Mkuu Mzee Mwanakijiji,
nadhani utakumbuka kwamba hata mimi nilipendekeza sana sheria hizi za kiislaam kuingizwa ktk sheria zetu badala ya mahakama ya kadhi na na sababu nilizitoa kwa pande zote mbili..
Ajabu umekuja na maswali ambayo nashindwa kuelewa unachojaribu kujenga hapa..
Kwanza kabisa tulisha sema kwamba Mahakama ya kadhi ni sawa na Civil Court inayo deal na kesi (maswala) za MADAI na siii Criminal cases kama mnavyotaka kuzipamba hoja zenu..
Hivyo maswali yako yote hayana nguvu kama utazingatia ni kitu gani kinachuhusiana zaidi na mahakama ya Kadhi..
Kwa mfano ukiwa una wake zaidi ya mmoja nini haki ya mke wa pili na wa Tatu..Sidhani kama wewe unaweza kunijibu.. na huwezi kumjibu hata Musuguli ambaye kaoa wake zaidi ya mmoja kwa kufuata mila na desturi za kabila lake..
Hapa kama wewe Mkristu swafi, nasema tena SAFI, sheria hii haiwezi kukufiokia kwa sababu utakuwa na mke mmoja tu. Ila hata wale wasiokuwa waislaam maadam wameamua kuona mke wa pili au tatu basi hawa wote waktakuwa na haki zao kwa mume aliyewaoa..Hii ni pamoja na watoto wote waliozaliwa ktk ndoa hizo. Kukataa kuwepo kwa sheria kwa sababu tu mnaona jina Kiislaam ni kutofikiri nje ya box la Udini..Kumbuka hata wale unaowaona sii wakristu wanataka sheria pamoja na kwamba dini au mila zao zinawaruhusu..
Kwa hiyo hofu yako ya hukumu na kufikiria sijui waktakatwa mikono au kupigwa mawe haihusiani pamoja na kwamba hata wakristu wakati wa Yesu walitumia adhabu hizo hizo za waislaam mnazozikataa leo. Kifupi hakuna aya wala sura inayokataza hukumu za kiislaam ambazo zimetumika toka enzi ya Ibrahim, hivyo madai yan kwamba hizi ni hukumu za mahakama za Kiislaam ni uzushi ambao mnashindwa kukubali Ukristu wenu wenyewe..
Kifupi mimi naunga mkono sana fikra hizi na labda shida kubwa itakuja pale ambapo kuna watoto nje ya ndoa.. Hapa ningeishauri serikali kutunga sheria ambayo itawabana wazzazi hasa wa kiume kuchukuwa responsibility ya mzazi pindi mtoto atakapojukana mzazi wake ni nani bila kujali swala la ndoa au laa..
Halafu kulingana na taarifa ya taasisi ya DNA imegundulika kwamba kati ya watoto 10 wanaozaliwa, sita huwa sii wa baba aliyejulishwa.. Hii ikiwa na maana ni asilimia 60 ya watoto hufungiwa baba mzazi (biological father)..Inabidi kila penye mashaka DNA ifanyike mapema kuweza kuepuka mgogoro baadaye..
Nje ya hapo mkuu ningependa sana uelewe kwanza nini mahakama ya kadhi kisha jenga hoja zako zinazohoji kesi au swala linalokutatiza toka mahakama hiyo na sii kuhoji tu mahakama kwa sababu ina jina la Uislaam.