Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Kaka hapa nakuona ulivyokua una vimba wakati unapokea maua kutoka kwa cuzo
Hahaha hii si sawa kabisa 😂😂😂
Kuna sehemu vijana nilikuwa nawahoji mpaka nikawa naitwa Zitto Kabwe kipindi hicho yuko CHADEMA
Kaka wewe pia ni msukuma 😅sikujua kuhusu hili please nipe mwaliko nije mwanza nile samaki fresh wa ziwani
Shaka ondoa 😃
Hilo tukio lako ni story fulani ya kusisimua 😢
Natamani nikuamini 🤔
Kwanini utamani ? Na hilo tukio ni la kweli ?
 
ShesRise_1 msome na Uncle Pascal Mayalla hapa

 
ShesRise_1 msome na Uncle Pascal Mayalla hapa


Sawa nitasoma
Halafu huyu nimemuomba kazi kwenye office yake hataki😢
Nisaidie kuongea nae basi kaka 😊
Manyanza
 
😂😂😂
Ukiwa kijijini ndichi kabisa ukiongea kisukuma unaonekana unawadharau na wao huwa wanatakakuongea kiswahili eti

Hakika
Kuna dada mmoja ni msukuma aliniambia kijijini kwao ukiongea kiswahili ukiwa ni binti unaambiwa umeanza umalaya😅😅

Kaka acheni hizo bana🤣
 
Kuna dada mmoja ni msukuma aliniambia kijijini kwao ukiongea kiswahili ukiwa ni binti unaambiwa umeanza umalaya😅😅

Kaka acheni hizo bana🤣
Bhanaa nitarudi na kisa kingine baadaye tuache wasukuma na misifa yetu
 
Kuna mwaka fulani, nilipata ajali mbaya sana ambayo ilinifanya nipoteze fahamu kwa takribani siku kumi kutokana na brain concussion. Baada ya hapo nilianza kipindi cha recovery, na kwa bahati nzuri hali yangu iliendelea kuimarika taratibu.

Siku moja, nikiwa natembea kwa miguu, nilikutana na dada mmoja ambaye sikuwahi kumfahamu wala kuonana naye kabla. Aliniita:

“Kaka, mambo?”
Nikajibu, “Poa.”

Kisha akaniambia:
“Kaka yangu, sikujui wala hatufahamiani, lakini lete mkono wako.”

Nilimpa mkono wangu. Akaanza kuangalia kiganja changu kwa muda, kisha akaniambia mambo ambayo kwa wakati huo yalinishtua sana.

Aliniambia kuwa nilikuwa nimepata ajali mbaya ya gari, kwamba nilikuwa nimeumia upande wa kushoto wa kichwa, na kwamba kulikuwa na tatizo kwenye mkono wangu wa kushoto kiasi kwamba haukuwa ukifanya kazi vizuri.

Nilishangaa sana kwa sababu hayo yalikuwa mambo ambayo kweli yalikuwa yametokea kwangu.

Nikamwambia:
“Ndiyo dada yangu, ni kweli.”

Kwa sababu tayari nilikuwa nimetoka kwenye ajali na nilikuwa bado kwenye kipindi cha recovery, maneno yake yalinifanya niingiwe na hofu.

Akanieleza kwamba kesho yake asubuhi niende nyumbani kwake nikiwa na tende, haluwa, asali, sukari ya mawe, ndizi mbivu mbili na mkate. Pia akaniambia niende na sarafu za mia mbili ili niwape watoto wataokuwepo.
Alisema anataka kunifanyia kisomo.

Kesho yake nilienda na vitu hivyo mpaka nyumbani kwake. Kisomo kikaanza. Kulikuwa na watoto waliokuwa wakisaidia, wengine wakipiga dufu. Vile vyakula viliandaliwa pamoja kwenye sahani, nami nikaambiwa nile.
Wakati kisomo kikiendelea, ghafla nilianza kutapika.

Nilitapika vitu vilivyofanana na viini vya mayai vilikuwa kama vinne na vilikuwa vikubwa. Koo lilianza kuuma sana. Baadaye nilitapika kitu kilichofanana na damu nyeusi.

Nilipoteza nguvu kabisa. Mwili ulikuwa hauna nguvu, nilikuwa na maumivu makali na nikaanza kulia kwa sababu ya maumivu.

Yule dada akanishika mabegani na kunitoa nje huku mwili wangu ukiwa umelegea.
Aliendelea kunisomea huku mimi nikiendelea kuhisi maumivu makali na mwili wangu ukawa kama unabanwa.

