Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Leo kuna matatizo kibao ya katiba na pia hata haya mambo na ujanja wa CCM ili kuepuka ile ilani yao ya kuanzisha Mahakama ya kadhi na pia, italeta usumbufu mkubwa kutumia sheria za kawaida kuingiza mambo kama haya, sasa majaji nao watakuwa wakina nani??
 
Nchi itakuwa na Sheria za kiislamu---SHARIA.... nchi Serikali Haina Dini......je Serikali ni nini?
 
Mkuu hizo nchi wewe unazosema zilianza na sheria za kidini ni kwa sababu wananchi wake walikuwa overwhelmingly wa dini fulani. Ndiyo maana unakuta nchi kama Saudi Araba inaongozwa kwa sharia kwa sababu karibia wananchi wote ni Waislamu na nchi si secular bali inadini. Tanzania Waislamu 35% na Wakristo 30% kwa maana hiyo hakuna dini ambayo ina an overwhelmingly the majority. Kabla ya kulinganisha Tanzania na nchi zingine tabua kwanza hali za nchi hizo zilivyo tofauti na kwetu. Tusipende kufanya kila kitu simply because nchi fulani nao walifanya.


Mkuu MwanaFalsafa1.
Hizi takwimu za idadi ya waislamu na wakristo umezipata wapi ?.Sensa zote zilizowahi kufanyika Tanzania hazijawahi kuwa na kipengele cha kuonyesha idadi ya watu kwakuangalia dini !.Umesema idadi ya waislamu ni 35% na wakristo 30%.mkuu unataka kutuaminisha kwamba Tanzania ina karibu ya watu 35% wasiokuwa na dini au wanaoabudu dini za jadi ?.tafadhali naomba ufafanuzi.
 
Kwahiyo kiufupi CCM iliwadanganya makusudi waislamu kwa kuwaahidi katika ilani yao jambo amabalo wanajuwa hawawezi kulitekeleza, eni wei, na warudi 2010 wawambie kwanini waislamu waendelee kuwaunga mkono?(decree nisi)
 
Mkuu MwanaFalsafa1.
Hizi takwimu za idadi ya waislamu na wakristo umezipata wapi ?.Sensa zote zilizowahi kufanyika Tanzania hazijawahi kuwa na kipengele cha kuonyesha idadi ya watu kwakuangalia dini !.Umesema idadi ya waislamu ni 35% na wakristo 30%.mkuu unataka kutuaminisha kwamba Tanzania ina karibu ya watu 35% wasiokuwa na dini au wanaoabudu dini za jadi ?.tafadhali naomba ufafanuzi.

Ripoti ya Sensa ya 2002 ilioanisha swala la dini na hiyo hapo juu ikawa ndio takwimu ukweli wake utajua mwenyewe
 
sasa ndugu zangu waislamu inakuwaje mtafute kuhukumiwa kwa sheria za kiislam? naona lianze hoja kuwa mahakama ya kitaifa haifai, kama tunachanganyikana wote katika nchi moja makosa yanafanywa pamoja au katika mazingira mamoja, inakuwaje mtu udai kuhukumiwa kwa sheria tofauti? na gharama za kuienesha watazibeba nani? Je ni kodi za waislam pekee?? AU na wakristo tutatozwa kodi za kurun mahakama hizo? kwanza ili iwe nini? kuwa na mahakama nyingi nyingi? sio ustaarabu hii ni nchi isiokuwa na dini, sawa tuelewane tu!!
 
Mkuu MwanaFalsafa1.
Hizi takwimu za idadi ya waislamu na wakristo umezipata wapi ?.Sensa zote zilizowahi kufanyika Tanzania hazijawahi kuwa na kipengele cha kuonyesha idadi ya watu kwakuangalia dini !.Umesema idadi ya waislamu ni 35% na wakristo 30%.mkuu unataka kutuaminisha kwamba Tanzania ina karibu ya watu 35% wasiokuwa na dini au wanaoabudu dini za jadi ?.tafadhali naomba ufafanuzi.

