Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Nziku,
Maswali ya mwanakijiji hayana sura kabisa kwa sababu yupo ndani ya kabati la Udini..

Madai mazito hayo mzee, lakini sitajaribu kujitetea.

Nilitaka niweke Katiba ya OIC. Kwa Tanzania kujiunga na Jumuiya hiyo ina maana inakubali Katiba hiyo. Nimetoa alternatives angalau mbili hapo juu na zote zitaiwezesha Tanzania kuhusiana na OIC rasmi pasipo kuwa mwanachama.

a. JK amteue Balozi Maalum wa kuiwakilisha Tanzania kwenye OIC. Mtindo huu umefanya na nchi kadhaa ikiwemo Marekani, Urusi, na hivi majuzi Maldives. Katika kufanya hivyo unakuwa na uhusiano na mawasiliano rasmi. Mkandara kuna ubaya gani kufanya hivyo maana tuna mabalozi katika sehemu mbalimbali na hata jumuiya mbalimbali.

b. Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu ya TAnzania (kama ipo) ijiunge na OIC na hilo hakuna mtu yeyote mwenye tatizo nalo.

c. Kama lengo ni misaada Tanzania ifanye bilateral agreements kama ilivyokuwa imefanya. Tayari tuna mikataba ya aina hiyo na Saudia, Qatar, Iran, Libya n.k na zote ni nchi za Kiislamu. Hakuna mtu mwenye tatizo hilo.

KWA NINI LAZIMA TUWE WANACHAMA NA KUKUBALI KATIBA YA OIC NA MALENGO YAKE YANAYOONGOZWA NA IBARA YA 2 YA KATIBA HIYO?
 
Madai mazito hayo mzee, lakini sitajaribu kujitetea.

Mkuu Mwanakijiji sijui kama umefuatilia vizuri na kujua kwamba hayo ni madai ya Mkandara na siyo mimi. Mimi nimeyatumia kumjibu Mkandara kwamba anapaswa ajibu kwa HOJA siyo tu kutoa madai aliyoyatoa. Soma aya ya mwisho ya Mkandara iliyoanza kwa neno Nziku...
 
uamuzi wa kikwete kulazimisha tujiunge na OIC...INAZIDI KUTUPA MASHAKA NA KUTUAMINISHA TUHUMA ZA HAMMIE RAJAB KUWA KIKWETE ALIPEWA MAMILIONI YA DOLA ZA KAMPENI NA IRAN...KWA MAKUBALIANO YA KUTEKELEZA BAADHI YA AJENDA..

1.KUUNGA MKONO MPANGO WA NUCLEAR WA IRAN....AMBAO NDIO JAMBO LA KWANZA ALILOFANYA KIKWETE ...NA UUNGWAJI MKONO HUO ULITANGAZWA RASMI KWENYE ZIARA YA MAKAMU WA RAIS IRAN..ALIYOMUWAKILISHA KIKWETE...

3.AJENDA YA PILI INAONEKANA WAZI NI KUINGIZA TANZANIA OIC KAMA NCHI ..BADALA YA KURUHUSU TAASISI KAMA BAKWATA ets ZIJIUNGE AU KUWA WATAZAMAJI TU KWENYE MIKUTANO YAO......HIII AJENDA IMELETWA NA WANA MIKAKATI NA ISSUE YA MAHAKAMA YA KADHI..ILI KWENYE KUFIKIA MUAFAKA ..MOJA YA AJENDA IPITE...KAMA SEHEMU YA MAKUBALIANO....MIMI NASEMA SITAKI MAHAKAMA YA KADHI WALA OIC...KUWA KWENYE KATIBA YETU....

SASA HATUJUI AJENDA ITAKAYODUATIA BAADA YA HII KUTOKA KWA HAO MABWANA WA KI IRAN ...WALIOHONGA PRE -PAID ...KWENYE KAMPENI ZAKE..ITAKUWA NINI...SI MNAJUA 2010 NI HIYO NA BADO PESA ZA KAMPENI ZINATAKIWA ,...UKIZINGATIA MAFISADI ..WADAU WENGINE NDIO HAO WANAJIFANYA WAPO HOI...
 
Nziku,

Mnapochambua katiba ya OIC unatafuta kitu gani?..
Je, mlifanya hivyo kutazama katiba ya Vatican, ama taasisi ya kikristu inasema nini?..
Nitarudia kusema kinachotakiwa kutazama ni kwetu sisi tunahitaji nini wala sio katiba ya nchi ama jumuiya kwa sababu kama ingekuwa tunatazama hivyo basi Marekani na China wasingekuwa wanashirikiana kibiashara..

Kabati la Udini ni sawa kabisa na vita baridi iliyokuwepo kati ya nchi za magharibi na mashariki... na inamchukua mtu asiyefungamana na upande wowote kuweza kuona athari za pande zote..Tatizo lenu hasa mkuu wangu Mwanakijiji kama nilivyoandika hapo juu mnatazama athari za upande mmoja tu huo wa shetani lakini huu mwingine ni Saint...Ndio hayo tunayaona na CCM wao kila siku wanasema Upinzani hauna hoja, watauza Uhuru na kuondoa amani iliyopo.. Kuna watu wanaamini kabisa Upinzani ni adui wa haki na utawala bora. hawapendi hata kusikia jina la Chadema na chochote kinachohusiana na Chadema ni evil..wakati huo huo sisi hapa tunachambua mabaya ya CCM na viongozi wabaya hatuhitaji kuuliza ni mazuri yapi yataletwa na Chadema ama kusoma katiba yao ili kukubali kuwepo kwa chama pinzani..these are scare tactics na Mwanakijiji kauvaa mkenge.
Kweli mimi na wewe tunatofautiana lakini tofauti zetu zipo ktk Uislaam sio Ukristu!.. kwa sababu nakubali kwa kila wanalolifanya maadam walengwa ni wananchi wenzangu, sina njaa hiyo...

