Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Rev. Kishoka,

Mkuu wangu tafadhali kuwa mkweli hata kama unataka kutetea kitu. Ni makosa makubwa kwa mtu yeyote yule kufananisha Vatican na Saudia kwa malengo ya usawa..au Vatican na OIC na hata OIC na Saudia..Hivi vitu vyote ni tofauti kabisa na havilingani hata kidogo..

1. Vatican ni Nchi ya Kikatoliki na pia ni Taasisi ya Kikatoliki.
2. Saudia ni nchi ya kiislaam inayoongozwa na Sultan ambaye hawakilishi Taasisi yoyote ya kidini isipokuwa Ufalme wao. Unajua mwenyewe jinsi hawa jamaa (Prince) wanavyopiga maji na Umalaya...
3. OIC ni Taasisi ya kiislaam na sio nchi..Hivyo kuna tofauti kubwa sana ktk vitu hivi mnavyojaribu kuvifananisha ila tu kama swala hapa ni uhusiano wa nchi yetu Tanzania na Taasisi ya kidini bila shaka Vatican mbali na kuwa ni nchi nayo pia ni Taasisi ya kidini... nadhani ndipo swali la Mwiba linapoingia akiitazama Vatican kama taasisi ya kikatoliki..
Ni katika mfumo huo wa Taasisi ya Kikatoliki ambayo hata madhehebu mengine ya Kikristu hayakubaliani na Vatican.. Mfumo wa uongozi wa Vatican kama nchi haupo sehemu yoyote duniani isipokuwa Vatican..Hawana mfumo wa mawaziri na wizara kama wetu, mtu kama Kardilali Pengo pamoja na kwamba ni Mtanzania lakini anawajibika kwa Pope wakati sii balozi wa Vatican..kusema ukweli Pope ni zaidi ya Rais ama Waziri mkuu ni kama Mungu mtu..(Utanisamehe lakini) he above them all hata ukitazam kwa mtazamo wowote ule.

Kwa hiyo pamoja na kwamba Vatican ni nchi kwa tafsiri yoyote ile haiwezi kuwa sawa na Saudia kwani pamoja na kuwa saudia ni nchi ya kiislaam haiongozwi na Sheikh Mkuu wa saudia Mufti, Sheikh Abdul-Aziz Âlush kama Vatican inavyoongozwa na Pope ambaye pia ni mkulu wa dhehebu la katoliki.
Kama utakumbuka mwaka 1979, Sunni Muslim fundamentalists (Ansaar Sunni) wali seize Msikiti wa Makka wakitaka kuufanya uwe sehemu nzima independent kama ilivyo Vatican..Waliona hakuna sababu ya sehemu ile kuwa chini ya Utawala wa Saudia hali ile ni sehemu takatifu na ati ilitakiwa kuwa kama Vatican. Yaani Vatican inayojitegemea iko ndani ya Italy na Makka walitaka iwe ndani ya Saudia lakini inaongozwa na viongozi wa dini.. haikuwezekana wakapigwa kishenzi na Makka ikarudi chini ya Utawala wa Sultan. Hadi kesho hawa jamaa wanajribu kila siku kumwondoa King madarakani hasa yule marehemu baba yao ndiye alikutana na majaribio mengi sana..
Kwa hiyo unaweza kabisa kuona tofauti kaati ya Vatican na Saudia au Iran..Tofauti ya OIC na Vatican ni kuhusiana na nchi tu lakini malengo ya kitaasisi wote wanalenga watu wao ktk nchi nyinginezo hata kama kuna mchanganyiko wa imani..
Ubishi uliopo hapa hauwezi kuwa na mafanikio kwa sababu sisi wote tumeshindwa kuangalia nje ya imani zetu na kukubali ukweli kwamba OIC ni Taasisi kama zilivyo taasisi nyinginezo za kidini..na yeyote anayepinga kuwepo uhusiano kati ya nchi yetu na na Vatican kwa sababu ya kuwa ni taasisi ya kikatoliki, mimi nitamwita mdini kwa sababu kanisa la katoliki limeweza sana kuwasaidia wananchi wetu kwa kila hali kuliko hata nchi kubwa kama marekani ambazo zinataka kuijenga nchi yetu toka juu kwenda chini hali hawa Vatican wanalenga pale penye matatizo yaani wanaijenga jjamii yetu kutoka chini.
Na kama naweza kuwajibu watu hao wanaopinga Vatican kama taasisi kuwa na ushirikiano nasi nitawaambia na nyie anzisheni zenu..period..
Haya ndiyo majibu ambayo kila siku wamekuwa wakiambiwa watu wenye imani tofauti na Ukatoliki na ajabu ni kwamba pamoja na kwamba wakristu wenye madhehebu nje ya Ukatoliki pamoja na waislaam wanakubaliana na msingi wa uhusiano kati ya Tanzania na Vatican inanishangaza sana pale tunapoipinga OIC kwa sababu tu sio nchi ila ni taasisi ya kidni... malengo ya taasisi hizi hayana tofauti kabisa labda yanaziidiana tu.
Vatican mbali na kuwa nchi ni Taasisi ya kidini..na sii kweli kabisa kama unaweza kulinganisha Vatican na Saudia au OIC..
Vatican ni kitu kilichokamilika na hakuna mfano wake hapa duniani kama nchi au jumuiya ya kidini...
 
