Kwa kweli mimi sikuwa najua kama Serikali yetu inauhusiano rasmi wa kibalozi na Vatikano! kwani tangu enzi za Mwalimu nchi yetu ilikuwa haina dini na katiba yetu iko wazi kabisa kuwa Serikali haina dini!
sasa haya yamekujaje tena kwani leo nimesoma gazeti moja linaripoti kauli za viongozi wa Kiislamu kuitaka Sirikali kusitisha uhusiano huo mara moja soma hapa ..http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/11/7/habari3.php na mimi nawaunga miguu na mikono viongozi hao kwa uwamuzi wao na kuwashauri waishitaki Serikali Mahakamani kwa kuvunja katiba ya nchi!
Kabla ya kuishitaki serikali kuvunja katiba ya nchi,
Wajishitaki wenyewe kwanza kwa kutaka kuilazimisha serikali kuvunja katiba ya nchi kuanzisha mahakama ya kadhi! ama ni mkuki kwa nguruwe?
Tangiapo nahisi hapo wanachanganya mambo kwani uhusiano uliopo ni wa kibalozi kama nchi na si uhusiano wa kidini!