John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Ubalozi wa Tanzania uliopo Urusi umetoa taarifa juu ya njia ambazo wanafunzi Watanzania walipo katika Chuo cha Taifa cha Sumy Nchini Ukraine wanazotakiwa kutumia pamoja na namba za simu kwa ajili ya mawasiliano wakati watakapokuwa wanaelekea sehemu salama kupokelewa.

Wanafunzi wanatakiwa kuelekea eneo la Sudja, watapokelewa na Jeshi la Urusi kisha kusafirishwa hadi Belgorod, hapo watakabidhiwa kwa maofisa wa Ubalozi wa Tanzania Nchini Urusi kwa taratibu za kurejeshwa Tanzania.

Wanafunzi wameshauriwa kutoka kwa makundi wakiwa na bendera ya Tanzania ili kuwatambulisha kwenye safe corridor, pia wanaweza kuwasiliana na timu ya mapokezi kwa namba za simu walizowapatia.

Wanafunzi Ukraine.jpg
 
Tungefanya kimyakimya kisha tutangaze baadaye. Au hatuna mawasiliano ya moja kwa moja na hao wanafunzi?
 
Ukiwa mbabe kwa watu wengi mwishowe unajikuta kila mtu anataka upigwe! Naona dalili USA inapoteza ushawishi wake dunian. Ni kama ina marafik wanafik tu ili wapate riziki kwake, waishi.
Watz wengi kwa level ya tunaopita vijiwen wako na Putin haijarishi kwanini. Kisa russia iko kinyume na USA!
 
Busara na hekma ya kutoegemea upande wowote zimeanza kulipa.
vijana wetu wanarudi salama n
Washauri wa Putin,imekuwa rahisi kumshawishi,ameanza kulegeza msimamo kidogo.
 
Ukiwa mbabe kwa watu wengi mwishowe unajikuta kila mtu anataka upigwe! Naona dalili USA inapoteza ushawishi wake dunian. Ni kama ina marafik wanafik tu ili wapate riziki kwake, waishi.
Watz wengi kwa level ya tunaopita vijiwen wako na Putin haijarishi kwanini. Kisa russia iko kinyume na USA!
Hao wote wanaomshabikia mrusi ndio timu kidugu!!wengi wao ni wale ambao ukiwasikiliza hata hawaelewi mambo, ila ni ushabiki tu kama wa yanga na simba!!
 
Ivi Urusi wametupa sh, ngapi na EU "NATO"
Wametupa sh ngapi, mbona tunajichanganya, 😆😆😆 wakizuiya mpunga wao huyu putin atamalizia miradi yetu kweli?.
 
Ubalozi wa Tanzania uliopo Urusi umetoa taarifa juu ya njia ambazo wanafunzi Watanzania walipo katika Chuo cha Taifa cha Sumy Nchini Ukraine wanazotakiwa kutumia pamoja na namba za simu kwa ajili ya mawasiliano wakati watakapokuwa wanaelekea sehemu salama kupokelewa.

Wanafunzi wanatakiwa kuelekea eneo la Sudja, watapokelewa na Jeshi la Urusi kisha kusafirishwa hadi Belgorod, hapo watakabidhiwa kwa maofisa wa Ubalozi wa Tanzania Nchini Urusi kwa taratibu za kurejeshwa Tanzania.

Wanafunzi wameshauriwa kutoka kwa makundi wakiwa na bendera ya Tanzania ili kuwatambulisha kwenye safe corridor, pia wanaweza kuwasiliana na timu ya mapokezi kwa namba za simu walizowapatia.

View attachment 2139767
Tanzania ilitumia akili kubwa sana juzi kwenye baraza la usalama UN kwa kujizuia kupiga kura. Kenya, Uganda, na Rwanda waliamua kupiga kura dhidi ya Urusi kama vile hakuna wanafunzi wao huko Ukraine.

Naamini uamuzi wa kutounga mkono upande wowote kwenye hiyo vita umesaidia wanafunzi wa Kitanzania kuwa salama kwa Warusi.

Vv
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom