Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Wewe naona umeshindwa kujitetea! Sasa unarukia hoja za watu tu. Zijibu basi hoja zangu kama kweli ni "nyepesi, nyepesi".

Siwezi kujibu hoja ambazo hazipo, wewe hapa huna hoja ila hoja ilikuwa ni ya Mwanakijiji, aliyesema kuwa Katoliki ina mahalkama zake! ndio poiint ya msingi pale sio anything else!

Ndio Vatican na Catholic Church viko joined at the hip, lakini kusema vatican ina mahakama ni tofauti na kusema Kanisa lina mahakama.

Kwazna ufafanue Vatican ni nini na Katholic ni nini?

Marekani ina mahakama, je sheria za mahakama hiyo zinaweza kukugusa mtanzania ambaye upo nchini mwako? Na zaidi ya hilo tunatoa kodi yetu kuendesha hiyo mahakama? Hapana.

Ndio maana Mwanakijiji, akasema kuwa ina mahakama zake, sio za dunia wala zetu, vipi una matatizo ya kuelewa maana ya maneno, "zake" huelewi maana yake ni nini?

Basicly hiyo point ya vatican kuwa na mahakama ni irrelevant kwenye sababu za kuanzisha mahakama ya kadhi.

Only kwa mtu mwenye uwezo mdogo wa kuelewa, lakini kwa mwenye uwezo mkubwa, ni kitu kidogo sana yaani kuanzishwa kwa mahakama hizo za Kadhi bila kelele, hakukuwa na asababu ya kupiga kelele mpaka bungeni!
 
Inabidi kwanza tukubaliane kuhusu maana ya mahakama. Kang yuko sahihi kwenye hili. Kilichoko kwenye makanisa ya Anglikana na Katholiki si Mahakama bali ni mifumo ya kuwekana sawa. Mahakama ni ya kudumu na inasimamia sheria. Dini katika secular states hazina sheria bali kanuni na miongozo kwa waumini wake. Muumini asipozifuata si kosa la jinai na sana sana hatua anayoweza kuchukuliwa ni kunyang'anywa uanachama wa hiyo jumuia. Lakini Vatican kama nchi ina sheria zake na askari wa kuzisimamia. Hizi sheria zinatumika kwenye nchi ya Vatican na si kwingineko. Mkatoliki anayekosea hapelekwi nchini Vatican bali kwa kiongozi wa dhehebu la wakatoliki anayeishi Vatican. Ndiyo maana yule Kaadinali mzambia alichoishia kufanywa ni kutengwa na sio kufungwa. Na hivi hivi kwa waanglikana. Uamuzi wa mwisho ni wa askofu mkuu wa jimbo lako. Askofu wa Canterbury hana mamlaka juu ya waumini wasioishi kwenye jimbo lake. Na ndiyo maana hana uwezo wowote wa kuwachukulia hatua Episcopals wa Marekani walipochagua shoga kuwa askofu. Si mahakama kilichopo huko.

Ndugu zetu wanachotaka kufanya ni kugeuza zile kanuni na miongozo inaowaongoza iwe sheria ambayo itasimamiwa na mahakama. Hapo kwangu mimi ndipo kwenye utata. Ina maana kuwa kutakuwa na mikondo miwili ya sheria nchini na sijui nani atakayeamua ipi inastahili kufuatwa, na nani na wakati gani. Je ataruhusiwa mtu ambaye ni muislamu (kwa kuzaliwa) kuikataa? Je katika masuala ya ndoa kama kila upande itapendelea sheria zake, ipi ita'prevail'? Na ufafanuzi wa nani wa hizi sheria utakaokuwa codified? Sheria ni lazima iwe inaeleweka sawasawa na wote wanaohusika ama sivyo itakuwa balaa. Pakitokea tofauti za interpretation ni chombo gani kitakachokuwa msimamizi wa mwisho? Na kadhalika na kadhalika.
 
Wewe sasa mchokozi!

1. Hizi mahakama zinatambuliwa na sheria za nchini mwetu?

2. Ziko katika katiba ya nchi?

3. Au ni kwa ajili ya wakatoliki na asiyetaka kuzitumia (hata kama ni mkatoliki) halazimishwi?

Haya ndio maneno uliyoyasema, as opposed na maneno ya Mwanakijiji kuwa Katholic ina mahakama zake, sio za dunia au za Tanzania,

neno zake inamaliza maswali yako yote kuhusiana na swali lako la mahakama hivyo kutambuliwa nchini kwetu, itatambuliwaje kwetu wakati ni mahakama ya Katholic?

