Mkuu,
Naomba tuelewane,interest za serikali ziko nyingi sio mfano,taking over the rule of law hapana.
Bakwata na serikali wana mahusiano ya karibu sana,mahusiano ambayo yana watia shaka waisilamu walio wengi ikiwemo na mimi,sasa kama kuta kua na siri kati ya Bakwata na Serikali sidhani kama serikali ita kuwa willing kushare hizo siri na chombo ambacho yenyewe haija husika hata kidogo katika kuiunda (yaani kama hiyo bill itapita basi waislamu wataunda chombo chao wao wenyewe na chombo hicho kitakua na mamaraka ya juu zaidi kuliko Bakwata na serikali itabidi itake isitake ishirikiane nacho hicho chombo) nakama hiyo itakuwa basi chombo hicho ndicho kitahusika na walfare ya waisilamu na uisilamu jambo lolote ambalo litaonyesha kuwakandamiza(au interests zao)
waisilamu au uisilamu litapingwa.
Pili Kadhi court haikuandikwa kwenye katiba ,ila serikali kupitia Bunge inatakiwa kuipitisha nakuikubari kama chombo cha Kiisilamu,na hiyo ndiyo nilisema ndio TATIZO kwani baada ya hapo BAKWATA will be out of the picture.
Serikali haitaki kuipoteza bakwata kwa sababu kadha wa kadha ikiwa kubwa ni chombo kilicho undwa na J.K.Nyerere baada ya kuvunja EAMWS kwa sababu zake za KIHISTORIA.
Tatu,ili ibada itimie kwa muisilamu mambo kama ndoa,mirathi,taraka na mfumo mzima wa maisha ya musilamu baada ya swala na dhaka nilazima yafatwe kama ilivyo takiwa ndani ya qurani na wanotaka kufahamu kwani si wote wenye kujua wanenda kwa KADHI ambaye ni msomi wa hari ya juu katika dini kwa maelezo ya ufasaha.
Mwisho,hizo habari za kunyongwa,mijeredi na kupigwa mawe ni Utawara wa SHARIA ambacho ni kitu tofauti na mahakama ya KADHI.