Tanzania ivunje uhusiano na Vatican mara moja.

Mwiba, mbona Tanzania haijavunja uhusiano na nchi za Kiislamu au hujui kinachojadiliwa hapa? Pili, unajua ni kwa nini Tanzania ina uhusiano na Vatican na pia kwa nini haijajiunga na taasisi yoyote ya Kikristu (kama ipo)?
 
Nashangaa unafiki wa baadhi ya Watanzania. nchi km Uganda ambayo ina waislamu kiduchu imekubali kujiunga na OIC ili kuwanufaisha waislamu wananchi wachache wafaidike na manufaa kutoka taasisi hiyo, na hakuna hasara waipatayo kama nchi. Lakini hapa kwetu misaada ya kidini na kimaendeleo kutoka Vatican, marekani na kwingineko ni ruksa kuingizwa bila vikwazo vyovyote. Tabu inakuja wakati taasisi za kiislamu za ughaibuni zinapotaka kuleta misaada ya kimaendeleo...kila aina ya visingizio vitabuniwa..kuanzia al-kaeeda, magaidi na kila jina baya litaitwa ilmradi kuzuia wasilam wasipate support kutoka nje. Hata viongozi wa dini kutoka nje wanadhibitiwa wakati wachungaji kutoka nchi mbalimbali duniani ambao si raia wametapakaa hadi vijijini kabisa bila kunyanyaswa. Lakini hayo yana mwisho.

Nakubaliana na wewe. Halafu kwa kuwa nchi yetu haina dini tutamteua "kafiri" John Pembe magufuli awe mwakilishi wetu katika OIC. PATAMU HAPO!
 
tatizo lako mdini!! Ndio maana unajitetea kwa maneno mengi...

Hayo mengine mie sijali....hata forums nzima hii mkiniona mie namna gani poa tu..lakini ktk mjadala huu mnaongea upuuzi na kisa ni udini!! Shame.

heshima mkuu.
Upuuzi is very subjective. Nafikiri ukichangia upuuzi nawe unakuwa mpuuzi.
Ingawa nakubaliana na wewe kuwa hoja hii imejaa udini.
Na kwa kuwa mimi ni mdini (means nina dini) nasema nooo to oic
 
OIC-Umoja wa nchi za kiislam. Iko wazi kabisa. Je Tanzania ni nchi ya Kiislam?
sio nchi ya kiislam lakini ni nchi yenye njaa na dhiki , na waislam wameliona hilo na wameamua kuisaidia . je kuna ubaya wowote. bush na serikali yake ya marekani kila mtu anawajua kama ni wauwaji wakubwa duniani na mnapokea msaada kutoka kwao . o i c na bush na serikali yake nani ana cv nzuri katika haki za binadamu?. punguzeni udini , tanzania sio nchi ya kikristo lakini sikukuu imewekwa jumapili na waislam wapo kimya hawajaomba iwe ijumaa. fikirini kabla kuleta hoja ambazo hazijengi zaidi ya kubomoa. misaada ya bush ina masharti mabaya kuliko misaada ya o i c. kataeni ya bush kwanza kabla ya kukataa ya o i c.
 
