Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,287
- 10,390
Acheni ubinafsi huo jamani, serikari inawajibu wa kuhudumia makundi mbalimbali ya kijamii ya kitanzania. Halafu mbona waislamu kwa miaka yote hapa nchini wanafanya kazi Ijumaa wakati ni siku yao ya kuabudu? Msiogope kukatwa mikono na kupigwa mawe mahakama ya kadhi ni maalumu kwa waislamu tuu. Mbona kenya ipo na hatujasikia malalamiko kama mtoayo nyie? Zaidi ya hoapo ilikuwepo tangu enzi za mkoloni wa kiingereza ila ilitilewa kiujanja baada ya uhuru mwaka 1963.
Wakristu wanapumzika jumapili si kwa vile ni siku yao ya kuabudu bali imani yao inasema kuwa wafanye kazi siku sita na ya saba waitenge kwa KUPUMZIKA na kumuabudu mungu. Kama vile ilivyo Sabbath kwa wayahudi ambapo hata kupika siku hiyo hakuruhusiwi. Sidhani kama waislamu wanakatazwa kufanya kazi siku ambayo wanaabudu! Vile vile sidhani kuwa kuna sheria inayomkataza mtu kufanya kazi jumapili na kupumzika ijumaa. Ni utaratibu tu ambao shirika au mtu aliyejiajiri anaweza kuufuata.
Kabla ya kutumia suala la Kenya kama mfano, ni lazima tuangalie mazingira yaliyopelekea mahakama hizo kuanzishwa na kama hayo mazingira na sababu yapo kwetu hivi sasa.