Kisha mkuu wangu hakuna kitu ambacho sisi tunategemea zaidi ya kile ambacho siku zote mmekuwa mkitusisitiza kufanya..Tumekuwa tukilalamika kuhusu mashule ya dini, hospital za dini, huduma za kusaidia maskini za kidini.. Na majibu yenu wala sii muda mrefu mlikuwa mkisema na nyie Waislaam jengeni zenu!...hatuna chombo isipokuwa hiki sasa mnaanza kuwa na sababu hadi mnaingia ktk makabati ya katiba kufukua fitna.. Binafsi niliona mna point nzuri sana mlipotoa hoja ile, kama kweli wakristu wameweza kujipanga wakasaidia ommunity zao inakuwaje nyie waislaam mshindwe hali nyie ni matajiri zaidi ya Wakristu ambao wanategemea zaka na sadaka za watu..Nilijiuliza swali hili nikiwa nje ya kabati na ndio maana nilisema mapungufu ya waislaam waziwazi jambo ambalo nina hakika hakuna mkristu wala wewe unaweza kusema mapungufu ya Ukristu. Kwa sababu hu question lolote ndani ya dini yako...
Hata hivyo organisation zote hizi pamoja na kwamba zinawasaidia watu wote katiba zao zinatatanisha.. maamuzi ya uongozi na ajira zao yanatatanisha lakini kama utakuwa nje ya sanduku la udini utaweza kuona kwa urahisi kwa katiba zao zimeandaliwa hivyo...Mwanakijiji Mbondei kuoa mke Mbondei sio Ukabila hata kidogo mkuu wangu...
Ninachopinga mimi a kuendelea kusisitiza ni ule mtazamo wa coca cola ndani ya chupa ya cola (OIC) na vyombo vingine vya kidini aidha Vatican au YMCA ambavyo ni sawa na cocacola ndani ya glass.. sasa tunabishana tofauti kati ya vitu hivi hali kinywaji kilichomo ndani ya chupa au glass ni kile kile...kisha tunajaribu ku define tofauti ya glass na chupa hali kinachotakiwa kuutazamwa hapa ni kinywaji chenyewe yaani Cocacola.. yenyewe!

Mzee Mwanakijiji,
Mkuu usinielewe vibaya sikusema wewe mdini isipokuwa nimesema umo katika kabati la udini...
 
Kamundu,

Point yako nzuri sana unaposema bei ya mafuta inaendana na market yaani demand na Supply lakini hapo hapo nataka unijibu swali moja maanake yaonyesha wazi wewe mwanauchumi mzuri..Utanisaidia sana.
Ikiwa bei ya mafuta inaendana na soko inakuwaje McCain anasisitiza kuchimba mafuta ya ndani marekani offshore ili kuondokana na tatizo la bei ya mafuta na pia kutegemea nchi za nje..Wakichimba mafuta kwao itasaidia kitu gani ikiwa bei inafuata market?
 
Kamundu,

Point yako nzuri sana unaposema bei ya mafuta inaendana na market yaani demand na Supply lakini hapo hapo nataka unijibu swali moja maanake yaonyesha wazi wewe mwanauchumi mzuri..Utanisaidia sana.
Ikiwa bei ya mafuta inaendana na soko inakuwaje McCain anasisitiza kuchimba mafuta ya ndani marekani offshore ili kuondokana na tatizo la bei ya mafuta na pia kutegemea nchi za nje..Wakichimba mafuta kwao itasaidia kitu gani ikiwa bei inafuata market?

Nadhani akili yako mkandara ni sawa tu na ya akina Membe, hauelewi kwamba wazalishaji na wasambazaji wanaweza kuinfluence bei ya soko la mafuta duniani kwa ku create artificial shortage then demand ikawa kubwa kuliko supply na bei kuwa juu. Haya ni mambo ya kiuchumi zaidi. USA kuzalisha mafuta kwao (offshore) wanaweza ku control internal price kwani watazalisha kulingana na mahitaji (Demand) yao. Membe asitudanganye hakuna faida yoyote ya nchi kujiunga na OIC
 
Hawa viongozi wetu kuanzia rais hadi mawaziri hawatufai, wameapa kuilinda katiba ya nchi lakini sijui ni kitu gani kinawafanya hadi waanze kuyumba. Haiwezekani watake kuuza uhuru na utu wetu kwa kisingizio cha kupata unafuu wa bei ya mafuta. wanantaka unafuu wa bei ya mafuta wakati tunauwezo wa kuyanunua na tukabaki huku serikali ikitoa ruzuku pale inapoona bei imezidi na tukabaki na uhuru wetu. Hili linawezekana na linawezekana tu pale usimamizi mzuri na makini wa mapato ya nchi ukiwepo na si ufisadi huu uliokithiri. Waache ubabaishaji wafanye mambo ya msingi. OIC itawasha moto
 
Mkandara. Unapenda kuuliza maswali tuliyokuwa tukiyaita yakipolisi au ghetto. Mfano ni hili ulilouliza.

Kuna jamaa aliwahi kuniambia kuwa mafilosofa wakigiriki walikuwa wakiwauliza wakristu wa kale kuwa kama huyo Mungu wanayemwamini ni mweza yote na hakuna linalomshinda, je anaweza kuumba jiwe asiloweza kulibeba? Swali lako ni kama hilo.

