Watu wa imani ndio watu gani?
Suala la watoto kuchelewa kutembea na hadi kuchanjiwa dawa ili waweze kutembea lipo sana katika jamii zetu, sasa mie napotoa mifano kama hiyo ili tuijadili unakuja kusema sie watu wa imani.
Watu wa imani ni watu gani? Hebu elezea ni kwa vp wewe unaishi kwa uthibitisho tu katika maisha yako ya kila siku.
Watu wa IMANI ni watu mnaomini katika MIUJIZA aka Superpower kama Mungu, Malaika, uchawi, majini na vitu kama hivyo ambavyo HAMUWEZI kuthibitisha uwepo wake
Unapotoa mfano toa mfano kwa kutumia LOGIC(akili) na sio IMANI
Yaani wewe ukisikia tu mtu karopoka kuhusu UCHAWI unaamini pale pale na kuja nao hapa JF kama ndio USHAHIDI wa hoja yako………,tuna jadili vipi sasa?
Mkuu nikikwambia leo nimekula Pilau naweza kuwa nakudanganya LAKINI uwezekano wa mimi kula pila upo kwa 100%…………… Nitofauti kabisa na nikikwambia leo nimekutana na paka akaanza kuongea……….
Swala fulani kuwepo kwenye jamii sio UTHIBITISHO kwamba ni la KWELI
Jamii ya Wachina zaidi ya Bilioni wanacho amini kuhusu Miungu yao ni FACT?
Ni KWELI Yesu ni Mungu kisa jamii ya wakristo wana amini hivyo? Vipi kuhusu jamii ya Vikings, Islam, Hindu nk?
Hivi unajua jamii ya kimasai ilikua inaamini nini kuhusu watoto wanaozaliwa na ulemavu wowote ule? Imani yao Ilikua ni kweli na sahihi?
Unajua Imani za jamii za kale zilivyokua KATILI Mkuu?