Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Mkandara,

Mbona unazidi kudanganya umma kwa kuchanganya mambo? Vatican ni nchi, kama Iran au Saudi Arabia ambazo ni nchi za kiislamu na zinaongozwa na wakuu wa dini. Hili ni pamoja na dai lako wiki mbili zilizopita kuwa Mfalme wa Saudi si mkuu wa dini! Sasa kwa kuwa unataka kupotosha umma kwa kauli kuwa mbona Tanzania ina ubalozi Vatican, sasa nakujibu, tuna balozi Saudi Arabia lakini hatuna balozi kamili Vatican. Balozi wa Tanzania Ujerumani anatuwakilisha Vatican kama vile Balozi wa Tanzania Saudi Arabia anavyotuwakilisha Iran!

http://www.tanemb.se/index.php?option=com_content&task=view&id=37&Itemid=54

Sasa tuanze kuchambua hizi nchi tatu, Saudi Arabia, Iran na Vatican

Tuanze na Saudi Arabia

Custodian of the Two Holy Mosques (
Arabic: خادم الحرمين الشريفين Ḫādim al-Ḥaramain al-Sharīfain), a historical term, was a pious title taken by some Caliphs and now by modern Saudi kings.
The first Saudi king to assume the title was Fahd bin Abdul Aziz in 1986. The current king, Abdullah bin Abdul Aziz, has taken the same title after the death of King Fahd in 2005. King Fahd replaced the term "His Majesty" with "Custodian of the Two Holy Mosques" because it was said that only God is All Majestic, therefore the term "His Majesty [The King]" was replaced with this term.


Kuhusiana na Katiba ya Saudi Arabia


Chapter 1: General Principles

Article 1 states that "God's Book and the Sunnah of His Prophet" are the country's constitution and Arabic is the official language with the capital at Riyadh.

Chapter 2: Monarchy

Article 7 proclaims the rights of the monarch. Next, per Article 8, "justice, consultation, and equality" shall be in accordance with Shari'ah.

Chapter 3: Features of the Saudi Family

Article 9 states that all members of each family in Saudi Arabia shall be reared "on the basis of the Islamic faith."

Chapter 4: Economic Principles

Article 18 guard the private property of citizens.
Article 21 calls for an "alms tax".

Chapter 5: Rights and Duties

Article 27 establishes a "system of social security" that has made Saudi Arabia a welfare state. It is become feasible without expropriation and high taxes due to the large supplies of oil and a population of fewer than 30 million people.

Chapter 6: The Authorities of the State


Islam as cornerstone of governance

Article 45 affirm that religious rulings must be in accordance with the " Holy Qur'an and the Prophet's Sunnah." To this end, a panel of Islamic clergy and research group shall be established.
According to Article 55, the king has to "rule according to the rulings of Islam and shall supervise the application of Shari'ah." Article 56 states that the king is the prime minister as well. Article 57 makes it clear that the king's cabinet and other lower-ranking officials must follow Islam. Those who deviate from this can be dismissed or punished.


Tuje Iran, pamoja na kuwa wana Raisi, lakini mkuu wa nchi ni Ayatolla na hii ni tafsiri ya Ayatollah

Ayatollah (Persian: آيت*الله; Arabic: آية الله; English: Sign of God) is a high ranking title given to Usuli Twelver Shi'a clerics. Those who carry the title are experts in Islamic studies such as jurisprudence, ethics, and philosophy and usually teach in Islamic seminaries.[citation needed] The next lower clerical rank is Hojatoleslam wal-muslemin.


Supreme Leader

The post of Supreme Leader (Persian: رهبر انقلاب, Rahbare Enqelab,[1] lit. Leader of the Revolution, or مقام رهبری, Maghame Rahbari,[2] lit. Leadership Authority) was created in the constitution of the Islamic Republic of Iran as the highest ranking political and religious authority of the nation, in accordance with the concept of Guardianship of the Islamic Jurists.[3] The title "Supreme" Leader (Persian: رهبر معظم, Rahbare Moazzam), is often used as a sign of respect; however, this terminology does not exist in the constitution.
Currently the Supreme Leader of Iran is Ali Khamenei.


Election of Supreme Leader

Mandate and status
The Supreme Leader is elected by the Assembly of Experts, which is also in charge of overseeing the Supreme Leader, and has the power to dismiss and replace him at any time. As the name indicates, the Supreme Leader is considered as the ultimate head of the Iranian political and governmental establishment, above that of Iran's president. According to the constitution, he has the last say in internal and foreign policies, control of the Islamic Revolutionary Guard Corps, and control of state broadcast and others (see below).
The President of Iran, who is elected by the public vote, is the Executive President (Head of government). In 1989, the Prime Minister's office was merged with the figurehead President's office to form the current post of President of Iran. However, certain executive powers, such as commandment of the armed forces and declaration of war and peace, remain in the hands of the Supreme Leader.[4]


