Mzee mwanakjj, andaa makala baba tuimalize hii issue kwa hoja. Wanaotaka kuliongelea suala hili kwa jazba waache waendelee, ni haki yao ya msingi humu JF.
Ladies and gentlemen JUST SAY NO!!!!!.
Hivi wengine nao wakisema just say YES itakuwaje?!! Tunataka YES or NO that has strong or at least reasonable supporting evidence.
Muslims are about 50% of TZ populace, their voice can not be ignored just by saying NO!!!! NO can not stand alone, it is not enough if it is not supported by facts.
Leo nimesikia kuwa eti kuna kundi la waislamu wanataka serikali isitishe uhusiano na VATICAN. Mwafikiri itatosha mtu aseme JUST HALT diplomatic relationship with vatican?? Alaa, ujinga gani huo??
Kesho pengine tutasikia wengine wakisema nao wanataka Ijumaa iwe siku ya mapumziko, hivyo serikali iamue kuwa na siku 3 za mapumziko au wafute moja kati ya J2 na Jumamosi, tutasemaje??? Nao wakitaka ofisi za serikali na mashirika ya umma zipambwe siku za EID kama zinavyokuwa kipindi cha X-MAS itakuwa udini??? Na mwingine akitaka mwaka mpya uwe kwa kalenda ya kiislamu itakuwaje???
Japo katika makala yake mwanakjj aliwalaumu wale mashekhe waliohojiwa katika Jenerali on Monday, kwa kuwaomba waislamu wawe watulivu, ukweli ni kuwa wale mashekhe kwa kauli yao ile wameitendea jambo jema sana nchi yao. Waislamu hawana subira pale wanapoona haki yao inachezewa (zaidi mtu anapotoa maneno ya kashfa kwa mtume na mwenyezi mungu). Nina hakika Mwanakjj alitumia busara kuelezea vile akijua fika kuwa kwa kuficha ukweli huo ingeimarisha subira ya waislamu katika jambo hili.
Yawezekana kabisa, kuwa si waislamu wote wanaotaka mahakama ya kadhi lakini ikumbukwe kuwa Unapozungumzia watu takribani 20 milion, moja ya kumi tu ya asilimia yao moja itatosha kuleta vurugu kubwa watakapoamua kuingia mitaani.
Hapa ndipo napoungana na mwanakjj, kuwa haya mambo yanahitaji hoja zilizo wazi, busara na hekima kuliko jazba. Ni vizuri tukalizungumzia suala hili tukiwa kitu kimoja badala ya kuwa SISI na WAO. SISI na WAO inapendeza tu tukiwa tunaizungumzia kwenye blogu, magazeti, TV, maofisini na sehemu kama hizo, ikifikia SISI na WAO mitaani ni Janga kuu la kitaifa!!!
Bado nina amini kuwa waTZ wanajali na kuthamini uhuru na amani tuliyonayo. Itachukuwa muda na nguvu nyingi kuvunja hazina hizo za nchi, hata hivyo tunawajibika kwa pamoja kuzilinda kwa gharama yoyote kwani hakuna kitu chenye thamani yake!!!