Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Kaka Halisi hiyo ndiyo Serikali ya Muungwana!,Hakuna kabisa Ethics za kazi,ukijua kuwa nae karibu basi utapata "Mlo",kashindwa kumsaidia Muhidin Ngurumo tu! ambaye alikesha usiku kucha kutwanga Msongo siku ya Harusi ya JK na Mama Salma,kipindi kile Muungwana alipokuwa Waziri wa Madini.
Kuingia kwenye Teuzi zake ni kuwakaribu nae tu!,wapo wababe wanaopata vyeo kwa kuogopwa,lakini hao ni wachache mno!,kwani nani alimpangia Ali Karume kwenda Italy? au ulisikia wapi kwamba kahamishwa kutoka Germany kwenda Italy? Zipo Teuzi nyingi zinafanyika kimya kimya kama hiyo ya Ali Siwa.

Nilikuwa sijui kama jamaa kao juzi juzi tu......? ama alishawahi kuoa kabla?
 
Papa Benedict XVI kuzuru Tanzania

*Asifu amani na upendo, ataka viendelee kudumu


Na Godfrey Lutego, Vatican City

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Benedict XVI amekubali mwaliko wa Rais Jakaya Kikwete kutembelea Tanzania baadaye na akasifu wananchi wake kwa amani na utulivu licha ya tofauti za kidini na kutaka waendelee kuishi hivyo.

Alisema hayo jana alipozungumza na Rais Kikwete kwenye maktaba yake binafsi makao makuu ya Vatikani, alikomwalika ikiwa ni sehemu ya mwaliko aliompa awali kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa madhehebu ya dini duniani utakaofanyika Napoli, Italia kesho, ulioandaliwa na taasisi ya Mt. Egidio inayojihusisha na masuala ya amani duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari walio kwenye msafara wake baada ya kutoka kwa Papa Benedict XVI, Rais Kikwete alisema katika hoteli ya Exedra alikofikia, kuwa kiongozi huyo alimweleza kufurahishwa kwake na amani na utulivu uliopo Tanzania na jinsi watu wake wanavyoishi kwa upendo, licha ya tofauti za dini mbali mbali zilizopo (
hivi kweli bado JK ana amini Tanzania bado ina AMANI na UTULIVU?).

Rais alisema kiongozi huyo wa Wakatoliki duniani, alimweleza kuwa Vatikani inafurahia uhusiano wa kiserikali na kidini uliopo kati yake na Tanzania, kwani ni kati ya nchi ambazo haziisumbui kuhusu masuala ya amani kutokana na watu wake kuishi vizuri ingawa ni wa madhehebu tofauti ya dini na vyama tofauti vya siasa.

Alisema kiongozi huyo alisema amefurahishwa kuona kuwa viongozi wa Serikali waliomfuatia Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere, wameendelea kudumisha misingi ya amani iliyowekwa naye wakati wa uongozi wake na yeye alimhakikishia kuwa ataendeleza ya watangulizi wake (
si aseme anaendeleza uporaji alioanzisha Mkapa pamoja na ufisadi!), na akamwomba aendelee kuibariki ibaki na amani, naye akaahidi Kanisa litaendelea kuiombea idumu katika amani, upendo na umoja ilionao.

Rais Kikwete alisema walizungumzia pia masuala ya afya na elimu ambapo Papa Benedict XVI alisema Kanisa limeona umuhimu wa elimu ya UKIMWI kujikinga na maambukizi na akaahidi kuendelea kusaidia Serikali katika hilo na elimu kwa jumla.

Alisema katika kuimarisha zaidi uhusiano na Kanisa na hasa Kiongozi huyo ambaye ni mpya akiwa amemrithi marehemu Papa Yohanne Paulo II aliyewahi kuzuru Tanzania, alimwalika Papa Benedict XVI na akakubali, lakini akasema atapanga ziara hiyo wakati atakapopanga kuzuru Afrika baada ya kumaliza ziara ya Marekani aliyokwishaipanga.