Baadaye akachukua wallet yangu, akatoa hela na kwenda sokoni kununua jogoo mwekundu. Alimchinja hapo hapo, ingawa wakati huo hali yangu ilikuwa mbaya kiasi kwamba sikuweza kufuatilia vizuri kila kilichokuwa kinaendelea.

Baada ya muda, hali yangu ilianza kurudi taratibu kwenye hali ya kawaida.

Baadaye yule dada akanieleza tafsiri yake ya kile kilichotokea.
Aliniambia kwamba nilikuwa nimetupiwa vitu vibaya vya kijini na kwamba kulikuwa na mambo ya kichawi yaliyokuwa yamefanywa dhidi yangu. Sababu aliyotoa ilikuwa kwamba kuna watu ambao hawakupenda maisha yangu na namna nilivyoishi na watu.

Hicho ndicho kisa nilichowahi kukipitia miaka kadhaa iliyopita.
Lakini ninapokifikiria leo, huwa najiuliza swali moja muhimu:

Je, kile nilichokipitia ni ushahidi wa uchawi, au ni tukio lililotokea ambalo baadaye lilipewa tafsiri ya kichawi?

Kwa upande wangu, narudi na hoja kuwa kuna tofauti kubwa kati ya tukio na tafsiri ya tukio.

Tukio lenyewe ni jambo nililoliona na kulipitia: nilikuwa na historia ya ajali, nilipata hali mbaya ya mwili wakati wa hicho kisomo, nilitapika, nilihisi maumivu makali, nikadhoofika na baadaye nikapata nafuu.

Lakini kusema kwamba chanzo cha tukio hilo kilikuwa ni “uchawi”, “jini” au mtu fulani kunitupia kitu kibaya ni tafsiri ya tukio.🤔

Na hapo ndipo ninapoona mjadala wa uchawi unakuwa mgumu.

Kwa sababu mtu anaweza kusema:
“Niliona hiki, kwa hiyo uchawi upo.”

Lakini kuona tukio na kulipa jina fulani si sawa na kuthibitisha chanzo chake

Inawezekana mtu akawa amepitia tukio la kweli kabisa, lakini maelezo aliyopata kuhusu chanzo cha tukio hilo yakawa hayana ushahidi wa kutosha.
 
Kuna mwaka fulani, nilipata ajali mbaya sana ambayo ilinifanya nipoteze fahamu kwa takribani siku kumi kutokana na brain concussion. Baada ya hapo nilianza kipindi cha recovery, na kwa bahati nzuri hali yangu iliendelea kuimarika taratibu.

Siku moja, nikiwa natembea kwa miguu, nilikutana na dada mmoja ambaye sikuwahi kumfahamu wala kuonana naye kabla. Aliniita:

“Kaka, mambo?”
Nikajibu, “Poa.”

Kisha akaniambia:
“Kaka yangu, sikujui wala hatufahamiani, lakini lete mkono wako.”

Nilimpa mkono wangu. Akaanza kuangalia kiganja changu kwa muda, kisha akaniambia mambo ambayo kwa wakati huo yalinishtua sana.

Aliniambia kuwa nilikuwa nimepata ajali mbaya ya gari, kwamba nilikuwa nimeumia upande wa kushoto wa kichwa, na kwamba kulikuwa na tatizo kwenye mkono wangu wa kushoto kiasi kwamba haukuwa ukifanya kazi vizuri.

Nilishangaa sana kwa sababu hayo yalikuwa mambo ambayo kweli yalikuwa yametokea kwangu.

Nikamwambia:
“Ndiyo dada yangu, ni kweli.”

Kwa sababu tayari nilikuwa nimetoka kwenye ajali na nilikuwa bado kwenye kipindi cha recovery, maneno yake yalinifanya niingiwe na hofu.

Akanieleza kwamba kesho yake asubuhi niende nyumbani kwake nikiwa na tende, haluwa, asali, sukari ya mawe, ndizi mbivu mbili na mkate. Pia akaniambia niende na sarafu za mia mbili ili niwape watoto wataokuwepo.
Alisema anataka kunifanyia kisomo.

Kesho yake nilienda na vitu hivyo mpaka nyumbani kwake. Kisomo kikaanza. Kulikuwa na watoto waliokuwa wakisaidia, wengine wakipiga dufu. Vile vyakula viliandaliwa pamoja kwenye sahani, nami nikaambiwa nile.
Wakati kisomo kikiendelea, ghafla nilianza kutapika.

Nilitapika vitu vilivyofanana na viini vya mayai vilikuwa kama vinne na vilikuwa vikubwa. Koo lilianza kuuma sana. Baadaye nilitapika kitu kilichofanana na damu nyeusi.

