Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Rev. Kishoka,
mkuu soma tena maeleoz yangu niliyomwandikia Kichuguuu...Utaelewa zaidi..

Kichuguu,
Shukran mkuu kwa kuuliza swali ambalo nadhani sijaligusia vizuri pamoja na kwamba umeshalipatia jibu...
Unajua mkuu kujiunga na jumuiya ya nchi za kiislaam sio kama mnavyofikiria kuwa hizi ni NCHI za KIISLAAM - Quote n Quote - bali ni nchi zenye UMMAH wa kiislaam kwa kiswahili nadhani ina maana ya UMATI wa kiislaam...Misingi yake haihusiani na utawala wa nchi hiyo upo ktk mfumo gani, haina maana kabisa kwamba nchi hizi ni za kiislaam kiutawala kwani ukweli ni kwamba
1. NCHI za KIISLAAM kwa maana ya kiutawala nadhani hazifiki hata 10..
2.Kuna nchi zilizotambua Uislaam kama ndio dini yake yaani state religion na nyingine
3. Ni secular states, ambazo zote (1,2 na 3) kwa jumla yake sidhani kama zinafika 40 dunia nzima.
Hizi zote zimetokana na Utawala uliopo na pengine ndio culture yao tofauti na sisi Tanzania.
Kama Marekani leo hii unapozungumzia culture ya nchi hiyo Ukristu ni lazima usimamiwe na kiongozi yeyote na hupimwa jinsi gani ameshika values na integrity...

Lakini ukirudi ktk mada hii husika utaona kwamba OIC ina wanachama zaidi ya 50, 57 to be exact kiasi kwamba hapa hapa Africa kuna nchi zaidi ya 10 ambazo hazina sheria wala katiba inayohusiana na Uislaam. kuna nchi wanachama kama Mauritania, Benin, Cameroon, Ivory Coast, Gabon, Uganda, Mozambique, Sierra Leone, Togo ambazo hazipo kabisa kuendesha nchi zao kwa misingi ya kidini iwe kuitwa nchi ya kiislaam, ama islaam kuwa dini ya nchi zao wala hazipo ktk mfumo wa secular states lakini nchi hizi ni wanachama wa OIC. Wakuu hatupo peke yetu ndani ya OIC kama nchi zinazoheshimu haki ya wananchi wake kuchagua na kuabudu dini waitakayo.

Zaidi ya hapo nchi hizi hazikujiunga jana wala juzi kiasi kwamba tusiweze kuwa na mifano hai kuonyesha malengo mabaya ya OIC kuhusiana na tuhuma ama mbegu mbaya mnazojaribu kupandikiza..Sisi Tanzania tuna tofauti gani kubwa na nchi hizo tena basi yawezekana nchi hizo zina waislaam wengi kuliko hata sisi iweje OIC wasianze na huko?..
Maamuzi ya kubadilisha nchi iwe ya kiislaam sio swala dogo wala la kufanyika mzaha kwa sababu ni lazima kushirikishwa wananchi. Ukiondoa nchi za kiarabu utaona kwamba nchi nyingi sana zimefikia hata Uamuzi wa Islaam kuwa state religion umefikiwa baada ya kupigwa kura ama chama kilichoshinda kilitumia sera za kidini na zikakubalika na wananchi wake... Tanzania hatujafikia usingizi mzito kiasi hicho na kifupi haiwezekani!

Labda kwa kusherehesha zaidi kiarabu ktk matumizi ya neno hili Nchi za kiislaam ni pmaoja na usemi unaozingatia sio nchi as nchi mnavyoichukulia bali WATU yaani UMMAH yaani kwa kiswahili tunasema UMATI ambao unaheshimu utawala uliopo madarakani, pia tofauti zetu na watu wengine lakini bado tunakumbushwa kuwa na mshikamano. OIC ni chombo ambacho kinajaribu kuyatazama mahitaji ya watu wake kwa kupitia serikali kuu na binafsi nadhani hii ni muhimu zaidi kuliko kupitia vyombo kama Bakwata ambavyo kwa tamaa ya fedha wanaweza kabisa kukaribisha magaidi au kuingiza siasa ktk misaada hiyo iwe ya fedha ama mali.

Kiusalama (National security) nilishasema kuwa ni bora kabisa swala lolote linalohusiana na misaada ya kidini hasa Waislaam kupitia serikali kuu kutokana na kuepuka viongozi wa dini kuwa wapambe wa mission kama hizi kwani hawa pia ni rahisi kutazama kila kitu wakiwa ndani ya sanduku la udini.. Hivyo OIC pamoja na kwamba imeanzishwa na waarabu hao kina Sultan wa Saudia ambaye mwenyewe na familia yake hawana Uislaam hata kidogo zaidi ya jina kubwa, hawa ni viongozi wa kisiasa (Sultan) na bahati nzuri wana ushirikiano mzuri na nchi za magharibi pia OIC ni chombo pekee cha waislaam UN, hivyo sidhani kama wanaweza kuingia na agenda nje ya yale wanayotaka kuyafanya. Hawa ni Lobbiest tu wanaotumia jina la dini kuonyesha fadhila zao na kwa sababu sisi wahitaji sioni ubaya wake as long as we control the floor!
Kama OIC ingekuwa imehusika kwa kiwango fulani cha matatizo ya nchi wanachama, ama imehusishwa na UDINI basi bila shaka hoja hii ingepata uzito wa kuendeleza discussion hii lakini hoja zote zilizomo humu zinapikwa na kugeuzwa geuzwa ili mradi zionekane zina mvuto bila ushahidi wa matukio.
Mkuu kwa kumalizia tu ni kwamba kwa nini lakini mnakuwa hamna imani na Uislaam kama dini kuna kitu gani kimewahi kutokea kwenu kiasi kwamba mnachofikiria kwanza ni kuwa Tanzania inataka kubadilishwa kuwa Nchi ya kiislaam...
I mean kuna ishara zipi mnazoziona ambazo mimi sizioni..
 
