Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Imani zilianzia Denmark?
Denmark ni miongoni mwa nchi za Ulaya na Imani tuliletewa na watu kutoka huko.
Nitafatilia kuhusu hayo maadhimisho asante kwa huo mfano!
Fuatilia; usidanganywe eti wazungu hawaamini uchawi au hakuna uchawi huko Ulaya.
Uchawi ulifundishwa kwa manufaa gani?
Nitapitia hilo andiko asante
Ulifundishwa ili wale wafundishaji ambao walikuwa ni miongoni mwa wale malaika waasi; waweze kukubalika katika jamii ya binadamu na ikawa ni hatua mojawapo ndipo wakawaoa binti wa binadamu.
Unauzwa wapi uchawi na gharama zake ni zipi?
Unataka kununua au kujifunza?
 
So wewe hapa upo upande gani Dosho12 kwa wazungu au kwenye utamaduni

Sawa naweza kukubaliana na wewe kwamba uchawi upo na unaweza kutumika kwa hizi njia ulizozitaja

Hivi huo uchawi una impact gani hasa zinazooneka ?
Impact zinaweza kuwepo ila tafsiri zikawa tofauti watu wawili waliopata tatizo moja mmoja akaenda hospitali na mwingine kwa mganga ila wote wakapata matibabu, dawa ile iwekwe sokoni inabidi iwe effective angalau asilimia 80 hii ina maanisha asilimia ishirini inaweza isitibu je tunaweza kusema dawa hazina impact vile kwenye uchawi huenda unafanya kazi namna hyo kwamba kuna wengine unakuwa effective na wengine unakataa,

Pia kwa kuwa uvhawi unatumia imani sana huenda kwa kuwa labda inatokana na energy labda kuna level flani ya energy yako unatakiwa uwe nayo ile uwe effective na unapo amini labda ndio umefika hyo level, ni kama vile madaktari mgonjwa akiwa kwenye hatua mbaya labda kwenye coma ndugu zake huwa wanambiwa angalau waongee naye huenda itasaidia ila kwa kawaida hii haingii akilini ila huenda kuongea naye anapata imani ya kupona na dawa zinafanya kazi vizuri kwa kuwa aliamini atapona, hujawahi kuona jinsi mtu anavyopata nguvu za ziada kwa kuwa tu kaamini kitu fulani anaweza so huenda uchawi unapo kuwa imani na kuwa commited sana ndio utaanza kuona impact zake
 
Mimi kwa mchango wangu ninaweza kushuhudia hiyo #1.
Huko Makete 1999 + Kulikuwa na Adhimisho la Mbio za mwenge (ziara iliyojumuisha watu wengi na kulikuwa na bendi ya muziki enzi hizo maarufu kama kimulimuli ya JKT-Mafinga). Kilikuwa ni kipindi cha mvua(Masika) na hivyo ili mvua isilete changamoto katika zoezi hilo; aliteuliwa mzee mmoja afanye kazi ya kuzuia na kufukuza mvua. Huyo mzee nilimwona na kumchunguza vizuri alichokuwa anafanya na nilienda mbali zaidi na kudodosa wasaidizi wake jinsi inavyokuwa na maelezo walionipa yaliniacha hoi. Na kweli Siku hiyo kutwa nzima eneo letu ambapo ndo mwenge ulikuwa unakimbizwa haikunyesha mvua hata manyunyu kidogo- hakuna. Sasa tuliite tukio hilo ni la nguvu za kichawi au vinginevyo ni coincidence mm cjui ila nnachokumbuka ni Mvua haikunyesha.
Hilo tukio wewe mwenyewe umelikosea jawabu basi tuliache kama lilivyo

Au tuombe mzee mwingine mwenye uwezo huo afanye marudio ili tuthibitishe

Mf: kipindi cha jua kali alete mvua
 
Denmark ni miongoni mwa nchi za Ulaya na Imani tuliletewa na watu kutoka huko.
Okay 👍
Fuatilia; usidanganywe eti wazungu hawaamini uchawi au hakuna uchawi huko Ulaya.
Nifuatilie kwa mtindo upi ili nipate ukweli maana wanaotembelea huko hawaoni hayo mambo ya ulozi
Ulifundishwa ili wale wafundishaji ambao walikuwa ni miongoni mwa wale malaika waasi; waweze kukubalika katika jamii ya binadamu na ikawa ni hatua mojawapo ndipo wakawaoa binti wa binadamu.
Hao malaika waasi wao walifundishwa uchawi na nani?
Unataka kununua au kujifunza?
Kujifunza nikivutiwa ninunue
 
Hilo tukio wewe mwenyewe umelikosea jawabu basi tuliache kama lilivyo

Au tuombe mzee mwingine mwenye uwezo huo afanye marudio ili tuthibitishe

Mf: kipindi cha jua kali alete mvua
Hapana sikukosa jawabu. Kama umenielewa nimesema nilimwona huyo mzee mteule na kumchunguza alichokuwa anafanya......
Kwa maneno rahisi au kwa uwazi zaidi naelewa ni kitu gani kinatakiwa ufanye ili Uweze kuizuia mvua hata kama wingu zito limetanda juu yenu. Kwa habari ya siku kuna jua kali alete mvua nakiri sijawahi kuona.
 