Shauku yote hii ya kutaka kujiunga na IOC ni kupanua wigo wa kutembeza kapu. Si unajua Mkwere nchi zote na taasisi nyingine kashatembeza bakuli kote sasa anatafuta wapi ambapo kapu halijapita alipitishe.
maana kwa
Bushi tayari,
Malkia tayari
Mwana mfalme wa saudia tayari
Ufalme wa UAE tayari
Barick tayari
Japani tayari
China tayari
Madrid tayari
Maximo tayari
Rusia tayari
Norad tayari


sasa imebakia IOC pekee lazima kapu lifike
 
Nilipoandika nilitoa source ya data nilizoandika kwa kuweka website ya UN, nipe source ya hizo data hapo juu, manake huenda ninacaught wrong data ili nisiingie kule kule kwa kusema uongo. Kama umeandika toka kichwani hiyo sio sahihi, manake kuna nchi ulizozitaja ziko ndani ya miungano.

Katika huu ulimwengu wa sayansi na teknologia, it takes so little effort kuingia hata google tu kupata info. Na kama huamini nilichokiandika sishangai kwani wengine ndivyo tulivyo ila kuuita uwongo ni mtazamo wako ingawa hauuziki ukweli. Siku njema.
 
Katika huu ulimwengu wa sayansi na teknologia, it takes so little effort kuingia hata google tu kupata info. Na kama huamini nilichokiandika sishangai kwani wengine ndivyo tulivyo ila kuuita uwongo ni mtazamo wako ingawa hauuziki ukweli. Siku njema.

Ukiamini kila kitu kinachotolewa katika mtandao utapotea. Unatakiwa uamini information zitokazo katika web zinazomilikiwa na mashirika yajulikanayo. Sasa unapotoa list za nchi ambazo ziko kama (Tanganyika na Zanzibar) kussoport Vatican ni nchi bado sikuelewi. Nimekupa web za UN, kuonesha Vatican si nchi, ni observer tu katika UN. Sasa toa source toka UN kwa uliyoyaandika, usipende kukata mada kabla hujajibu eti nisearch kwa google.
 
Sidhani kama kuna tatizo lolote katika hili la serikali kusaidia waumini wa dhehebu fulani. Kama Membe amesema ruksa kujiunga OIC kwa faida ya waislamu wa Tanzania .

Kama Membe angekuwa mwungana angesema kama unavyosema hapa kuwa Tanzania inakusudia kujiunga na OIC ili kuwasaidia ndugu zetu waislamu kuharakisha kueneza dini yao Tanzania. Na sio kusema kwa maslahi ya taifa. Hivi kweli mtu ukiwa mhitaji na maskini ndio kila anayetaka kukusaidia unakubali msaada wake bila hata kufikiri malengo aliyo nayo mtoa msaada?

Soma malengo ya OIC. Kutoa misaada na mikopo ni kivutio katika mallengo makuu waliyonayo ya kueneza imani yao. Hiyo ni njia na kwa watu maskini inafanya kazi vizuri sana. Na wanasema wazi katika Cairo declaration of human rights yao kuwa hatimaye sharia ndio kipimo cha haki za watu kwao.
"The Cairo Declaration of Human Rights in Islam (CDHRI) is a declaration of the member states of the Organisation of the Islamic Conference, which provides an overview on the Islamic perspective on human rights, and affirms Islamic Shari'ah as its sole source."

Kama ni suala la mahusiano ya Tz na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran au Vatican hiyo sioni shida.Lakini Tanzania ikiingia uanachama wa World Lutheran Federation au OIC lazima hapa kujiuliza. Mi nashauri BAKWATA ijiunge na OIC na siyo nchi yenye watu wa dini mbali mbali.
 
Tunajiunga na OIC kwa maslahi ya nani jamani? Ya Nchi au kikundi fulani cha Wananchi? Hivi tunadhani kujiunga na OIC kutapunguza umaskini wa Watz au dini fulani? Yaani serikali itakuwa na kazi ya kujiunga na kila Shirika kwa manufaa ya kikundi cha dini au kabila fulani kwa niaba ya kikundi husika?

WaTz tuache ubwege, Umasikini wetu hautapunguzwa wala kuisha kwa kuwa na Uhusiano na Shirika au Nchi yeyote, hapo ni kuongeza Utegemezi na kuchochea umasikini. Lazima tujinasue na huo utumwa, hali yetu ya Uchumi na maisha itaboreshwa na sisi bila kutegema msaada kutoka popote pale, tukifanikiwa kuondokana na hiyo akili ya utegemezi, umasikini tutauaga.