Mkandara,

Kama mimi si muumini wa dini ya Kiislamu katika nchi ambayo si ya Kiislamu, kwa nini nikubali Serikali ya nchi yangu ikiunge na jumuiya ambayo sharti la kwanza ni nchi mwanachama lazima iwe nchi ya kiislamu?
 
Rev.Kishoka,
Mkandara,

Kama mimi si muumini wa dini ya Kiislamu katika nchi ambayo si ya Kiislamu, kwa nini nikubali Serikali ya nchi yangu ikiunge na jumuiya ambayo sharti la kwanza ni nchi mwanachama lazima iwe nchi ya kiislamu?
Kwa sababu mhitaji ni ndugu yako Muislaam...na nimekwambia nini maana ya nchi ya kiiislaam, wewe huna haja kabisa ya kujihusisha na lolote ikiwa hupendi ni sawa na chukulia kuna msiba ama harusi... ingia msikitini, jumuika na waislaam ndugu zako kwenye furaha ama msiba kwa sababu anayeoa ama kufiwa ni rafiki na ndugu yako.. Waache wafanye ibada zao kwa lugha zao na kadhalika lakini kuwa nao ktk furaha au maombolezi kwa sababu ni ndugu zako sio swala la sikufiwa mimi...
Huo ndio undugu ama niseme urafiki lakini unapokataa kuingia msikitini kwa kujitazama wewe dini yako kama sababu mkuu wangu HUKUTAKA kuhudhuria harusi ama mazishi na wala huyo jamaa sio ndugu wala rafiki yako - huo undugu ni wa kinafiki...

Mkuu sisi maisha yetu miaka yote 24/7 tunakutana na Ukristu, mashuleni, hospital, Mahotelini, mahakamani, kote utakuta kama sio Biblia kuna sanamu la Yesu msalabani..Tena ni sheria kuwa na hivyo vitu hadi Magereza, ni maisha ambayo mnayaogopa wakati sisi waislaam na watu wa imani nyingine tunaona poa tu na tunajiunga na vyombo hivi ndani ya Community zetu na tunapokea hizo glass ya wine iwe maharusini au msibani..Hata siku moja hatujafikiria kwamba nia yenu ni kutaka kutubadilisha imani zetu za dini, kwa sababu we have the last say!...

Mkuu wenye Uhuru wa kuamini na kuabudu ni WATU , watu ndio wanatakiwa kuwa na uhuru huo kuchagua dini waitakayo na wakafanya ibada zao bila kuingiliwa na serikali... Waislaam miaka yote hawana uhuru huo na wanalazimishwa kufuata mengi ya Ukristu watake wasitake..nini mnazungumzia kulazimishwa as if ktk maisha yenu mmekwisha experience kulazimishwa!..

Well, Unajua nini mkuu wangu, mada hii imenisaidia sana kuona jinsi sisi Watanzania tunavyoshindwa ktk mambo mengi ya kijamiii hasa ktk kusimamisha UMOJA wetu. Hizi Tabaka za kidini, za roho ya kikorosho kufikiria KWA NINI?... What about me! hata kama umezaja friji vyakula, ulafi, Umaskini, Njaa na imani ya kitumwa ni vitu ambavyo naanza kuamini kwamba kamwe hatuwezi kufanikisha kitu. Yawezekana hata Mafisadi ni roho ya kwa nini, tunakuwa informed wrong makusudi na watu wenye roho za kwa nini!....

Na naanza kuamini hizi jitihada za kisiasa nchini haziwezi kufika popote na pengine nitaanza kuitazama upya nafasi yangu ktk Utawala uliopo kwani yawezekana kabisa kuwa hizi mbinu za kumchafua Kikwete jina lake kwa sababu tu ni Muislaam.i...Kuna uwezekano ambao binafsi sikuwahi kuutazama lakini sasa (coming out of the box) naanza kuamini kuna kitu zaidi ya utawala mbaya...sababu KIKWETE ni Muislaam, and they want him out!.
 
ahhh nshachoka kusoma threads zisizo na kichwa wala miguu...hii imekaa vizuri sana hii...ngoja niisome tokea mwanzo kisha nipick watu wa kujadiliana nao ...lakini nasema mapema kuwa tutaendaweee na mwishowe wale walimeza BLUE PILL najua watasema aidha ihamishwe aau ifutwe au wataomba tufungiwe kama kwenye ile ya ya Dr MASAU
 
Na naanza kuamini hizi jitihada za kisiasa nchini haziwezi kufika popote na pengine nitaanza kuitazama upya nafasi yangu ktk Utawala uliopo kwani yawezekana kabisa kuwa hizi mbinu za kumchafua Kikwete jina lake kwa sababu tu ni Muislaam.i...Kuna uwezekano ambao binafsi sikuwahi kuutazama lakini sasa (coming out of the box) naanza kuamini kuna kitu zaidi ya utawala mbaya...sababu KIKWETE ni Muislaam, and they want him out!.