"Mainland: Christian 30%, Muslim 35%, indigenous beliefs 35%; Zanzibar: more than 99% Muslim"- Tanzania Facts

"Religions:
mainland - Christian 30%, Muslim 35%, indigenous beliefs 35%; Zanzibar - more than 99% Muslim"-
Tanzania People 2009, CIA World Factbook

Nimekupa source mbili mkuu na zote zinasema kitu hicho hicho kimoja. Ukitaka kuhakiki nenda tu mwenyewe kwenye hizo website.
 
"Mainland: Christian 30%, Muslim 35%, indigenous beliefs 35%; Zanzibar: more than 99% Muslim"- Tanzania Facts

"Religions:
mainland - Christian 30%, Muslim 35%, 35%; Zanzibar - more than 99% Muslim"- Tanzania People 2009, CIA World Factbook

Nimekupa source mbili mkuu na zote zinasema kitu hicho hicho kimoja. Ukitaka kuhakiki nenda tu mwenyewe kwenye hizo website.

Mku soo what? point yako nini hasa.. yaani sheria zisitungwe kwa sababu Tanzania ina dini tatu tofauti..
Ebu nikuulize wewe mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa tumpe sheria gani apate haki yake! waislaam hawana solution na Wakristu pia hawana jibu kwa sababu dini zote hizi hazitambui mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa.. Lakini tukitazama sheria za Asili, hao unaowaita wenye indigenous belief wanayo solution..Kwa nini tusiitumie hukumu yao kumpa haki mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa.. ili hali nchi yetu haina sheria kuzuia watu kufanya kitendo hicho nje ya ndoa..Tuache tu maadam inafuata hukumu ya Kiasili kinyume cha matwakwa ya waislaam na Wakristu!

Unafikiri serikali ikichukua sheria za Asili na kuzitumia ktk mahakama zetu za madai watafanya kosa kwa sababu nchi yetu ina dini tatu tofauti.. Mkuu nani wa kum blame hapa ikiwa Waislaam na Wakristu ndio wanaozaa nje ya ndoa, kinyume cha dini zetu...Leo unazivuta dini ktk sheria wakati unajua fika kwamba uloyafanya ni makosa...Mkuu hizi ni hukumu tunzozungumzia sio sheria ya kuzuia watu kufanya wanayoyafanya..

Hata Jizi huwa na sababu ya kuiba, sheria hutungwa kumlinda victim aliyeibiwa na tunatazama uzito wa hukumu kulingana na makosa.. badala ya kukatwa mikono kama Waislaam na watu wa asilia (indigenous) walivyokuwa wakihukumu, tunachukua njia ya kati ya kumfunga Jela ambayo ilitumika zaidi na tawala za Kikristu..Tatizo liko wapi! wote tunakubaliana na maamuzi hayo bila kujali dini zetu zinatuambia hukumu gani itumike..
 
Tanzania kama wanasema kuwa haina dini bora kubaki hivi hivi kuliko kubatiza sheria katika mahakama zetu, zitakuja kuleta shida sana katika Taifa letu
 
Tanzania kama wanasema kuwa haina dini bora kubaki hivi hivi kuliko kubatiza sheria katika mahakama zetu, zitakuja kuleta shida sana katika Taifa letu
Shida gani... wewe kama una wake wanne na wewe ni mkristu unataka sheria gani itumike au sheria gani itungwe kuwapa haki wake hao!
Acha kuwa na mke zaidi ya mmoja kama dini yako inavyokuamru utaepuka sheria ya kiislaam inayotaka kuwekwa lakini hatuwezi kuacha nchi ikiyumba hovyo wakati mnaoa na kuwarubuni wanawake kama vile wao ni vifaa kwa kutumiwa ovyo.
 