Yaani serikali na Wanasiasa wetu mkakati wa kuondokana na umasikini ni lazima ujiunge na Taasisi fulani ili upate msaada wa kujikomboa kutoka umasikini? Naogopa sana!

Yaani leo tujiunge na OIC kesho tuajiunga na WCC (World Church Council) Wakristo wakiomba iwe hivyo?

Tuache ujuha, nadhani hawa Viongozi wetu wanachosaka ni uhalali wa kuendelea kuwa madarakani kwa gharama yoyote, wameshindwa kuweka mikakati ya kuitoa nchi yetu kwenye umasikini sasa wanatafuta njia rahisi ya kupata uhalali wa kuwepo madarakani, na ndo maana CCM wakaweka Ilani maalum kwa watu maalum na wanataka kuhakikisha angalau walifurahishe kundi hilo kwa kuipeleka nchi yetu OIC, ikishindikana sijui 2010 watawadanganyaje?

WaTz tusidanganywe, maisha Bora hayatakuja kwa kujiunga na taasisi fulani fulani bali kuweka mikakati ya makusudi na kukomesha rushwa na ufisadi na kutumia raslimali zetu vizuri.
 
Rev. Kishoka,

Mkuu wangu tafadhali kuwa mkweli hata kama unataka kutetea kitu. Ni makosa makubwa kwa mtu yeyote yule kufananisha Vatican na Saudia kwa malengo ya usawa..au Vatican na OIC na hata OIC na Saudia..Hivi vitu vyote ni tofauti kabisa na havilingani hata kidogo..

1. Vatican ni Nchi ya Kikatoliki na pia ni Taasisi ya Kikatoliki.
2. Saudia ni nchi ya kiislaam inayoongozwa na Sultan ambaye hawakilishi Taasisi yoyote ya kidini isipokuwa Ufalme wao. Unajua mwenyewe jinsi hawa jamaa (Prince) wanavyopiga maji na Umalaya...
3. OIC ni Taasisi ya kiislaam na sio nchi..Hivyo kuna tofauti kubwa sana ktk vitu hivi mnavyojaribu kuvifananisha ila tu kama swala hapa ni uhusiano wa nchi yetu Tanzania na Taasisi ya kidini bila shaka Vatican mbali na kuwa ni nchi nayo pia ni Taasisi ya kidini... nadhani ndipo swali la Mwiba linapoingia akiitazama Vatican kama taasisi ya kikatoliki..
Ni katika mfumo huo wa Taasisi ya Kikatoliki ambayo hata madhehebu mengine ya Kikristu hayakubaliani na Vatican.. Mfumo wa uongozi wa Vatican kama nchi haupo sehemu yoyote duniani isipokuwa Vatican..Hawana mfumo wa mawaziri na wizara kama wetu, mtu kama Kardilali Pengo pamoja na kwamba ni Mtanzania lakini anawajibika kwa Pope wakati sii balozi wa Vatican..kusema ukweli Pope ni zaidi ya Rais ama Waziri mkuu ni kama Mungu mtu..(Utanisamehe lakini) he above them all hata ukitazam kwa mtazamo wowote ule.