Mkandara ,

Sasa naona huu mjadala unaelekea pabaya na kwa kiasi fulani naona unataka kuingiza

udini . Watu hawamcriiticize Kikwete kwa sababu ya dini yake pale kwa kushindwa kuitetea

katiba yetu ya Jamhuri ya muungano . Je Mkapa nayetutasema kwa sababu alikuwa mkristo

ndio maana watu walimpinga ?
 
Rufiji,

Je Mkapa nayetutasema kwa sababu alikuwa mkristo
ndio maana watu walimpinga ?
Mkuu Yawezekana kabisa.. mimi sikuwahi kuona hivyo ila sasa naanza kuamini kwamba hoja nyingi humu ndani zinategemea na mtu/watu wanaozungumziwa, sio issue yenyewe na faida ama madhara yake..hata kama ina faida then ni kwa kina nani?..dini gani, kabila gani na mengineyo mengi tu. Yawezekana kabisa kuwa Mkapa kasemwa kwa mazuri na mabaya yake, akitangulizwa kuwa ni mkristu kwanza...binafsi sikuona hivyo kwa sababu muda wote nilikuwa nje ya box hilo la udini lakini yawezekana kabisa all along - dini imekuwa mbele ya hoja za watu.

Mkuu inachosha, mimi nipo ktk jumuiya zetu za Watanzania na nimeyaona mengi yenye sura kama hii na huwa nashindwa kabisa kuelewa isipokuwa inabidi nikubali hali halisi. Ni tatizo ambalo kila Mtanzania analizungmzia iwe US, UK Japan U name it sisi Watanzania tunajenga Uadui baina yetu pasipo sababu kabisa.
Hatuna mapenzi ya nchi wala ndugu zetu hata kidogo isipokuwa nafsi zetu sisi wenyewe. Maskini kwa njaa zao wana roho mbaya, matajiri kwa ulafi wao wana roho mbaya yaani - NDIVYO TULIVYO......
 
Bro Mkandara,

Marekani, Canada, India, China, Pakistani zimetupa misaada bila kuweka masharti ya Udini. Zimetupa misaada huku inajulikana wazi kuwa kuna umasikini katika nchi zao.

Nilichokiletea hoja ni kile cha kusema kuwa OIC inajali maslahi ya Waislamu wa Nchi za Kiislamu na kutaka kuyafanya yawe bora. Ndiyo maana nikauliza, hizo nchi tajiri za Kiislamu, zimefanya nini kuondoa Umasikini na Unyonge kwa jamii zao katika nchi zao kabla ya kukimbilia kusajili nchi za kiafrika na kusema kuwa ni kwa kutumia Udini pekee ndipo maslahi ya Waislamu kushinda Unyonge na Umasikini kutakuwa na mafanikio kwa kujiunga kwenye umoja huu?

Mada hii inahusu OIC na Uislamu, si Marekani, China, Canada, India au UK.

Kama mada ingekuwa inazungumzia kwa nini Tanzania iwe mwanachama wa UN, AU, Commonwealth, WB,IMF, Non-Allign, Comesa na kuhoji mshikamano wa kiuchumi na vita dhidi ya Umasikini na Unyonge, nako ningehoji kama ninavyohoji peremende ya Ubepari na Demokrasia tunayolishwa na Marekani huku kwao kwenyewe kuna Umasikini, Unyonge na Ubaguzi!

Unajua hii thread inaonyesha rangi za watu mbali mbali na hasa kwenye suala la Unidini na Uislam na waislam in partucular


Kila kukicha unatuletea think pieces na kusema kweli nakala zako zinaonyesha upeo wako ulivyo mrefu lakini si mpana kwenye kuchangania hili la SAKATA YA TANZANIA KUJIUNGA NA OIC tangu miaka ya 1990's


kKwa taarifa yako MCHUNGAJI KISHOKA msimamo wa awali wa serikali wa kukataa kujiunga na jumuiya ya waislamu ya OIC ikidai kuzingatia maoni na hisia za Wakristo wakati ambapo hapa Tanzania upo Ubalozi wa Vatican ambao haunza zaidi ya kusimamia maslahi ya kanisa katoliki na wafuasi wake.


Labda ningekushauri MCHNGAJI KISHOKA ungepitia tuu baadhi ya maandiko Vatican, ikishajichimbia katika nchi huingia mkataba wa upendeleo na serikali unaoitwa Concordats.


Kama ulikuwa hujui basi kwa taarifa yako Concordats ni makubaliano ya kisiasa kati ya Vatican na nchi zilizo na Balozi ambapo ukatoliki hupewa nafasi pekee ya upendeleo katika nchi.


Katika kitabu kuhusu Vatican kinachoitwa Church, State and Diplomacy kwenye ukurasa wa 279 mwandishi Paul Blanshard ameandika kuwa kanisa katoliki huingia mkataba huo na serikali halafu huwa mstari wa mbele kueneza sera za serikali kutenganishwa na dini.