Its more better to incorporate within the existing laws rather than establishing Kadhi Court. Tanzania never favour any religion, we must respect this
 
Shida gani... wewe kama una wake wanne na wewe ni mkristu unataka sheria gani itumike au sheria gani itungwe kuwapa haki wake hao!
Acha kuwa na mke zaidi ya mmoja kama dini yako inavyokuamru utaepuka sheria ya kiislaam inayotaka kuwekwa lakini hatuwezi kuacha nchi ikiyumba hovyo wakati mnaoa na kuwarubuni wanawake kama vile wao ni vifaa kwa kutumiwa ovyo.
Sasa mzee wangu Kuoa wake wengi hiyo ni moral issue siyo mpaka mahakama iwepo?? hakuna haja ya masuala ya uhuru wa mtu kuingiliwa na mahakama?? Maana walishaanza kusema kuna haki ya mwanamke kutoa mimba na hiyo nayo unasemaje?? Mimi nasema kuwa mtu kuwa na wake wengi au mmoja ni hiari yake mwenyewe, Je vipi kuhusu Divoice?? Maana kama na sisi tukisema kuwa kuiga mambo kama ya walaya kule America tunaweza kupoteza kabisa misingi ya Taifa, maana. Mimi kwa maoni yangu sheria zetu zinatosha kabisa na kusiwe na haja ya kuongeza sheria za Kislamu hapa kwenye sheria zetu, Kama tumeamua kuwa cellullar state basi tuwe hivyo, lakini kufanya hivi kwa ajili ya kuwapendezesha watu fulani ni kinyume kabisa na katiba, Hivyo na watu wengine wakija nao na kusema kuw wanataka kuweka sheria za kanisa kwenye sheria za nchi watasema nini??Kama kweli tukitaka kubaki hivihivi mambo ya dini yawe ni uhuru wa mtu binafsi kuliko sasa hivi. Je na watu wasio na Dini waseme nini?? je Naye Kakobe akija kudai mambo yake ya msingi yawe sheria tuseme nini??
 
Josh Michael,
Uhuru wa mtu unaozungumzia ni kitendo cha kuoa iwe mmoja au wake wanne lakini haki ya wanawake hao lazima ilindwe sii tu kwamba unapotaka kuoa wake wanne iwe ni ni swala la wahusika..Sasa ikiwa wewe hukubaliani na lolote linalohusiana ni lazima uliweke wazi.. Kwa mfano haki wanayopewa wanawake kulingana kifungu kadhaa inamuonea mwanamme..

Ndio maana nikasema kwamba sheria zinazovutwa ndani ya katiba yetu ni baada ya wewe ku practise kile unachokiona ni haki yako lakini hutakiwi ku abuse hiyo haki yako.. Sheria zitawalinda wahusika wote ni utaratibu mbele ya maamuzi ya haki yako . Hata ktk Biashara mkuu wangu ukitaka kuuza nyanya ni mapenzi yako, lakini kuna sheria zinaingia ktk kitendo cha uuzaji nyanya kuwalinda wateja..
 
Halafu ikisemwa hapa kuwa Tanzania kuna udini (hivyo watu watibu ugonjwa huu badala ya kujaribu kuuficha) mimacho na mipovu inawatokaaaa..... Phewwwww

Miafrika bana ndivyo tulivyo
 
Serikali kuingiza sheria za Kiislamu katika Sheria za Nchi ili zitumike katika mahakama zote kunaweza kuwa ni kinyume na Katiba yetu. Katiba inatamka kwamba kila raia ni sawa mbele ya sheria.

Kwa mfano, itakuwa ni kukinzana endapo kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu (ilyoingizwa ktk sheria za nchi) itakuwa ni halali kutokumrithisha mjane mali fulani iliyoachwa na marehemu mumewe. Mjane huyo huyo angeweza kurithishwa mali hiyo hiyo kwa mujibu wa sheria ya nchi. Kwa maneno mengine, sheria zetu zilizoidhinishwa na Bunge na kuingizwa ktk Statute Book, zisibague raia kutokana na dini zao.

Ni ukweli usiopingika kwamba mashauri mengi baina ya WaTz. sasa yanasuluhishwa na vikao vya ukoo kutegemea mila na desturi za jamii husika. Mashauri mengine hushughulikiwa na vikao vinavyoshirikisha viongozi wa dini, bora tu wahusika wakubaliane na maamuzi au ushauri wa msuluhishi.

