ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,600
- 21,650
Mastory ya bey
Hello my people natumaini mko poa kabisa, bey yupo gud kama kawaGratitude /kuonyesha shukrani au appreciation katika maisha ni jambo kubwa sana
Huwa tunaambiwa wenye kushukuru au kuonyesha shukrani kwa Mola wetu huwa wanaongezewa au huzidishiwa zaidi
Tuwe watu wenye shukrani kwa kila neema tuliyo barikiwa na Mola wetu,wewe unatamani viatu vizur basi jua wengine hawana hata hiyo miguu
Unalalamika kazi yako haikulipi vizur kuna watu wanatamani nao wangekuwa wanatoka asubuhi kama wewe walau wakabangaize chochote
Unalalamika huna hela lakini kuna wenzako hawana hela na hawana afya nzur pia,ebu imagine afya yako ni mgogoro halafu uwakika wa kuingiza chochote huna
Kifupi kila mtu ana vita ambayo anapigana nayo,wewe una hiki na huna kile,mwenzako ana kile na hana hiki,ili mradi kila mmoja wetu anapambana na changamoto zake
Kwahiyo let us count our blessings, na tutambue kwamba kila mtu kuna neema ambazo amepewa na nyengine amekosa,kwahiyo tushukuru kwa kila jambo na wala tusikufuru.