Wajibu wa Supreme Leader

Functions and duties of The Supreme Leader

  1. Delineation of the general policies of the Islamic Republic of Iran after consultation with the Nation's Expediency Discernment Council.
  2. Supervision over the proper execution of the general policies of the systems.
  3. Issuing decrees for national referendums.
  4. Assuming supreme command of the armed forces.
  5. Declaration of war and peace, and the mobilization of the armed forces.
  6. Appointment, dismissal, and acceptance of resignation of:
    1. the fuqaha' on the Guardian Council.
    2. the supreme judicial authority of the country.
    3. the head of the radio and television network of the Islamic Republic of Iran.
    4. the chief of the joint staff.
    5. the chief commander of the Army of the Guardians of the Islamic Revolution.
    6. the supreme commanders of the armed forces.
  7. Resolving differences between the three wings of the armed forces and regulation of their relations.
  8. Resolving the problems, which cannot be solved by conventional methods, through the Nation's Expediency Council.
  9. Signing the decree formalizing the elections in Iran for the President of the Republic by the people.
  10. Dismissal of the President of the Republic, with due regard for the interests of the country, after the Supreme Court holds him guilty of the violation of his constitutional duties, or after a vote of the Islamic Consultative Assembly (Parliament) testifying to his incompetence on the basis of Article 89 of the Constitution.
  11. Pardoning or reducing the sentences of convicts, within the framework of Islamic criteria, on a recommendation (to that effect) from the head of the Judiciary. The Leader may delegate part of his duties and powers to another person.
Politics of Iran

The politics and government of Iran takes place in the framework of a
republic with an Islamic ideology. The December 1979 constitution, and its 1989 amendment, define the political, economic, and social order of the Islamic Republic of Iran. It declares that Shi'a Islam of the Jaafari (Usuli) school of thought is Iran's official religion


Sasa tumalizie na Vatican au Holy See

While all
episcopal sees can be referred to as holy, the expression “the Holy See” (without further specification) is normally used in international relations (as well as in the canon law of the Catholic Church)[1] to refer to the central government of the Catholic Church, headed by the Bishop of Rome, commonly called the Pope. The Holy See should not be confused with the Vatican City State, which came into existence only in 1929, while the Holy See dates back to early Christian times. Ambassadors are officially accredited not to the Vatican City State but to "the Holy See", and papal representatives to states and international organizations are recognized as representing the Holy See, not the Vatican City State.


Inaendelea

The Pope governs the Catholic Church through the Roman Curia. The Roman Curia consists of a complex of offices that administer church affairs at the highest level, including the Secretariat of State, nine Congregations, three Tribunals, eleven Pontifical Councils, and seven Pontifical Commissions. The Secretariat of State, under the Cardinal Secretary of State, directs and coordinates the Curia. The current incumbent, Cardinal Tarcisio Bertone, is the See's equivalent of a prime minister. Archbishop Dominique Mamberti, Secretary of the Section for Relations with States of the Secretariat of State, acts as the Holy See's foreign minister. Bertone and Mamberti were named in their respective roles by Pope Benedict XVI in September 2006.
The Secretariat of State is the only body of the Curia that is situated within Vatican City. The others are in buildings in different parts of Rome that have extraterritorial rights similar to that of embassies.
Among the most active of the major Curial institutions are the Congregation for the Doctrine of the Faith, which oversees the Catholic Church's doctrine; the Congregation for Bishops, which coordinates the appointment of bishops worldwide; the Congregation for the Evangelization of Peoples, which oversees all missionary activities; and the Pontifical Council for Justice and Peace, which deals with international peace and social issues.
Three tribunals are responsible for judicial power. The Sacra Rota is responsible for normal appeals, including decrees of nullity for marriages, with the Apostolic Signatura being the administrative court of appeal and highest ecclesiastical court. The Apostolic Penitentiary is different from those two and, instead of dealing with contentious cases, issues absolutions, dispensations, and indulgences.
The Prefecture for the Economic Affairs of the Holy See coordinates the finances of the Holy See departments and supervises the administration of all offices, whatever be their degree of autonomy, that manage these finances. The most important of these is the Administration of the Patrimony of the Apostolic See.
The Prefecture of the Papal Household is responsible for the organization of the papal household, audiences, and ceremonies (apart from the strictly liturgical part).
The Holy See does not dissolve upon a Pope's death or resignation. It instead operates under a different set of laws sede vacante. During this interregnum, the heads of the dicasteries of the Roman Curia (such as the prefects of congregations) cease immediately to hold office, the only exceptions being the Major Penitentiary, who continues his important role regarding absolutions and dispensations, and the Cardinal Camerlengo, who administers the temporalities (i.e., properties and finances) of the See of St. Peter during this period. The government of the See, and therefore of the Catholic Church, then falls to the College of Cardinals. Canon law prohibits the College and the Camerlengo from introducing any innovations or novelties in the government of the Church during this period.