Kwa hiyo pamoja na kwamba Vatican ni nchi kwa tafsiri yoyote ile haiwezi kuwa sawa na Saudia kwani pamoja na kuwa saudia ni nchi ya kiislaam haiongozwi na Sheikh Mkuu wa saudia Mufti, Sheikh Abdul-Aziz Âlush kama Vatican inavyoongozwa na Pope ambaye pia ni mkulu wa dhehebu la katoliki.
Kama utakumbuka mwaka 1979, Sunni Muslim fundamentalists (Ansaar Sunni) wali seize Msikiti wa Makka wakitaka kuufanya uwe sehemu nzima independent kama ilivyo Vatican..Waliona hakuna sababu ya sehemu ile kuwa chini ya Utawala wa Saudia hali ile ni sehemu takatifu na ati ilitakiwa kuwa kama Vatican. Yaani Vatican inayojitegemea iko ndani ya Italy na Makka walitaka iwe ndani ya Saudia lakini inaongozwa na viongozi wa dini.. haikuwezekana wakapigwa kishenzi na Makka ikarudi chini ya Utawala wa Sultan. Hadi kesho hawa jamaa wanajribu kila siku kumwondoa King madarakani hasa yule marehemu baba yao ndiye alikutana na majaribio mengi sana..
Kwa hiyo unaweza kabisa kuona tofauti kaati ya Vatican na Saudia au Iran..Tofauti ya OIC na Vatican ni kuhusiana na nchi tu lakini malengo ya kitaasisi wote wanalenga watu wao ktk nchi nyinginezo hata kama kuna mchanganyiko wa imani..
Ubishi uliopo hapa hauwezi kuwa na mafanikio kwa sababu sisi wote tumeshindwa kuangalia nje ya imani zetu na kukubali ukweli kwamba OIC ni Taasisi kama zilivyo taasisi nyinginezo za kidini..na yeyote anayepinga kuwepo uhusiano kati ya nchi yetu na na Vatican kwa sababu ya kuwa ni taasisi ya kikatoliki, mimi nitamwita mdini kwa sababu kanisa la katoliki limeweza sana kuwasaidia wananchi wetu kwa kila hali kuliko hata nchi kubwa kama marekani ambazo zinataka kuijenga nchi yetu toka juu kwenda chini hali hawa Vatican wanalenga pale penye matatizo yaani wanaijenga jjamii yetu kutoka chini.
Na kama naweza kuwajibu watu hao wanaopinga Vatican kama taasisi kuwa na ushirikiano nasi nitawaambia na nyie anzisheni zenu..period..
Haya ndiyo majibu ambayo kila siku wamekuwa wakiambiwa watu wenye imani tofauti na Ukatoliki na ajabu ni kwamba pamoja na kwamba wakristu wenye madhehebu nje ya Ukatoliki pamoja na waislaam wanakubaliana na msingi wa uhusiano kati ya Tanzania na Vatican inanishangaza sana pale tunapoipinga OIC kwa sababu tu sio nchi ila ni taasisi ya kidni... malengo ya taasisi hizi hayana tofauti kabisa labda yanaziidiana tu.
Vatican mbali na kuwa nchi ni Taasisi ya kidini..na sii kweli kabisa kama unaweza kulinganisha Vatican na Saudia au OIC..
Vatican ni kitu kilichokamilika na hakuna mfano wake hapa duniani kama nchi au jumuiya ya kidini...

Kama nimeelewa vizuri mlinganisho wako ni kwamba tujiunge tu na OIC kwa vile Vatican ina mwakilishi wake hapa na pia wa Tanzania yupo Vatican. Mimi nadhani hoja ni kwa nini tunajiunga na OIC na wakati lengo la OIC ni kuendeleza uislamu na maslahi ya Waislamu wakati nchi yetu haina dini.

Vatican ni city-state na kama unavyosema Rais wake ni Papa. Ukijiunga na Vatican hupaswi kuendeleza au kutetea maslahi ya Kanisa Katoliki ila tu haki za msingi za watu.

Mimi nadhani ipo haja ya kuliangalia vizuri swala hili tusije tukaingizwa kwenye matatizo mengine. Watu wanaogopa uislamu kwa sababu ya sheria zake ni kali mno: mfano, kupiga watu mawe mpaka wafe, kutetea adhabu ya kifo, kukata watu mikono wakiiba, wengine wanasema uislamu unawanyanyasa wanawake (wanakuwa 'regarded' kama 'impure' wakiwa katika siku zao 'as if' wanataka wenyewe wakati ndivyo walivyoumbwa) na paia msimamo wake wa kudhani wasio waislamu siyo "watu" bali makafiri, nk.
 
MagobeT,
Mkuu soma vizuri maelezo wa watu kabla hujahukumu...
Kama hukuelewa nilichoandika itakuwa vigumu sana mimi kukufahamisha na naweza kutumia hoja za kipuuzi kama zako...
Mathlan ni wapi kumeandikwa Papa ni rais wa Vatican?...Lini papa kasimama UN kama rais wa Vatican?, mbona sijasikia demokrasia ikipiganiwa Vatican huyo rais hukaa miaka mingapi na kuna vyama vingapi vya Upinzani..
Kama Zanzibar sio NCHI kwa tafsiri mnayoitoa nionyeshe ishara hizo huko Vatican..

