Mtu anayekataa uchawi kuwa haupo jua kuwa hajafikiwa na madhars yake moja mwa moja. Ni kawaida kwa mwanadamu kubisha na kupinga jambo ambalo hana uwezo wa kuliona,kulisikia ama kulishika.
Mfano tunaona kuna watu wanakataa uwepo wa Mungu kwasababu tu hawamuoni, hawamsikii au hawawezi kumkaribia. Vivyo hivyo uchawi na majini ni miongoni mwa vitu vya ghaibu (unseen) kwa maana visivyoonekana kwa macho haya ya kibinadamu. Ila ukweli ni kuwa vipo.
Mfano majini wapo wengi kuliko sisi wanadamu hapa duniani ni vile Mungu katuzuia tusiweze kuwaona kwa macho yetu ya kibinadamu mpk pale wanapochukua maumbile ya vitu tulivyozoea kuviona kama vile nyoka,ng'e, mbwa mweusi n.k...
Hakika siku ya Qiyama watu waliomkataa Mungu hapa duniani watabaki midomo wazi sana pale watakapoweza kuona kwa macho yao unati mkubwa sana wa majini na malaika.