Nitakipendaje kitu, dini au imani ambayo sikubaliani nayo? Kwa vile siupendi ubepari si kuwa siwapendi mabepari? Kwa vile Obama na wakina Kennedy hawaipendi itikadi ya wakina McCain, haina maana hawampendi mfuasi wa itikadi hiyo! Hata wewe ukiniambia leo kuwa unaupenda ukristu sitakuamini kwa sababu hauwezi kuupenda ukristu bila kumkubali Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu kitu ambacho ni blasphemous kwa yeyote aliye muislamu kamili! Kumtambua na kumkubali Kristo kama Mtume Issa bin Maryam na kuukataa uungu wake hakutoshi. Sasa leo nikasirike au nikuone mnafiki ati kwa sababu hauupendi ukristu? Kwangu mimi ni muhimu zaidi kunipenda kama binadamu kuliko kama mfuasi wa dini fulani au itikadi fulani. Unajaribu tena kupindisha maneno kwa kuingiza swala la maslahi ambalo halipo. Au mfano wa mwanamke kwa sababu hauwezi kuitoa uuke/jinsia (feminity) katika uanamke wake. Uuke/jinsia wake si chaguo kama ilivyokuwa dini. Uuke/jinsia si itikadi au imani. Mwanamke hawezi kuamka leo akasema kuwa amevutiwa kuwa mwanaume na ikawa hivyo bila kubadilisha kitu kilicho basic katika uhai wake! Kwa hali hiyo ni vigumu kumpenda mwanamke na kutoupenda uanamke. Vile vile siupendi ukristu kwa sababu ya maslahi yake bali kwa faraja inayonipa kiroho. Mimi ndiye ninayetoa sadaka na kutumikia imani yangu na si otherwise. Lakini cha msingi ni kuwa hii ni imani tu. Nitaweza kuiacha na kuikana siku yeyote bila kupoteza uutu wangu. Ni watu wenye msimamo wako wanaojumuisha uutu na imani ndiyo mlio hatari maana pasipo na imani hamuoni utu wa mtu. mathalani kwa vile siupendi na kuukubali uislamu basi nimepoteza uutu wangu na sistahili kuishi. Kwangu mimi, kunipenda kama binadamu kuna umuhimu zaidi kuliko kunipenda kwa vile ni mkristu!

Mtazamo kama huo ndiyo unaokuletea matatizo katika mjadala huu. Kwanza umejaribu kukana kuwa OIC ni shirika lenye muelekeo wa kidini kwa sababu tu halitimizi vigezo vyako (kutajwa kwenye Quran, kuongozwa na viongozi wa dini n.k.) hata kama katiba yake yenyewe inasema tofauti. Unashindwa vile vile kuamini kuwa watu wanaweza kupinga sisi kujiunga nao kwa kuangalia katiba tuu bila kujali muelekeo wa dini. Kwako wewe, wote wanaopinga chombo cha kidini ni kwa sababu hawaipendi dini hiyo which could not be further from the truth. Mimi mkristu na sina tatizo na sisi kujiunga na OIC. Bila shaka kuna waislamu ambao wanapinga sisi kujiunga na OIC kutokana na migongano ya kikatiba na si kidini.

Naam, nawapenda waislamu kwa sababu ni binadamu na si kwa sababu ya dini yao. Wakiacha dini yao kesho, mimi nitaendelea kuwapenda maana kinachotuunganisha ni ubinadamu wetu na si imani, itikadi, jinsia au rangi zetu.
 
Hivi kwa nini wakina Mkandara na wengine wanaona tatizo kukubali kuwa OIC ni chombo cha kidini. Badala ya kutaka kuturubuni na upuuzi huo wa bei ya mafuta si waseme wazi tu kuwa kujiunga kwetu kutasaidia jumuia yetu ya waislamu ( na wengine by extension) kwa miradi ya maendeleo. Naamini kuwa tukijiunga miradi inayosuasua kama hicho Chuo Kikuu cha Kiislamu kilicho Morogoro itapata uhai mpya!
 
...mdini wewe tunakujua huna lolote,kwanini usiende kujiunga na sheikh ponda mtengeneze jamhuri yenu ya kiislam mwembechai? good news watu kama wewe na divisive politics zenu za udini hamna support zaidi ya malunatics wenzenu wanaoteka misikiti kariakoo.



Nadhani wewe una Chuki na mimi.
ila kweli mimi ni MDINI Mislam safi.
Mimi sikuchangia lolote zaidi ya ku-quote post ya JOKA KUU kwa kuona kwamba yeye amesema vyema kuhusu ili swala na sikuaegemea upande wowote.
 
Kwa wakristo wa nchi hii wenye chuki kama Philemon Mikael, endapo kuna jambo lolote ambalo litainufaisha nchi kwa 98% na waislam asilimia 2% bora jambo hilo likosekane!

Acheni maroho mabaya na machuki mliyopandikizwa!

Wewe PM na wenzako; one thing you should note, ni kuwa kizazi cha sasa cha waislam sio kile cha miaka ya 60 kilichowapokea wakati wa kudai uhuru, kisha mkafanya mliyo fanya na leo mnawatukana bila kujali wema mliotendewa baada ya kutoka mlikotoka.

Kiazazi cha sasa, kama ni shule nao wanazo, wanachapa kazi na zaidi uadui wenu wanaujua vema.

Tutakula sahani moja na hizo chuki zenu. Nchi hii ni yetu sote.

NN.
 
Heee jamani nimesema naomba darasa leo imekuwa tena swala la Mkandara?...
Sasa ikiwa ni mashirika ya mafuta ambayo yanaweza kucheza mchezo wa demand kwani hayo mafuta ya Marekani yatachimbwa na kina nani!...si mashirika hayo hayo?
Nimeuliza hivi kwa sababu nililkuwa najiuliza swali hili kila mara mimi mwenyewe, Hiyo point ya McCain kuhusiana na uchimbaji mafuta ndani ya Marekani kama sababu ya kuwashushia wananchi mzigo wa bei.Na Kwa nini hoja hiyo inapokelewa na Wachumi wa Marekani ambao wanaelewa fika kwamba mashirika ya Mafuta ndio wanaocheza mchezo wote huu na wala sio nchi za kiarabu...

Kama mtasoma vizuri mtaona kwamba sikugusia kabisa swala la OIC, lakini ajabu ni kwamba akili yenu ipo ktk UDINI na kila linaloulizwa mnajaribu kumtazama muulizaji ni dini gani hata kama swali lenyewe halihusiani na dini...
Ndugu zangu acheni CHUKI yenu, sisi Waislaam tumesoma shuile zenu, tumevbadil;isha majina yetu ili kukidhi matakwa ya Taasisi zenu. Walimu wa Kiislaam wamefukuzwa kazi baada ya shule nyingi kuchukuliwa na Makanisa, lakini hujasikia tukihema kama mnavyohema nyie... Laukama mngepitia tuliyopitia sisi sidhani kama nchi hii ingekuwa na Usalama....
Kifupi hoja ya OIC nimeeleza kwa kirefu na nime cover kila angle kuhusiana na shuku zenu lakini kwa sababu ya NJAA na IMANI mlizokuwa washed nazo hamuwezi tena kupima....
 
sorry, I got to respond to this.