Impact zinaweza kuwepo ila tafsiri zikawa tofauti watu wawili waliopata tatizo moja mmoja akaenda hospitali na mwingine kwa mganga ila wote wakapata matibabu, dawa ile iwekwe sokoni inabidi iwe effective angalau asilimia 80 hii ina maanisha asilimia ishirini inaweza isitibu je tunaweza kusema dawa hazina impact vile kwenye uchawi huenda unafanya kazi namna hyo kwamba kuna wengine unakuwa effective na wengine unakataa,

Pia kwa kuwa uvhawi unatumia imani sana huenda kwa kuwa labda inatokana na energy labda kuna level flani ya energy yako unatakiwa uwe nayo ile uwe effective na unapo amini labda ndio umefika hyo level, ni kama vile madaktari mgonjwa akiwa kwenye hatua mbaya labda kwenye coma ndugu zake huwa wanambiwa angalau waongee naye huenda itasaidia ila kwa kawaida hii haingii akilini ila huenda kuongea naye anapata imani ya kupona na dawa zinafanya kazi vizuri kwa kuwa aliamini atapona, hujawahi kuona jinsi mtu anavyopata nguvu za ziada kwa kuwa tu kaamini kitu fulani anaweza so huenda uchawi unapo kuwa imani na kuwa commited sana ndio utaanza kuona impact zake
Kwahiyo unakubali kwamba ili uchawi uwepo au ufanye kazi inabidi uwe na imani nao kwanza ?
Yaani akili yako kwanza ikubali sio?

Tofauti na kipimo cha hospital uamini au usiamini kama ugonjwa upo utapata majibu bila kuitaji kiwango cha imani yako kwenye kipimo?
 
Hapana sikukosa jawabu. Kama umenielewa nimesema nilimwona huyo mzee mteule na kumchunguza alichokuwa anafanya......
Kwa maneno rahisi au kwa uwazi zaidi naelewa ni kitu gani kinatakiwa ufanye ili Uweze kuizuia mvua hata kama wingu zito limetanda juu yenu. Kwa habari ya siku kuna jua kali alete mvua nakiri sijawahi kuona.
Kwahiyo hilo tendo ndiyo uchawi wenyewe na lilikua ni halisi?
Tuseme ndiyo

Kwanini sasa hiyo nguvu ya kuzuia kama ipo isiwe kinyume chake pia yaan kuleta au kuvuta

Au hiyo nguvu inatumika kwa upande mmoja?
 
Kwahiyo unakubali kwamba ili uchawi uwepo au ufanye kazi inabidi uwe na imani nao kwanza ?
Yaani akili yako kwanza ikubali sio?

Tofauti na kipimo cha hospital uamini au usiamini kama ugonjwa upo utapata majibu bila kuitaji kiwango cha imani yako kwenye kipimo?
Ndio, kwa kuwa unaweza kupata dalili za kichawi ila ukaona labda ni akili yako inakudanganya, maana kitu alichofanya mzungu ni kufanya dalili zote za uchawi zionakane kama ni mambo ya saikolojia tu
 
Okay 👍

Nifuatilie kwa mtindo upi ili nipate ukweli maana wanaotembelea huko hawaoni hayo mambo ya ulozi
Personally nimekuwako huko Chuo cha Slagelse Technical School na sijasimuliwa ila nimejionea mwenyewe live. Kama unao marafiki wenyeji wa huko jaribu kuwauliza juu ya hizo habari
Hao malaika waasi wao walifundishwa uchawi na nani?
Hili ni sawa na kumwuliza Mwl. wako wa somo fulani e.g. Maths eti mwl. ww ulifundishwa na nani kwamba Formula ya kusolve Quadratic eqns inatoa jawabu sahihi? Hapo ninamaanisha ni mpaka watafutwe hao malaika halafu wahojiwe-huenda wakatuambia/wakatujibu. Mimi nimesoma ndani ya kitabu cha Henoko. (Uki-google utakipata hicho kitabu).
Kujifunza nikivutiwa ninunue
Nakushauri kaa mbali na jambo hilo kwani "Once in; no way out".
 
Kwahiyo hilo tendo ndiyo uchawi wenyewe na lilikua ni halisi?
Tuseme ndiyo

Kwanini sasa hiyo nguvu ya kuzuia kama ipo isiwe kinyume chake pia yaan kuleta au kuvuta

Au hiyo nguvu inatumika kwa upande mmoja?
Sijawahi kushuhudia tukio mubashara la kuleta mvua. Vinginevyo ningeweka hapa.
 