Kuhusu Vatican City/State
Vatican City [ˈvætɪkən ˈsɪti] (help·info), officially State of the Vatican City (Italian: Stato della Città del Vaticano), is a landlocked sovereign city-state whose territory consists of a walled enclave within the city of Rome. At approximately 44 hectares (110 acres), and with a population of around 800, it is the smallest independent state in the world by both population and area.[2][3][4]
Vatican City is a city-state. It came into existence only in 1929. It is thus clearly distinct from the central authority of the Roman Catholic Church, known as the Holy See, which existed long before 1929. Ordinances of Vatican City are published in Italian. Official documents of the Holy See are issued mainly in Latin. The two entities even have distinct passports: the Holy See, not being a country, only issues diplomatic and service passports; the state of Vatican City issues normal passports. In both cases the number of passports issued is extremely limited.


Kuhusu Pope
The Pope (from Latin: "papa" or "father" from Greek πάπας, pápas, "papa", Papa in Italian) is the Bishop of Rome, the leader of the Roman Catholic Church[1] and head of state of Vatican City. The current (265th) pope is Pope Benedict XVI, who was elected April 19, 2005 in papal conclave.
The office of the pope is called the Papacy; his ecclesiastical jurisdiction is called the "Holy See" (Sancta Sedes in Latin) or "Apostolic See" (the latter on the basis that both St. Peter and St. Paul were martyred at Rome).
In addition to his spiritual role, the pope is Head of State of the independent sovereign state of the Vatican City, a city-state entirely enclaved by the city of Rome. Before 1870, the pope's temporal authority extended over a large area of central Italy: the territory of the Papal States. The papacy retained sovereign authority over the Papal States until the Italian unification of 1870; a final political settlement with the Italian government was not reached until the Lateran Treaty of 1929.
For over a thousand years, popes played powerful roles in Western Europe, often struggling with monarchs for power over wide-ranging affairs of church and state,[2] crowning emperors (Charlemagne was the first emperor crowned by a pope) and regulating disputes among secular rulers.[3] The Bishop of Rome continued to be nominally allied with and part of the civil structure of the (Byzantine) Roman Empire until the 8th century, when the Donation of Pepin gave Rome and the surrounding area to the full sovereignty of the pope, over which the popes already had been de facto rulers, creating the Papal States that lasted until 1870. For centuries, the forged Donation of Constantine also provided the basis for the papacy's claim of political supremacy over the entire former Western Roman Empire.
Gradually forced to give up secular power, popes have come to focus again almost exclusively on spiritual matters.[2] Over the centuries, popes' claims of spiritual authority have been ever more clearly expressed since the first centuries, culminating in the proclamation of the dogma of papal infallibility for those rare occasions the pope speaks ex cathedra (literally "from the chair (of Peter)") when issuing a solemn definition of faith or morals.[2] The last such occasion was in the year 1950 with the definition of the dogma of the Assumption of Mary.


Sasa tukirudi kwenye OIC, OIC si nchi bali ni mkusanyiko wa nchi kama UN, AU au Commonwealth. Sasa kwa specific, OIC inasema ni jumuiya ya nchi za Kiislamu, swali kwako je Tanzania ni nchi ya Kiislamu kama ni nchi ya Kiislamu, tangu lini?

Usianze kupoteza watu bwana kwa hili la kuchanganya OIC na Vatican! Changanya Vatican na Saudi Aarabia au Iran, we will be on same page, lakini kusema OIC na Vatican are same huo ni uongo na upotoshaji mkubwa!
 
Hivi leo katika baraza kuu la OIC wakiamua na kusema hakuna dini nyingine duniani ila Islamu pekee na kutaka wanachama wake wahakikishe ni Islam pekee ndiyo inakuwa dini kwa kuwa Mtume kasema, je sisi ambao tunakimbilia kujiunga kama nchitutakuwaje huku tuna Wakristo, Wapagani na dini nyingine?

Je leo OIC wakikaza uzi na kusema hawalitamui Taifa la Israeli na kuanzisha vita dhidi ya Israeli huku Watanzania walio Wakristo na kama kuna waabudu wa Uzayuni wanataka Tanzania itambue Taifa la Israeli kwa kuwa imani yao inasema kuwa Israeli ndilo Taifa teule, jambo hili litaamuliwa vipi na Serikali ambayo imejiunga OIC kama nchi?

Akija Rais Mkristo mwenye msimamo tofauti na wa Kikwete na Membe akasema anafuata katiba ya nchi ya kutofungamana na dini na kuvunja na kuitoa Tanzania kama nchi, dola na Serikali yake katika uanachama wa OIC, je jambo hili litapokewaje?

Je labda akaja Rais Mkristo au Mpagani au yeyote ambaye si Muislamu, akafungua Ubalozi Tel Aviv na kuitambua Israeli kwa kuwa anashinikizwa na Wananchi wake ambao ni wafuasi wa Imani yake ambao wanadai kuwa Israeli ndilo Taifa la milele kama maandiko yao yanavyosema na kudai kuwa kuwa na mahusiano na Israeli kutawasaidia ndugu hawa Watanzania, jambo hili litapokewaje?

Ndiyo maana narudi kwenye kauli yangu ya awali, kwa nini Bakwata isijiunge na OIC na si kuishinikiza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujiunga OIC?