Nziku,

Mnapochambua katiba ya OIC unatafuta kitu gani?..

Binafsi ninaangalia ili kuona ni kwanini tunajiunga na jumuiya fulani. Tumeshaingizwa kwenye mikataba mingi ya ajabu ajabu kwa sababu hatukusoma "fine prints". Serikali inaposema "lazima tujiunga na IOC hakuna kugeuka" nasema sawa. Basi tuelewe hiyo jumuiya ina malengo gani, ina mfumo gani n.k Hivyo tunaangalia Katiba. Tusijiunge na kitu ambacho hatukijui. Kuna ubaya gani hapo?

Kukubali jumuiya fulani na kujiunga nayo ina maana unakubali Katiba yake. Leo nikiamua kujiunga CCM ina maana nakubali Katiba ya CCM, malengo yake, na itikadi zake. Kwa vile nchi inayotakiwa kujiunga ni ya Watanzania, kuna ubaya gani kwa Mtanzania kuangalia Katiba hiyo ambacho nchi yake inaingizwa? Unatushauri tusiiangalie?


Je, mlifanya hivyo kutazama katiba ya Vatican, ama taasisi ya kikristu inasema nini?..

Vitu viwili tofauti. Hadi hivi sasa Serikali ya Tanzania haijaamua kujiunga kama nchi kwenye CARITAS (shirika la misaada la Wakatoliki), na wala haijaamua kujiunga na Jesuit Refugee Services (JRS). Siku Kikwete akilazimisha Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Kikristu tutampinga vile vile na tutaangalia hizo Katiba za jumuiya hizo zinasemaje.

Unless una mfano wa Tanzania kutaka kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kikristu.

Kwenye suala la Vatican swali lako liko misplaced. Kwanini hujauliza mbona hatujaulizia Katiba ya Iran nchi ambayo inaoongozwa na kiongozi wa kidini, ambayo ni declared Islamic State? Kwanini umechagua Vatican tu isipokuwa kwa sababu ni nchi ya Kikatoliki na siyo Jumuiya ya Nchi za Wakatoliki? Hili la Vatican itabidi nilifafanua na kuonesha jinsi gani hoja zinazotolewa ni kinyume na mantiki, nyepesi na zenye lengo la kugusa hisia na siyo uhalisia.

Nitarudia kusema kinachotakiwa kutazama ni kwetu sisi tunahitaji nini wala sio katiba ya nchi ama jumuiya kwa sababu kama ingekuwa tunatazama hivyo basi Marekani na China wasingekuwa wanashirikiana kibiashara..

Wrong analogy. Kushirikiana kiuchumi ni tofauti na kujiunga na jumuiya ambayo mojawapo ya malengo yake ni kuwa na Economic Integration na baadaye Islamic Common Market. Hakuna Mtanzania mwenye akili timamu ambaye atapinga kuhusiana kiuchumi na nchi za Kiislamu kwani tayari mahusiano hayo yapo. Tuna mahusiano ya kiuchumi na Saudia, Oman, Qatar, Iran, Libya, n.k n.k Sina tatizo hilo na wala siitahi kusoma Katiba za nchi hizo kujadili mahusiano yetu.

Tatizo ni kuwa suala la IOC siyo suala la mahusiano ya kiuchumi, ni suala la uanachama. Kwanini Tanzania isiwe na mahusiano ya kiuchumi na IOC au nchi wanachama wa IOC pasipo kulazimishwa kujiunga?

Kabati la Udini ni sawa kabisa na vita baridi iliyokuwepo kati ya nchi za magharibi na mashariki... na inamchukua mtu asiyefungamana na upande wowote kuweza kuona athari za pande zote..Tatizo lenu hasa mkuu wangu Mwanakijiji kama nilivyoandika hapo juu mnatazama athari za upande mmoja tu huo wa shetani lakini huu mwingine ni Saint...

Mzee kuweza kuelewa kabati la udini ni lazima uelewe consistence. Mtu aliye kwenye Kabati la Udini hachagui wapi Kabati hilo linafunguliwa. Ukifungua Kabati la udini, chini kuna udini, katikati kuna udini na juu kuna udini. Kuna Consistence.

Msimamo wangu ni kuwa Tanzania inaweza kuingia makubaliano baina ya nchi na nchi (bilateral agreement) na nchi zote za Kiislamu na kupata misaada ile ile pasipo kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu. Kwanini huo uwe udini? Ninaposema JK aweze kumteua Balozi wa Tanzania kwenye OIC (na Katiba yao inaruhusu hilo) na huyo mtu awakilishe maslahi ya Tanzania (siyo ya Waislamu wa Tanzania tu) kwenye IOC kuna ubaya gani? Mtu mwenye udini angesema hataki mahusiano na nchi za Kiislamu au jumuiya za Kiislamu.

Hivyo ukiangalia utaona kuwa wewe unaangalia suala hili kwa kuangalia dini zaidi kuliko hali halisi. Kwamba kwa vile mtu anatoa maoni tofauti na kujenga hoja iliyo dhahiri basi hatakii mema Uislamu. This is trivialization of reality.

Ndio hayo tunayaona na CCM wao kila siku wanasema Upinzani hauna hoja, watauza Uhuru na kuondoa amani iliyopo.. Kuna watu wanaamini kabisa Upinzani ni adui wa haki na utawala bora. hawapendi hata kusikia jina la Chadema na chochote kinachohusiana na Chadema ni evil..wakati huo huo sisi hapa tunachambua mabaya ya CCM na viongozi wabaya hatuhitaji kuuliza ni mazuri yapi yataletwa na Chadema ama kusoma katiba yao ili kukubali kuwepo kwa chama pinzani..