Mkuu naweza kuzua maswali mengi kuhusiana na Vatican na tukaendelea kubishana hadi kesho kwa jambo la kijinga kabisa, hali sisi wote tunafahamu kwamba Vatican sio NCHI tu bali pia ni TAASISI ya kidini. Kama taasisi, Vatican pia ina lengo la kuendeleza Ukatoliki kwa maslahi ya Wakatoliki wakati nchi yetu haina dini...ndilo swali la kina Mwiba hawakusisitiza tuvunje uhusiano kama mnavyotaka kuepusha hoja za msingi... badala ya nyie kufikiria ktk kipimo hicho mnazua sababu za kuibeba vatican hali hamkubali sababu zozote zinazohusiana na OIC.. How do U expect Muslim watakubali sababu zenu ambazo kwa fikra zao hakuna tofauti na OIC kama taasisi..
 
mtoto akizaliwa pale zanzibar atakuwa mwislamu, akizaliwa kule rombo atakuwa mkatoliki, akizaliwa mzake pale dodoma atakuwa mu anglikan, akizaliwa marangu mtoni atakuwa mlutheri, akizaliwa kipera kule iringa atakuwa mu-orthodox, akizaliwa kule kandete tukuyu atakuwa monrovian, ugomvi wa nini? kuna aliyechagua azaliwe mahali hapo na kujikuta na dini hiyo? ngozi yetu na utaifa letu ndo muhimi zaidi
 
Mkandara,Magobe T,Rev.Kishoka,...

..mimi nafikiri tujiunge tu na OIC. tumebishana kuhusu suala hili for more than 15 years na bado tuko palepale tulipoanzia.

..tujiunge tu ili wananchi tupate wasaa wa kutafakari na kujadili masuala mengine ambayo pia yana umuhimu kwa taifa letu.

..watu wanadai OIC, lakini wanasahau kwamba financiers wakubwa ni nchi zinazojitambulisha kama Islamic Republics ambazo tayari tuna mahusiano nazo mazuri tu na ya muda mrefu.

..tayari tuna uhusiano na Saudi Arabia, Iran, Kuwait, Egypt, Malaysia, Indonesia, Pakistan, na nchi nyingine zinazojitambulisha kama Islamic Republic.

..kama ni misaada basi hizo Islamic Republic zingeshatusaidia na kumaliza matatizo ya Waislamu na Watanzania kwa ujumla.

..tumeshasaidiwa sana tu na kwa muda mrefu. kuna kipindi tulikuwa tunaongoza Afrika nzima kwa kupewa misaada na mikopo toka kila kona ya dunia.

..tumepata misaada toka kila mahali, scandinavia,eu,uk,usa,china,india,korea, iran,kuwait fund, saudi fund,you mention. ukweli ni kwamba bado tumekwama.

..OIC itakuja, hapana shaka watasaidia hapa na pale kama hao waliowatangulia, lakini nina hakika hawawezi kutukomboa toka kuwa nchi masikini kwenda kujitegemea.

..binafsi sijaona nchi iliyoendelea kwa kusaidiwa. inafika wakati tunapaswa kukusanya nguvu zetu wenyewe ili tuinuke kimaisha na kiuchumi.

..mjadala huu na hatua ya kujiunga na OIC ni moja ya hatua za sisi kujitambua kama Taifa.
 
Katiba ya nchi inaruhusu na je? Tanzania itaingia kwenye mashirika mengine ya dini

No going back on OIC, says minister

2008-09-01 09:51:57
By Austin Beyadi


The Government has said it will continue with the process of joining the Organization of Islamic Conference (OIC) in spite of some opposition.

Foreign Affairs and International Cooperation deputy minister Seif Iddi told The Guardian in an exclusive interview in Dar es Salaam on Friday that there was no plan to shelve the idea.

``The government will start working on the issue by first involving Zanzibar, being the centre of the subject,`` he said.

Iddi said he was due to travel to the Isles over the weekend to meet Speaker of the House of Representatives to discuss Tanzania joining the OIC as a sovereign state. He indicated that he would also meet some other officials during the trip.

``Tanzania commits no mistake by joining the OIC because it stands to benefit,`` he said. He added that the National Assembly would be given feedback on the discussions.

``We are convinced that there is nothing wrong with Tanzania joining the OIC. We believe we stand a better chance to benefit from the organisation. This will include solving the problem of unstable and high oil prices,`` he said, adding:

``Tanzania will not be guided by Islamic laws because the OIC, just like any other development organisation, has nothing to do with Islamic laws.``

Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe told the National Assembly in Dodoma last month that there was no harm in Tanzania joining the OIC.

According to him, a meeting between Union government officials and members of the House of Representatives held this year had made the resolution.

He said they had come to learn that 21 countries in the world, including Christian countries, had joined the organisation.