Maslahi ya nchi ambayo ni jukumu la Serikali, hayana dini. Ila jamii kwa ubinafsi na taasisi zake ambazo ni huru, zina ruhusa kujiunga na mashirika na jumuiya za kidini, kwa manufaa yao yawe ya kiuchumi, kiroho au mengineyo.

Tunapalilia matatizo makubwa kutokana na kutokuwa makini!
 
Mwanakijiji,
Uliyetoa mfano wa CCM na kujiunga mtu binafsi ni WEWE, mimi nimeuchambua tu usemi wako...

Rev. Kishoka,
Kwa nini unafikiria kuwa OIC inaweza kusema hakuna dini nyingine yoyote duniani isipokuwa Uislaam?... come on now usiwe nawe umefungiwa katika sandukui la Udini.. unaaandika vitu ambavyo havuiwezekani... Sasa What if Vatican wakisema hivyop? as a fact wameisha sema hivyo suiku nyingi na kuita Uislaam kuwa ni dini ya mashetani!...
Na hizi chulki zenu zinatokana na maneno kama hayo... wapo waislaam wenye mtazamo kama wenu na hawa sio watu ambao nategemea kusikia zuri toka kwao kuhusiana na Ukristu.
Na ukweli ni kwamba chuki hizi zinaletwa na watu kama nyie ambao mna quote vitu toka vichwani mwenu nje ya Biblia au Kura...Ni mawazo ya kina Bush (Evangelist) na Alqaeda (Ansaar Sunni) ambao sasa wameamua kutumia dini kama chombo cha kueneza dini zao...
U smart than that mkuu wangu...
 
Mkandara kuna ubaya gani wa kuwa na Balozi wa Tanzania kwenye IOC bila kulazimishwa kujiunga?
 
Mkamap,
Mkuu sasa hivi umeishiwa hoja kabisa.... yaani unataka kutueleza kuwa OIC ni sawa na Gongo?...mbona imefikia matusi sasa, acha uchizi mkuu wangu unapoanza vioja.
mwisho ningeomba nukuu ya hotuba ya Membe inayosisitiza kujiunga kwetu na OIC kutapunguza bei ya mafuta...kisha tutaendelea.. tusitoke ktk mstari mkuu.

Mkandara

Chizi ni yule anayeshindwa kuitambua katiba na sheria kwa kudhania vinginevyo.

Mfano CHIZI anaweza akachukua jiwe akakubonda nalo lakini ktk akili yake imemwambia kua hiyo ni haki yake ya msingi.

Ama chizi unaweza mwita yeye akatimua mbio lakini ktk akili yake kutimua huko mbio kulikua na maana ya kukuambia MAMBO VIPI ndugu yangu.

Kifupi CHIZI hua ana katiba na sheria zake mwenyewe kichwani ambazo siku zote au mara nyingi hukinzana na KATIBA ya NCHI pia SHERIA zinazomuongoza na zinazotumiwa na jamii nzima iliyo ya wengi.

OIC kufananisha na GONGO ni wewe mwenyewe ndio umezifananisha sio mimi.

Mimi nilicho fananisha ni jinsi gani katiba na sheria nchi hadi nchi zinavyotofautiana na kufanya kazi tofauti tofauti.
Na nikasema kufananisha nchi kimsingi ya kikatiba na sheria ni UELEWA LEGEVU.
 
Nafikiri OIC stands for organization of Islamic countries! Au kwa kiswahili Umoja wa nchi za Kiislamu! Kama siku hizi wamebadili na kuwa ni umoja wa nchi zinazozalisha mafuta basi tuambiwe au ni umoja wa nchi za kiisalmu na za zisizo na dini (za kikafiri)!!
 
Nchi yetu imetulia hii, watu wameshindwa kuboresha uchumi wanataka kuzalisha migogoro ya ndani. Mbona Jumuia za kutusaidia mojaa kwa moja kama PTA zilitushinda tukachomoka. Hii ya Africa Mashariki tu tunajitahidi kulinda maslahi ya taifa letu kwa nguvu zote.. Kulikoni leo OIC membe na wizara yake wanapigia debe. Nafikiri Diria alikuwa amefanya makosa madogo zaidi kuliko anayotaka kufanya Membe! KAma ni hoja yake binafsi au ya kutumwa lazima ajue kuwa nchi haiwezi kuendeshwa kwa kupendezesha masikio ya watu wachache.
 
Mwanakijiji,

Mkuu wangu umeuliza kwa nini Tanzania isiwe na balozi OIC badala ya kujiunga... Hapa mkuu naona unazidi kunichanganya ama kujichanganya wewe mwenyewe..Sielewi unaposema tuwe na balozi ktk Organization ambayo sio NCHI wala tawala isipokuwa chombo cha waislaam.. Mkuu tumeshazungumza sana huko nyuma hakuna haja ya kurudia yale ambayo nimekwisha cover..Ilikuwa kwanza katiba yetu, mara katiba yao sasa tunaingia ubalozi sijui kwa malengo gani!

