Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. Baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo.

Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;

1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address

2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)

3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:

1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.

2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.

3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY

Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi

4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.

PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?


Hii iko hivi....

1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.

2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.

FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:

1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.

Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao

Uzuri wao:
watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,

2: COMGATEWAY
Link: http://comgateway.com/ - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..

3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.

4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao

5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.

STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.

HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.

Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..

Help Mwl.RCT
Mkuu nimekuelewa Sana ila napenda kufahamu kutoka kwako na kwa yeyote mwenye kufahamu vipi kuhusu Hawa AliExpress wako vizur maana sijawahi kulitumia ila ndio nataka niagize mzigo kupitia wao wajuzi NAOMBA ufafanuzi Asante.
 
Kuna mtu yoyote katumia kampuni la ali express na kupokea mzigo wake wa quality ile na nzuri?
Vipi mwl Ushawahi kuwatumia hawa ali express?
Ndio, ni miaka kadhaa sasa naendelea kuwatumia.

Quality
- Bidhaa za viwango vyote hupatikana, high quality na low quality ni wewe utakavyochagua bidhaa husika, WYSIWYG

1569459267085.png
 
Ndio, ni miaka kadhaa sasa naendelea kuwatumia.

Quality
- Bidhaa za viwango vyote hupatikana, high quality na low quality ni wewe utakavyochagua bidhaa husika, WYSIWYG

View attachment 1216168
Mkuu nahitaji laptop yenye uwezo mkubwa na graphics nzuri kwa ajili ya CAD programs. Hivi nikiagiza kodi inahusika pia? Na njia gani salama ya kupokea/kutuma iliyo salama?
 
Hivi nikiagiza kodi inahusika pia?
Computer & computer parts hazina kodi, bali kuna VAT asilimia 18 uya invoice itakayo ambatana na mzigo husika.
Na njia gani salama ya kupokea/ kutuma iliyo salama?
Bila shaka unazungumzia kutuma fedha.
- Bank deposit
- Mobile benking
Zaidi angalia hapa: www.bit.ly/101buy4me
laptop yenye uwezo mkubwa na graphics nzuri kwa ajili ya CAD programs
Sema bajeti yako ni TZS ngapi ili wadau washauri ipi ya kununua.
Waweza angalia hapa www. amazon . com
 
M-pesa ndo mpango mzma haina makato ya kuendeshea akaunt afu simpo kuapdet
Hivi M_ pesa mastercard haisumbui?
Kuna pesa yangu mpaka sasa hivi haijarudi na nikiwapigia voda wanasema kuna shida kwenye upande wa mastercard. Wiki ya pili sasa.
Huu usumbufu ni kwangu tu au kwa wote?
 
Hivi M_ pesa mastercard haisumbui?
Kuna pesa yangu mpaka sasa hivi haijarudi na nikiwapigia voda wanasema kuna shida kwenye upande wa mastercard. Wiki ya pili sasa.
Huu usumbufu ni kwangu tu au kwa wote?
Ata mm inshantokea but system inakua idle tu ila mzgo ulirud fresh
 
Ata mm inshantokea but system inakua idle tu ila mzgo ulirud fresh
Mimi bado haijarudi aisee. Nahisi wananizungusha. Cha ajabu nikiangalia salio linasoma sifuri wakati pesa nilishaweka. Nikijaribu kutoa pesa kwenye kadi naambiwa''server error''. Huku Kwenye account ya Mpesa pesa haipo. Yaani Mastercard hamna pesa, M_pesa nako hamna pesa.
Mpaka naona kero.
Hawa M_pesa mastercard naona wanataka kunitia shaka.
 
Huwa naweka pesa nktaka kununua kitu bac
Mimi bado haijarudi aisee. Nahisi wananizungusha. Cha ajabu nikiangalia salio linasoma sifuri wakati pesa nilishaweka. Nikijaribu kutoa pesa kwenye kadi naambiwa''server error''. Huku Kwenye account ya Mpesa pesa haipo. Yaani Mastercard hamna pesa, M_pesa nako hamna pesa.
Mpaka naona kero.
Hawa M_pesa mastercard naona wanataka kunitia shaka.
 
Mimi bado haijarudi aisee. Nahisi wananizungusha. Cha ajabu nikiangalia salio linasoma sifuri wakati pesa nilishaweka. Nikijaribu kutoa pesa kwenye kadi naambiwa''server error''. Huku Kwenye account ya Mpesa pesa haipo. Yaani Mastercard hamna pesa, M_pesa nako hamna pesa.
Mpaka naona kero.
Hawa M_pesa mastercard naona wanataka kunitia shaka.
Ila wakomalie coz kuna wahudum wa voda wasojua kitu
 
Nomba msaada wa kununua laptop hii wapendwa, hasa upande wa hapa nchini mambo ya kodi tofauti na gharama nitakazo lipia mtandaoni kwa maana ya purchase cost+ transportation cost
laptop.PNG
 
Tengene
Nomba msaada wa kununua laptop hii wapendwa, hasa upande wa hapa nchini mambo ya kodi tofauti na gharama nitakazo lipia mtandaoni kwa maana ya purchase cost+ transportation costView attachment 1254507
Tengeneza akaunti ya M-pesa Master card kisha convert hizo $ kuwa shillings ili ujue utalipia kiasi gani. Halafu weka sh zinazozidi kidogo kwenye M-pesa Master card kisha walipe. Subiria mzigo ukufikie sio ngumu ni kuclick tu.
 
Msaada tafadhali kwa wale mliowahi kununua bidhaa kutoka indianmart..uaminifu wao upoje?
 
Back
Top Bottom