"Tumemwomba atutembelee na amekubali. Anasema anajua umuhimu wa Afrika lakini akasema anapanga kwanza ziara ya Marekani. Tunatarajia akipanga ya Afrika, atakuja pia Tanzania. Tulimkumbusha pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Vatikani kuhusu ombi letu tulipokutana naye na akasema lazima Papa atatembelea Tanzania, kwani ina sifa ya pekee katika Kanisa Katoliki duniani, kutokana na kutoa Kardinali wa kwanza Mwafrika, marehemu Mwadhama Laurean Kardinali Rugambwa na Naibu wa Waziri huyo sasa ni Mtanzania, Padri Novatus Rugambwa, anayeshughulikia uhamiaji, hivyo alisema watatufikiria kuwamo kwenye ziara yake," Rais aliwambia waandishi wa habari.

Rais Kikwete alisema alimpatia Papa Benedict IXVI zawadi ya meza ya mchezo wa chess ya mti wa mpingo naye akampa zawadi ya medali ya dhahabu ya Upapa yenye picha yake kwa mbele na maandishi kwa nyuma huku mkewe na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Benard Membe, Waziri wa Chakula na Kilimo, Bw. Stephen Wassira, Waziri wa Utalii Zanzibar, Samia Suluhu Hassan na viongozi waliokuwa kwenye msafara huo wa Rais wakipewa zawadi pia na kusalimiana naye.


Source: Majira
 
Kwa Mungu (Jehova/God) ni kwa wote, hata waujai kama Bush, Osama, hata mafioso kama kina Berlusconi nao ni kwao. Kuna wanaojidai mbele za watu kuwa wao ni wa mungu na wengine si wa mungu hao wanachemsha, Mungu ndiio anajua nani ni wake na nani si wake. Unaweza kushangaa Osama anaweza kuruhisiwa kuingia huko Vatican na Fred Maro akakataliwa, this is world.
 
katika marais, JK katia fora kwa kusafiri. akihesabiwa siku alokuwa nje ya nchi na zile alokuwa ndani ya nchi, za nje ya nchi karibia zitakuwa nyingi zaidi.

JK tatua matatizo ya wananchi wako ndani ya nchi tafadhali, misaada bila ya utendaji ni sawa na mbwa kumbita dog tu
 
akikaa nyumbani maswali mengi bwana, hata ningekuwa mimi kama sina majibu na sina mpango wa kutafuta majibu nifanye nini..? kuyoyoma tu kwa fedha za wapika kula..
 
Hivi ktk hili la kumtembelea Papa hatuoni kuna jambo jema la kukubaliwa kwa mwaliko wa kutembelea Tanzania, basi hatuwezi hata kumpongeza kwa hilo?

Nakubaliana na Kada kwa mwendo huu hata haoi waliokuwa wanaichukulia JF kama serious forum wanaona kumbe ni genge la walalamishi fulani...
 
MI nadhani tungetofautisha mialiko na mapokezi mbali mbali ya Mwungwana na mafanikio yake kama rais. Suala la kumpongeza tumpongeze ya nini? Rais yoyote akimtembelea papa anampa mwaliko na yeye anakubali, whether he goes is another issue. George w. Bush na Tony Blair wote walienda, wakamwalika na alikubali lakini sikumwona akienda! And btw akija Papa it has nothing to do with the sitting president but the expectations and calculations of the Catholic church (i.e. increase its base in Africa and Latin America, as its base dwindles in Europe).
Kuhusu mafanikio ya safari za nje za Mwungwana, sioni kama kuna mafanikio, unless it translates into meaningful investment, reduction in inflation (btw it's through the roof!), etc na vikafanyiwa kazi ndani ya nchi. Otherwise it will be more and more ahadi hewa!
 
NOthing JK is going to do will be worthy it lakini watu katika uhai wa KIKWETE wanaona ubaya wake tu LAKINI SUBIRI siku ATAKAPOFARIKI (simuombei mabaya lakini kila kiumbe kitaonja umauti ) ndio utajua wengi wanafiki na kuanza kulia machozi ya unafiki na wataanza kutaja yote mazuri hata yale yaliyokuwa mabaya ! ama kweli binadamu ni sumu kwa binadamu mwenyewe na hapa JF i prooved that !
 
KadaMpinzani,
Sidhani kama watu wanazungumzia mabaya ya JK ila wanaeleza umuhimu wa hizi safari kwa faida ya nchi.

sawa kaenda kumtembelea Pope lakini isiwe sifa hii maanake kinachotangulia ni kupewa sifa kabla ya hoja pinzani. Kwa hiyo tunapotaka kumsifia inabidi tutazame kinachofuatia kwa maslahi ya Watanzania na kama hakuna sioni sababu ya kumpa sifa, unless kama kungekuwepo na mawasiliano mabaya kati ya Tanzania na Vatican.