Hoja yoyote ikiwekwa hapa JF, inatakiwa kuchangiwa na kila mtu ukitaka kumalizana na mtoa hoja basi labda mfanyie kwenye PM, kama sijaridhika na majibu au maswali ni haki yangu kuongeza hoja au majibu, that is all nothing personal ndio maana ya forum!
 
Hoja yako ya msingi kuacha hayo mengine ni hii:-

Mimi sijakuelewa. Nilidhani mahakama ili iwe functional ni lazima itambulike na sheria za nchi ilipo. Ama sivyo ni makubaliano tu ya jamii yasio na uzito wowote kisheria!

Nilichosema kule nyuma ni hiki hapa chini:-

Mahakama za Vatican, kuwa functiionable sio lazima zitambuliwe na sisi Tanzania, na hata hizo za Tanzani zikikubaliwa sio lazima zitambuliwe na Vatican, lakini haina maana kuwa hazitatambuliwa kama mahakama popote zilipo, kulingana na sheria za lile taifa!
Ahsante Mkuu!
 
neno zake inamaliza maswali yako yote kuhusiana na swali lako la mahakama hivyo kutambuliwa nchini kwetu, itatambuliwaje kwetu wakati ni mahakama ya Katholic?

Kwani hao katholics si raia wa nchi hii? Kutotambuliwa kwake hakuhusiani na kuwa ni ya katholiks bali msimamo wetu wa kutenganisha dini na masuala ya serikali. Dini si sehemu ya dola. Ikiwa hivyo tunakuwa theocracy na si secular kama tulivyo.

Hapana Mkuu. Kati ya mimi na wewe kuna personal issues. Hamna haja ya kuficha.
 
Last edited:
Inabidi kwanza tukubaliane kuhusu maana ya mahakama. Kang yuko sahihi kwenye hili. Kilichoko kwenye makanisa ya Anglikana na Katholiki si Mahakama bali ni mifumo ya kuwekana sawa. Mahakama ni ya kudumu na inasimamia sheria.

Hapa uko sawa, tatizo ni kwamba mahakama ya Katholic inatambuliwa kisheria na Vatican, kwa hiyo in te case ya Vatican na Katholic hoja yako hai-apply.

Dini katika secular states hazina sheria bali kanuni na miongozo kwa waumini wake. Muumini asipozifuata si kosa la jinai na sana sana hatua anayoweza kuchukuliwa ni kunyang'anywa uanachama wa hiyo jumuia.

Hapa sawa sawa kabisaa na ndio maana ninashangaa hii hoja ya mahakama ya kadhi kwenda bungeni, hakukuwa na ulazima kwa sababu hatutazitambua kisheria hizi mahakama za kidini!.

Lakini Vatican kama nchi ina sheria zake na askari wa kuzisimamia. Hizi sheria zinatumika kwenye nchi ya Vatican na si kwingineko. Mkatoliki anayekosea hapelekwi nchini Vatican bali kwa kiongozi wa dhehebu la wakatoliki anayeishi Vatican. Ndiyo maana yule Kaadinali mzambia alichoishia kufanywa ni kutengwa na sio kufungwa. Na hivi hivi kwa waanglikana. Uamuzi wa mwisho ni wa askofu mkuu wa jimbo lako. Askofu wa Canterbury hana mamlaka juu ya waumini wasioishi kwenye jimbo lake. Na ndiyo maana hana uwezo wowote wa kuwachukulia hatua Episcopals wa Marekani walipochagua shoga kuwa askofu. Si mahakama kilichopo huko.

Uamuzi wa mahakama ya Katholic unatambuliwa na sheria za Vatican, ni tofauti kabisa na Angilcana ambao hawana nchi ya kuwatambua kisheria.

Ndugu zetu wanachotaka kufanya ni kugeuza zile kanuni na miongozo inaowaongoza iwe sheria ambayo itasimamiwa na mahakama. Hapo kwangu mimi ndipo kwenye utata. Ina maana kuwa kutakuwa na mikondo miwili ya sheria nchini na sijui nani atakayeamua ipi inastahili kufuatwa, na nani na wakati gani. Je ataruhusiwa mtu ambaye ni muislamu (kwa kuzaliwa) kuikataa? Je katika masuala ya ndoa kama kila upande itapendelea sheria zake, ipi ita'prevail'? Na ufafanuzi wa nani wa hizi sheria utakaokuwa codified? Sheria ni lazima iwe inaeleweka sawasawa na wote wanaohusika ama sivyo itakuwa balaa. Pakitokea tofauti za interpretation ni chombo gani kitakachokuwa msimamizi wa mwisho? Na kadhalika na kadhalika.

