JMUSHI1, MC na wengine:
Kwanza wanabodi nawasalimia nyote munaonifahamu na musionifahamu kwani ni muda mrefu sana sikuwa nikiandika bali niliamuwa kuwa mtazamaji tu baada ya kuona ushabiki umezidi nani atachaguliwa na nani...
Sasa nikirudi ktk ujumbe wangu wa kuunga mkono tamko la viongozi wa Kiislamu dhidi ya Serikali nadhani baadhi yenu munaufahamu mdogo sana juu ya uhusiano baina ya Serikali na Vatikano kwa upande mmoja na mahusiano na Serikali zenye kuongozwa Kiislamu! kwa kweli kama mutakuwa munajibu hoja kiushabiki shabiki bila ya uchunguzi basi hii inathibitisha mapungufu fulani!
Waislamu wanazungumzia kusitishwa uhusiano ulio rasmi na Vatikano yaani Serikali kuwa na uhusiano wa kiBalozi! sasa munaposema Kama Serikali itasitisha uhusiano na Kanisa Katoliki basi haina budi kusitisha uhusiano na Serikali za Saudia, Iran au Sudan!!!! POINTLESS!!!!!
Kama munakumbuka Miaka 7 iliyopita Maaskofu wa Baraza la Kanisa la Pentekoste la Tanzania(PCT), walitoa kitabu kinachoitaka serikali iitishe kura ya maoni kwanza, kabla ya kuamua kujiunga na Jumuiya ya Mkutano wa Kiislamu, (OIC), ili kupata ridhaa za Watanzania.
Kitabu hicho, kilichopewa jina la "Amani katika Tanzania italindwa kwa:kutenganisha Dini na Mamlaka ya nchi", kinaeleza kuwa kitendo cha serikali ya Tanzania kutaka kujiunga na OIC si jambo dogo. Nijambo linalowahusu Watanzania wote, Waislamu na wasiokuwa Waislam, na hata wale wasiokuwa na dini yo yote.
Kwa mujibu wa kitabu hicho inaelezwa jambo hilo, halifai kujadiliwa kijuujuu tu, kwa kupitia katika vyombo vya habari, na wala haifai kuachiliwa Bunge peke yake kuamua juu ya jambo zito kama hilo.
Halmashauri Kuu ya Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, kwa kupitia katika kitabu hicho, imesisitiza serikali iitishe kura ya maoni ili ipate kuelewa msimamo wa Watanzania wote, wa dini mbalimbali, juu ya jambo hilo.
Katika kutaka kufafanua zaidi juu ya jambo hilo, Halmashauri hiyo imesema, "Lakini si kazi ya Bunge kutunga sheria za kidini, kwa kuwa OIC ni taasisi ya kidini, ni muhimu taasisi nyingine za kidini zilizopo hapa nchini nazo zishirikishwe kikamilifu katika uamuzi mzito kama huu."
Kwa ufupi, Maaskofu wa Kanisa la Pentekoste, katika kitabu hicho, wametilia mashaka uhusiano huo kama utaanzishwa. Wamedai kuwa lengo la misaada inayotolewa na taasisi hiyo ni kwa ajili ya kutaka kueneza imani ya dini hiyo katika nchi wanachama. Maaskofu hao wamesema kuwa kama Tanzaniai tajiunga na taasisi hiyo basi itakuwa ni sawa na kuwasilimisha Watanzania bila ya nidhaa yao!
Inaonekana kuwa kitabu hicho kimetolewa na Kanisa la Pentekoste, kama ni onyo kwa serikali isijiunge na OIC, baada ya kumsikia mgombea wa kiti cha urais wa Zanzibar mwaka 2000, kwa tiketi ya CCM, Rais Amani Karume katika madahalo ulioandaliwa na shirika la utangazaji la BBC, akisema kuwa serikali imekwishafanya utafiti na imeona kuwa Tanzania ijiunge na taasisi hiyo, kwa kupitia serikali ya Muungano, na siyo kupitia serikali ya Zanzibar.
Kwa vyovyote vile, mtazamo huo wa Maaskofu, umekosa uadilifu kama ulivyo msimamo wenu hapa wanabodi. Ni mtazamo ulioelekezwa katika kuuangalia upande mmoja tu wa shilingi na kuupuuzia upande wa pili. Ni mtazamo chongo! Ni sawa na mtu mwenye macho mawili lakini akaamua, kwa makusudi, kufumba jicho moja na kuangalia kwa jicho moja.
Kama serikali ya Tanzania haifai kujiunga na OIC, bila ya kuitisha kura ya maoni, eti kwa sababu OIC ni taasisi ya kidini; basi lazima tukubali kuwa kwa hoja hiyohiyo, serikali hiyo ya Tanzania itakuwa imefanya kosa kuanzisha uhusiano, tena wa kibalozi, na Vatikano, ambayo ni taasisi ya kidini, na siyo nchi yenye raia! kama vile Saudia na Iran!!
Uhusiano huo wa serikali ya Tanzania na Vatikano, ingawa ni uhusiano baina ya nchi hii na Kanisa Katoliki duniani, lakini jambo la kustaajabisha hakuna yeyote anayehoji juu ya uhusiano huo, si serikali wala makanisa ya Kikristo! tena na nyinyi wana Forum munaendeleza wimbo uleule wa kudai Vatikano ni nchi Kamili! tangu lini Taasisi ya kidini ikawa nchi ndani ya nchi!
Mwaka 1992 Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilitaka kuwa mwanachama wa O.I.C.ili ijikwamue kiuchumi kutokana na misaada na mikopo isiyo na riba inayotolewa na jumuiya hiyo ya Waislamu.
Hatua hiyo ya Serikali ya Mapinduzi ilizua mtafaruku ndani ya Bunge, CCM, Serikali na katika vyombo vya habari, kwamba ililenga kuiingiza Zanzibar katika Sharia za Kiislamu na hatimaye kuisilimisha Jamhuri ya Muungano.Lakini Bunge, Serikali na hasa Mwalimu Nyerere, waliipinga kweli kweli, Mwalimu Nyerere kwa mikutano ya hadhara na ya waandishi wa habari alipinga hatua ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano kujiunga na Shirika la O.I.C.",
Mtu yoyote mwenye akili timamu anatambua O.I.C. haina malengo ya kusilimisha bali kusaidia nchi wanachama wake kuboresha hali za kijamii kama Msumbiji ni nchi yenye Wakiristo wengi lakini ni mwanachama wa OIC wala hakuna anaesilimishwa huko!
Mlokole Bush alipotaka kuitawala Iraq alidai Sadam anasilaha za maangamizi kama anavyodai Mlokole Mtikila kuwa mahakama za Kadhi ni ugaidi na zikianzishwa basi Wakiristo watakatwa vichwa!! upuuzi ule ule kama madai ya BUSH!!
Wakiristo wa TZ inawahusu nini kuanzishwa mahakama za Kadhi? pilipili ziko shamba zawawasha nini? kama Biblia haina sheria za kuhukumia waumini wake kwanini Waislamu wasiruhusiwe kutumia baadhi ya sheria za Kurani kama vile mirathi na ndoa?
Mbona Zanzibar na Kenya mahakama za kadhi zinafanya kazi kwa ufanisi mzuri sana wala hatujasikia watu kukatwa vichwa!!
Tuache udini na tujibu hoja!