Originally Posted by Dr.Khamis
Mzee Mwanakijiji Tanzania kuna Mashekhe wa aina mbali mbali na wengi wao wamesoma tu Quran lakini kwa bahati mbaya hawakusoma Biblia au Turat(Torah).
1.Ndoa kwa mfano imelezwa vizuri ni nani mtu aoe na ni wake wangapi. Vile vile talaka pia zimelezwa katika Quran na jinsi zinzvyotolewa.
Kuelezwa vizuri katika Quran si hoja kuwa kusikuwepo mahakama ya kadhi,ikumbukwe hii field pana kama zilivyo zingine katika Quran na hadith,kuna ambao wana PhD katika hiyo field.Kadhi ni mtu mwenye hiyo taaluma na anahukumu kwa mujibu wa mafundisho na mazingira ya tukio husika.
2. Sasa Muislamu akioa mke wake wa Kikristo/Kiyahud katika ofisi ya Kiserikali inayohusika na ndoa hiyo Mahakama ya kadhi haitaitambua ndoa hiyo
?
Bro ...hapo naomba ufikirie vema uone pumba ipo wapi.
3. Kama Muslamu ana Life Insuarance yake na akafariki hiyo Mahakama ya kadhi itawarithisha vipi mke na wanawe?
4.Sheria za Life Insuarance zinataka mke apewe urithi na watoto. Lakini pengine aliyefariki ameandika statement maalum kuhusu urithi wake basi hiyo statement itafuatwa na Kampuni ya Life Insuarance kwa vile huo ndio WASIA WA MWENYEWE.
Insurance kama ni sehemu halali ya marehemu itagaiwa kama mali zingine kwa mujibu wa sheria husika.........Bro,katika vitu vya mwanzo vinavyozingatiwa katika mirathi kwa mujibu wa uislam ni WASIA WA MAREHEMU......hapa unahitaji kwenda shule juu ya hilo.
5. Katika Quran amendikwa kwamba mtu ukiona kwamba pengine siku zako za kufa haziko mbali umuachie mkeo posho la mwaka mmoja. Wangapi wanafanya hivi?
Bro,hapo naomba ushahidi wa hiyo aya katika Quran...pia kama kuna maelezo yoyote ikiwa huyo marehemu hakuwa na hilo posho mwaka inakuwaje?
6.Watanzania wangapi ambao wanaifuata Quran kama inavyotakiwa?
Dah...,Bro,hii ni challenge kwangu...nashukuru sana kunikumbusha,ALLAH atujalie kuifanyia kazi.
7. Kuna vitu vingi ambavyo Mwenyenzi Mungu amevirahisha kwa waja wake. Kwa mfano mtu mwezi wa Rammadhani akiwa safarini anarusiwa kula na akirudi kwakwe azilipe zile siku ambazo hakufunga. Pia swala ya aduhuri na alaasiri anaweza kuzijumlisha akiwa safarini , Ishaa na Maghribi pia
.
Hapo umepatia....hizo aya zapatikana katika Suratul Baqara,ingawa kwa mwenye kutaka kutekeleza hiyo rukhsa akiwa safarini(akiwa mgonjwa kwa case ya kufunga Ramadhani) anahitaji maelezo ya namna ya kufanya....yaani ajue anajumlishaje hizo alasiri na adhuhur(kwa mfano)
8.Kama mwenyewe Mnyenzi Mungu amarahisisha vitu kwa waja wake kwa nini sisi Watanzania tunataka kuvifanya vigumu?
Hapa ndugu taratibu kidogo.....kuna speficity katika utekelezaji wa ibada,sio mtindo wa logic....,mwanamke akiwa katika hedhi ni rukhsa kutoswali na hatakiwi kulipia ile swala ilyompita,lakini hata mtu uwe mgonjwa vipi maadam unafahamu(uko conscious) watakiwa uswali...sasa ukianza kuleta logic...utauliza swali..kwa nini mwenye hedhi ambaye ni mzima kiafya asiswali na huyu mgonjwa alazimike kuswali....,kurahisishiwa katika moja haina maana ni the same katika lingine.
9.Watanzania wangapi wanafuata Sunna za Mtume?,Waulize hao Mashekhe wa Tanzania Mtume Muhammad (S.A.W) alikuwa akiamka usiku na kuswali rakaa 11 za Swalat TAHJUUD na kumalizia na swala ya WITRI kabla ya swala ya Alfajiri(Asubuhi), ni wangapi kati ya hao Mashekhe wanaofanya hivyo?
Hii ni challenge nyingine......nimeipokea,shukran tena.......ALLAH atuongoze katika hili
TUSIVURUGE NJI KWA SABABU YA KUUNDA MAHAKA YA KWANZA!
Sifikirii kwamba litachukua sura hii......
OBEY THE PROPPHET (Muhammad (S.A.W)) AND OBEY THOSE IN POWER.hii ni aya mojawapo katika Quran. Those in Power hapa ni serkali na mahakama yake.
Yap...hii ni quotation sahihi,kuwa na hiyo mahakama hakuendi kinyume na hii quotation kabisa...hii inatufundisha kuwa tunapokuwa katika chini ya mamlaka fulani..hata kama si ya kiislam tunatakiwa tutii viongozi wa pale so long kuwa hawatutoi katika uislaam ama kutuzuia na ibada....na ndio maana hata hizi habari za maandamano and the like kama kuchochea vurugu n.k ni vitu ambavyo kwa uelewa wangu wa uislam ni vya kupingwa...napongeza hatua zinazochukuliwa katika kuendea hili suala la kadhi kuwa si kwa kutumia fujo(kwa mujibu wa thread hii...maana siko Tz sijui inakuaje)