Unajua mkuu wangu, leo inabidi niseme mengine ambayo sikupenda kuyaweza kapa isipokuwa inanilazimu sasa hivi..Unajua siku zote mwanamme mzinifu huwa anachezwa chale sana kuliko hata mkewe ambaye uzinifu haupo ktk damu yake pamoja na kwamba anaweza kufanya hivyo...Kwa hiyo mwanaume wa namna hii hapendi mkewe kuwa na marafiki na hasa pale anapoona mkewe akianza hulka ambayo inafanana na yake basi hufikiria kwamba mkewe anataka au amesha anza kutembea nje...Nitasherehesha maneno yangu hapa chini..

Hofu yenu kubwa sana ni OIC kama taasisi iliyobeba jina la Uislaam..hakuna zaidi ya hapo haya mengine ni visingizio tu kwani ni ktk tabia zenu mliweza kuanzisha jumuiya kibao, zinazofanya kazi kama OIC na zinatambulika na UN, leo hiki chombo kimoja cha kiislaam chenye wawakilishi wake UN imekuwa taabu kukubalika Tanzania kwa sababu tu kimebeba jina la NCHI za Kiislaam..
Mkuu wangu, ktk Uislaam hakuna mtu juu ya mwenzake isipokuwa yule mwenye kufanya ibada. OIC ni sauti ya waislaam ambayo ni muhimu sana kwa waislaam wa Tanzania kwani kwa miaka mingi tumekuwa tukidhalilishwa kwa mengi ambayo hayana maana kuyaweka hapa..na itakuwa napotosha mada hii ikiwa nitaingia ktk kabati la Udini..

Nadhani nimezungumza vya kutosha kuhusiana na issue hii ya OIC na kama kuna mtu hakupata kunielewa, then nadhani hakuna mtu anaweza kumwambia kitu...
Nitamalizia kwa kusema kama mngekuwa na mifano ya mabaya ya OIC kutokana na record ya nchi zilizojiunga hapo ningewasikiliza lakini hizi habari za kuzua fikra za kile ambacho kinaweza kutokea wakati hamna mfano hata mmoja... duh mkuu wangu kusema kweli nitashindwa mimi.
 
Mimi naona huu mjadala autafika kokote kwani watu wa pande zote mbili wamekuwa "closed minded " , tatizo kubwa inapokuja kwenye masuala ya diini wanadamu wanatumia moyo katika kufikiri .
 
OK,
Sijaandika lolote kwenye hii thread lakini ngoja nidonoshe kidogo kuwa endapo serikali inasema kuwa tunaweza kuwa mwanachama wa umoja wa nchi za kiislamu ni kuashiria kwamba imeshaamua kuwa Tanzania ni nchi ya kiislamu. Sasa je, sisi tusiokuwa waislamu tulie tu? Yaani hatuna nchi tena hapa Tanzania? Nisingekuwa na tatizo kama OIC ni club ya nchi zenye waislamu, lakini kama ni umoja wa nchi za kiisalamu, hapo ndipo ninapoona tatizo.

Ingawa hakuna madhara yoyote kwa nchi kuwa mwanachama wa umaoja wa nchi za kiislamu, tatizo kubwa linakuwa ni kwa serikali iliyopewa jukumu la kulinda na kuheshimu identities za raia wake: waislamu na wasiokuwa waislamu.
 
Kichuguu,

..hoja yoyote ile inayohusu DINI ni ngumu sana kuijadili.

..suala hili linahitaji kiongozi anayeheshimika sana kulijengea hoja kwamba tujiunge au tusijiunge. tatizo kiongozi huyo hatuna Tanzania ya sasa hivi.

..serikali imefikia kusema uongo wa waziwazi eti tukijiunga tutafaidika kwa kupata mafuta kwa bei ya chee/kutupa.

..mimi ningewaelewa kama wangesema kwamba OIC inaweza kutusaidia ktk miradi kama Morogoro Islamic University, na mingine ya namna hiyo.

..mradi kama wa Chuo Kikuu faida zake ni kwa jamii nzima bila kujali imani,rangi,kabila,au jinsia.

..pia wawe sincere kwamba tunachotafuta huko ni MISAADA na wala siyo kitu kingine.
 
JokaKuu, na watakaposema lengo ni misaada watuambie kuwa hakukuwa na njia nyingine yoyote ya kupata misaada hiyo isipokuwa kujiunga.
 
Kichuguu,
Shukran mkuu kwa kuuliza swali ambalo nadhani sijaligusia vizuri pamoja na kwamba umeshalipatia jibu...
Unajua mkuu kujiunga na jumuiya ya nchi za kiislaam sio kama mnavyofikiria kuwa hizi ni NCHI za KIISLAAM - Quote n Quote - bali ni nchi zenye UMMAH wa kiislaam kwa kiswahili nadhani ina maana ya UMATI wa kiislaam...Misingi yake haihusiani na utawala wa nchi hiyo upo ktk mfumo gani, haina maana kabisa kwamba nchi hizi ni za kiislaam kiutawala kwani ukweli ni kwamba
1. NCHI za KIISLAAM kwa maana ya kiutawala nadhani hazifiki hata 10..
2.Kuna nchi zilizotambua Uislaam kama ndio dini yake yaani state religion na nyingine
3. Ni secular states, ambazo zote (1,2 na 3) kwa jumla yake sidhani kama zinafika 40 dunia nzima.
Hizi zote zimetokana na Utawala uliopo na pengine ndio culture yao tofauti na sisi Tanzania.
Kama Marekani leo hii unapozungumzia culture ya nchi hiyo Ukristu ni lazima usimamiwe na kiongozi yeyote na hupimwa jinsi gani ameshika values na integrity...