Kutokana na ukweli huu, nashauri Serikali iruhusu kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi kwa madhumuni ya kushughulkia mashauri, yasiyo ya jinai, baina ya waumini wa Kiislamu wanaokubali kwa ridhaa yao wenyewe kutumia mahakama hiyo. Mahakama ya Kadhi isajiliwe kama taasisi huru chini ya Sheria ya Taasisi Zisizo za Kiserikali (Non-Govermental Organizations).

Kama NGOs zingine, Mahakama ya Kadhi isitegemee ruzuku toka Serikalini, bali iruhusiwe kukusanya michango ya hiari toka kwa waumini wa Kiislamu nchini na wafadhili wengine wa ndani na nje.

Kama NGOs zingine, Mahakama ya Kadhi iwajibike kutoa taarifa kwa Serikali juu ya mashughuli yake kila mwaka; na mapato na matumizi yake yawe ya wazi na yaweze kukaguliwa na Mkaguzi anayetambulika nchini kisheria.

Ijulikane na itambuliwe kwamba Muumini yeyote wa Kiislamu anayepeleka shauri lake mbele ya Mahakama ya Kadhi, asiporidhika na hukumu au uamuzi wa Mahakama, anaweza kukata rufaa katika mahakama ya kiraia. Mpangilio huu utahakikisha Waislamu wanaotaka watapeleka mashauri yao Mahakama ya Kadhi, na Statute Book yetu itabaki na Sheria zinazo-apply kwa raia wote bila kubagua.
 
Mkandara,
Unasema point moja kubwa sana sana. Hii kweli ni tatizo kubwa sana sana kwa mila zatu na mchanyato wa dini. Tatizo moja ni kuwa mie kama Ng'wana Itimba, nina mke mmoja na nyumba ndogo ambayo kila mtu anaifahamu ila official ni kwamba haipo na huenda hata tumezaa tayari. Sasa itakapokuja kwenye mashtaka, unataka nikashitakiwe wapi? Ukinigusa tu kunipeleka kwenye mahakama ya Kiislamu hapo utakuwa umeleta ugomvi mkubwa sana. Atakayeamua hivyo, hata kama ni wewe Mkandara, basi familia yote ya Sikonge itakukalia kooni. Sheick ninamuheshimu na kuheshimu maamuzi yake na anayoyafundisha, ila siwezi kufuata wala kusikiliza maneno yoyote ya Kiislamu kama naona yanaingiliana na imani yangu ya Kikristo cha Kinyamwezi.
Kama nilivyoanza, lazima niseme kuwakuna tatizo na hili lazima litungiwe sheria. Kama ni kuhukumu Waislam walioowa wake wengi au kuzaa na kuachaniza watoto (kwa wakristo na wasio na dini pia) basi zitungwe sheria bila kujali dini ya mtu na hizi ziwe zinatolewa na Mahakimu. Ukinipeleka kwa Sheick na kunipa quraani na kusema nikiri ntasema kweli, ujuwe hata sitaki basi ntandanya na ukiuliza kwa nini ntakuambia sababu ni kuwa mie quraani ni kitabu tu, ingawa najua kwa wengine ni maandiko matakatifu. Sasa hebu fikiri ikiletwa sheria ya KIHINDI na umefanya kosa la kuvunja sheria za kihindi na unapelekwa UKAMSUJUDIE NG'OMBE, kweli utafanya hivyo? Ije sheria kuwa usile ng'ombe kwakuwa huyo ni Mungu........

Kama lilivyo swala la ZEUTAMU, Tanzania inaidi kuandika sheria nyingi upya kulingana na hali yetu ya sasa. Ila wakati tunaandika, tusijiingize kwenye mambo ya dini. Kama kuna sheria tunataka ziingizwe ila zinatoka kwenye vitabu vya dini, basi tukubaliane na iwe hivyo, na ukienda mahakamani basi unaapa kwa kutumia dini yako ingawa unaweza kukutwa wahukumiwa na sheria za JAMHURI zilizotoka kwenye Biblia au Quraani au sijui kitabu cha dini gani ....ehhhmay be torati......huko nako kunaweza kuwa na sheria nzuri tu kutusaidia.
 