Nakushauri uende ukafanye kusoma library andaa hoja zako kwa makini kabla ya kuja na hoja ambazo tunakawaida ya kuzisoma kwa lightweights wa JF .You can do better than this
 
Na naanza kuamini hizi jitihada za kisiasa nchini haziwezi kufika popote na pengine nitaanza kuitazama upya nafasi yangu ktk Utawala uliopo kwani yawezekana kabisa kuwa hizi mbinu za kumchafua Kikwete jina lake kwa sababu tu ni Muislaam.i...Kuna uwezekano ambao binafsi sikuwahi kuutazama lakini sasa (coming out of the box) naanza kuamini kuna kitu zaidi ya utawala mbaya...sababu KIKWETE ni Muislaam, and they want him out!

Pole SANA Mkandara, it took u so long kuwajua hawa. Mie nilishawajua dhamira zao kitambo.

Ndio ukubwa huo, "kua nawe uyaone oooo" ( Zahir Ally - Zoro )
 
Ihamishwe🙂


Kitila ,


Hata siku moja hatuwezi kusolve matatizo yetu by sweeping them under the rug, tumeshaona madhara yake kwenye suala la Zanzibar kwani Nyerere alifikiri ataweza kusolve matatizo kwa kuwazuia watu kusema . Hii sio hoja ya dini ya dini hata kidogo bali ni hoja ya siasa .

Game Theory , nakubalina na wewe asilimia mia moja kwamba kama kuna wtu wanaona sio sahihi kwa Tanzania kujiunga na OIC basi vile vile ni lazima watu hao pia waone sio sahihi kwa Tanzania kuwa na ubalozi vatican . Mimi naona kusudi tuishi kwa amani na upendo lazima tukubali ku- compromise basi tukubali tujiunge na hiyo OIC .

Kwa upande mwingine kitu kinachoniumiza kichwa na hii mentality ya kufikiri ya kuwa ili tuendelee ni lazima tupate misaada . Hii ni moja ya mentality mbaya sana mabayo itatufanya tuendelee kuwa slaves katika nchi yetu.
 
Mkandara na Mtalii mumeenda mbali mno mpka mnapotea sasa! mh huku ndo kutetea hoja yenu ya kutaka kujiunga na OIC? Kwa upande mwingine inadhihirisha ubaya wa maamuzi tata kama haya ya PIC na mahakama ya kadhi. Kama Mkuu wangu Mkandara na Mtalii mmeshaathiriwa na hizo hoja na kuingia kwenye udini sasa wananchi wa kawaida wenye elimu ndogo kabisa wenye uzoefu mdogo kabisa katika masuala ya kitaifa itakuwaje?

come on Mkandara, hivi Lowasa, Mkapa ni dini gani? mbona wanapigiwa kelele sana!
 
Mkandara na Mtalii mumeenda mbali mno mpka mnapotea sasa! mh huku ndo kutetea hoja yenu ya kutaka kujiunga na OIC? Kwa upande mwingine inadhihirisha ubaya wa maamuzi tata kama haya ya PIC na mahakama ya kadhi. Kama Mkuu wangu Mkandara na Mtalii mmeshaathiriwa na hizo hoja na kuingia kwenye udini sasa wananchi wa kawaida wenye elimu ndogo kabisa wenye uzoefu mdogo kabisa katika masuala ya kitaifa itakuwaje?

come on Mkandara, hivi Lowasa, Mkapa ni dini gani? mbona wanapigiwa kelele sana!


kwani wewe ulikua hujui Lowasa,Mkapa,Mramba,Balali,Chenge,Yona,Kalamangi wote ni waiislamu ,tangia leo on uelewe hivyo.
kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi
 
U

Labda ningekushauri MCHNGAJI KISHOKA ungepitia tuu baadhi ya maandiko Vatican, ikishajichimbia katika nchi huingia mkataba wa upendeleo na serikali unaoitwa Concordats.

ama ulikuwa hujui basi kwa taarifa yako Concordats ni makubaliano ya kisiasa kati ya Vatican na nchi zilizo na Balozi ambapo ukatoliki hupewa nafasi pekee ya upendeleo katika nchi.

Katika kitabu kuhusu Vatican kinachoitwa Church, State and Diplomacy kwenye ukurasa wa 279 mwandishi Paul Blanshard ameandika kuwa kanisa katoliki huingia mkataba huo na serikali halafu huwa mstari wa mbele kueneza sera za serikali kutenganishwa na dini.