Lakini ukirudi ktk mada hii husika utaona kwamba OIC ina wanachama zaidi ya 50, 57 to be exact kiasi kwamba hapa hapa Africa kuna nchi zaidi ya 10 ambazo hazina sheria wala katiba inayohusiana na Uislaam. kuna nchi wanachama kama Mauritania, Benin, Cameroon, Ivory Coast, Gabon, Uganda, Mozambique, Sierra Leone, Togo ambazo hazipo kabisa kuendesha nchi zao kwa misingi ya kidini iwe kuitwa nchi ya kiislaam, ama islaam kuwa dini ya nchi zao wala hazipo ktk mfumo wa secular states lakini nchi hizi ni wanachama wa OIC. Wakuu hatupo peke yetu ndani ya OIC kama nchi zinazoheshimu haki ya wananchi wake kuchagua na kuabudu dini waitakayo.

Zaidi ya hapo nchi hizi hazikujiunga jana wala juzi kiasi kwamba tusiweze kuwa na mifano hai kuonyesha malengo mabaya ya OIC kuhusiana na tuhuma ama mbegu mbaya mnazojaribu kupandikiza..Sisi Tanzania tuna tofauti gani kubwa na nchi hizo tena basi yawezekana nchi hizo zina waislaam wengi kuliko hata sisi iweje OIC wasianze na huko?..
Maamuzi ya kubadilisha nchi iwe ya kiislaam sio swala dogo wala la kufanyika mzaha kwa sababu ni lazima kushirikishwa wananchi. Ukiondoa nchi za kiarabu utaona kwamba nchi nyingi sana zimefikia hata Uamuzi wa Islaam kuwa state religion umefikiwa baada ya kupigwa kura ama chama kilichoshinda kilitumia sera za kidini na zikakubalika na wananchi wake... Tanzania hatujafikia usingizi mzito kiasi hicho na kifupi haiwezekani!

Labda kwa kusherehesha zaidi kiarabu ktk matumizi ya neno hili Nchi za kiislaam ni pmaoja na usemi unaozingatia sio nchi as nchi mnavyoichukulia bali WATU yaani UMMAH yaani kwa kiswahili tunasema UMATI ambao unaheshimu utawala uliopo madarakani, pia tofauti zetu na watu wengine lakini bado tunakumbushwa kuwa na mshikamano. OIC ni chombo ambacho kinajaribu kuyatazama mahitaji ya watu wake kwa kupitia serikali kuu na binafsi nadhani hii ni muhimu zaidi kuliko kupitia vyombo kama Bakwata ambavyo kwa tamaa ya fedha wanaweza kabisa kukaribisha magaidi au kuingiza siasa ktk misaada hiyo iwe ya fedha ama mali.

Kiusalama (National security) nilishasema kuwa ni bora kabisa swala lolote linalohusiana na misaada ya kidini hasa Waislaam kupitia serikali kuu kutokana na kuepuka viongozi wa dini kuwa wapambe wa mission kama hizi kwani hawa pia ni rahisi kutazama kila kitu wakiwa ndani ya sanduku la udini.. Hivyo OIC pamoja na kwamba imeanzishwa na waarabu hao kina Sultan wa Saudia ambaye mwenyewe na familia yake hawana Uislaam hata kidogo zaidi ya jina kubwa, hawa ni viongozi wa kisiasa (Sultan) na bahati nzuri wana ushirikiano mzuri na nchi za magharibi pia OIC ni chombo pekee cha waislaam UN, hivyo sidhani kama wanaweza kuingia na agenda nje ya yale wanayotaka kuyafanya. Hawa ni Lobbiest tu wanaotumia jina la dini kuonyesha fadhila zao na kwa sababu sisi wahitaji sioni ubaya wake as long as we control the floor!
Kama OIC ingekuwa imehusika kwa kiwango fulani cha matatizo ya nchi wanachama, ama imehusishwa na UDINI basi bila shaka hoja hii ingepata uzito wa kuendeleza discussion hii lakini hoja zote zilizomo humu zinapikwa na kugeuzwa geuzwa ili mradi zionekane zina mvuto bila ushahidi wa matukio.
Mkuu kwa kumalizia tu ni kwamba kwa nini lakini mnakuwa hamna imani na Uislaam kama dini kuna kitu gani kimewahi kutokea kwenu kiasi kwamba mnachofikiria kwanza ni kuwa Tanzania inataka kubadilishwa kuwa Nchi ya kiislaam...
I mean kuna ishara zipi mnazoziona ambazo mimi sizioni..
 
