yaliyotolewa lini?
b. Ulifanywa na nani ?
c. Kwa mbinu au utaratibu gani wa kisayansi (methodology)?
d. Ulimalizika lini?
e. Ripoti yake iko wapi?

Kama kulikuwa na utafiti wowote wa kutosha natoa changamoto kwa Membe na wahusika wa "utafiti" huo kuweka hadharani ripoti ya utafiti wao kabla hawajalitumbukiza Taifa kwenye OIC. Tunafahamu suala la Mahakama ya Kadhi limehusisha Bunge na tumeambiwa kuwa mapendekezo yake yameshapelekwa kunako husika n.k Lakini kwenye OIC tunaambiwa tu "umefanyika".

Vyanzo mbalimbali vinaonesha kuwa hakuna utafiti uliofanyika isipokuwa uamuzi umechukuliwa bila kufanya utafiti wa kina.
 
Mwanakijiji na wengine,

Badala ya kuuliza methodologies za utafiti tulioambiwa kwamba ulifanywa, sisi JF tuje na mjadala wa kuangalia madhara na faida za OIC. Naona katika suala hili JF tumepoteza dira kwani bado hatujachambua MABAYA na MAZURI ya OIC, na sasa tunajaribu kurefusha mada kwa kuuliza methodologies za utafiti.

Mchango wetu wana JF uwe ni pamoja na kuelimisha wasomaji juu ya FAIDA na HASARA za OIC. Wala hatuhitaji akina Membe & Co watueleze hili. Cha ajabu kurasa takriba 40 zimepita na hakuna anayempinga Membe kwa kueleza namna Tanzania itakavyoumia kwa kujiunga na OIC.

Kujaza kurasa kwa kulinganisha OIC na Vatican hakusaidii chochote na, to my view, beyond the scope of the motion. Wana JF tupeni madhara ya Tz kujiunga na OIC, vinginevyo madai ya Membe hayana mjadala.

Binafsi nimeshindwa kuja na angalau hasara moja ya Tz kujiunga na OIC, na nategemea kuelimishwa/eleweshwa kupita JF.
 
Mgonjwa, ina maana tukiona faida ni nyingi kuliko hasara hatuna budi kujiunga? Kipimo kiwe ni faida na hasara tu?
 
Mwanakijiji na wengine,

Badala ya kuuliza methodologies za utafiti tulioambiwa kwamba ulifanywa, sisi JF tuje na mjadala wa kuangalia madhara na faida za OIC. Naona katika suala hili JF tumepoteza dira kwani bado hatujachambua MABAYA na MAZURI ya OIC, na sasa tunajaribu kurefusha mada kwa kuuliza methodologies za utafiti.

Mchango wetu wana JF uwe ni pamoja na kuelimisha wasomaji juu ya FAIDA na HASARA za OIC. Wala hatuhitaji akina Membe & Co watueleze hili. Cha ajabu kurasa takriba 40 zimepita na hakuna anayempinga Membe kwa kueleza namna Tanzania itakavyoumia kwa kujiunga na OIC.

Kujaza kurasa kwa kulinganisha OIC na Vatican hakusaidii chochote na, to my view, beyond the scope of the motion. Wana JF tupeni madhara ya Tz kujiunga na OIC, vinginevyo madai ya Membe hayana mjadala.

Binafsi nimeshindwa kuja na angalau hasara moja ya Tz kujiunga na OIC, na nategemea kuelimishwa/eleweshwa kupita JF.

Faida ya/ za kujiunga ni zipi?
 
faida za kujiunga na OIC:

a. Tutapata misaada
b. Jamii ya Waislamu wataridhika kuhusiana na chombo cha Kiislamu na hivyo itakuwa rahisi kupata misaada.
c. Tutakuwa tumejiunga na nchi nyingine ambazo nazo ni wanachama wa OIC na hivyo kuwa karibu katika kusaidiana na wanachama wenzetu.
d. OIC itasaidia kujenga vyuo kama kile cha Uganda
e. OIC kwa vile ina nchi nyingi zinazozalisha mafuta itatusaidia kupunguza bei ya mafuta na hilo litawanufaisha watu wote siyo waislamu tu.
f. Itatatusaidia kuchukua msimamo wa pamoja katika masuala ya kimataifa hasa katika kutetea haki za Wapalestina ili wawe na nchi yao ambapo Al Quds al Sharrif (Yerusalemu) ni makao makuu.
g. Itatusaidia kushiriki katika kulinda maslahi ya jamii ya Kiislamu popote duniani.
h. Itatusaida kuwa katika mchakato mzuri wa hatimaye kuwa sehemu ya Soko la Uchumi la Nchi za Kiislamu ambapo hatimaye tutakuwa katika Jumuiya ya Uchumi wa Nchi za Kiislamu. Hili litakuwa na faida kubwa sana za kiuchumi kama masuala ya kodi, kusafirisha bidhaa, mikopo isiyo na riba n.k


Kuna niliyosahau?

i.
 
Mwanakijiji,
Mkuu bado umo katika kabati la udini kwa hiyo hizosababu zako za utunzi kama unavyotunga ngonjera haziwezi kubadilisha ukweli kwamba OIC ni chombo cha kiislaam kilichokubalika na UN hivyo kinashirikiana moja kwa moja na UN ( katibu mkuu) ktk maswala mengi ya kijamii kama zilivyo vyombo vingine vya UN ambavyo pia tumejiunga..

Kilichobakia kuleni wembe!
 
Mwanakijiji,
Mkuu bado umo katika kabati la udini kwa hiyo hizosababu zako za utunzi kama unavyotunga ngonjera haziwezi kubadilisha ukweli kwamba OIC ni chombo cha kiislaam kilichokubalika na UN hivyo kinashirikiana moja kwa moja na UN ( katibu mkuu) ktk maswala mengi ya kijamii kama zilivyo vyombo vingine vya UN ambavyo pia tumejiunga..

Kilichobakia kuleni wembe!


hahahahah.. kati ya faida nilizoziweka hapo juu ipi si ya kweli, nimeitunga, na haina msingi? Nitafurahi ukinikosoa badala ya kunichagulia kabati.
 
Mwanakijiji,
ZOTE!...
Hivi nikuulize wewe kitu kimoja kidogo sana... Zile nchi 12 zilizotokana na watoto wa Yakubu (Jacob), unazifahamu (unazikumbuka) majina yake?....
 
Back
Top Bottom