Nakushauri uende ukafanye kusoma library andaa hoja zako kwa makini kabla ya kuja na hoja ambazo tunakawaida ya kuzisoma kwa lightweights wa JF .You can do better than this


Sisi watanzania watu wa ajabu sana. Uhusiano wetu wa kibalozi hauna maana kwamba ni lazima tuwe tunafanana na nchi hizo kwa mambo yao ya ndani. Vatican ni nchi ndiyo ina balozi hata Iran ambaye toka mwaka jana 2007 alikuwa Archbishop Jean-Paul Aimé Gobel. Vile vile Iran ina mwakilishi wake Vatican. Nakupeni hiyo mfano kuonyesha kwamba Vatican pamoja na kuwa ni makao makuu ya wakatoliki haina uhusiano wa kibalozi na nchi za kikatoliki tu ina uhusiano na nchi zote ambazo pia zinapenda kuwa na uhusiano. Iran kama nchi ya kiislamu na wengine wanaiona kama Vatican ya Mashia inashirikiana na kibalozi na Vatican ambayo ni makao makuu ya wakatoliki. Hivyo kulihusisha suala la Vatican aidha ni kutojua uhusiano wa kimataifa au pia kukataa uungwana wa kibinadamu kwamba mtu mnayeshirikiana naye siyo lazima awe kama wewe cha msingi awe anakukubali wewe ulivyo na ana uheshimu uhusiano wenu. Hivyo ushauri wangu ni kwamba serikali haitakiwi kuburuza watu kwenye masuala kama haya, kama kuna umuhimu wa kujiunga basi katiba iangaliwe na serikali iweke utaratibu wa kujiunga mashirika yote ambayo yana maslahi ya kidini au kihali kwa watanzania. Na huu ni mjadala ambao ni wawatanzania wote maana unahusu serikali yao.
 
[/COLOR][/I]

Sisi watanzania watu wa ajabu sana. Uhusiano wetu wa kibalozi hauna maana kwamba ni lazima tuwe tunafanana na nchi hizo kwa mambo yao ya ndani. Vatican ni nchi ndiyo ina balozi hata Iran ambaye toka mwaka jana 2007 alikuwa Archbishop Jean-Paul Aimé Gobel. Vile vile Iran ina mwakilishi wake Vatican. Nakupeni hiyo mfano kuonyesha kwamba Vatican pamoja na kuwa ni makao makuu ya wakatoliki haina uhusiano wa kibalozi na nchi za kikatoliki tu ina uhusiano na nchi zote ambazo pia zinapenda kuwa na uhusiano. Iran kama nchi ya kiislamu na wengine wanaiona kama Vatican ya Mashia inashirikiana na kibalozi na Vatican ambayo ni makao makuu ya wakatoliki. Hivyo kulihusisha suala la Vatican aidha ni kutojua uhusiano wa kimataifa au pia kukataa uungwana wa kibinadamu kwamba mtu mnayeshirikiana naye siyo lazima awe kama wewe cha msingi awe anakukubali wewe ulivyo na ana uheshimu uhusiano wenu. Hivyo ushauri wangu ni kwamba serikali haitakiwi kuburuza watu kwenye masuala kama haya, kama kuna umuhimu wa kujiunga basi katiba iangaliwe na serikali iweke utaratibu wa kujiunga mashirika yote ambayo yana maslahi ya kidini au kihali kwa watanzania. Na huu ni mjadala ambao ni wawatanzania wote maana unahusu serikali yao.

Na kikubwa zaidi
Watanzania ili tufanye jambo lazima kwanza jirani awe ameshakwisha lifanya na kwa uchanganuzi wetu ni lazima tufananishe jinsi jirani alivyofanya na kwa kujenga hoja lazima tufananishe vitu visivyofananika.

Tutaendelea kubaki nyuma maana sisi mawazo yetu hayawezi kua in first place na hatuwezi na jinsi tulivyo wadhaifu hatuwezi jenga hoja zetu wenyewe na kuzama ndani kutia mchanganuo yakinifu.

Utasikia tumekwenda Zambia kupata utaalamu wa kilimo wakati SUA ipo ama tumekwenda norway kupata utaalamu jinsi ya kuiingia mikataba,utasikia tumekwenda ghana kupata uzoefu jinsi ya kunufaika na madini ama utasikia tumekwenda rwanda kujifunza jinsi walivyofanikiwa ktk IT wakati watalaam wa IT rwanda ni watanzania.
Ama utasikia tumekwenda Kenya kujifunza jinsi KADHI ilivyofanikiwa ama tumekwenda Uganda ,somalia,afrika ya kati kujifunza jinsi tutakavyoingia OIC.

Mimi ningependa kuiuliza serikali yetu INATUSOMESHA SISI WATANZANIA ili ije kutu underate sio?
Mimi hapa kuna jamaa kila siku ananizomea kwa kuniambia nchi yenu yani haina hata wataalamu wa KUSOMA MIKATABA na kuielewa??kila siku huyu jamaa ananisonosha kwa hilo kila tukikutana.

HIVI sisi watanzania tutakua lini huru wa KIMAWAZO na FIKRA???
 
Issue hapa siyo OIC wala KAdhi bali issue hapa ni feelings walizonazo waislam ambao wanayo SIEGE MENTALITY kuwa wanaoneka wa kila kitu kinachoendelea Tanzania. Yaani wanaonewa na SERIKALI plus CCM na tawi lao la BAKWATA

sasa kama mnataka kwanza kubalini kuwa OIC na ZANZIBAR KUWA NCHI na hoja za Kadhi ni end product ya dharau ya serikali ya CCM kuchelea kukubali kama kuna tatizo

sasa nikupe mfano mdogo tuuu...nakumbuka katika mjadala huuu kuna watu siku za nyuma walishwahi kuuliza mbona BAKWATA hawajatoa tamko? Ukweli ni kuwa ndani ya JF tuna watu wanapiga porojo bila kuangalia facts on the ground ni zipi. Mfano ni BAKWATA na Waislamu.