Mwalimu Kichuguu,

Hii gombania goli ya kudai Tanzania ni nchi ya Kiislamu, haijaanza majuzi wala 1993 wakati Diria alivyoiiniza Tanzania (Zanzibar) OIC!

Mwaka 1988, mtu mmoja ninaye mfahamu, alikuwa Bonn, wakati Diria ni balozi. Katika circle za diplomats, ilikuwa inafahamika kuwa Diria anatangaza kuwa Tanzania ni nchi ya Kiislamu.

So the plot hata kama ni kusadikika au ni maneno ya mtaani sasa limekuwa kweli, na wanasiasa wetu wamekimbilia kutoa kauli kujiunga na OIC bila hata kuuliza wananchi au wawakilishi wao.

It is funny kuwa suala la muafaka wa kuwa na serikali ya mseto Zanzibar, wananchi wanapewa jukumu la kupigia kura, lakini Tanzania kama nchi na Serikali yake kujiunga OIC, ni uamuzi wa Serikali na hakuna mjadala!

I wonder how much money have our representative and government be paid off or what sort of blackmail has CCM have to give in to for Tanzania to join OIC!
 
Bro Mkandara,

Mbona unaandikia mate wakati wino upo?

Kasome katiba na charter ya OIC, haizungumzii umati, inazungumzia kuwa ni jumuiya ya nchi za kiislamu, si jumuiya ya nchi zenye waislamu!
 
Mwanakijiji,

Mkuu wangu umeuliza kwa nini Tanzania isiwe na balozi OIC badala ya kujiunga... Hapa mkuu naona unazidi kunichanganya ama kujichanganya wewe mwenyewe..Sielewi unaposema tuwe na balozi ktk Organization ambayo sio NCHI wala tawala isipokuwa chombo cha waislaam..

Mzee kuwa na Balozi humo ni kitu ambacho tunaweza kufanya kwani hakivunji Katiba yetu, na hatuwi wanachama lakini tunakuwa na uhusiano rasmi. Nitakuwa mwongo nikisema OIC si kitu. OIC ni kama jumuiya ya African Union, au EU. Tofauti kubwani kuwa hizo nyingine zimeunganishwa na jiografia na historia na OIC imeunganishwa na dini.

Lakini kuwa na mahusiano na OIC ni vizuri na mimi sina tatizo nalo hata kidogo kama unavyofikiria. Napenda tuwe na mahusiano rasmi na OIC lakini vile inavyopaswa siyo vile inavyolazimishwa. Zipo njia mbili tu rasmi ambazo Tanzania inaweza kuwa na uhusiano na OIC bila kuwa na tatizo lolote lile. Kuteua Balozi kama walivyofanya nchi kadhaa ambazo zinaitambua OIC kama jumuiya muhimu au kuziambia jumuiya za Kiislamu TAnzania au Afrika ya Mashariki kujiunga kama Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu.

Mkandara, tunaweza kuwa na mahusiano yanayokubalika, yasiyo na utata, na yasiyo kulazimishwa na OIC. Mahusiano hayo ni aidha kuteua Balozi wa TAnzania OIC na wao wakateua Balozi wao Tanzania au Mwakilishi wa OIC Tanzania au hivyo vingine.

Kwanini hili wazo la kuwa na Ubalozi ambalo linakubalika ndani ya Katiba yao kwani hailazimishi huyo Balozi awe Muislamu au nchi iwe na WAislamu wengi isipokwa hiyo nchi iwe ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa tu? Kwanini hili wazo unalipinga, hutaki kulisikia na hulipi nafasi ya kutafakari? Nakusihi liangalie nje ya dini na uone uzuri wake.

Ni compromise nzuri, inaonesha tunaheshimu Waislamu, tunashirikiana na hatuleti mgongano kati yetu usio wa lazima. Sasa ubaya wake ni nini?
 
Mwanakijiji,
Toka lini umekuwa na imani na katiba yetu! toka swala la OIC limeanza ama!.
Ebu tazama upande wako kisha nambie katiba ina apply wapi!..Sipendi kuona dini zikimiliki ELIMU wala AFYA za watu kwa faida zao...damn sipendi kwenda huko mkuu tuyaache kama yalivyo lakini nipe sababu za maana kuhusiana na OIC kama Organisation.........period.
OIC ni WATU (waislaam) sio nchi hivyo balozi anawakilisha nchi hali viongozi wanaweza toka nchi yoyote ile...hapa mbona haiingii akilini mkuu. Balozi wa Organisation sijawahi kuona unless awe mtu wa nje kushuhudia yanayofanyika ndani which I believe imeshafanyika...Hivi kweli unaweza kuwa na Balozi UN bila kuwa mwanachama!... labda Balozi Observer. After all why? kitu gani kitufanye tufikie uamuzi kama huo hali hakuna record ya kujiunga na OIC..kisha basi maneno yako haya hapa:-
Kwanini hili wazo la kuwa na Ubalozi ambalo linakubalika ndani ya Katiba yao kwani hailazimishi huyo Balozi awe Muislamu au nchi iwe na WAislamu wengi isipokwa hiyo nchi iwe ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa tu?
Yanapungua kusema sababu kwa nini tuwe na balozi badala ya kujiunga, kwa manufaa gani hasa!.. sema tatizo lako hasa ni kitu gani kinachofanya tuweke balozi kama sio hisia zako kama Mkristu.! Unapokuwa balozi unajenga fikra kwamba nchi hii ni ya Kikristu vile vile! kwani balozi anasimamia hisia zako lakini sio za Mkandara.. Hiyo katiba tumesha maliza long time mkuu. Na nina hakika hata viongozi wa Kanisa Katoliki wameshapitisha... I know how the system works bro!
Nitarudia kusema mkuu mimi simo ndani ya sanduku la udini na nachukia sana kila linalofanywa na dini ama madhehebu nchini ktk kujenga ubaguzi wa jamii yetu kidini, lakini ndivyo ilivyo, waislaam wana muda wa kufanya catch up!
 
