Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Eeh ni issue za saikolojia ukiambiwa umerogwa hapo hapo unaanza kuona mauza uza wakati kabla ulikua huyaoni
Kwani mkuu unaposema ni issue ya saikolojia una maanisha nini hasa? Maana kwa mfano hata mtu ambaye alikuwa na ukimwi ila hajui ikitokea akaenda kupima na kugundua ana huo ugonjwa pia ataanza kuona mauzauza na ndipo ataanza kuugua wakati huko kabla alikuwa anaishi vizuri tu.
 
Kwani mkuu unaposema ni issue ya saikolojia una maanisha nini hasa? Maana kwa mfano hata mtu ambaye alikuwa na ukimwi ila hajui ikitokea akaenda kupima na kugundua ana huo ugonjwa pia ataanza kuona mauzauza na ndipo ataanza kuugua wakati huko kabla alikuwa anaishi vizuri tu.
Mkuu ukimwi umepimwa kwenye vipimo vya kisayansi ukaonekana
Huo uchawi umepimwa vipi?
 
Mkuu ukimwi umepimwa kwenye vipimo vya kisayansi ukaonekana
Huo uchawi umepimwa vipi?
Mie nazungumzia hiyo point ya saikolojia kuona mauzauza baada ya kuambiwa umerogwa au una ukimwi, hayo ya kuuona kabisa ukimwi kwenye kipimo ni mjadala mwengine ambao nao unabishaniwa ila sio mada yetu.
 
Nendq kaishi Sumbawanga vijijini au Gamboshi halafu uwaambie wazee kwamba"uchawi hakuna ni mambo ya kisaikolojia tu" halafu sikilizia matokeo ndani ya mwezi mmoja utapata majibu
Kwanini aende mbali na eneo analoishi kana kwamba huo mji anapoishi amezunguka kote na kukosa kuona hiyo nguvu ya uchawi hadi aende huko sumbawanga?
 
Mie nazungumzia hiyo point ya saikolojia kuona mauzauza baada ya kuambiwa umerogwa au una ukimwi, hayo ya kuuona kabisa ukimwi kwenye kipimo ni mjadala mwengine ambao nao unabishaniwa ila sio mada yetu.
Ooh sawa mkuu lakini mimi swala la uchawi inabaki kua dhana tu
 
Kwanini aende mbali na eneo analoishi kana kwamba huo mji anapoishi amezunguka kote na kukosa kuona hiyo nguvu ya uchawi hadi aende huko sumbawanga?
Ni kwq sababu kwa mazingira ya mijini watu wameachana na hayo mambo wako bize kusaka noti ila mikoani bado hayo mambo yanaendelea
 
Kwanini aende mbali na eneo analoishi kana kwamba huo mji anapoishi amezunguka kote na kukosa kuona hiyo nguvu ya uchawi hadi aende huko sumbawanga?
Labda huko ndiyo kuna makonki
 
Sio kila kitu ambacho kimetajwa kwenye vitabu vya dini ni cha kweli.

Vitabu vya dini vimetaja uongo mwingi sana ambapo uchawi nao ni mojawapo ya uongo huo
Uongo mwingine ni upi uliotajwa kwenye vitabu vya dini?

Wakati tukiwa shule za msingi tulikuwa tunalipia Tsh 50 au 100 kuweza kuingia kwenye maonesho maalumu ya mazingaombwe.
Unaweza kuelezea ni nini ambacho kilikuwa kinatokea kwenye hayo maenesho, kwa mfano tunaona mtu anameza ndizi halafu inatokea puani kama ilivyo. Au jamaa anachana makaratasi na kuyaweka kwenye kikapu, akifanya anayoyajua anakuja kutoa pesa.

Elezea dhana ya mazingaombwe ilikuwa inafanikishwa na nini?
 
Mfano mtu anaenda kwa mganga ili kuroga watu wafarakane kama ni wapenzi waachane, sasa hapo ni saikolojia gani mganga anaweza kutumia kwa huyo mtu ili akubali kweli uchawi umejibu kwa matokeo ya hao watu kufarakana?
 
Uongo mwingine ni upi uliotajwa kwenye vitabu vya dini?

Wakati tukiwa shule za msingi tulikuwa tunalipia Tsh 50 au 100 kuweza kuingia kwenye maonesho maalumu ya mazingaombwe.
Unaweza kuelezea ni nini ambacho kilikuwa kinatokea kwenye hayo maenesho, kwa mfano tunaona mtu anameza ndizi halafu inatokea puani kama ilivyo. Au jamaa anachana makaratasi na kuyaweka kwenye kikapu, akifanya anayoyajua anakuja kutoa pesa.

Elezea dhana ya mazingaombwe ilikuwa inafanikishwa na nini?

mazingaombwe ni nini



1787045810660.png

1787045810726.png

1787045810746.png

+2





Mazingaombwe ni sanaa ya udanganyifu wa macho au vitendo vya ajabu vinavyofanywa na mtu ili kuburudisha, ambapo vitu vinaonekana kufanyika lakini kiuhalisia ni mbinu za kisayansi, wepesi wa mikono, au saikolojia badala ya uchawi wa kweli. [1, 2, 3]

Sifa za Mazingaombwe
    • Kiini macho: Huwafanya watazamaji kuona vitu ambavyo havipo au kutokea kwa namna ya tofauti na uhalisia.
    • Sanaa na Burudani: Hutumika kwenye maonyesho ya sarakasi, majukwaani, na televisheni.
    • Mbinu za Siri: Msanii hutumia vifaa maalumu au kasi ya mikono kuficha ukweli wa jinsi tendo linavyofanyika.
 
Mfano mtu anaenda kwa mganga ili kuroga watu wafarakane kama ni wapenzi waachane, sasa hapo ni saikolojia gani mganga anaweza kutumia kwa huyo mtu ili akubali kweli uchawi umejibu kwa matokeo ya hao watu kufarakana?
Hivi kweli watu wanaweza kufarakana kwa mtindo huo?
Sio kwamba kutokuelewana ndiyo chanzo kikuu cha mahusiano kuharibika ?
 
Back
Top Bottom