Hapa ninaungana na wewe kwa 100%.
 
Hoja yako ya msingi kuacha hayo mengine ni hii:-



Nilichosema kule nyuma ni hiki hapa chini:-

Mahakama za Vatican, kuwa functiionable sio lazima zitambuliwe na sisi Tanzania, na hata hizo za Tanzani zikikubaliwa sio lazima zitambuliwe na Vatican, lakini haina maana kuwa hazitatambuliwa kama mahakama popote zilipo, kulingana na sheria za lile taifa!
Ahsante Mkuu!

Hapa si una'state the obvious? Zitakuwaje mahakama kama hazitambuliwi na sheria za taifa zilizopo? Kwani ukisema hizo za tanzania zikikbaliwa una maana gani? Kukubaliwa na nani kama sio na sheria za Tanzania?
 
Kwani hao katholics si raia wa nchi hii? Kutotambuliwa kwake hakuhusiani na kuwa ya katholiks bali msimamo wetu wa kutenganisha dini na masuala ya serikali. Dini si sehemu ya dola. Ikiwa hivyo tunakuwa theocracy na si secular kama tulivyo.

Wanaweza kuwa raia wa nchi hii, lakini wakihukumiwa na Katholic na ile hukumu kutambuliwa na Vatican, ni lazima tufuate, kwa mfano m-Tanzania aliyekuwa Askofu wa Katholic amehukumiwa na mahakama ya Katholic na kutolewa uaskofu, sisi Tanzania hatuwezi kusema kuwa tunamtambua bado kuwa ni askofu na kumpa haki a uaskofu, sasa kwa kufanya hivyo tunakuwa tunaheshimu uamuzi wa mahakama ya Katholic, lakini haina maana kuwa sasa dini imekuwa sehemu ya dola hapa kwetu.

Hapana Mkuu. Kati ya mimi na wewe kuna personal issues. Hamna haja ya kuficha.

Hizo personal ishus ni wewe ndiye unazo against mimi, kama ulivyojionyesha this week, lakini mimi kila siku ya Mungu nina deal na watu wengi sana sina muda mwingi wa kukumbuka ishus za jana na zinamhusu nani,

mimi ninakuja hapa kukata ishus za taifa bila kujali upande wa pili kuna nani, nitakuwa mwehu kuwa na personal ishus na mtu kwenye internent tena nisiyemjua, that is insane! mimi ni kukata ishus tu toka siku nilipoingia hapa, uliponikuta na mpaka leo, wembe wangu ni ule ule tu!
 
Uamuzi wa mahakama ya Katholic unatambuliwa na sheria za Vatican, ni tofauti kabisa na Angilcana ambao hawana nchi ya kuwatambua kisheria.

Unachanganya ukatoliki na nchi ya Vatican. Kwa vile Papa ni kiongozi wa Vatican hakumaanishi kuwa wakatoliki wote ni raia wa Vatican. Kutambuliwa na sheria za vatican hakuna maana yeyote kwa mkatoliki raia wa Tanzania. Kuna maana tu kama muumini na sio kama raia!
 
mimi ninakuja hapa kukata ishus za taifa bila kujali upande wa pili kuna nani, nitakuwa mwehu kuwa na personal ishus na mtu kwenye internent tena nisiyemjua, that is insane! mimi ni kukata ishus tu toka siku nilipoingia hapa, uliponikuta na mpaka leo, wembe wangu ni ule ule tu!

Huu ni uongo, Mkuu. Kwani Kuhani unamjua? Lakini tuyaache yalivyo na tuendelee na mjadala.
 
Hapa si una'state the obvious? Zitakuwaje mahakama kama hazitambuliwi na sheria za taifa zilizopo?

Neno mamhakama hsa nothing to do na kutambuliwa au kutotambuliwa na sheria za local, kijijini kwetu mtu akishikwa na wizi hufikishwa kwenye mahakama ya wananchi, ambayo mzee anyeheshimiwa kijijini huamua yule mwizi afanyiwe nini, serikali haitambui hizi mahakama, lakini haina maana kuwa sio mahakama kwa maana ya mahakama.