Nilipoteza nguvu kabisa. Mwili ulikuwa hauna nguvu, nilikuwa na maumivu makali na nikaanza kulia kwa sababu ya maumivu.

Yule dada akanishika mabegani na kunitoa nje huku mwili wangu ukiwa umelegea.
Aliendelea kunisomea huku mimi nikiendelea kuhisi maumivu makali na mwili wangu ukawa kama unabanwa.

Baadaye akachukua wallet yangu, akatoa hela na kwenda sokoni kununua jogoo mwekundu. Alimchinja hapo hapo, ingawa wakati huo hali yangu ilikuwa mbaya kiasi kwamba sikuweza kufuatilia vizuri kila kilichokuwa kinaendelea.

Baada ya muda, hali yangu ilianza kurudi taratibu kwenye hali ya kawaida.

Baadaye yule dada akanieleza tafsiri yake ya kile kilichotokea.
Aliniambia kwamba nilikuwa nimetupiwa vitu vibaya vya kijini na kwamba kulikuwa na mambo ya kichawi yaliyokuwa yamefanywa dhidi yangu. Sababu aliyotoa ilikuwa kwamba kuna watu ambao hawakupenda maisha yangu na namna nilivyoishi na watu.

Hicho ndicho kisa nilichowahi kukipitia miaka kadhaa iliyopita.
Lakini ninapokifikiria leo, huwa najiuliza swali moja muhimu:

Je, kile nilichokipitia ni ushahidi wa uchawi, au ni tukio lililotokea ambalo baadaye lilipewa tafsiri ya kichawi?

Kwa upande wangu, narudi na hoja kuwa kuna tofauti kubwa kati ya tukio na tafsiri ya tukio.

Tukio lenyewe ni jambo nililoliona na kulipitia: nilikuwa na historia ya ajali, nilipata hali mbaya ya mwili wakati wa hicho kisomo, nilitapika, nilihisi maumivu makali, nikadhoofika na baadaye nikapata nafuu.

Lakini kusema kwamba chanzo cha tukio hilo kilikuwa ni “uchawi”, “jini” au mtu fulani kunitupia kitu kibaya ni tafsiri ya tukio.🤔

Na hapo ndipo ninapoona mjadala wa uchawi unakuwa mgumu.

Kwa sababu mtu anaweza kusema:
“Niliona hiki, kwa hiyo uchawi upo.”

Lakini kuona tukio na kulipa jina fulani si sawa na kuthibitisha chanzo chake

Inawezekana mtu akawa amepitia tukio la kweli kabisa, lakini maelezo aliyopata kuhusu chanzo cha tukio hilo yakawa hayana ushahidi wa kutosha.
Kaka Manyanza kwanza asante kwa kutenga muda wako kuandika na kisha kushare hapa Shukrani sana bro

1 Nikianza na hilo tukio la ajali, ambalo kwa kawaida ni tukio halisi kwa sababu ajali ilitokea na kila mtu aliona madhara ya hiyo ajali
Madhara hayo yalionekana mpaka kufikia hatua ya wewe kulala kwa siku zote hizo bila fahamu

2. Kuhusu huyo dada kukuambia umepata ajali na umeumia sehemu fulani

Hili halipaswi kuwa jambo la ajabu sana kwa sababu eti hukuwahi kumuona hapo kabla

Nasema hivi kwa sababu ulipata ajali kwenye mazingira ambayo kulikuwa na watu, na watu waliona au walisikia kuhusu hiyo ajali
Sasa kaka vipi kama huyo dada alisikia au alipewa taarifa kutoka kwenye chanzo ambacho wewe hukijui?

Kuhusu kufanyiwa kisomo, nadhani hii ni issue ya chano, sio?
Mtu mwenye majini hulishwa chano kwa mtindo kama huo
Mara nyingi hutumika vitu kama halua, tende na vinginevyo
Nimeona haya mambo ya chano kwa sababu familia yangu ni pure Muslim

Sasa kuhusu issue ya kutapika baada ya kisomo ukizingatia pia ulikuwa unaumwa na ulikuwa na maumivu ya kichwa, vipi kama zile ngoma na kelele za dufu zilikukera ukahisi kizunguzungu na hatimaye ukatapika?
Inawezekana pia vile ulivyovitapika vilitokana na hali hiyo

Lakini licha ya yote hayo bado kuna kosekana ushahidi wa kutosha kua ni kweli wewe uli rogwa na hao inaosemekana walikua hawapendi unavyo interact na watu na maisha yako kwa ujumla na hii ni kwa mjibu wa huyo dada mganga

So kwa mkanganyiko huu na kukosekana ushahidi strong basi uchawi unabaki kama dhana (theory)
 
Back
Top Bottom