Pili, umezungumzia sana kuhusu kijiwe hiki kuwa na negative comment kwa viongozi wetu wakati wewe umesahau kwamba hizi comment zinatokana na utangulizi wa sifa mahala ambapo hapahitaji sifa ila informative.

Hadi sasa hivi sidhani kama kuna mtu anamchukia JK isipokuwa wananchi wapo disappointed kiasi kwamba inampa nafasi kiongozi wetu kurekebisha baadhi ya makosa ama maswala yanayotuhusu. Ikiwa disappointment ni kashfa basi sidhani kama tutaweza wafahamisha viongozi wetu matatizo ktk lugha nyingine..

Kumbuka alivyoingia madarakani, alitembelea wananchi na sehemu ambazo kweli zilihitaji Uongozi wake kuziboresha lakini kipi kimetokea? nothing leo hii hawezi hata kutembelea sehemu hizo kesha zisahau kabisa na lini mara ya mwisho kafika Hospitalini ama huko Kariakoo kuangalia kama kumetokeas mabadiliko yoyote. Pato la mwananchi bado linategemea nje ya mshahara. Kumbuka wakati wa Nyerere wafanyakazi wote waliweza kula ktk migahawa wakitegemea mshahara wao, leo hii kila Mtanzania anakula kwa mama ntilie.. chakula cha Azam ama Chef hakishikiki. Ni mfano mdogo sana lakini unakupa sura ya jinsi maisha yalivyopanda....tunashukuru mitumba bado kuwepo pamoja na kwamba Mwinyi alisema ni swala la dharura.

KadaMpinzani,
JK na viongozi wetu wanatazama nje kabisa ya mahitaji ya nchi yetu. Tanzania inahitaji investment na hatuwezi kuwavuta kama nchi haikuweka misingi bora ktk miundombinu na Policies ambazo zinavuta wawekeshaji ktk nyanja tunazozihitaji.

Ni jukumu letu sisi kufahamu tuinatakiwa kuwa nchi ya aina gani na ndio mikakati yote inaelekezwa huko. Hatuna dira yoyote, hatufahamu kama viwanda, Kilimo ama madini ndio priority kubwa ya Uongozi wetu ila tunawaachia wawekeshaji wao watuamlie wapi tunakwenda. Nchi inajengwa kwa misaada na mapokezi ya kodi zinazotokana na Umalaya.. (kuuza nchi).
Utanisamehe JK kumwona Pope haina sifa ni makruh (waarabu husema) haiongezi wala kupunguza shida za Mwananchi.
 
Miye natoa pongezi kwa JK kwa kumtembelea Baba Mtakatifu na kutoa zawadi kwake.
 
Hivi ktk hili la kumtembelea Papa hatuoni kuna jambo jema la kukubaliwa kwa mwaliko wa kutembelea Tanzania, basi hatuwezi hata kumpongeza kwa hilo?

Nakubaliana na Kada kwa mwendo huu hata haoi waliokuwa wanaichukulia JF kama serious forum wanaona kumbe ni genge la walalamishi fulani...

I am with you on this, nafikiri umefika wakati sasa tutafute exactly nini hasa kazi za rais, na tuziweke hapa, Mzee MMJ, ninakuaminia kwa hilo tuwekee nini hasa kazi za rais, ili tuache kulalamika bila guidance!
 
Mtoto wa Mkulima,Kithuku,Field Marshall,Mkandara,Mwanakijiji,
Kuna kipindi Frederick Sumaye alikwenda Marekani na msafara wake ulitumia sh 500 million. Wananchi tulilalamika sana. Sasa jiulize Kikwete amefanya ziara ngapi kama alizofanya Sumaye, na taifa limeingia gharama kiasi gani.

Imefikia Raisi mpaka anafanya stop over kutembelea vilabu vya mpira-- Real Madrid. Hivi kuna Watanzania walimtuma akafanye hivyo? Hivi Ilani ya CCM ndiyo inamuelekeza afanye ziara za namna hiyo?

Majuzi Raisi amekwenda Umoja wa Mataifa na akahutubia. Alichokisema huko wala hakikuwa na uzito wowote ule. Hakukuwa na umuhimu kwa Tanzania kumtuma Raisi wetu ukizingatia kwamba hatukuwa na jambo lolote zito tulilohitaji kulielezea huko UN. Kuna nchi nyingi tu zilituma wawakilishi kama Mawaziri wa Mambo ya Nje n.k.