Kwa taarifa yenu BAKWATA haina heshima ndani ya jamii za waislam Tanzania hivyo kutegemea eti watoe tamko lenye hoja za kueleweka ni kichekesho na msidhangae kusikia kuwa tamko linaandaliwa Mtaa wa Lumumba kisha linapelekwa Kindoni ili litolewe

In short BAKWATA iliasisiwa kwa shinikizo la serikali mwaka 1968 baada ya kuivunja jumuiya ya East African Muslim Welfare Society iliyoundwa na Waislamu wenyewe kwa ridhaa yao. Jumuiya hiyo ilikuwa na mali, majumba, shule na Misikiti.


Vyote vikaporwa na kukabidhiwa BAKWATA. Waislamu walizipinga hatua hizo na ndiyo maana hadi leo BAKWATA haina ridhaa ya Waislamu ila wachache tu wanaolindwa na katiba ya kidikteta iliyompa mamlaka makubwa Mufti wao. Lakini pamoja na uchache wao, BAKWATA hao hao bado hawaelewani hata juzi mmeona yule shee mkuu wao alipotoka India alifanya nini


Waislamu wengi TZ wameamua kujiendeshea mambo yao kupitia jumuiya zao mbalimbali hawana haja na BAKWATA na BAKWATA wenyewe wanajua! Kwa ushahidi mzuri, BAKWATA inashindwa hata kupata pesa kwa Waislamu za kuitisha mkutano wao mkuu kiasi cha kuchangiwa na Makanisa kama ilivyokuwa mwaka 1994.

Lakini baya zaidi, watendaji wako wanadhani wanayo haki ya kuwalazimisha Waislamu kuwa chini ya BAKWATA. Sasa kutoa hoja eti OIC ilikuwa ni kuwaridhisha waislam ni kiini macho tuuu kwani ukweli unajulikana kuwa akina POLICARP PENGO walikuwa mstari wa mbele kupinga hilo lisitokee na ilifika point nakumbuka walitu walikuwa wanajiuliza kwa nini asichukue form za kugombea ubunge CCM ili ijulikane moja tuu
 
kwani wewe ulikua hujui Lowasa,Mkapa,Mramba,Balali,Chenge,Yona,Kalamangi wote ni waiislamu ,tangia leo on uelewe hivyo.
kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi

umenivunja mbavu Mkuu, eehh hhee!!!
 
Issue hapa siyo OIC wala KAdhi bali issue hapa ni feelings walizonazo waislam ambao wanayo SIEGE MENTALITY kuwa wanaoneka wa kila kitu kinachoendelea Tanzania. Yaani wanaonewa na SERIKALI plus CCM na tawi lao la BAKWATA

sasa kama mnataka kwanza kubalini kuwa OIC na ZANZIBAR KUWA NCHI na hoja za Kadhi ni end product ya dharau ya serikali ya CCM kuchelea kukubali kama kuna tatizo

sasa nikupe mfano mdogo tuuu...nakumbuka katika mjadala huuu kuna watu siku za nyuma walishwahi kuuliza mbona BAKWATA hawajatoa tamko? Ukweli ni kuwa ndani ya JF tuna watu wanapiga porojo bila kuangalia facts on the ground ni zipi. Mfano ni BAKWATA na Waislamu.


Kwa taarifa yenu BAKWATA haina heshima ndani ya jamii za waislam Tanzania hivyo kutegemea eti watoe tamko lenye hoja za kueleweka ni kichekesho na msidhangae kusikia kuwa tamko linaandaliwa Mtaa wa Lumumba kisha linapelekwa Kindoni ili litolewe

In short BAKWATA iliasisiwa kwa shinikizo la serikali mwaka 1968 baada ya kuivunja jumuiya ya East African Muslim Welfare Society iliyoundwa na Waislamu wenyewe kwa ridhaa yao. Jumuiya hiyo ilikuwa na mali, majumba, shule na Misikiti.


Vyote vikaporwa na kukabidhiwa BAKWATA. Waislamu walizipinga hatua hizo na ndiyo maana hadi leo BAKWATA haina ridhaa ya Waislamu ila wachache tu wanaolindwa na katiba ya kidikteta iliyompa mamlaka makubwa Mufti wao. Lakini pamoja na uchache wao, BAKWATA hao hao bado hawaelewani hata juzi mmeona yule shee mkuu wao alipotoka India alifanya nini


Waislamu wengi TZ wameamua kujiendeshea mambo yao kupitia jumuiya zao mbalimbali hawana haja na BAKWATA na BAKWATA wenyewe wanajua! Kwa ushahidi mzuri, BAKWATA inashindwa hata kupata pesa kwa Waislamu za kuitisha mkutano wao mkuu kiasi cha kuchangiwa na Makanisa kama ilivyokuwa mwaka 1994.

Lakini baya zaidi, watendaji wako wanadhani wanayo haki ya kuwalazimisha Waislamu kuwa chini ya BAKWATA. Sasa kutoa hoja eti OIC ilikuwa ni kuwaridhisha waislam ni kiini macho tuuu kwani ukweli unajulikana kuwa akina POLICARP PENGO walikuwa mstari wa mbele kupinga hilo lisitokee na ilifika point nakumbuka walitu walikuwa wanajiuliza kwa nini asichukue form za kugombea ubunge CCM ili ijulikane moja tuu

Mkuu
mimi naamini kuna ka kundi ndani ya uislamu kanakoendekeza mentality ya kuonewa. kwa ajili ya manufaa yao.