Kwani ukisema hizo za tanzania zikikbaliwa una maana gani? Kukubaliwa na nani kama sio na sheria za Tanzania?

Off course kukubaliwa na Tanzania, maana yake ni kisheria za jamhuri yetu, na ndio naamini kuwa ni sababu ya hii ishu ya kadhi kupelekwa bungeni, ninaamini kuna mtu anyetaka kutambuliwa kwa hizi mahakama kisheria pia.
 
Unachanganya ukatoliki na nchi ya Vatican. Kwa vile Papa ni kiongozi wa Vatican hakumaanishi kuwa wakatoliki wote ni raia wa Vatican. Kutambuliwa na sheria za vatican hakuna maana yeyote kwa mkatoliki raia wa Tanzania. Kuna maana tu kama muumini na sio kama raia!

Wa-Katholic wote makao makuu ya uumini wao upo Vatican, ambako kuna mahakama inayoweza kutoa hukumu kwa a Katholic kiongozi na ile hukumu ikatambuliwa na serikali yetu.
 
Huu ni uongo, Mkuu. Kwani Kuhani unamjua? Lakini tuyaache yalivyo na tuendelee na mjadala.

I have no clue kabisaa, umesema who? yaani ni member wa hapa au?

okay kesho mkuu naingia kulala!
 
Wanaweza kuwa raia wa nchi hii, lakini wakihukumiwa na Katholic na ile hukumu kutambuliwa na Vatican, ni lazima tufuate, kwa mfano m-Tanzania aliyekuwa Askofu wa Katholic amehukumiwa na mahakama ya Katholic na kutolewa uaskofu, sisi Tanzania hatuwezi kusema kuwa tunamtambua bado kuwa ni askofu na kumpa haki a uaskofu, sasa kwa kufanya hivyo tunakuwa tunaheshimu uamuzi wa mahakama ya Katholic, lakini haina maana kuwa sasa dini imekuwa sehemu ya dola hapa kwetu.

Unachanganya mambo. Serikali ya Tanzania haimpi mtu haki ya uaskofu bali ni lile kanisa linalotoa haki hiyo. Serikali inamtambua kiongozi yeyote wa jumuia halali aliyekubalika na hiyo jumuia, iwe ya kidini, michezo na kadhalika. Ndiyo maana Balozi wa vatican anatambuliwa kama mwakilishi wa nchi ya Vatican na sio kama kiongozi wa dhehebu la wakatoliki. Uongozi wake katika dhehebu hilo ni kati yake na waumini wa dhehebu hilo na si serikali. Huyo Askofu aliyetemwa na wakatoliki akianzisha dhehebu lake na kupewa uaskofu na dhehebu hilo bila shaka serikali itamtambua kama askofu bila kujali mtazamo wa Vatican. Kwa maneno mengine Vatican haiwezi kuikataza serikali ya Tanzania kumtambua kwa vile tu wao wamemtema. Itakachoweza kufanya ni kumkataza kujiita mkatoliki maana hiyo ni trade mark yao!
 
Unachanganya mambo. Serikali ya Tanzania haimpi mtu haki ya uaskofu bali ni lile kanisa linalotoa haki hiyo.

Sikusema haya!

Serikali inamtambua kiongozi yeyote wa jumuia halali aliyekubalika na hiyo jumuia, iwe ya kidini, michezo na kadhalika. Ndiyo maana Balozi wa vatican anatambuliwa kama mwakilishi wa nchi ya Vatican na sio kama kiongozi wa dhehebu la wakatoliki.

Hapa unachanganya ishu, askofu wa Katholic na balozi wa Vatican ni vitu viwili tofauti kabisaaa!

Uongozi wake katika dhehebu hilo ni kati yake na waumini wa dhehebu hilo na si serikali. Huyo Askofu aliyetemwa na wakatoliki akianzisha dhehebu lake na kupewa uaskofu na dhehebu hilo bila shaka serikali itamtambua kama askofu bila kujali mtazamo wa Vatican. Kwa maneno mengine Vatican haiwezi kuikataza serikali ya Tanzania kumtambua kwa vile tu wao wamemtema. Itakachoweza kufanya ni kumkataza kujiita mkatoliki maana hiyo ni trade mark yao!