Kilasara,
Je ukizuka ugomvi kati ya Muislaam na Mkristo itakuwaje?
Kama mie ni Muislaam na napata habari kuwa umenishtaki kwenye mahakama ya kadhi, ninapata habari na siku hiyo naenda kubatizwa na kuwa Muislaam au mpagani, unafikiri ukiniburuza mahakama ya kadhi, nitakuja? Mtanileta kwa nguvu? Huoni kwa njaa ya Tanzania, watu watakuwa wanajiingiza kwenye Uislaam au kujitoa kutokana na wapi wanaona ni mteremko? Mtu akipinga hukumu ya mahakama ya kadhi mtamfanya nini? Hii itakwa ni mahakama au sehemu ya kusuluhisha migogoro na kupeana mawaidha?
 
Mimi nilikataa kuwepo kwa mahakama za kadhi kwa sababu za kiufundi na kiutendaji; kwamba wakati mwingine tutamfanya mtu ambaye si mtu wa dini fulani (si mwislam) kulazimika kutoa maamuzi ambayo yataathiri watu wa imani fulani tu.

Kimsingi nitapinga hii integration vile vile kwa sababu za kiufundi au kiutendaji. Itakuwaje pale ambapo sheria ya kiislam inapingana na sheria ya nchi? Ni sheria ipi itaprevail? Kwa mfano; sheria za nchi zinasema mme atarithiwa na mke. Sheria ya kiislam inamgawanyo tofauti. Sasa itakapotokea mtu mmoja kupinga uamzi unaotumia sheria ya kidini itakuwaje? Hatutazifanya hizi sheria zionekane subordinate?

Nakumbuka zamani kwenye sheria ya ardhi, kulikuwa na ruhusa ya kutumia customery law. Lakini nakumbuka movements za wanawake zilisababishwa hiki kipengele cha customery law kwenye ardhi kimeondolewa. Sasa tunataka tu-insert islamic law!

Vipi mahakimu wakristo, watakuwa na uwezo wa kuhukumu kutumia sheria za kiislam? Ninavyojua mgawanyo wa mahakimu kwenye mahakama zetu hauzingatii dini. Sasa mtu akisema mimi hapa nataka nihukumiwe kwa sheria za kiislam, itabidi atafutwe hakimu mwislam? Au itabidi kila mahakama iwe na mahakimu waislam kwa ajili ya kuhukumu kesi za waislam?

Vipi mahakimu watakaohukumu kutumia sheria za kiislam? Kwenye mtaala wa sheria najua kuna specialty ya islamic law. Sasa ikiwa mkristo anataka na akasomea islamic law ataruhusiwa kuhukumu waislam?

Mimi shida yangu, ni pale ambapo kabla ya kuhudumiwa itabidi uwe unaulizwa kwanza dini yako. Hili tunaweza kuliona jambo jepesi tu leo, lakini litatutoa jasho kesho.

Kusema sheria zilizopo ni za kikristo kwa sababu nyingi zilitungwa wakati viongozi ni wakristo ni kutoitendea haki historia yetu. Historia yetu inaonesha kuwa mchakato wote wa kupata uhuru waislam walishiriki sana katika capacity mbali mbali. Hivi tunadhani hawa waislam wao walikuwa mbumbumbu kiasi hicho kwamba waliruhusu nchi yao itungiwe sheria za kikristu? Hili linanisikitisha kidogo, tunaonekana kudharau kila kilichofanyika huko nyuma.
 
Solution ni ama tukubaliane kuwa na sheria moja inayojali maslahi ya makundi yote ya kidini bila kujiingiza katika mambo yao. Ninavyojua sheria za kidini mara nyingi au zote ziko attached kwenye mifumo ya kidini kwa maana kuwa waamuzi na watafsiri wa sheria hizo huwa ni viongozi wa dini. Itakuwaje hukumu ya jaji itakapotofautiana na msimamo wa viongozi wa kidini?

