2259hrs
Mastory ya Bey
My people mmeshindaje,habar za kutwa nzima,hope mko poa kabisa,tunakutana tena kwenye kijiwe cha Mastory ya Bey
Guys leo bwana nataka kuzungumzia swala Zima la kupokea simu,kuna hii shu simu inapigwa halafu unaisikilizia weee kisha ndio unaipokea,hii sio poa kabisa,unawapotezea watu muda
Unajua mtu akikupigia simu ina maana ana shida ya chap,muongee mmalizane kisha aendelee na mishe nyingine,na sio wakati wa wewe kumsikilizisha muito wa simu muda mrefu
Simu ipo mkononi je kuna haja gani ya kuchelewesha kuipokea,unafanya hivyo ili uonekane uko busy au,sikia stop wasting people's time mtu akikupigia just pokea chap na msikilize kila mtu aendelee na mishe zake
Mimi bwana sina mambo mengi ,kwanza kile kitendo cha kuacha simu iite muda mrefu naona kero,yani imeita tu chap nareceive tunamalizana fasta
Kuna siku moja mzazi mwenzangu ile kapiga tu chap nikapokea,akasema duh simu ilikuwa mkononi nini? Nikamjibu si inaitwa simu ya mkononi au,akabaki anacheka tu
Kwahiyo ebu tuache zile mbanga za kupotezeana muda,simu imepigwa chap pokea msikilize anayekupigia chap tu mnamalizana,kusikiliziana ni nyie na baby wako lakini sio kila mtu unataka kumuweka pending kama una mmudu vile au kwasababu simu ni yako🤣🤣 ndio maana unaamua kuchelewa kupokea,tuache ujinga bwana!!!