Kakundi hako ndiko kanapiga kelele duniani kote kwamba waislamu wanapigwa vita wakati waislamu wenyewe halisi wako bomba sana.

Kakundi hako ndiko kana tawi lake la kupiga propaganda kua BAKWATA ni ya CCM na ya kwamba waislamu wanaonewa.

Kakundi hako bado kanaenda mbali zaidi ndani ya waislamu wema kuteka misikiti yao na kusema wanaonewa waislamu ndani ya uislamu.

kakundi hako bado ndio hua kana tabia yakuanzisha mapinduzi ya uongonzi ndani ya misikiti ya waislamu kakiwa na hoja ya kulinda uislamu na maslahi ya waislamu ndani ya uislamu.

kakundi hako ndiko hua kanafanya vurumai na hatimaye ngumi kurushwa ndani ya misikiti kila mara kakiwa na sera zile zile kua waislamu wanaonewa ndani ya uislamu.

Hivyo hoja ya kuonewa mwislamu nje ya uislamu kwa kakundi haka si ya kushangaa maana kakundi haka ka kiislamu hua kanaonewa ndani ya waislamu sasa itakua je? nje.
 
Mkuu
mimi naamini kuna ka kundi ndani ya uislamu kanakoendekeza mentality ya kuonewa. kwa ajili ya manufaa yao.

Kakundi hako ndiko kanapiga kelele duniani kote kwamba waislamu wanapigwa vita wakati waislamu wenyewe halisi wako bomba sana.

Kakundi hako ndiko kana tawi lake la kupiga propaganda kua BAKWATA ni ya CCM na ya kwamba waislamu wanaonewa.

Kakundi hako bado kanaenda mbali zaidi ndani ya waislamu wema kuteka misikiti yao na kusema wanaonewa waislamu ndani ya uislamu.

kakundi hako bado ndio hua kana tabia yakuanzisha mapinduzi ya uongonzi ndani ya misikiti ya waislamu kakiwa na hoja ya kulinda uislamu na maslahi ya waislamu.

kakundi hako ndiko hua kanafanya vurumai na hatimaye ngumi kurushwa ndani ya misikiti kila mara kakiwa na sera zile zile kua waislamu wanaonewa ndani ya uislamu.

Hivyo hoja ya kuonewa mwislamu nje ya uislamu kwa kakundi haka si ya kushangaa maana kakundi haka ka kiislamu hua kanaonewa ndani ya waislamu sasa itakua je? nje.

nimekupata lakini kuna kipande hiki naona umekisahau:



In short BAKWATA iliasisiwa kwa shinikizo la serikali mwaka 1968 baada ya kuivunja jumuiya ya East African Muslim Welfare Society iliyoundwa na Waislamu wenyewe kwa ridhaa yao. Jumuiya hiyo ilikuwa na mali, majumba, shule na Misikiti.


Vyote vikaporwa na kukabidhiwa BAKWATA. Waislamu walizipinga hatua hizo na ndiyo maana hadi leo BAKWATA haina ridhaa ya Waislamu ila wachache tu wanaolindwa na katiba ya kidikteta iliyompa mamlaka makubwa Mufti wao. Lakini pamoja na uchache wao, BAKWATA hao hao bado hawaelewani hata juzi mmeona yule shee mkuu wao alipotoka India alifanya nini



Je unao ushahidi utakao onyesha tofauti na yaliyoandikwa hao juu?
 
Mkuu Game Theory! Mbona unaturudisha nyuma? Hayo ya EAMWS tulishayajadili kwa kirefu. Kwangu mimi ni kukataa kwa waislamu katakata kuona ushiriki wa waislamu wenzao katika kuua jumuia hii na kumtwika mzigo wote mkatoliki Julius. Mkatoliki huyo huyo aliyenyang'anya jumuia za dini yake mashule na mahospitali na kuyafanya ya umma. Waislamu hao hao wanaanza kudai kutotendewa haki na wakristu lakini wanasahau kuwa ni mkatoliki mwingine aitwae Ben aliyekabidhi Chuo cha shirika la umma ili kiwe cha kiislamu! Leo wanasema kabisa kuwa Bakwata haiwakilishi jumuia ya waislamu bila kutuambia ni nani anayewakilisha hiyo jamii. Hivi kweli wanataka kutuambia kuwa kuna uwezekano kweli wa kupatikana mwakilishi wa jamii yao ambaye atakubaliwa na wote? Leo wanadai tujiunge na OIC ili tupate misaada. Hivi hiyo misaada ikipatikana na kupitishwa serikalini wataacha kweli kuona mkono wa wamisheni katika kuipotosha? Tangu nikiwa shule ya msingi nimekuwa naona jiwe la msingi la Chuo Kikuu cha waislamu pale Chang'ombe. Leo waislamu hao hao wameshupaliana baada ya muislamu mwenzao kuelekea kuwazidi kete!