Au tukubaliane kujenga taifa virtual la kiislam ndani ya jamhuri hii ya muungano wa Tanzania. Ujanja ujanja mwingine utatuingiza matatani tu.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji,
nadhani utakumbuka kwamba hata mimi nilipendekeza sana sheria hizi za kiislaam kuingizwa ktk sheria zetu badala ya mahakama ya kadhi na na sababu nilizitoa kwa pande zote mbili..
Ajabu umekuja na maswali ambayo nashindwa kuelewa unachojaribu kujenga hapa..
Kwanza kabisa tulisha sema kwamba Mahakama ya kadhi ni sawa na Civil Court inayo deal na kesi (maswala) za MADAI na siii Criminal cases kama mnavyotaka kuzipamba hoja zenu..
Hivyo maswali yako yote hayana nguvu kama utazingatia ni kitu gani kinachuhusiana zaidi na mahakama ya Kadhi..
Kwa mfano ukiwa una wake zaidi ya mmoja nini haki ya mke wa pili na wa Tatu..Sidhani kama wewe unaweza kunijibu.. na huwezi kumjibu hata Musuguli ambaye kaoa wake zaidi ya mmoja kwa kufuata mila na desturi za kabila lake..
Hapa kama wewe Mkristu swafi, nasema tena SAFI, sheria hii haiwezi kukufiokia kwa sababu utakuwa na mke mmoja tu. Ila hata wale wasiokuwa waislaam maadam wameamua kuona mke wa pili au tatu basi hawa wote waktakuwa na haki zao kwa mume aliyewaoa..Hii ni pamoja na watoto wote waliozaliwa ktk ndoa hizo. Kukataa kuwepo kwa sheria kwa sababu tu mnaona jina Kiislaam ni kutofikiri nje ya box la Udini..Kumbuka hata wale unaowaona sii wakristu wanataka sheria pamoja na kwamba dini au mila zao zinawaruhusu..

Kwa hiyo hofu yako ya hukumu na kufikiria sijui waktakatwa mikono au kupigwa mawe haihusiani pamoja na kwamba hata wakristu wakati wa Yesu walitumia adhabu hizo hizo za waislaam mnazozikataa leo. Kifupi hakuna aya wala sura inayokataza hukumu za kiislaam ambazo zimetumika toka enzi ya Ibrahim, hivyo madai yan kwamba hizi ni hukumu za mahakama za Kiislaam ni uzushi ambao mnashindwa kukubali Ukristu wenu wenyewe..

Kifupi mimi naunga mkono sana fikra hizi na labda shida kubwa itakuja pale ambapo kuna watoto nje ya ndoa.. Hapa ningeishauri serikali kutunga sheria ambayo itawabana wazzazi hasa wa kiume kuchukuwa responsibility ya mzazi pindi mtoto atakapojukana mzazi wake ni nani bila kujali swala la ndoa au laa..

Halafu kulingana na taarifa ya taasisi ya DNA imegundulika kwamba kati ya watoto 10 wanaozaliwa, sita huwa sii wa baba aliyejulishwa.. Hii ikiwa na maana ni asilimia 60 ya watoto hufungiwa baba mzazi (biological father)..Inabidi kila penye mashaka DNA ifanyike mapema kuweza kuepuka mgogoro baadaye..
Nje ya hapo mkuu ningependa sana uelewe kwanza nini mahakama ya kadhi kisha jenga hoja zako zinazohoji kesi au swala linalokutatiza toka mahakama hiyo na sii kuhoji tu mahakama kwa sababu ina jina la Uislaam.


Ningependa kukusahihisha hapo. Wakati wa Yesu, hazikuwa sheria za Kikristo. Hizi sheria ni za kiyahudi na zinatumika mpaka leo. Zinapatikani katika Torati (Torah). Tafadhali, Usipotoshe watu kwa kuongea usichojua.