Halafu hizi safari wakirudi hawatuelezi wametumia gharama kiasi gani. Wanapiga chenga tu, kueleza kwamba kuna fund fulani zimekuwa released. Ukichunguza unakuta siyo Tanzania pekeyake iliyopata funds hizo, na Maraisi wa hizo nchi nyingine hawakulazimika kwenda Washington/New York ili kupata funds hizo.

Hao wanaoshangilia Papa kutembelea Tanzania hivi wanaelewa gharama za ugeni wake? Watanzania tuache kupiga siasa. Kila jambo tunalolifanya tulipime faida zake za kiuchumi na ulazima wake.

NB:
Wizara ya Mambo ya Nje ina Waziri na Manaibu wawili. Pia tunao Mabalozi. Hii ni mara ya kwanza wizara hiyo kuwa na Manaibu wawili. Tena hiyo imefanyika baada ya kumega Wizara ya Afrika Mashariki toka Wizara ya Mambo ya Nje.

Katika mazingira kama hayo ulitegemea Raisi atakuwa na muda mwingi wa kushughulikia matatizo ndani ya nchi.
 
I am with you on this, nafikiri umefika wakati sasa tutafute exactly nini hasa kazi za rais, na tuziweke hapa, Mzee MMJ, ninakuaminia kwa hilo tuwekee nini hasa kazi za rais, ili tuache kulalamika bila guidance!

sasa unategemea mwanakijiji akuandikie hapa kazi za rais ukidhani yeye ndio anayempangia rais nini cha kufanya ? mhm.............. am out !
 
kwa kweli kalenda ya muungwana inafurahisha!!

kama yuko kwenye honey moon vile!!doh!!ni kweli yeye ni RAIS na anahitaji kuzurula nje ya nchi atakavyo!!lakini je??can we aford matumizi yake??

hata ndani ya nyumba kama mzazi familia inajiweza basi kila weekend ni kwenda park,movie,vacations..,short trips na vitu kama hivyo!!

lakini kama familia haijiwezi weekend ni wakati wa kwenda shambani(kama familia husika ni waalimu) kupalilia vidogo vilivyopo!!

sasa je nci yetu inajiweza??can we afford luxuries za mh wetu??

mwaka wa kwanza alisema anahitaji kujulikana..,wamemjua..,mwaka wa pili akasema anatafuta investors (jifanye hujui msemo wa kibaya chajitembeza...,chema chajiuza)

mwaka wa 3 atatwambia nini sijui..,nadhani atasema anaenda kusaini mikataba!!

duh!!
 
Kuombea watu ndio kazi ya Papa humwombea hata fisadi apate mwanga aokoke!.. Kizuri ni kwamba Papa katupa sifa Wadanganyika kwa utulivu na amani...sijui kama inatusaidia maanake ndio mwenzetu kesha pata hizo baraka za Papa... nadhani hii inaweza kuwa sifa kwake katuwahi ktk uwanja wa dua na maombi.
 
Sitashangaa kusikia jamaa anajisifia kuwa juhudi zake zimemfanya Papa aahidi kuja Tanzania, 'kutoa misaada'.
Mwanakiji, Nchimbi alisema kuwa raisi hawezi kukaa ikulu 'kulinda njiwa', kwa hiyo lazima atasafiri kama mara mbili tatu kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Ningependa sana kama angezuru Mkoani Mbeya pia, atoe ufafanuzi wa mbolea ya ruzuku, maana wakulima hawaelewi kabisa somo la mawaziri na wakuu wa wilaya.
 
ali siwa alikuwa mkurugenzi wa mambo ya ndani wa usalama wa taifa(ni moja ya nafasi nyeti nchini),na ni moja ya majina yaliyotajwa kumridhi apson lakini inasemekana kulikuwa na walakini kidogo nafasi ikaenda kwa othmana rashid,
 
KadaMpinzani,
Hatuna dira yoyote, hatufahamu kama viwanda, Kilimo ama madini ndio priority kubwa ya Uongozi wetu ila tunawaachia wawekeshaji wao watuamlie wapi tunakwenda.
In fact nikitumia maneno ya rais mwenyewe, hatujui ni kwa nini sisi ni masikini hadi leo.....
 
Back
Top Bottom