Mzee mtu atakayetaka kujiunga na CCM au upinzani bila kujua Katiba yao hatustahili. Haitoshi kushabikia tu bali kujua nini watu hao wanasimamia ili ukubaliane nao.

Sehemu mojawapo ya Katiba ya OIC inasema kuwa inataka kuhakikisha kuwa Wapalestina hatimaye wanakuwa na nchi yao na Yerusalemu kuwa makao yake makuu. Huu ni msimamo wa IOC, je huu ni msimamo wa Tanzania? Unataka kusema kuwa tunaweza kujiunga na Jumuiya ambayo hatuikubali malengo yake au Katiba yake na tukawa wanachama kamili?

these are scare tactics na Mwanakijiji kauvaa mkenge.

Scare tactis za vipi? Mimi sina hofu na mwislamu yeyote au jumuiya yoyote ya Waislamu. Nimekaa na kukulia kati ya Waislamu. Ninaujua Uislamu kuliko watu wengi sana. Mimi si miongoni mwa watu wanaolinganisha Uislamu na Ughaidi, au Uislamu na vitu vyovyote hasi. Nimejifunza toka Uislamu mambo mengi na mchango wa Waislamu na Waarabu katika maendeleo ya falsafa Ulimwenguni, sayansi na hisabati ni vitu ambavyo ni mjinga tu hatovijua.

Nilishasema hata huko nyuma sina tatizo kama Tanzania itaongozwa na viongozi wote waislamu! Kwa kadiri ya kwamba wanaoongoza kwa Katiba yetu. Wanaotishia ni wale ambao hawataki kucompromise na kutaka wapate kila wanachotaka kwa sababu ni waislamu na kuwa wasipopata basi "kunaweza kutokea machafuko". Wanaotisha ni wale ambao hawaachi kutumia lugha ya vitisho. Nafahamu wewe si mmoja wao. Lakini wapo ambao Tanzania isipojiunga IOC, wasipopewa Kadhi, wasipofanyiwa hiki au kile basi wanaona ni affront dhidi ya Waislamu.

Kweli mimi na wewe tunatofautiana lakini tofauti zetu zipo ktk Uislaam sio Ukristu!.. kwa sababu nakubali kwa kila wanalolifanya maadam walengwa ni wananchi wenzangu, sina njaa hiyo...

Hatuwezi kukubali kwa vile kinachotakiwa kufanywa ni kizuri basi tushangilie bila kuuliza kinafanywa na nani na kwa misingi gani. Jinsi ninavyokusoma ni kuwa unaona kama vile IOC itawasaidia Waislamu wa Tanzania na hawa wakristu wana "ka wivu" ka aina fulani dhidi ya mafanikio hayo. Unaonekana kama unataka kusema kuwa Wakristu wakubali IOC wasiwazuilie waislamu misaada. Kama hivyo ndivyo basi nadhani you are missing a point.

Sipingi IOC kutoa misaada kwa Waislamu. Ninachopinga ni kutuwekea precondition kuwa ili Waislamu wa Tanzania wapewe misaada basi LAZIMA tujiunge na IOC. This is daylight blackmail. Ina maana tusipojiunga na IOC hakuna misaada itakayotolewa? Kama ni hivyo unaona hilo ni sawa?

Leo hii kuna mashule na mahospitali ya Kikristu nchini, yanatoa misaada ya kila aina na jumuiya nyingine nyingi tu za nje zinatoa misaada. Hakuna mojawapo inayotaka tuwe wanachama kama nchi ili tupewe misaada. Kuna SIDA, IDA, USAID, JICA n.k hakuna inayosema ili tuwasaidie Watanzania basi nchi yenu iwe mwanachama. Kwanini IOC itake hivyo? Misaada hii inayofungamana na uanachama ni misaada ya kupokelewa kweli?


Kisha mkuu wangu hakuna kitu ambacho sisi tunategemea zaidi ya kile ambacho siku zote mmekuwa mkitusisitiza kufanya..Tumekuwa tukilalamika kuhusu mashule ya dini, hospital za dini, huduma za kusaidia maskini za kidini.. Na majibu yenu wala sii muda mrefu mlikuwa mkisema na nyie Waislaam jengeni zenu!...hatuna chombo isipokuwa hiki sasa mnaanza kuwa na sababu hadi mnaingia ktk makabati ya katiba kufukua fitna..

Mkandara, hivi IOC imewahi kutoa msaada gani kwa Waislamu wa Tanzania hadi hivi sasa? Je Waislamu wa Tanzania wamewahi kuomba msaada gani toka IOC? Waislamu wana haki na wajibu wa kupata misaada kutoka sehemu mbalimbali na tayari wanafanya hivyo. Kuna misaada inayoingia kupitia taasisi nyingi tu za Kiislamu na hakuna mtu anayepiga kelele, linapokuja hili la OIC kwanini hadi tuwe wanachama ndio tusaidiwe?

Sasa kama hilo ni muhimu kuna ubaya gani kuangalia Katiba ya hiyo jumuiya ili tujue tunajiunga na kitu gani? Unataka tujiunga kichwa kichwa halafu huko mbeleni tuanze kugongana ilikuwaje tujiunge?

Binafsi niliona mna point nzuri sana mlipotoa hoja ile, kama kweli wakristu wameweza kujipanga wakasaidia ommunity zao inakuwaje nyie waislaam mshindwe hali nyie ni matajiri zaidi ya Wakristu ambao wanategemea zaka na sadaka za watu..

Mzee sijui ni nani amewahi kusema kuwa Waislamu wa Tanzania ni matajiri zaidi kuliko wakristu au vice versa kwani hilo linahitaji takwimu na vigezo vya takwimu hizo. Na sijui kama huo utajiri unatokana na dini ya mtu. Na je ni kweli wakristu wanategemea zaidi zaka na sadaka? Kuna haja ya kuangalia hicho ulichonacho ili niweze kukubali au kupinga so far sina sababu ya kujibu mere speculation.

Nilijiuliza swali hili nikiwa nje ya kabati na ndio maana nilisema mapungufu ya waislaam waziwazi jambo ambalo nina hakika hakuna mkristu wala wewe unaweza kusema mapungufu ya Ukristu. Kwa sababu hu question lolote ndani ya dini yako...