Hapa watu wanapinga sisi kujiunga na OIC kwa sabau inapingana na katiba yetu. badala ya kuonyesha namna gani ambavyo kujiunga huko hakutapingana na katiba yetu, wao wanatoa mifano wa nchi nyingine ambazo nina uhakika kuwa hawajui katiba zao zinasema nini. Badala ya kushindana na hoja wanakimbilia kudai kuwa hawapendwi kwa sababu wao ni waislamu! Mimi kama mmisheni naamini kwa dhati kabisa kuwa bila kutokea waislamu wenye uchungu wa dhati na wenzao na kuanza kuwaambia ukweli kuwa mchawi wao yuko miongoni mwao hata tukijiunga na OIC haitasaidia kitu!

Mimi mmisheni naamini kuwa kuna malalamiko mengi ya ndugu zetu ni ya msingi na sisi wamisheni kwa sababu hayatupati huwa hatuyaoni. Tatizo ni kuwa badala ya kukaa pamoja na kuangalia namna gani sisi kama jamii tunaweza kutatua tunakimbilia kunyosheana vidole. Hiyo haitajenga hata siku moja. Badala ya kuleta suala hili kama fait acompli, tungeambiana faida zake na kuangalia namna gani ya kurekebisha katiba yetu ( kama patakuwa na haja) ili ituruhusu kujiunga. Badala ya kujaribu kudanganya kuwa OIC si taasisi ya kidini, hii ingewekwa wazi. Natumaini tungefanya hivi tungeweza kujadili hii ishu kama watu wazima badala ya kujikuta tunamsikia kiongozi wa dini akipinga kujiunga kwetu na OIC halafu akakiri kuwa hata katiba yake haijui! Au mtu anatetea kujiunga nae hata katiba yake haijui. Tuvute pumzi kwanza. Hili suala linatuhusu sote.
 
Mkuu Game Theory! Mbona unaturudisha nyuma? Hayo ya EAMWS tulishayajadili kwa kirefu. Kwangu mimi ni kukataa kwa waislamu katakata kuona ushiriki wa waislamu wenzao katika kuua jumuia hii na kumtwika mzigo wote mkatoliki Julius. Mkatoliki huyo huyo aliyenyang'anya jumuia za dini yake mashule na mahospitali na kuyafanya ya umma. Waislamu hao hao wanaanza kudai kutotendewa haki na wakristu lakini wanasahau kuwa ni mkatoliki mwingine aitwae Ben aliyekabidhi Chuo cha shirika la umma ili kiwe cha kiislamu! Leo wanasema kabisa kuwa Bakwata haiwakilishi jumuia ya waislamu bila kutuambia ni nani anayewakilisha hiyo jamii. Hivi kweli wanataka kutuambia kuwa kuna uwezekano kweli wa kupatikana mwakilishi wa jamii yao ambaye atakubaliwa na wote? Leo wanadai tujiunge na OIC ili tupate misaada. Hivi hiyo misaada ikipatikana na kupitishwa serikalini wataacha kweli kuona mkono wa wamisheni katika kuipotosha? Tangu nikiwa shule ya msingi nimekuwa naona jiwe la msingi la Chuo Kikuu cha waislamu pale Chang'ombe. Leo waislamu hao hao wameshupaliana baada ya muislamu mwenzao kuelekea kuwazidi kete!

Hapa watu wanapinga sisi kujiunga na OIC kwa sabau inapingana na katiba yetu. badala ya kuonyesha namna gani ambavyo kujiunga huko hakutapingana na katiba yetu, wao wanatoa mifano wa nchi nyingine ambazo nina uhakika kuwa hawajui katiba zao zinasema nini. Badala ya kushindana na hoja wanakimbilia kudai kuwa hawapendwi kwa sababu wao ni waislamu! Mimi kama mmisheni naamini kwa dhati kabisa kuwa bila kutokea waislamu wenye uchungu wa dhati na wenzao na kuanza kuwaambia ukweli kuwa mchawi wao yuko miongoni mwao hata tukijiunga na OIC haitasaidia kitu!

Mimi mmisheni naamini kuwa kuna malalamiko mengi ya ndugu zetu ni ya msingi na sisi wamisheni kwa sababu hayatupati huwa hatuyaoni. Tatizo ni kuwa badala ya kukaa pamoja na kuangalia namna gani sisi kama jamii tunaweza kutatua tunakimbilia kunyosheana vidole. Hiyo haitajenga hata siku moja. Badala ya kuleta suala hili kama fait acompli, tungeambiana faida zake na kuangalia namna gani ya kurekebisha katiba yetu ( kama patakuwa na haja) ili ituruhusu kujiunga. Badala ya kujaribu kudanganya kuwa OIC si taasisi ya kidini, hii ingewekwa wazi. Natumaini tungefanya hivi tungeweza kujadili hii ishu kama watu wazima badala ya kujikuta tunamsikia kiongozi wa dini akipinga kujiunga kwetu na OIC halafu akakiri kuwa hata katiba yake haijui! Au mtu anatetea kujiunga nae hata katiba yake haijui. Tuvute pumzi kwanza. Hili suala linatuhusu sote.


Huwezi kuzungmzia OIC ila kuzungumzia feelings za waislam na jinsi wanalvychukulia huu mjadala mzima
 
Back
Top Bottom