In the early 1990s, Zanzibar attempted to join the OIC, but was blocked by the Union government on grounds that, being part of the Union, had no mandate to join international organisations.

However, Membe said the government had thoroughly worked on the issue and come to the conclusion that there was nothing wrong for Tanzania to join the organisation.

SOURCE: Guardian
 
Yes.....Membe kichwa...sasa mkuu atuletee duo citizen...
Najua wapo vikorosho wengine wataibuka na hoja zao kama kawaida..
 
``We are convinced that there is nothing wrong with Tanzania joining the OIC. We believe we stand a better chance to benefit from the organisation. This will include solving the problem of unstable and high oil prices,``

Hiki ndicho kinachonitibua! Kupenda shortcut na kutegemea dezo.

Kujiunga na OIC sio panacea ya matatizo yetu ya umaskini na wala sidhani kama tutapata unafuu wowote kwenye bei ya mafuta. Bei ya mafuta na OIC wala havihusiani!
 
``The government will start working on the issue by first involving Zanzibar, being the centre of the subject,`` he said.

Iddi said he was due to travel to the Isles over the weekend to meet Speaker of the House of Representatives to discuss Tanzania joining the OIC as a sovereign state. He indicated that he would also meet some other officials during the trip.

``Tanzania commits no mistake by joining the OIC because it stands to benefit,`` he said. He added that the National Assembly would be given feedback on the discussions.

``We are convinced that there is nothing wrong with Tanzania joining the OIC. We believe we stand a better chance to benefit from the organisation. This will include solving the problem of unstable and high oil prices,`` he said, adding:

``Tanzania will not be guided by Islamic laws because the OIC, just like any other development organisation, has nothing to do with Islamic laws.``
SOURCE: Guardian

Now you all see what I told everyone that the joining of OIC was a Political Compromise to settle the Zanzibar dust on Muungano?

However kuna uongo mwingine kuhusu suala la bei za mafuta. I have worked on Investment companies na bei ya mafuta haiendani kwa urafiki wa ushikaji.

Watanzania msidanganywe kuwa tutapata mafuta ya bei nafuu kwa kujiunga OIC! Kama OIC ingekuwa na nia ya kutoa mafuta ya Bei nafuu kwa nchi masikini, nchi za OIC ambazo ziko OPEC zingefanya hivyo kwa kuwa ni wajibu wao kutokana na imani.

This is a day light lie from our government!
 
..............``We are convinced that there is nothing wrong with Tanzania joining the OIC. We believe we stand a better chance to benefit from the organisation. This will include solving the problem of unstable and high oil prices,`` he said, adding: ...........

.......mmmmhhh!.......Hivi kuna ugumu gani kuweka hizo benefits hadharani (kwa watu) watu tukazijadili na kuona ukweli....na kuondoa mzizi wa fitina?

....kuhusu ku-solve problems ya prices za Oil........mmmhh, Mh Waziri hebu tupe maelezo ya kina kidogo
 
.......mmmmhhh!.......Hivi kuna ugumu gani kuweka hizo benefits hadharani (kwa watu) watu tukazijadili na kuona ukweli....na kuondoa mzizi wa fitina?

....kuhusu ku-solve problems ya prices za Oil........mmmhh, Mh Waziri hebu tupe maelezo ya kina kidogo

Ogah,

Unajua wanasiasa wa Tanzania wanafikiri kila Mtanzania ni mbumbumbu!

Lakini kwa upande mwingine, hii inaonyesha wazi ni jinsi gani waandishi wetu wa habari walivyo vihiyo wa mambo ya uchumi na dunia kwa ujumla. Kwa nini hawakumuuliza maswali magumu kuhusiana na majibu hya kijinga aliyowapa?

Hivi waandishi wetu hawajui hata kidogo ni jinsi gani bei za mafuta zinazofanya kazi na kutokea? je wanajua ni lini bei ya pipa moja itamfikia mtumiaji mafuta?

Waziri anadanganya umma unakubali, wako wapi wachumi na wataalamu wa kununua mafuta kumjibu Waziri hata Membe alipotoa kauli hiyo wakati wa Bajeti?

Leo tutaanza kuambiwa Serikali haiwezi kupandisha mishahara ya watumishi wake kutokana na Kimbunga cha Gustav huku Marekani kuharibu mfumo wa Uchumi wa Dunia!
 
Back
Top Bottom