Watu wanaweza kuzungumzia mambo yao au ya wengine. Tukitaka kuangalia mapungufu ya dini za watu n.k tunaweza kufanya hivyo. Hilo hata hivyo halihusiani na OIC. OIC ni taasisi ya kidini, yenye malengo ya kidini, inayoongozwa na Katiba inayotambua dini fulani rasmi. Tanzania kama nchi haiwezi kujiunga huko. Hilo halisemi lolote juu ya mapungufu ya Uislamu au nguvu zake.

Hata hivyo organisation zote hizi pamoja na kwamba zinawasaidia watu wote katiba zao zinatatanisha.. maamuzi ya uongozi na ajira zao yanatatanisha lakini kama utakuwa nje ya sanduku la udini utaweza kuona kwa urahisi kwa katiba zao zimeandaliwa hivyo...

Katiba hazitatanishi; zinajieleza wazi ili kusiwe na utata. Katiba ya OIC iko wazi na ndio maana nchi zaidi ya 50 zimekubali kujiunga nao. Tanzania ikijiunga ina maana inakubaliana na Katiba hiyo, siyo utata uliomo kwenye Katiba hiyo.

Mwanakijiji Mbondei kuoa mke Mbondei sio Ukabila hata kidogo mkuu wangu...

Hili ni kweli, lakini Mbondei akisimama na kusema kuwa wenye kustahili kuolewa na Wabondei ni Wabondei, na ndoa zozote kati ya Mbondei na mtu mwingine hazitambuliki, na ya kuwa hata zile za Wabondei zifungwe kwa Kibondei huo ni ukabila.
Ninachopinga mimi a kuendelea kusisitiza ni ule mtazamo wa coca cola ndani ya chupa ya cola (OIC) na vyombo vingine vya kidini aidha Vatican au YMCA ambavyo ni sawa na cocacola ndani ya glass..

Once again, Vatican siyo chombo fulani cha Kidini, Kanisa Katoliki ni chombo cha kidini. Hili sijui tutalielewesha vipi. Huwezi kulinganisha Vatican na IOC au YMCA. Ukifanya hivyo itabidi useme Iran na Syria ambazo zina balozi nchini ni vyombo vya kidini. Hivi Mkandara hadi hivi sasa hukubali kuwa VATICAN ni nchi kamili na hakimiya?

sasa tunabishana tofauti kati ya vitu hivi hali kinywaji kilichomo ndani ya chupa au glass ni kile kile...kisha tunajaribu ku define tofauti ya glass na chupa hali kinachotakiwa kuutazamwa hapa ni kinywaji chenyewe yaani Cocacola.. yenyewe!

Tatizo ni kuwa wengine hatunywi Coca Cola, lakini wanataka kutulazimisha!

Mzee Mwanakijiji,
Mkuu usinielewe vibaya sikusema wewe mdini isipokuwa nimesema umo katika kabati la udini...

Katika hili Kabati nadhani wewe nawe una droo yako hapo hapo mkuu. Lakini sidhani kama mimi au wewe tunaangalia suala hili kwa udini kwa sababu kama nikweli basi kile unachodai mimi nimo sidhani kama wewe uko mbali nacho.
 
Heee jamani nimesema naomba darasa leo imekuwa tena swala la Mkandara?...
Sasa ikiwa ni mashirika ya mafuta ambayo yanaweza kucheza mchezo wa demand kwani hayo mafuta ya Marekani yatachimbwa na kina nani!...si mashirika hayo hayo?
Nimeuliza hivi kwa sababu nililkuwa najiuliza swali hili kila mara mimi mwenyewe, Hiyo point ya McCain kuhusiana na uchimbaji mafuta ndani ya Marekani kama sababu ya kuwashushia wananchi mzigo wa bei.Na Kwa nini hoja hiyo inapokelewa na Wachumi wa Marekani ambao wanaelewa fika kwamba mashirika ya Mafuta ndio wanaocheza mchezo wote huu na wala sio nchi za kiarabu...

Kama mtasoma vizuri mtaona kwamba sikugusia kabisa swala la OIC, lakini ajabu ni kwamba akili yenu ipo ktk UDINI na kila linaloulizwa mnajaribu kumtazama muulizaji ni dini gani hata kama swali lenyewe halihusiani na dini...
Ndugu zangu acheni CHUKI yenu, sisi Waislaam tumesoma shuile zenu, tumevbadil;isha majina yetu ili kukidhi matakwa ya Taasisi zenu. Walimu wa Kiislaam wamefukuzwa kazi baada ya shule nyingi kuchukuliwa na Makanisa, lakini hujasikia tukihema kama mnavyohema nyie... Laukama mngepitia tuliyopitia sisi sidhani kama nchi hii ingekuwa na Usalama....
Kifupi hoja ya OIC nimeeleza kwa kirefu na nime cover kila angle kuhusiana na shuku zenu lakini kwa sababu ya NJAA na IMANI mlizokuwa washed nazo hamuwezi tena kupima....

Usitupotoshe Mkuu. Pendekezo la McCain la kuchimba mafuta ukingoni mwa marekani ni kwa ajili ya kupunguza utegemezi wa marekani wa mafuta kutoka nchi ambazo aidha hawaelewani ( Venezuela n.k) au kuna uwezekano wa kutoelewana baadae ( urusi). McCain na Hillary Clinton ( Obama alikataa) walipendekeza kutoa msamaha wa kodi kwa mashirika ya mafuta kwa masharti kuwa nao wapunguze bei ya mafuta kwa watumiaji. Wachumi wote walikubaliana na Obama kuwa hizi ni McNomics na zimelengwa kutafuta cheap popularity.

Mbona hauzungumzii mashule, mazahanati na mahospitali ambayo mashirika ya kikristu yalinyang'anywa? Mbona hauzungumzii kupewa majengo ya Chuo cha Tanesco kuwa Chuo kikuu cha kiislamu? Mbona hauoni tatizo watoto wetu kulazimishwa kuvaa hijab wakitaka kusoma shule za kiislaam (Al Muntazir n.k.). Hivi yote haya mngetendewa kweli nchi yetu ingekalika? Hizo shule unazodai zimechukuliwa na wakristu si zilikuwa zao kabla ya kutaifishwa?

