Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,894
- 11,378
Naamini kuwa kilichochangia sisi watu wa bara kutokuwa na migongano ya kidini au ya kikabila ni kuwa toka awali juhudi zilifanywa kutuchanganya bila kuangalia dini zetu au kabila letu. Tumekuwa pamoja, tumesoma pamoja , tumefungwa pamoja na tumezikana pamoja bila kuambiwa huyu kwa sababu tu ya imani yake ni tofauti na wewe. Kwa hali hiyo tumejuana na kushibana kiasi ambapo wale wa kizazi changu ni vigumu kumchukia yule ambaye si wa dini yako maana utakuta marafiki zako na ndugu zako wengi wanatoka dini hiyo. Leo hii tumeanza kusoma kila mmoja kivyake kuanzia chekechea hadi chuo kikuu. Na hili la kutuambia kuwa wenzetu watakuwa wanahukumiwa tofauti na wengine kutazidisha ufa ulioanza kujitokeza katika jamii yetu. Tunakanyaga kwenye utelezi na tusipoangalia tutaishia kubaya.