Mwanakijiji,
Toka lini umekuwa na imani na katiba yetu! toka swala la OIC limeanza ama!.

Mzee ninaiheshimu Katiba yetu kwani ni Katiba halali. Pamoja na hayo naikosoa na kuonesha mapungufu yake. Mapungufu yaliyomo kwenye Katiba hayaifanyi Katiba kutokuwa halali. Hivyo, sijaanza leo kuikubali Katiba yetu kwani nikiikataa ina maana hakuna Bunge, Mahakama, wala Rais. Katiba yetu ina mapungufu mengi sana na tunahitaji Katiba mpya. Hilo haliifanyi kuwa siyo Katiba halali.

Ebu tazama upande wako kisha nambie katiba ina apply wapi!..Sipendi kuona dini zikimiliki ELIMU wala AFYA za watu kwa faida zao...damn sipendi kwenda huko mkuu tuyaache kama yalivyo lakini nipe sababu za maana kuhusiana na OIC kama Organisation.........period.

Mzee OIC ni jumuiya nzuri, ina malengo mazuri kwa mujibu wa Katiba yake, iko tayari kushirikiana na nchi mbalimbali. Ni jumuiya ambayo ina lengo la kuinua maisha ya Waislamu na kuweka sauti ya nchi za Kiislamu duniani isikike. Hii ni haki yao kama vile AU ilivyo sauti ya Waafrika au SADC ikitaka kuinua maisha ya watu wa eneo letu la Afrika au ECOWAS kuinua maisha ya watu wa Afrika ya Magharibi.

Kama umefuata hoja zangu, hakuna mahali niliposema OIC ni jumuiya mbaya, ya hatari au isiyofaa kuhusiana nayo. Sijasema hivyo, siwezi kusema hivyo, na sitaki kusema hivyo.

Nitarudia kusema mkuu mimi simo ndani ya sanduku la udini na nachukia sana kila linalofanywa na dini ama madhehebu nchini ktk kujenga ubaguzi wa jamii yetu kidini, lakini ndivyo ilivyo, waislaam wana muda wa kufanya catch up!


Mzee utanielewa nilipo ukishanitoa kwenye kabati la Udini ulikonibandika. Siongozwi na udini naongozwa na mantiki ya hali halisi. Kama Kikwete na CCM wanataka Tanzania iwe nchi ya Kiislamu waseme hivyo nitakubali wamefanya hivyo na hakutakuwa na mjadala itakuwa ni jukumu la wengine kubadilisha kama hawataki. Kama wameshaamua kuwa Waislamu ni wengi zaidi ya Wakristu nchini na kutokana na sababu hiyo basi nchi inaweza kuwa ya Kiislamu au kuitwa ya Kiislamu hata kama siyo rasmi watuambie tu kwani hiyo itakubaliana na Katiba ya OIC. Hivyo ndivyo Amin alivyosema kuhusu Uganda na ndiyo akaweza kuiingiza Uganda OIC.

Wakituambia ukweli sidhani kama tutaandamana kupinga. Lakini hili la kutulazimisha kwa sababu wana vibendera na vimulimuli nawakatalia.
 
Mwanakijiji,

OIC ni WATU (waislaam) sio nchi hivyo balozi anawakilisha nchi hali viongozi wanaweza toka nchi yoyote ile...hapa mbona haiingii akilini mkuu. Balozi wa Organisation sijawahi kuona unless awe mtu wa nje kushuhudia yanayofanyika ndani which I believe imeshafanyika...Hivi kweli unaweza kuwa na Balozi UN bila kuwa mwanachama!... labda Balozi Observer. After all why? kitu gani kitufanye tufikie uamuzi kama huo hali hakuna record ya kujiunga na OIC..

mzee soma Katiba ya OIC basi maana naona tunabishana wakati mwenzangu hata hujui kuwa Katiba ya OIC inatoa nafasi ya nchi kuwa na balozi wake na tayari nchi kama Urusi na Marekani zina Mabalozi OIC. Soma Katiba yao. Unless hutambui Katiba ya OIC wewe unatambua watu tu na siyo hiyo Jumuiya. Kama hilo ni kweli, kwanini tujiunga na watu wengine? Si tunaweza kufanya hivyo na nchi zao?
 
Back
Top Bottom