Unadai kuwa tunaogopa kuukosoa ukristu wakati hapo ulipo unajuwa wazi kuwa ukikosoa uislamu katika nchi inayojiita ya kiislamu adhabu yake ni nini? Hapo unapoishi katiba ya nchi hiyo inakulinda hata ukitaka kuusema ukristu kwa namna yeyote unayotaka. Mlikuwa na mihadhara ya kuukosoa ukristu. Je uliwahi kusikia mkristu yeyote au kiongozi wa dini (pamoja na wakina Mtikila) akidai kuwa wanaofanya hivyo wanastahili kuchinjwa? Mbona wenzetu mliandamana kudai Salman Rushdie auawe bila hata kusoma aliandika nini? Wangapi mmewatishia kuwasomea Al Badir (?) kwa sababu tu ya kutofautiana nao!

Mkuu, udini umekujaa kiasi cha kushindwa kukubali kuwa pengine hawa wanaopinga kujiunga na OIC ni kutokana na migongano ya kikatiba na si vinginevyo. Kwako wewe, yeyote anayepinga taasisi ya uislamu ana chuki na waislamu. Badala ya kuonyesha vipi kujiunga na taasisi hiyo hakupingani na katiba unakazania kulinganisha taasisi kama YMCA ambayo nchi yetu haijajiunga bali ni taasisi za wakristu wakitanzania ndiyo waliojiunga! Kwako wewe dini ni muhimu kuliko utaifa au ubinadamu tofauti na wengine ambao tunatofautisha dini na ubinadamu. Unatushutumu kuwa tumejaa njaa wakati hoja ya wenzako kubwa ni kuwa tujiunge na hiyo taasisi ili tupewe misaada! Unatusema sisi wakati wewe umetanguliza kibakuli?

Iko kazi!
 
Hawa akina jk wanacheza mchezo wa ajabu sana.

Siku mimi nitakapokua Rais nitaitoa Tanzania kwenye jumuia yoyote ya kidini na kuwatia kolokoloni watu wote waliovunja katiba ya nchi.

Mambo yote yaneendeshwa kwa kufuata katiba na sheria ,hata kama katiba ama sheria haitendi haki ni lazima ifuatwe vivyohivyo.
Mfano UGANDA wanaruhusu pombe ya GONGO wakati kwetu ni kosa hapa ina maana wanywaji wa gongo waandamane nao waseme hawatendewi haki maana GONGO uganda ni halali na kenya CHAN"GAA nacho halali? ,mfano EASTERN europe wanakunywa pombe yenye alcohol percent 70% wakati kwetu ilipigwa marufuku BINGWA iliyokua na percent 8%.
Hivyo mambo ya kufananisha nchi kwa misingi ya katiba na sheria ni ULEGEVU wa uelewa.

Hakuna msaada unaokusaidia wala hakuna mtu asiyekujua anayekupa msaada ila anachokupa ni UTUMWA.

Hatuogopi kusema tutasema Nchi karibia 90% za Afrika zilizo ktk OIC ni MaSIKINI,pia karibu zote zina vita za wenyewe kwa wenyewe .Huyo Membe atuambie OIC imeshindwa nini kuzisaidia bei ya mafuta na kimaendeleo nchi zilizo mwanachama.

Huyo membe ana uhakika Msumbiji,Uganda,Somalia ,Afrika ya kati.benini na kwingine bei ya mafuta ipo chini??

Nitamnukuu mtanzania "anayeona udini si mdini ila anayefanya matendo ya kidini huyo ndio mdini." hivyo anayetulazimisha kutupeleka ktk nchi za kidini huyo ndio mdini na anatakiwa aogopwe kama NUNGUNUNGU.

JK lazima naye atambue hata kama ni mdini tutamuonya na tutamwambia KITENDO hicho akikipitisha cha kutupeleka OIC atambue kabisa UDINI atakua ameurejesha rasmi nchini. ya kwamba kutatokea vyama vikuu viwili UKRISTU na UISLAMU na wananchi watachagua wagombea kwa misingi ya UDINI yani CCM,CHADEMA ,CUF havitaangaliwa tena.
 
Mkamap,
Mkuu sasa hivi umeishiwa hoja kabisa.... yaani unataka kutueleza kuwa OIC ni sawa na Gongo?...mbona imefikia matusi sasa, acha uchizi mkuu wangu unapoanza vioja.
mwisho ningeomba nukuu ya hotuba ya Membe inayosisitiza kujiunga kwetu na OIC kutapunguza bei ya mafuta...kisha tutaendelea.. tusitoke ktk mstari mkuu.
 
Mwanakijiji,
sorry, I got to respond to this.


Quote:
Originally Posted by Mkandara
Nziku,

Mnapochambua katiba ya OIC unatafuta kitu gani?..

Binafsi ninaangalia ili kuona ni kwanini tunajiunga na jumuiya fulani. Tumeshaingizwa kwenye mikataba mingi ya ajabu ajabu kwa sababu hatukusoma "fine prints". Serikali inaposema "lazima tujiunga na IOC hakuna kugeuka" nasema sawa. Basi tuelewe hiyo jumuiya ina malengo gani, ina mfumo gani n.k Hivyo tunaangalia Katiba. Tusijiunge na kitu ambacho hatukijui. Kuna ubaya gani hapo?

Kukubali jumuiya fulani na kujiunga nayo ina maana unakubali Katiba yake. Leo nikiamua kujiunga CCM ina maana nakubali Katiba ya CCM, malengo yake, na itikadi zake. Kwa vile nchi inayotakiwa kujiunga ni ya Watanzania, kuna ubaya gani kwa Mtanzania kuangalia Katiba hiyo ambacho nchi yake inaingizwa? Unatushauri tusiiangalie?
...

