Mastory ya bey
Za jioni watu wangu natumaini mko gud kabisa,tumshukuru Mola wetu kwa neema ya uhai
Kila mtu katika nyakati fulani fulani katika maisha hutokea akafanya maamuzi ambayo sio sahihi, na maamuzi hayo huenda yakamuathiri yeye binafsi au yakawaathiri wapendwa wake
Hivyo tunajikuta tuna bakia na Majuto na kujilaumu sana,kwanini nilifanya vile niliyofanya,je lau nisingefanya vile huenda mambo yangekuwa tofauti leo
Iko hivi watu wangu tusijilaumu sana kwasababu by the time we made that decision hatukutegemea kwamba mambo yangekuwa kinyume na matarajia yetu,tulitarajia kupata matokeo mazuri kutokana na maamuzi hayo
Kwahiyo sisi hatujakamilika tumeumbwa kufanya makosa,lau tusingefanya makosa basi tusingekuwa wanaadamu,kwahiyo makosa ni sehemu ya maisha yetu,kwahiyo just chill na usijilaumu sana
Maisha lazima yasonge mbele kwani sisi sio wa kwanza kufanya makosa,walifanya wenzetu kwahiyo siyo jambo geni tusijilaumu kwamba sisi ndio wakosaji kivileee
Kuanzia sasa baada ya kusoma hii notes board badilisha mtazamo wako,Sahau yote yaliyo pita na songa mbele,focus wakati uliopo na kheri kubwa itapatikana
Kumbuka unapobadilisha mawazo yako basi unabadilisha dunia yako