Ndio, kwa kuwa unaweza kupata dalili za kichawi ila ukaona labda ni akili yako inakudanganya, maana kitu alichofanya mzungu ni kufanya dalili zote za uchawi zionakane kama ni mambo ya saikolojia tu
Kwahiyo hapa tunagawana upande
Mimi kwa kua uchawi sijaupokea katika akili yangu na kuumini siwezi kuona nguvu yake

Na hata nikiona hicho wewe unachokiita uchawi mimi nita chukulia kama mambo ya saikolojia tu

Huku wewe ukiamini kua uchawi upo kwa sababu akili yako na imani vinakiri
Na mwisho huo uchawi una jidhihirisha kwako kwa sababu umeuamini

Hapo sawa dosho12
 
Kwahiyo hapa tunagawana upande
Mimi kwa kua uchawi sijaupokea katika akili yangu na kuumini siwezi kuona nguvu yake

Na hata nikiona hicho wewe unachokiita uchawi mimi nita chukulia kama mambo ya saikolojia tu

Huku ukiamini kua uchawi upo kwa sababu aliki yako na imani vinakiri
Na mwisho huo uchawi una jidhihirisha kwako kwa sababu umeuamini

Hapo sawa dosho12
ShesRise_1 Hapo sawa, ishu ni mapokeo tu na jinsi aklii yako ulivyoizoesha, mi pia sijawahi kukutana na tukio la uhakika la kuamini ni uchawi huwa najiambia nitakuwa sikuona,kusikia vizuri maana matukio yote nakuwa peke yangu ila nikishushudia na mtu itakuwa ni vizuri ila naamini uchawi upo maana naamini hizi zote ni approach walizotumia watu wa zamani kutaka kujaribu kujua jinsi mwili wa mwanadamu na ulimwengu inavyofanya kazi,

Ukisoma quantum mechanics vitu kama entanglement na superpostion kwamba kitu kinaweza kuwa sehemu mbili tofauti au kitu kuwa connected hata kiwe na umbali gani ila kama hiki kikiwa hivi hapo hapo na kingine kinakuwa kama mwezake hii yote inaelezea ulimwengu haupo kama tunavyojua na ndio maana naipa possibilty kubwa kuwa uchawi unaweza kuwepo ila jinsi ya ku elezea kwa watu ueleweke ndio vigumu
 
ShesRise_1 Hapo sawa, ishu ni mapokeo tu na jinsi aklii yako ulivyoizoesha, mi pia sijawahi kukutana na tukio la uhakika la kuamini ni uchawi huwa najiambia nitakuwa sikuona,kusikia vizuri maana matukio yote nakuwa peke yangu ila nikishushudia na mtu itakuwa ni vizuri ila naamini uchawi upo maana naamini hizi zote ni approach walizotumia watu wa zamani kutaka kujaribu kujua jinsi mwili wa mwanadamu na ulimwengu inavyofanya kazi,

Ukisoma quantum mechanics vitu kama entanglement na superpostion kwamba kitu kinaweza kuwa sehemu mbili tofauti au kitu kuwa connected hata kiwe na umbali gani ila kama hiki kikiwa hivi hapo hapo na kingine kinakuwa kama mwezake hii yote inaelezea ulimwengu haupo kama tunavyojua na ndio maana naipa possibilty kubwa kuwa uchawi unaweza kuwepo ila jinsi ya ku elezea kwa watu ueleweke ndio vigumu
Umeeleweka sana kaka
Shukran sana karibu tena my friend
 
Personally nimekuwako huko Chuo cha Slagelse Technical School na sijasimuliwa ila nimejionea mwenyewe live. Kama unao marafiki wenyeji wa huko jaribu kuwauliza juu ya hizo habari

Hili ni sawa na kumwuliza Mwl. wako wa somo fulani e.g. Maths eti mwl. ww ulifundishwa na nani kwamba Formula ya kusolve Quadratic eqns inatoa jawabu sahihi? Hapo ninamaanisha ni mpaka watafutwe hao malaika halafu wahojiwe-huenda wakatuambia/wakatujibu. Mimi nimesoma ndani ya kitabu cha Henoko. (Uki-google utakipata hicho kitabu).

Nakushauri kaa mbali na jambo hilo kwani "Once in; no way out".
Sawa mkuu asante kwa maoni yako hope tumemaliza vizuri mimi na wewe

Mengine tutazidi kuelekezana kwenye mijadala mingine zaidi shukrani bro
 
Mbona unaleta mifano ya matapeli wa mjini ili kuhalalisha hoja yako?

Hao wanaoomba picha na namba za simu ni matapeli tu kama matapeli wengine. Uchawi halisi hautegemei google maps au taarifa za kibenki kumfikia mtu. Umekariri wewe.
Utapeli na uchawi havitengani
 
Uchawi upo tena kwa makundi tofauti na kazi tofauti (wachawi,waloz,wamazingaumbwe,majini,mizimu na hata wazungu wanatambua kwa majina ya kikwao kama gosti,mirako,wichikrafti,)
 
Uchawi,ulozi ni sayansi ya asili tena ya kale ila wapo wanaoisujudu kupitia njia za kale na wapo tunaoiabudu kupitia njia za kisasa
 
Back
Top Bottom