Mkuu wangu nimesema toka mwanzo tatizo lako upo ktk sanduku la Udini na umeitazama katiba hiyo ukiwa ndani ya hilo kabati lililofukizwa udi wa ibada ya jumapili bila kuelewa kwamba katiba ya OIC inalenga watu fulani kati ya kundi zima....Tunaweza kabisa kujiunga na jumuiya ya dunia ya walemavu na ikaitwa jumuiya ya Walemavu pasiwepo na tatizo kabisa..Na bila shaka katiba yao itawagusa zaidi Walemavu...
Kwa mfano wako wa kujiunga na CCM, mkuu wewe unaweza kuwa Liberal ktk maisha yako na jinsi unavyoendesha familia yako, lakini haina maana utakataa kujiunga na Chadema kwa sababu tu katiba ya Chadema imelenga upande wa Conservative....Kitu unachotakiwa kutazama sio maisha yako wewe na familia yako kuchagua chama isipokuwa unatazama zaidi mfumo gani unaweza kuiendeleza NCHI ktk mazingira yaliyopo..Kwa hiyo tatizo la huu mjadala ni pale mnapoangalia maisha yenu kama wakristu basi hata katiba ya Taasisi hizi iwe sawa na maisha yenu nyumbani, hata kama walengwa ni jirani ama kwa manufaa mengine nje ya nyumba yako...

Mkuu mimi hapa ni Liberal nikiwa nchi hii lakini kulingana na mazingira ya Tanzania najua fika kwamba Conservative ndio njia..Ni sababu hiyo imenifanya kujiunga na Chadema, na siwezi kusema siwezi kujiunga na chama chochote kwa sababu katiba zao zinapingana na imani yangu ya dini au nyumbani kwangu kuna watu wenye imani au mrengo tofauti na ule wa Conservative.
Hivi ndivyo mnavyoipokea na kuipima OIC. Hukubaliani nayo kaa pembeni nenda na Vatican ambayo ina manufaa kwako... period. Hukubaliani na CCM jiunge Chadema maadam hakuna mfarakano na Uadui baina ya vyama hivi...As a matter of fact sisi wananchi ndio tunaojenga sana Uadui kati ya vyama vya siasa kutokana na shuku zetu kama hizi.

Mkuu kama nilivyosema mwanzo wewe Mbondei kuoa mke Mbondei sii Ukabila!..na wewe kutazama sifa/kasoro za mchumba wako sii kosa hata kidogo ila kosa ni pale utakapo mchambua mwanamke uke wake, uzuri wake kutokana na kabila lake hasa pale umeisha weka mashaka ya kabila hilo. Hutaweza kunamtendea haki huyo mwanamke.na hasa pale utakapo sema siwezi kuoa mke huyo kwa sababu ni Mhaya!..
 
Mkandara.. kujiunga kwa mtu binafsi kwenye chama si sawa na nchi nzima kujiunga kwenye jumuiya fulani. Mimi na wewe tunaweza kujiunga au kutoka jumuiya, chama au ushirika wowote ule bila hata kufikiria mara mbili.

Leo hii mimi mtu mweusi nikiamua kujiunga na KKK watu watanishangaa lakini nikielezea kuwa naamini wanayosema na nakubali misimamo yao basi watu hawatanishangaa. Naweza kujiunga na kikundi cha AA au NA (alcoholic and narcotics anonymous respectively). Lakini katika kujiunga kwangu nao lazima nikubali misimamo yao na misimamo yao ina reflect principles zangu.

Siwezi kujiunga ili na mimi nionekane nimo humo.

Hadi sasa hujaeleza ubaya wa Tanzania kuwa na Balozi OIC. Na pia hujaeleza ubaya wa Tanzania kuingia mikataba ya maendeleo na ushirikiano na nchi moja moja za Kiislamu kitu ambacho sina tatizo nalo na sidhani kuna Mtanzania yeyote mwenye tatizo hilo. Naomba unisaidie kuna ubaya gani kufanya hivyo hadi lazima tujiunge nao wakati Katiba yao iko kinyume na maslahi ya Taifa zima? Kama lengo la jumuiya hiyo ni watu wachache kwa mujibu wa hiyo Katiba kuna ubaya gani watu hao wakajiunga badala ya nchi nzima kulazimishwa kujiunga?
 


He said they had come to learn that 21 countries in the world, including Christian countries, had joined the organisation.


So what... is.. is... is... is.... is it a sufficient and adequate justification...?

Earlier on, debating on the budget estimates of the ministry of Foreign Affairs and International Cooperation yesterday evening, the MP for Kigoma South, Manju Msambya said Tanzania would benefit a lot by joining the OIC.

Faida ikiwa 7 hasara zikawa 8 jumla yake ni ngapi , hey, kwa nini mnatuambia mna information nyingi then mnatoa maelezo kuhusu faida tu, mshasahau kuwa hofu yetu wananchi si uchache wa faida bali ni wingi wa hasara!!?

``Joining the OIC would help the country get rid of high prices of oil,`` he said, adding that Guinea, Gabon, Ivory Coast and Mozambique had joined the organisation.

Kwa faida ya nani hapa!! hizi kamba tu, mbona mlipunguza kodi ya mafuta na bei zikapanda tu hapa nchini. Au mnafikiri hatujui ile hasara inayopata taifa kwa kuondoa hiyo kodi imegeuka faida kwa nani!!


Hey, it is enough to be friends with OIC members countries na kama wana nia ya kutusaidia katika tatizo la mafuta watatusaidia tu. wasitufunge kamba. Basi kama ndio lengo la kujiunga huko KWA NINI TUSIJIUNGE OPEC KABISA, au ndio tunatoa rushwa kwa kujiunga uanachama, ehe he hehe, viongozi wetu wa enzi hizi bwana!!!?

[/QUOTE]
 
Kila mtu anajua kwa sasa kuna issue nene na za moto sana hapa nchini, kuna uwezekano mkubwa haya madude yanaibuliwa ku-divert attentions zetu wenye nchi toka kwenye ma EPA na ma KIWIRA na ma RICHRICH!!
 
Back
Top Bottom