Serikali kuingiza sheria za Kiislamu katika Sheria za Nchi ili zitumike katika mahakama zote kunaweza kuwa ni kinyume na Katiba yetu. Katiba inatamka kwamba kila raia ni sawa mbele ya sheria.

Kwa mfano, itakuwa ni kukinzana endapo kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu (ilyoingizwa ktk sheria za nchi) itakuwa ni halali kutokumrithisha mjane mali fulani iliyoachwa na marehemu mumewe. Mjane huyo huyo angeweza kurithishwa mali hiyo hiyo kwa mujibu wa sheria ya nchi. Kwa maneno mengine, sheria zetu zilizoidhinishwa na Bunge na kuingizwa ktk Statute Book, zisibague raia kutokana na dini zao.


Ni ukweli usiopingika kwamba mashauri mengi baina ya WaTz. sasa yanasuluhishwa na vikao vya ukoo kutegemea mila na desturi za jamii husika. Mashauri mengine hushughulikiwa na vikao vinavyoshirikisha viongozi wa dini, bora tu wahusika wakubaliane na maamuzi au ushauri wa msuluhishi.

Kutokana na ukweli huu, nashauri Serikali iruhusu kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi kwa madhumuni ya kushughulkia mashauri, yasiyo ya jinai, baina ya waumini wa Kiislamu wanaokubali kwa ridhaa yao wenyewe kutumia mahakama hiyo. Mahakama ya Kadhi isajiliwe kama taasisi huru chini ya Sheria ya Taasisi Zisizo za Kiserikali (Non-Govermental Organizations).

Kama NGOs zingine, Mahakama ya Kadhi isitegemee ruzuku toka Serikalini, bali iruhusiwe kukusanya michango ya hiari toka kwa waumini wa Kiislamu nchini na wafadhili wengine wa ndani na nje.

Kama NGOs zingine, Mahakama ya Kadhi iwajibike kutoa taarifa kwa Serikali juu ya mashughuli yake kila mwaka; na mapato na matumizi yake yawe ya wazi na yaweze kukaguliwa na Mkaguzi anayetambulika nchini kisheria.

Ijulikane na itambuliwe kwamba Muumini yeyote wa Kiislamu anayepeleka shauri lake mbele ya Mahakama ya Kadhi, asiporidhika na hukumu au uamuzi wa Mahakama, anaweza kukata rufaa katika mahakama ya kiraia. Mpangilio huu utahakikisha Waislamu wanaotaka watapeleka mashauri yao Mahakama ya Kadhi, na Statute Book yetu itabaki na Sheria zinazo-apply kwa raia wote bila kubagua.

Hapo mwanzo umeandika vizuri sana. Nchi haiwezi kuwa na sheria mbili zitakazobagua wananchi wake. Sheria inatakiwa ifanye kazi bila kuangalia mtu. Na tunapoingiza sheria za dini, basi hapo kunaweza kuwa na tatizo. Kama dini ya mtu inaruhusu kuwa na wake wengi, na sheria hairuhusu, basi sheria itawale, kwa maana tunaishi chini ya sheria na sio dini. Kama tatizo ni watoto wa nje ya ndoa, sheria iangalie namna ya kuwalinda. Lakini kuingiza sheria za dini katika nchi isiyo ya kidini, itakuja kuleta matatizo.

Mwisho kabisa kuhususuggestion yako ya mahakama iliyo NGO. Sidhani kama inawezekana. Maana huwezi kuwa na mahakama inayofuata sheria zake, alafu ukasema haina nguvu. Kazi ya mahakama ni kusimamia sheria. Sasa kama hiyo mahakama-NGO haisimamii sheria basi haitakiwi kuitwa mahakama. Labda watafute jina lingine, na ikutane kwa ajili ya kutoa maoni, na sio sheria.
Mwisho kabisa, Sheria ya ndoa inafahamika, na watu wanaoingia katika uhusiano uliofanana na ndoa, basi wajue kuwa sio ndoa, na chochote kitakachotokea, hawapo-covered na hiyo sheria. Kwa maneno mengine, Umoja wao hautambuliki na sheria.
 
Back
Top Bottom