Akitemwa na Vatican ni lazima serikali iheshimu hilo, lakini akingiia tena kanisa lingine ni another ishu, ambayo sikuisema kabisaa.
 
Hoja ya mahakama ya kadhi haina lengo la mwendelezo wa ibada kwa waislamu,lengo kuu hapa ni mwendelezo wa NIA ya yule Rais aliyetaka kuifanya Tanzania iwe The United Islamic Republic Of Tanzania,kwa bahati nzuri wasomi wakamshtukia.

Kuweni makini,tafuteni mizizi ya udini ndani ya nchi hii,then mtapata pa kuanzia.
 
Padre Karugendo na Dr. Slaa wanaijua vizuri VATICAN. Watusaidie kidogo. Nadhani Serikali inachelewesha kuruhusu Mahakama ya Kadhi irudi tena Nchini. Tukajifunze tu kwa wenzetu hapa jirani zinafanyaje kazi. Kujifanya Serikali yetu haina DINI sio kigezo na nadhani sio kweli sana. Naziona BIBLIA na KORANI hadi Ikulu zinatumika wakati wa VIAPO.
BUNGENI kila siku wanaanza na SALA/SWALA?
 
sasa wakileta hoja ya Ubalozi mbona tunazo balozi za jamhuri za Kiislamu kama Morocco, Libya na Iran? Na kwa upande wa Iran kiongozi wake ni Ayatollah?

Kaka unajua zaidi ya hili. Hizi ni balozi za mataifa (sovereign states) na sio balozi za asasi za kiimani kama ilivyo VATICAN. Ndio maana hata katika UN Vatican ina status tofauti na Tanzania ama IRAN......

Sina tatizo na kuwa na ubalozi wa VATICAN popote pale lakini si busara kwa mtu kama wewe kuingia kwenye hii tone ya ushindani iliyojaa ubabaishaji badala ya kuendelea kuwa objective kama ulivyoanza hapo mwanzoni....hizi arguments za kiushindani/kipinzani zina wenyewe....na wewe si mmojawapo....waachie kina mtikila, mrema na bassalehh na wa aina yao humu barazani...

Tanzanianjema
 
Mimi sioni ubaya kukiwa na taasis au mfumo wa kuendeleza ibada..swala ninaloliona linaleta utata ni bajeti.. Mahakama y akadhi ikihuishwa kwenye mfumo wa serikali maana yake itabidi serikali iwajibike kwa kila namna. Je walipa kodi wasio wa dini husika kwanini wachangie? Mahakama hizo zinapaswa kujitegemea bila kutumia pesa za serikali.

Acheni ubinafsi huo jamani, serikari inawajibu wa kuhudumia makundi mbalimbali ya kijamii ya kitanzania. Halafu mbona waislamu kwa miaka yote hapa nchini wanafanya kazi Ijumaa wakati ni siku yao ya kuabudu? Msiogope kukatwa mikono na kupigwa mawe mahakama ya kadhi ni maalumu kwa waislamu tuu. Mbona kenya ipo na hatujasikia malalamiko kama mtoayo nyie? Zaidi ya hoapo ilikuwepo tangu enzi za mkoloni wa kiingereza ila ilitilewa kiujanja baada ya uhuru mwaka 1963.
 
Hoja ya mahakama ya kadhi haina lengo la mwendelezo wa ibada kwa waislamu,lengo kuu hapa ni mwendelezo wa NIA ya yule Rais aliyetaka kuifanya Tanzania iwe The United Islamic Republic Of Tanzania,kwa bahati nzuri wasomi wakamshtukia.

Kuweni makini,tafuteni mizizi ya udini ndani ya nchi hii,then mtapata pa kuanzia.

Fikira duni kama hizi ndio tatizo na sio mahakama ya kadhi ama ubalozi wa Vatican......

Kwa wanaodai kuwa wakristu nao wapewe nafasi ya kutumia canon laws atafute msomi wa Jurispudence amfafanulie kuhusu misingi na asili ya mfumo wa sheria tunaotumia halafu ndio ajenge hoja zake.......

Kingine jamani tunapofuta uhalali wa hoja zetu tujitahidi kutafuta personalities za kutumi kama references.....huwezi ukamchukulia fashisti kama mtikila ama bassaleh kuwa kiongoza muono chako katika kutetea tanzania ya wote.....

Tanzanianjema
 
Back
Top Bottom